Uchaguzi 2020 Hatimaye CCM na mgombea wao waanza kutumia chopa kama usafiri wa kampeni

Uchaguzi 2020 Hatimaye CCM na mgombea wao waanza kutumia chopa kama usafiri wa kampeni

Very Risky...

Acheni tu. Kwani kuna jipya lipi mtaongea. Kula kodi za masikini tu.

Stay put.. Msubiri kutawanyika hapo 28th oct.
 
Hilo dude lilishawahi kumuangusha yeye na yule askari anayejiita Kova. Aachane nalo atumie tu hiyo mibarabara yake anayojivunia.
 
Hapana hili lisitokee! Pombe ikimwagika tutaahirisha uchaguzi halafu majamaa yakajipange upya! Twende na Pombe yetu tu mpaka mwisho!
kwani katiba inasema hivyo? jikumbushe wakati wa Mkapa
 
Hatimaye Chama Cha Mapinduzi kimeamua kuanza kutumia chopa kama sehemu ya usafiri wa kampeni zake.

Chopa hiyo itaanza kutumika kwenye nusu ya pili ya harakati za kampeni kuelekea October 28,chopa hiyo yenye usajili wa 5Y-HSN imekodiwa toka nchini Kenya kwa mmoja wa wanasiasa na mfanyabiashara maarufu Ndugu Simeon Nyachae.

Simon Nyachae, mwanasiasa wa County ya Kisii nchini Kenya, ni rafiki na mshirika pia wa Rais Magufuli, kwani hapo awali wakati wa Utawala wa Mwai Kibaki, Nyachae aliwahi kuhudumu kama Waziri wa barabara.

Wakati Muungano wa Rais Kibaki wa NARC ulipoanza kudhoofika kwenye uungwaji mkono, chama cha FORD-People cha Nyachae kikajiunga naye, na rais Mwai Kibaki akamteua Nyachae kama Waziri wa Nishati na baadae akampa kuwa waziri wa Barabara.

Nyachae alitajwa katika ripoti ya Waki kama mmoja wa wahusika wa vurugu za baada ya uchaguzi wa 2007-2008 ambapo zaidi ya watu 1,600 walifariki.

Aliaminika kupanga mashambulizi dhidi ya viongozi wa upinzani wa ODM.

Aligombea na kupoteza uchaguzi wa ubunge wa mwaka 2007.

Helicopter hiyo haitatumika na Mgombea wa Urais kwenye kampeni bali itatumika na Baadhi ya wagombea wa viti vya Ubunge,Mgombea wa Urais atatembea kwa Usafiri wa gari ili kufanya coverage kwenye mitaa na vijiji vyote.
 
Kifo cha Akwilina kinafanana na machafuko ya Kenya 2007? Hii Chadema yetu imejaa watu gani?

Ndio maana nimesema majaribio ilikuwa kifo kile. Maana kifo kile kilisababishwa na siasa za dhuluma, ambazo kwa sasa imekuwa ni muendelezo.
 
Helicopter hiyo haitatumika na Mgombea wa Urais kwenye kampeni bali itatumika na Baadhi ya wagombea wa viti vya Ubunge,Mgombea wa Urais atatembea kwa Usafiri wa gari ili kufanya coverage kwenye mitaa na vijiji vyote.

Kwanza sidhani kama protokali zinaruhusu sitting president kusafiri kwa chopa ya kiraia. chopa nyingi za Afrika haziaminiki

Na kwanza akikumbuka ile ajali aliyopata ya chopa ya jeshi akiwa yeye, makamu wa rais Bilal na Kova sidhani kama atapanda hiyo kitu
 
Wakati Chadema wamejiandaa kutumia chopa na kisha kuzuiwa...Polepole alisema wao wanatumia barabara ili wakutane na wapiga kura.
Leo imekuaje tena?
Kuna maeneo unaweza kuendesha gari mwendo mrefu bila kuona watu, pia kuna maeneo mengi Magu katembelea hivi karibuni kabla ya kampeini kuanza na mwisho kabisa natambua pole pole ni mwanasiasa na kwakweli unahitaji kuwa na akili ya Hali ya juu Sana kumwelewa Politician..anakufanya uwe mwanafalsafa Kwa kumsikiliza ili uchambue ni lipi anasema ukweli na ni lipi anapiga politik.. Huwezi kuwa na akili ya wastani ukamwelewa mwanasiasa, ni either uwe shallow au smart kuishi na mwanasiasa.
 
Back
Top Bottom