Uchaguzi 2020 Hatimaye CCM na mgombea wao waanza kutumia chopa kama usafiri wa kampeni

Uchaguzi 2020 Hatimaye CCM na mgombea wao waanza kutumia chopa kama usafiri wa kampeni

barafu

JF-Expert Member
Joined
Apr 28, 2013
Posts
6,739
Reaction score
32,880
1600586590839.jpg

Hatimaye Chama Cha Mapinduzi kimeamua kuanza kutumia chopa kama sehemu ya usafiri wa kampeni zake.

Chopa hiyo itaanza kutumika kwenye nusu ya pili ya harakati za kampeni kuelekea October 28,chopa hiyo yenye usajili wa 5Y-HSN imekodiwa toka nchini Kenya kwa mmoja wa wanasiasa na mfanyabiashara maarufu Ndugu Simeon Nyachae.

Simon Nyachae, mwanasiasa wa County ya Kisii nchini Kenya, ni rafiki na mshirika pia wa Rais Magufuli, kwani hapo awali wakati wa Utawala wa Mwai Kibaki, Nyachae aliwahi kuhudumu kama Waziri wa barabara.

Wakati Muungano wa Rais Kibaki wa NARC ulipoanza kudhoofika kwenye uungwaji mkono, chama cha FORD-People cha Nyachae kikajiunga naye, na rais Mwai Kibaki akamteua Nyachae kama Waziri wa Nishati na baadae akampa kuwa waziri wa Barabara.

Nyachae alitajwa katika ripoti ya Waki kama mmoja wa wahusika wa vurugu za baada ya uchaguzi wa 2007-2008 ambapo zaidi ya watu 1,600 walifariki.

Aliaminika kupanga mashambulizi dhidi ya viongozi wa upinzani wa ODM.

Aligombea na kupoteza uchaguzi wa ubunge wa mwaka 2007.
 
Maendeleo ya vitu au watu?
Kama mmegundua mmekosea si mbadilishe? Siku za kampeni bado zipo zaidi ya 30, ni suala la kuomba radhi na kubadilisha slogan. Kama mmeona vitu haviwasaidii njooni tuungane kuhimizaaendeleo ya watu ili walete vitu. Kwa nini uteseke kushabikia madege huku hospitali zikibaki majengo tu bila dawa?
 
Nyachae alitajwa katika ripoti ya Waki kama mmoja wa wahusika wa vurugu za baada ya uchaguzi wa 2007-2008 ambapo zaidi ya watu 1,600 walifariki.

Aliaminika kupanga mashambulizi dhidi ya viongozi wa upinzani wa ODM.

Aligombea na kupoteza uchaguzi wa ubunge wa mwaka 2007
Hapa ndiyo pa Muhimu sana barafu. Ili likitokea wasiseme hukuwaambia
 
Kama mmegundua mmekosea si mbadilishe? Siku za kampeni bado zipo zaidi ya 30, ni suala la kuomba radhi na kubadilisha slogan. Kama mmeona vitu haviwasaidii njooni tuungane kuhimizaaendeleo ya watu ili walete vitu. Kwa nini uteseke kushabikia madege huku hospitali zikibaki majengo tu bila dawa?
Sasa ukiketa dawa bila hospital utakuwa unawasambazia watu nyumbani..au ukiwanunulia watu magari bila barabara hizo gari watakuwa wanazipaki nyumbani kwa maonyesho?
 
View attachment 1575038


Nyachae alitajwa katika ripoti ya Waki kama mmoja wa wahusika wa vurugu za baada ya uchaguzi wa 2007-2008 ambapo zaidi ya watu 1,600 walifariki.

Aliaminika kupanga mashambulizi dhidi ya viongozi wa upinzani wa ODM.

Aligombea na kupoteza uchaguzi wa ubunge wa mwaka 2007.

Kipande hiki kinatoa ujumbe kuwa huyo Nyachae sio kwamba ametoa tu Helikopta, pia atatoa mbinu jinsi ya kutekeleza mauaji kwenye uchaguzi huu dhidi ya wapinzani. Ujumbe huu unaeleza mengi kwa jicho la tatu.
 
Kipande hiki kinatoa ujumbe kuwa huyo Nyachae sio kwamba ametoa tu Helikopta, pia atatoa mbinu jinsi ya kutekeleza mauaji kwenye uchaguzi huu dhidi ya wapinzani. Ujumbe huu unaeleza mengi kwa jicho la tatu.
Alafu na wewe unajiona umepost kitu cha maana!
 
Back
Top Bottom