Tetesi: Hatimaye "Chato International Airport" kuzinduliwa rasmi mwezi Aprili

Tetesi: Hatimaye "Chato International Airport" kuzinduliwa rasmi mwezi Aprili

Tatizo lenu mmelewa ulevi wa madaraka, kama suala ni kupata upendeleo mngeanza na mambo ya msingi kwenu kama ugonjwa wa mnyauko wa migomba, awasaidie research na suluhisho mngeondokana na njaa kali mliyonayo sasa.

Basi la Sabuni au Lushanga kwenda Chato halijazi abiria nauli chini ya elfu kumi mtajaza ndege nyie? Tumieni upendeleo huu wa raisi kutoka kwenu awasaidie vya maana sio white elephants.

Hakuna mmiliki wa ndege Chato, hakuna kiwanda zaidi ya ginnery ya ushirika, hakuna hata Hotel pale zaidi ya tule tu Lodge tuchafu nani apande ndege kwenda Chato mtukufu akitoka. Mwanakijiji wa Ilyamchele atapanda ndege?

Sio tu kulewa madaraka ila wamelewa mbenge , hivi chato na Geita wapi kumeendelea na kuna kuwa kwa haraka? hata kasamwa ni better kuliko chato, kwa nini tusiangalie walau eneo karibu na Geita tukajenga huo uwanja to boost and rapid growth of Geita region? kama tu mini-Bus zenye abilia 23 haziwezi kujaza abiria kutoka chato iweje kwa ndenge? tuweni na vipaumbele kama Taifa, tujenge viwanja hivi kulingana na mahitaji ya kiuchumi Tanzania sio mahitaji ya kikanda ,mfano wadau wengi wanadai Serengeti ndio hitaji kuu sasa hivi basi nguvu ya chato ilitakiwa ihamishiwe Musoma/Tarime/Mwanza nk.
 
Ni ujinga na upumbavu kwa mpigo kuinyanyapaa "itikadi"
Mnaweza kuweka uchambuzi mzuri sana ila ukakosa mashiko kwa kuwa tu una lengo la kiitikadi zaidi.

Mimi huwa najiuliza, je suppose tungechagua huko, kwa bahati mbaya sana umeshindwa kujiendesha wenyewe mkaamua kuturudishia walewale waliokimbia huku baada ya kukatwa je mngeweza kutujengea nchi kweli?, au mngeishia kuandika uchambuzi kama huu wakati mkishuhudia barabara ya Chalinze-Moshi ikiwekwa 4 ways, na kiwanja kama hicho cha chato kikijengwa Hai au Monduli?

Maana wenzetu wa upinzani mmekuwa mabingwa ya kuchambua msivyoviweza, mmekuwa wazuri theoretically but you are not practically oriented, mambo yenu mengi yanakwenda kinyume lakini kwa vile kafanya yule, basi you keep quite kama vile hamuoni huku ukisubiri uongee likifanyika upande wa pili.

Kaskazini ilijengeka mapema kwavile watu wa kaskazini walipata fursa, wakakumbuka kwao ili wapate kwenda mapumzikoni kila mwaka, sasa acha fursa zinapopatikana sehemu zingine basi wazitumie fursa hizo, huku mkiwa wavumilivu mkisubiri 2020 ,
 
Ni kosa la KATIBA yetu ya Nchi haielekezi SHERIA, SERA, VIPAUMBELE vya TAIFA ambavyo vitafuatwa na kiongozi anayeingia madarakani kutekeleza sera na vipaumbele vya Taifa kuanzia pale ambapo kiongozi aliyepita ameachia, matokeo yake vyama vya Siasa kwa kiasi kikubwa huwaachia wagombea wao kutengeneza sera na vipaumbele pindi wakishinda uchaguzi matokeo yake utaona kila kiongozi anayeingia madarakani anakuya na YAKE..........

Hujui Kiongozi ajae atasema nini.....!!!! Miradi kuachwa, Sera kubadilishwa au kufutwa.......!!!!
MAONI YA KATIBA YA WANANCHI ILIKUWA SULUHISHO.............
 
Mkuu barafu. Nikushukuru kwa kuanzisha mada.

Hilo la uwanja kujengwa chato binafsi sioni kwanini usijengwe huko. Labda kama ungeonyesha ni kwanini chato panastahili uwanja mdogo kuliko unaojengwa kuliko sababu ulizotoa.

Hoja yangu inahusu kuboresha uwanja wa Mwanza kuhudumia mbuga ya Serengeti.

Ki mantiki. Sehemu kubwa ya mbuga ya serengeti ipo mkoani mara na si zaidi ya kilometa 110 kwa barabara kutoka makao makuu ya mkoa hadi kuingia mbugani kwa kupitia barabara ya Musoma - Arusha na haifiki kilometa 70 kwa kupitia barabara ya Musoma - Mwanza. Mbuga hii ipo kwenye wilaya za Serengeti Tarime na Bunda. Ambapo Wilaya ya Serengeti inamiliki eneo kubwa zaidi.

Sehemu ndogoya mbuga hii iliyobaki ipo mkoani SIMIYU katika wilaya za Itilima na Bariadi. Mkoa wa mwanza ulikoma kumiliki mbuga hii baada ya kuanzishwa mkoa wa simiyu.

Mipango ya kujenga kiwanja cha ndege kuhudumia mbuga ya serengeti ni ya muda mrefu ambapo awali ilikuwa uwanja mkubwa wa kisasa ujengwe Musoma au Bunda ili kuhudumia mbuga hii. Na uwanja mdogo wa Mugumu uboreshwe. Eneo la uwanja lilibainishwa na juzi kati enzi za Utawala wa Kikwete lilipimwa upya. Mpango huu uliambatana na kuboresha air strip ya mugumu iwe na viwango vya sasa vya uwanja kama wa Arusha na pia kujenga barabara kutoka Musoma hadi Arusha.

Utekelezaji wake unapigwa figisu hadi leo ambapo hakuna kiwanja. Air strip wala barabara iliyojengwa. Sababu mojawapo ni hoja zilizotolewa na wana kaskazini kwamba bora kuijenga KIA ili ihudumie mbuga zote zilizoko kaskazini mwa nchi.

Uwanja wa KIA UKAJENGWA. Na tagu wakati huo mbuga ya serengeti ikajulikana kwamba ipo arusha kama ambavyo tunaambiwa mlima kilimanjaro upo nchini Kenya. Mkoa wa mara ukakosa mapato ya utalii kwa maana ya viingilio vya wageni mbugani na uwekezaji wa miundombinu kama taasisi za utalii mfano hoteli, vyuo majengi ya taasisi za umma nk. na miundombinu hii kwa wingi imeendelea kujengwa Arusha tangu wakati huo,na kuhalalisha mkoa wa arusha kumiliki mbuga ya Serengeti.

Awamu ya pili ya kujenga uwanja mkoani mara ni huo uwanja wa Serengeti ulioutaja kwenye andiko lako.

Hii ilikuwa zaidi inachochewa na maombi kutika kwa mwekezaji aliyewekeza pale Gurumeti.

Kama ulivyogusia. Uwanja huu pia haukujengwa kutokana na figisu za wanaharakati wa ndani na nje ya nchi. Ambapo jamaa zetu wa kaskazini waliungana na Wakanya kukwamisha ujenzi.

Hivyo badala ya kupugia debe uwanja wa Mwanza kuhudumia serengeti ungesema ukweli kwamba uwanja wa kuihudumia mbuga hii ujengwe ndani au karibu na mbuga hii. Nani ya mkoa wa mara au wa sumiyu.

Lengo hapa ni kuonyesha uhalisia. Sote tunakubali uwanja wa ndege wa mwanza unahitajika na ulitakiwa uwepo kabla ya ule wa KIA.

Suala la kuhudumia mbuga ya serengeti ama kutokea KIA au uwanja wa ndege wa Mwanza hakuta tofauti kubwa maana bado usafiri wa magari wenye kuchukua muda mrefu njiani utatumika.

Tuseme tu kwamba lazima kuwe na uwanja wa ndege wa kisasa unaokidhi mahitaji ya sasa na baadae NDANI YA MKOA WA MARA au MKOA WA SIMIYU ili kuihudumia hii mbuga.

Wenzetu wa-kenya wanajenga viwanja vya ndege vikubwa vilivyi katika umbali usiokuwa mkubwa ilimradi kuna sababu. Mfano angalia umbali wa viwanja vya Nairobi Kia na Taveta. Pia Nairobi Nakuuru Masai Mara na Kisumu. Au hapa Tanzania kuna Kia Arusha na Moshi.

Basi ni halali kujenga na kuboresha viwanja vya Mwanza Kigoma Simiyu Tabora Singida Shinyanga Chato Bukoba na MUSOMA kwa ukubwa tofauti kulingana na vigezo vya kiuchumi kijamii na kijiografia.

Msisitizo ni kwamba mbuga ya serengeti italeta faida kwa taifa hili kama serikali watanzania wote na wakazi wa mikoa ya Mara na Simiyu wataona umuhimu wa kuwekeza kwenye miundombinu ya kuihudumia mbuga hiyo. Kama maji barabara hoteli uwanja wa ndege nk. ndani ya mikoa husika.
Daaa kama nakuona vile unavyoongea...
 
Kipigi,

Naungana na wewe.

Pist yake kwangu imekosa mantiki pale aliposema uwanja wa chato usijengwe ili kuboresha wa mwanza wakati anatambua kwamba

1. Maboresho ya uwanja wa mwanza yanaendelea hadi sasa na ujenzi wa uwanja wa chato hauja athiri maboresho ya uwanja wa mwanza.

2. Kuna uhitaji wa kujenga uwanja wa ndege kuhudumia mbuga ya serengeti. Badala ya kupiga debe uwanja huo ujengwe ndani au karibu na mbuga hiyo anashadadia uwanja wa mwanza ndio uhudumie serengeti ilhali upo miles away.

Ni seme tu kwamba badala ya kulalamikia uwanja kujengwa chato. Tusifie na kudai ujenzi na uboreshaji wa viwanja vingine vingi tu vinavyohitajika kote nchini kulingana mahitaji ya sasa na ya baadae.

Lengo isiwe kukataa maendeleo yasiwepo eneo flani bali yapelekwe kwa wakati kulingana na mahitaji na faida zitakazopatijana.
Ni sawa na kuweka taa za barabarani chato huku miji mikubwa inayozunguka chato na yenye magari mengi na watu wengi hakuna. Mfano Geita mjini hakuna, katoro hakuna, bukoba hata kakola hakuna unaweka chato .
Ni bora wangeboresha stand za Geita, chato ambazo zinatumiwa na watu wengi na magari mengi kuliko uwanja wa ndege wa 4D, hizo emirates, precision air n.k zinapandwa na watu wangapi kwenda chato kila SKU na kwa kivutio kipi? Huu ni ubinafsi tu hakuna hoja ya maana hapo
 
Mpaka sasa Serikali kupitia Mamlaka ya Viwanja vya ndege Tanzania inamiliki viwanja vya ndege 58(ukijumlisha na Chato itakuwa 59),na wakati Uwanja wa ndege wa KIA ukiwa mikononi mwa Kampuni ya KADCO. TANAPA inamiliki karibu viwanja 26(Vingi vikiwa ni Airstrips),NCAA 2 na viwanja binafsi 93.


Ningependa kujifunza
KIA inamilikiwa na KADCO .....hii ni taasisi gani na code ya uwanja huu ni ngapi

Je viwanja hivi vina code gani na vimepewa code hizo kutokana na kukidhi vigezo gani
Songwe
Arusha
Mtwara
Tanga
Dodoma
Iringa
Mafia
Bukoba
Tabora
Kigoma
Katavi

Na kama kuna vingine vyenye lami please jazia
 
Huna lolote kinachokusumbua ni wivu tu unajifichia kwenye uchumi nani amekwambia wa Mwanza hautajengwa??? utakapojengwa wewe mwenyewe utasema wanajenga tu kanda ya ziwa!!! unataka Kiongozi wa nchi aende kwa baiskeli nyumbani kwake???? mbona hatujakusikia ukihoji barabara zilizojengwa tena siku nyingi na miundo mbinu ya umeme hadi huko polini ambako hata watu wanaenda kwa msimu!!!!
Nyie watu wapi hamuelewi?Hoja ya mleta mada si kukataa kujengwa kwa uwanja huko,ila kiwango cha kiwanja kinachojengwa sambamba na muitikio wa kiuchumi.

Huyu huyu mnamuita mnafiki,mlimsifia wakati analeta habari za bombadia na watu tukawa tuanazipinga!!Sasa leo kawa mnafiki?Hakuna anayekaa kujemgwa huko,lkn je ni ujenzi wa kiwango gani?
 
Yaani centre ya EAC uipeleke Kagera (sijui ulitaka kumaanisha Bukoba) utakuwa na akili wewe?
Wewe ulitaka uipeleke arusha?? Kwa kuzingatia videos vipi. ...au kwanza kwa vigezo vipiii???


Forums ninkati kwa Tanzania. ....je kagera ama bukoba na moshi ipi uko katikati mwa EAC !!!

Natumai utawaza kwa akili
 
Nimesoma mada kwa marefu na mapana yake,bahati mbaya wapo baadhi ya wachangiaji wana viwango vidogo sana vya uchangiaji.Hatuna namna ya kuwaondoa labda mods wangeweza kusaidia.

Mfano mleta mada kaeleza vizuri kwanini ujenzi wa uwanja CHATO ni kukosa mwelekeo,anakuja mtu utadhani kalazimishwa kuchangia "Eti kwani Chato ipo Sudani" mwingine mbona KIA ilipojengwa Bomang'ombe kulikuwa na nini.Unabaki kushangaa na kujiuliza maswali kibao ni jinsi gani shule,college... vimezalisha watu wa hovyo kwa kiwango hiki.Watu hawapendi kushughulisha bongo zao wanasema hovyo hovyo.

Nirejee kwenye mada.

Mosi,Ujenzi wa uwanja wa CHATO ulikuwepo katika mipango tangu mwanzo au uliibuka baada ya Dr Magufuli kuchaguliwa ?.Katika ilani ya CCM ujenzi wa viwanja vya ndege kiwanja cha ndege cha Chato kipo ?.

Pili,Ujenzi wa uwanja wa ndege unaambatana na sababu za kiuchumi,kijamii,kiusalama na nk.Kabla ujenzi haujaanza mambo yote yalingatiwa au tuliamua kwakuwa Rais anatoka eneo hilo,ikiwa ni hivyo maana yake tutakuwa tunafanya maamuzi kwa kuangalia maeneo wanakotoka viongozi na si kuangalia sababu za kiuchumi ?.

Tatu,Suala la kujenga miundombinu based on wanakotoka viongozi si jambo geni Afrika.Ukisoma historia ya kijiji cha Yamoussoukro alichozaliwa kiongozi wa mwanzo wa taifa la Ivory Coast Mh Felix Houphouet Boigny ambacho baadae kiligeuzwa makao makuu ya serekali badala ya Abdjan.Mh Felix Houphouet Boigny alianza na ujenzi wa kanisa kubwa dunia Basillica of our Lady of peace,ujenzi wa uwanja wa ndege wenye uwezo wa kutua ndege aina ya Concord (Afrika wakati huo vilikuwa viwili tu Gbadolite na Yamoussoukro Airport) na majengo ya kisasa kwaajili ya shughuli za kiserekali.Ukienda kule Zaire sasa Congo aliyekuwa Rais wake Marehemu Mobutu Sese Seko Kuku Ngbendu Wa Za Banga hakuishiwa vituko alijenga uwanja wa ndege mkubwa kuliko wowote Afrika wakati huo Gbadolite International Airport,Jumba la starehe na miundombinu ya kisasa kijiji alichozaliwa leo ni mahame kabisa hakuna kinachoendelea kwakuwa wakati wa ujenzi hawakuzingatia masuala ya uchumi,jamii,usalama na nk.

6ac1e86b-e8c1-4fca-9315-6ec69282701c-2060x1236.jpeg




9d5f02a2-ede1-4780-a3ed-4caab3e01c40-2060x1297.jpeg


Control tower ilivyosasa.

32c0ddd8-e5eb-4fa4-b6c0-3805d94c844a-2060x1236.jpeg


6d73d197-4957-470f-a8d8-759750857478-2060x1236.jpeg

c0bbd0b0-921c-429e-890d-9012e63bdd67-2060x1267.jpeg


Baadhi ya majengo yamegeuzwa madarasa.

5bc122d3-6dfb-4be9-9371-ce6cdced7cc0-2060x1297.jpeg


Hotel ya kifahari leo haina wageni hata kiduchu.

15e1b139-0e60-47ee-b399-42e6abd8eb0d-2060x1280.jpeg


Hata Mbuzi hawapatiki.

be82b6c0-d5ec-404a-89db-9ea00f76fbdf-2060x1373.jpeg


Bwawa la kuogelea lilivyo sasa.

846cec32-beba-4019-bfba-d759a5705dba-2060x1236.jpeg


a30f0956-7897-40fc-8669-34d79a0a2bda-2060x1236.jpeg



Ulevi wa madaraka ulivyoteketeza mabilioni ya fedha za walipa kodi katika uwekezaji wa kijinga.
 
Nawashangaa sana wabongo, what economic potentials are you referring and leave away Rubondo game reserve.Mwaka Jana mheshimiwa Raila odinga alitumia sikukuu ya mwaka mpya kwenda kupumzika kama mtalii yeye na familia yake.Lakini jiulize alifikaje huko? Alitumia Helicopita ya kukodi ambayo gharama zake kurudi Tena mana ziko juu. Kibiashara feedback tunapata kutoka kwa customers wetu.Hatuwezi jua feedbacks za wateja zinasemaje.Lakini tu nadhani kuna with kutoka kwa wateja wa high rank like Raila wameshauri uboreshaji. Tumezoea kusikia traditional mbunga za wanyama Kama serengeti, ngorongoro, Lakini Rubondo Nani anajua? Ambako tunaambiwa kuna ndege adimu duniani wako kule huwezi kuwapata popote duniani.Acha cha to internaltional airport ijengwe bana tukaone ndege adimu duniani. Raila kaanza wengine tufuate
 
Chato

Chato town, population = 17,508. Chato district population = 365,000

Economic activitiy = nothing significant apart from subsistence farming which depend on rain. Contributes less than 1 percent to the GDP.
Tourist attractions = none

At the same time Songwe airport, the main airport serving the southern highlands, an area with more than 5 mil people and also being the bread basket of Tanzania doesn't have runway lights till today!

Mwanza airport yenyewe upanuzi wake has been going on at such a slow pace for the past 2 years and at times even stalled!

We are willing to spend billions on someone's vanity project ambayo will generates nothing in return and adds little value, lakini tunaache sehemu where the money would have been better spent.

A small airport would have been fine, lakini sio kujenga an airport with a runway that could almost "rival" JNIA, at a town/district with a population lower than some suburbs in Dar.

Someone needs to look at themself in the mirror and reevaluate the choices they have been making so far.
Mkuu wasiojua wanashangilia lakini project imesimama juzi juzi Makame amepita na kiswahili kingine tumerogwa
 
hahahaaaahaaaaaaaaaaaa hii kweli ni hatari kibwa sana maana watu wanafanya vitu bila kiangalia kesho itakuaje
 
Mkuu,
Rais ana jukumu la kuhakikisha si majirani zake tu bali taifa zima linapata makazi bora, ni jukumu lake kutoa umasikini, Maradhi na Ujinga TANZANIA.

Sasa kwa Kujenga huo uwanja hivyo vitu vitatu Umasikini, Maradhi na Ujinga vitapungua hapo Chato.

Lakini pia angewauliza hao majirani zake sina hakika kama watasema awajengee uwanja wa ndege.
Jukumu lako wacha kulalamika. Pray your part. Uwanja hauna shida mbona wa songwe ulipelekwa polini hakuna aliye seema!!

Infact wa bukoba wanamalizia kulipa fidia ili uhanze kujengwa!! Sijui utakuja na hoja kuwa wajengewe nyumba kwanza!!!
 
Mnaweza kuweka uchambuzi mzuri sana ila ukakosa mashiko kwa kuwa tu una lengo la kiitikadi zaidi.

Mimi huwa najiuliza, je suppose tungechagua huko, kwa bahati mbaya sana umeshindwa kujiendesha wenyewe mkaamua kuturudishia walewale waliokimbia huku baada ya kukatwa je mngeweza kutujengea nchi kweli?, au mngeishia kuandika uchambuzi kama huu wakati mkishuhudia barabara ya Chalinze-Moshi ikiwekwa 4 ways, na kiwanja kama hicho cha chato kikijengwa Hai au Monduli?
Jaribu kupambana na changamoto nje ya vyama na utafanikiwa sana ila kila ukikosolewa tu ni lawama toka chama fulani, kwani wewe huna shida kabisa au mapungufu, kama unayo, nani huwa anakusaidia kukuweka sawa, ni wa chama chako tu au hata wasiojuwa nini maana ya chama.

Maana wenzetu wa upinzani mmekuwa mabingwa ya kuchambua msivyoviweza, mmekuwa wazuri theoretically but you are not practically oriented, mambo yenu mengi yanakwenda kinyume lakini kwa vile kafanya yule, basi you keep quite kama vile hamuoni huku ukisubiri uongee likifanyika upande wa pili.

Kaskazini ilijengeka mapema kwavile watu wa kaskazini walipata fursa, wakakumbuka kwao ili wapate kwenda mapumzikoni kila mwaka, sasa acha fursa zinapopatikana sehemu zingine basi wazitumie fursa hizo, huku mkiwa wavumilivu mkisubiri 2020 ,
 
Wewe ulitaka uipeleke arusha?? Kwa kuzingatia videos vipi. ...au kwanza kwa vigezo vipiii???


Forums ninkati kwa Tanzania. ....je kagera ama bukoba na moshi ipi uko katikati mwa EAC !!!

Natumai utawaza kwa akili
Acha pombe,,, kumbuka EAC ni mpaka bahari YA Hindi huko Sasa chukua eneo lote hilo uone kama centre CYO Arushaa
 
Wacha kubabaisha watu bwana. Unahisi wale wanao kwenda mleba au biharamuro ama geita ama katoro ama kahama watalazimika kutumia mabasi..

Usisemehe mifuko yavwenzio kama Nina hela wenzako wanazo. Na habari ya viwanda na hayo mengine yatakuja.
Wewe ndio mbabaishaji na hujawahi kupanda ndege hata mara moja. Kweli kabisa naenda Kahama nipande ndege kwenda Chato halafu nisafiri toka Chato hadi Kahama nisishukie uwanja wa ndege wa Buzwagi kwa Auric au Shinyanga? Au naenda Muleba nisishukie Bukoba niende Chato. Ndio maana watu wote wenye uelewa wameshauri kama kipaumbele ni uwanja wa ndege kwa ajili ya makabira ya huko kwenu basi uwanja wa kimataifa ungejengwa Omukajunguti na sio Chato. Mimi naifahamu Chato toka miaka ya 90 nimepiga sana madili kule maeneo ya Mwendakulima, Mwabasabi, Munekezi, Nyakayonda, Lubambangwe na tulikuwa tunalala kwenye Guest ya mzee wetu Makufuli enzi hizo na naheshimu raisi kuwa na uwanja wa ndege nyumbani kwake asitumie muda mrefu safarini, lakini sio uwanja wa ndege wa kiwango cha kimataifa kwa kuwa nchi yetu bado maskini haina uwezo wa kujenga viwanja vya kimataifa kila mkoa au wilaya. Bukoba kwenyewe ndege hazijai ndo iwe huko Chato? Nyerere alishawashtukia nyie ni wabinafsi toka siku nyingi
 
Back
Top Bottom