Uchaguzi 2020 Hatimaye CCM na mgombea wao waanza kutumia chopa kama usafiri wa kampeni

Uchaguzi 2020 Hatimaye CCM na mgombea wao waanza kutumia chopa kama usafiri wa kampeni

Usafiri wa chopa sio salama kabisa, usije ukawapiga chini kama wale wa 2015.
 
Mkuu I
Barafu mtaalam wa midege is back.

Kaka toka jamaa asitishe kulete midege,ukatuacha humu jukwaani.

Nikadhani umetoweka. Nafurahi kukuona tena.
Mkuu ID name yako inanikumbusha mbali sana kuhusu wazungu wawili wenye gari ya Malawi
 
Jamaa alishadondoka na helicopter...nikae kimya
 
Hatimaye Chama Cha Mapinduzi kimeamua kuanza kutumia chopa kama sehemu ya usafiri wa kampeni zake.

Chopa hiyo itaanza kutumika kwenye nusu ya pili ya harakati za kampeni kuelekea October 28,chopa hiyo yenye usajili wa 5Y-HSN imekodiwa toka nchini Kenya kwa mmoja wa wanasiasa na mfanyabiashara maarufu Ndugu Simeon Nyachae.

Simon Nyachae, mwanasiasa wa County ya Kisii nchini Kenya, ni rafiki na mshirika pia wa Rais Magufuli, kwani hapo awali wakati wa Utawala wa Mwai Kibaki, Nyachae aliwahi kuhudumu kama Waziri wa barabara.

Wakati Muungano wa Rais Kibaki wa NARC ulipoanza kudhoofika kwenye uungwaji mkono, chama cha FORD-People cha Nyachae kikajiunga naye, na rais Mwai Kibaki akamteua Nyachae kama Waziri wa Nishati na baadae akampa kuwa waziri wa Barabara.

Nyachae alitajwa katika ripoti ya Waki kama mmoja wa wahusika wa vurugu za baada ya uchaguzi wa 2007-2008 ambapo zaidi ya watu 1,600 walifariki.

Aliaminika kupanga mashambulizi dhidi ya viongozi wa upinzani wa ODM.

Aligombea na kupoteza uchaguzi wa ubunge wa mwaka 2007.
Kweli nimeamini tuonyeshe rafiki zako tukujue tabia zako
 
Yalimuonea wivu Lissu alipotaka kutumia helikopta ushamba na ulimbukeni nizigo mzito sana .
 
Alafu kuna lijitu hapa linapiga kelele Eti magufuli apewe tano tena!!!

Nimeshasema na nasema tena kwa ufedhuli na uzandiki alioufanya Magufuli dhidi ya watanzania wenzake tukimpa tena miaka 5 hata shetani atatushangaa
 
Alafu kuna lijitu hapa linapiga kelele Eti magufuli apewe tano tena!!!

Nimeshasema na nasema tena kwa ufedhuli na uzandiki alioufanya Magufuli dhidi ya watanzania wenzake tukimpa tena miaka 5 hata shetani atatushangaa!!

Yaani Chadema wamefanyiwa figisu za wazi kabisa mchana kweupe kuhusu kutumia chopa alafu CCM haohao nao wanaenda kutumia Chopa alafu Kuna mtu na akili zake bado anashawishi magufuli achaguliwe tena!!!

Kati ya kipindi murua ambacho Mungu katuwekea kutupima akili Watanzania ni kipindi hiki. Kusema kweli kwa roho mbaya na uzandiki wa Magufuli na CCM yake hata shetani atatushangaa tukimchagua tena. Si Mungu tu!
 
Maelezo mengine hayakuwa na umuhimu kabisa.
 
Hapo ndipo mnapokosea
Siku nyingine huwa nawaeleza halafu hamfuati, niliwaambia mnichague mimi mkasema sawa, nikawaambia mnichagulie na mbunge wa CCM hamkunichagulia, nataka niwaeleze ukweli wala siwafichi asingekuwa Kapuya hii barabara nisingeijenga". Dkt.Magufuli
 
Alafu kuna lijitu hapa linapiga kelele Eti magufuli apewe tano tena!!!

Nimeshasema na nasema tena kwa ufedhuli na uzandiki alioufanya Magufuli dhidi ya watanzania wenzake tukimpa tena miaka 5 hata shetani atatushangaa!!

Yaani Chadema wamefanyiwa figisu za wazi kabisa mchana kweupe kuhusu kutumia chopa alafu CCM haohao nao wanaenda kutumia Chopa alafu Kuna mtu na akili zake bado anashawishi magufuli achaguliwe tena!!!

Kati ya kipindi murua ambacho Mungu katuwekea kutupima akili Watanzania ni kipindi hiki. Kusema kweli kwa roho mbaya na uzandiki wa Magufuli na CCM yake hata shetani atatushangaa tukimchagua tena. Si Mungu tu!
Mtu mwenye roho mbaya anajenga barabara, hospitali, kusaidia walioonewa, kupambana na rushwa na uonevu?

Mtu mwenye roho mbaya hafanani hata kidogo na Rais Magufuli
 
Kwahiyo kutumia chopa ni kuishiwa pumzi?

CHADEMA ina watu wengine wa hovyo kabisa mmoja wapo ni wewe
Kutumia Chopa kwa hali ya kawaida si kuishiwa pumzi hata CHADEMA walipanga kutumia Chopa wafike nchi nzima lakini kwa kuwa hawakuonyesha wameishiwa pumzi walizuiwa kutumia Chopa na wanaendelea na kampeni. CCM baada ya karibu mwezi kwenye kampeini wamegundua wameishiwa pumzi na kuamua kutumia Chopa muda uliobaki lakini ili nao wasizuiwe wanaithibitishia Mamlaka ya Safari za Anga kuwa wako hoi kwa kupiga push-up mbele ya Chopa. Watapata kibali hata kama Nyachae (babu wa rubani wa CHADEMA) mwenyewe atakuwa rubani.
 
Mtu mwenye roho mbaya anajenga barabara, hospitali, kusaidia walioonewa, kupambana na rushwa na uonevu?

Mtu mwenye roho mbaya hafanani hata kidogo na Rais Magufuli
Hata tupate raisi Jini hospitali zitajengwa tu!! Hajengi kwa pesa zake ni hela za kodi za wananchi.
Roho mbaya ya mtu inaonekana kwenye matendo yake dhidi ya watu wengine hasa anaoona wamemzidi au wako kwenye nafasi ya kumzidi.
 
Magufuli anahangaikia nini?? Si amejenga mabarabara na amenunua madege na ameunda meli??!!
 
Kwa hiyo hawataki kutumia barabara walizozijenga?
 
Back
Top Bottom