Tetesi: Hatimaye "Chato International Airport" kuzinduliwa rasmi mwezi Aprili

Tetesi: Hatimaye "Chato International Airport" kuzinduliwa rasmi mwezi Aprili

Uwanja umeshajengwa, mvimbe mpasuke mtajijua wenyewe.

Watetea mafisadi na wabaguzi wakubwa nyinyi( malofa)
Ukiyaja kujua ufahami wetu watz ni ea sija gani basi soma mawazo ya huyu mwasita kama siyo mwasaba. haiingii akilini mtu katoa uchambuzi wa kitaalamu nawe baada ya kujibu kitaalamu unajibu kifenengefenenge. taifa ili kuna mambo yanaudhi. mtu anatoa hoja nzuri na si mwanachama wa chama chochote, basi kwa kuwa anampinga mkuu basi huyo utaambiwa si mwanaccm bali mpinzani. akiandika jambo muislam lenye mashiko basi mkiristo anasema huyu lazima ni muislam. akiandika uchambuzi mzuri ka huu na yawezekana mr barafu anatoke chato, utasikia huyu ni wa kasikazini. kama taifa kea style hii hatutafika. uwanja huu hauna manufaa.kutoka bukoba to chato ni zaidi ya km 130, geita ni kama km >100, bihalamulo ni km 100, ngara, >200, kahama 250 nk. ni watu gani watatumia uwanja huu tofauti na mtukufu?
 
Uwanja umeshajengwa, mvimbe mpasuke mtajijua wenyewe.

Watetea mafisadi na wabaguzi wakubwa nyinyi( malofa)
Ukiyaja kujua ufahami wetu watz ni wa aina gani basi soma mawazo ya huyu mwasita kama siyo mwasaba. haiingii akilini mtu katoa uchambuzi wa kitaalamu nawe baada ya kujibu kitaalamu unajibu kifenengefenenge. taifa ili kuna mambo yanaudhi. mtu anatoa hoja nzuri na si mwanachama wa chama chochote, basi kwa kuwa anampinga mkuu basi huyo utaambiwa si mwanaccm bali mpinzani. akiandika jambo muislam lenye mashiko basi mkiristo anasema huyu lazima ni muislam alkadharika kama muandishi ni mkiristo utasikia muislam anasema huyu si mwenzetu. mtu akiandika uchambuzi mzuri ka huu na yawezekana mr barafu anatoke chato, utasikia huyu ni wa kasikazini. kama taifa kwa style hii hatutafika. uwanja huu hauna manufaa. kutoka bukoba to chato ni zaidi ya km 130, geita ni kama km >100, bihalamulo ni km 100, ngara, >200, kahama 250 nk. ni watu gani watatumia uwanja huu tofauti na mtukufu?
 
Kwani bajeti ya huo uwanja ni shilingi ngapi?

I wish I could cry! Kuko wapi kumu enzi Baba wa Taifa Mwl. Nyerere(RIP) kwa Viongozi uchwara wa CCM?
Baba wa Taifa alikaa Ikulu zaidi ya miongo 2! Leo JPM ana mwaka tu tayari anajenga International Airport kwao! This is ridiculous.Baba wa Taifa hakuwahi kufanya ujinga kama huu! Hatuoni Kiwanja CHA NDEGE CHA KIMATAIFA PALE BUTIAMA wala MUSOMA yenyewe!
Je, Magufuli anafikiria nini huko mbele kwa muktadha huu?Je, yawezekana ni dalili ya kuanza kuweka mazingira ya kuitawala Tanzania kwa miaka mingi ijayo kama dikteta?
 
I wish I could cry! Kuko wapi kumu enzi Baba wa Taifa Mwl. Nyerere(RIP) kwa Viongozi uchwara wa CCM?
Baba wa Taifa alikaa Ikulu zaidi ya miongo 2! Leo JPM ana mwaka tu tayari anajenga International Airport kwao! This is ridiculous.Baba wa Taifa hakuwahi kufanya ujinga kama huu! Hatuoni Kiwanja CHA NDEGE CHA KIMATAIFA PALE BUTIAMA wala MUSOMA yenyewe!
Je, Magufuli anafikiria nini huko mbele kwa muktadha huu?Je, yawezekana ni dalili ya kuanza kuweka mazingira ya kuitawala Tanzania kwa miaka mingi ijayo kama dikteta?
***
WAZEE WA CHAMA WANALO JIBU LAKE.....!/
*wafanyaje 2020, kabla jambo halija zua jambo.
 
Hoja hii inatokana na mapungufu ya kutafuta habari kwa kina

Tulijadili sana hapa JF kwaini KIA ilijengwa.
Mpango wa pili wa maendeleo 1964-1969. Tazama sababu za ujenzi wa kiwanja hicho na historia yake
Ni fair point, usiishie hapo tueleze kwa ukubwa unaotarajiwa nini faida za ujenzi wa uwanja huo? Hicho ndicho muhimu kujadili hapa
Tunarudi pale pale, kuwekeza lazima kuwe na sababu.
Hautuwezi kuwekeza kiwanja kikubwa Segera bila sababu.

Hakuna kashfa ya Chato, kinachohojiwa ni sababu nzuri tu ziwe za kiuchumi, kijamii au kiusalama. Tunaomba msaada wa hiloHakuna tatizo kabisa.

Korogwe ilikuwa council wakati wa Mkoloni.
Ni Moja ya Wilaya kongwe katika taifa hili haina Kiwanja.

Tunduru ni Wilaya Kongwe katika Taifa hili, kiwanja chake ni airstrip tu

Hatuhitaji kiwanja nyumbani Bondei- Muheza kwasababu ni saa 1 kutoka Pongwe Tanga

Hatuhitaji Kiwanja Kisarawe kwasababu ni saa 1 kutoka JNIA

Hatuhitaji likiwanja likubwa Mkuranga na Nyamato kwasababu ni saa 1 kufika JNIA

Tunahitaji kuwekeza kwa malengo.

Hatuhitaji uwanja mkubwa Kigoma, tunahitaji Reli ya STG na daraja la maragarasi kwasababu kiuchumi ina maana sana.

Hoja yako kuwa kila Wilaya iwe na kiwanja ni mfu.

Hatuhitaji kiwanja Kibaha na ni ujinga uliotukuka kuwekeza tu likiwanja kwasababu baada ya miaka 20 litakuwa na faida

Ni akili pevu kama fedha hizo zitajenga reli ya Mtwara-Liganga

Hatuhitaji likiwanja likuubwa Wilaya ya Butiama ili watumiaji 6 watumie.

Tunahitaji fedha hizo kujenga reli ya kuunganisha Musoma na Mwanza

Inatosha Ningemuomba JPM na serikali yake wafikirie kuunganisha reli ya kati ifike Musoma

Uwanja wa Musoma ulikuwa kama airstrip wakati huo EA Airways DC ikitua.

Niliona kwa macho yangu wakati mkuu wa mkoa akiwa Kisoki kama si Wasira na Mkurgenzi akiwa Marehemu Khalidi aliyejenga Makondeko.

Ndege ziliposhindwa kutua mkandarasi aliyeweka 'moram' ni P.F.Nyakutonya

Hii Jet ya Rais ilifanyiwa majaribio baada ya uwanja kukamilika.

Mgeni wa kwanza kutua alikuwa Chancellor wa Ujerumani Wilbrandt akimtembelea Nyerere Butiama

Nyerere hakukifiri njia nzuri ni kujenga kiwanja kikubwa.

Mahitaji ya watu wa Mara yalikuwa Daraja la Kirumi lililojengwa na Maulidad & Rose.

Matete yalibomoa kwanza,niliona nikitoka Kinesi, niliogopa boti za Hosea na maji
Tukapita pale Kirumi kwa kivuko ambacho kilikuwa ni hatari

Daraja la Kirumi lilitumika na KAMATA na Tanganyika Bus wakati yanapitia Kenya kwenda Mwanza. Barabara ya kati ilikuwa haipitiki kwa baadhi ya nyakati

Kirumi ni kiungo kizuri hadi sasa kati ya Tanzania na nchi jirani za Kenya na Uganda

Huo ndio uwekezaji wenye tija.

Nyerere angeweza kujenga uwanja Butiama mkubwa tu.

Alifikiria Taifa kwanza na si yeye kama mtu

Hapa niwaalike wakubwa tutete ya enzi Jasusi na JokaKuu
Mleta mada ameongelea umuhimu wa ujenzi wa uwanja wa kuhudumia mbuga ya serengeti. Na akapendekeza uwanja wa mwanza. Na hapo ndipo nimetofautiana naye. Wewe hili unaliongeleaje?

Mleta mada ametia sababu dhaifu ya idadi ya watu kuwa ndiyo hoja yake ya kutojenga kiwanja chato inaposimamia. Ndiyo maana nikamuuliza wakati KIA inajengwa kulikuwa na wakaazi wangapi BOMANG'OMBE.
 
Ili la CHATO on a serious note mwenzenu nimekwazwa maana naangalia faida zake kwa uchumi wa Tz bado naona Nyota.
Anyway naendelea kusoma maoni ya wadau labda mishowe ntakuja kuwa convinced uwepo wa iki kiwanja.
Nakubaliana na wadau kuwa uwanja karibu na Serengeti NP ni jambo la muhimu mno ukizingatia tuko na mabombadia then boing 787 izi mbuga plus Ruaha NP lazima tuzitengnezee mazingira utalii wetu ukue
 
Mkuu barafu. Nikushukuru kwa kuanzisha mada.

Hilo la uwanja kujengwa chato binafsi sioni kwanini usijengwe huko. Labda kama ungeonyesha ni kwanini chato panastahili uwanja mdogo kuliko unaojengwa kuliko sababu ulizotoa.

Hoja yangu inahusu kuboresha uwanja wa Mwanza kuhudumia mbuga ya Serengeti.

Ki mantiki. Sehemu kubwa ya mbuga ya serengeti ipo mkoani mara na si zaidi ya kilometa 110 kwa barabara kutoka makao makuu ya mkoa hadi kuingia mbugani kwa kupitia barabara ya Musoma - Arusha na haifiki kilometa 70 kwa kupitia barabara ya Musoma - Mwanza. Mbuga hii ipo kwenye wilaya za Serengeti Tarime na Bunda. Ambapo Wilaya ya Serengeti inamiliki eneo kubwa zaidi.

Sehemu ndogoya mbuga hii iliyobaki ipo mkoani SIMIYU katika wilaya za Itilima na Bariadi. Mkoa wa mwanza ulikoma kumiliki mbuga hii baada ya kuanzishwa mkoa wa simiyu.

Mipango ya kujenga kiwanja cha ndege kuhudumia mbuga ya serengeti ni ya muda mrefu ambapo awali ilikuwa uwanja mkubwa wa kisasa ujengwe Musoma au Bunda ili kuhudumia mbuga hii. Na uwanja mdogo wa Mugumu uboreshwe. Eneo la uwanja lilibainishwa na juzi kati enzi za Utawala wa Kikwete lilipimwa upya. Mpango huu uliambatana na kuboresha air strip ya mugumu iwe na viwango vya sasa vya uwanja kama wa Arusha na pia kujenga barabara kutoka Musoma hadi Arusha.

Utekelezaji wake unapigwa figisu hadi leo ambapo hakuna kiwanja. Air strip wala barabara iliyojengwa. Sababu mojawapo ni hoja zilizotolewa na wana kaskazini kwamba bora kuijenga KIA ili ihudumie mbuga zote zilizoko kaskazini mwa nchi.

Uwanja wa KIA UKAJENGWA. Na tagu wakati huo mbuga ya serengeti ikajulikana kwamba ipo arusha kama ambavyo tunaambiwa mlima kilimanjaro upo nchini Kenya. Mkoa wa mara ukakosa mapato ya utalii kwa maana ya viingilio vya wageni mbugani na uwekezaji wa miundombinu kama taasisi za utalii mfano hoteli, vyuo majengi ya taasisi za umma nk. na miundombinu hii kwa wingi imeendelea kujengwa Arusha tangu wakati huo,na kuhalalisha mkoa wa arusha kumiliki mbuga ya Serengeti.

Awamu ya pili ya kujenga uwanja mkoani mara ni huo uwanja wa Serengeti ulioutaja kwenye andiko lako.

Hii ilikuwa zaidi inachochewa na maombi kutika kwa mwekezaji aliyewekeza pale Gurumeti.

Kama ulivyogusia. Uwanja huu pia haukujengwa kutokana na figisu za wanaharakati wa ndani na nje ya nchi. Ambapo jamaa zetu wa kaskazini waliungana na Wakanya kukwamisha ujenzi.

Hivyo badala ya kupugia debe uwanja wa Mwanza kuhudumia serengeti ungesema ukweli kwamba uwanja wa kuihudumia mbuga hii ujengwe ndani au karibu na mbuga hii. Nani ya mkoa wa mara au wa sumiyu.

Lengo hapa ni kuonyesha uhalisia. Sote tunakubali uwanja wa ndege wa mwanza unahitajika na ulitakiwa uwepo kabla ya ule wa KIA.

Suala la kuhudumia mbuga ya serengeti ama kutokea KIA au uwanja wa ndege wa Mwanza hakuta tofauti kubwa maana bado usafiri wa magari wenye kuchukua muda mrefu njiani utatumika.

Tuseme tu kwamba lazima kuwe na uwanja wa ndege wa kisasa unaokidhi mahitaji ya sasa na baadae NDANI YA MKOA WA MARA au MKOA WA SIMIYU ili kuihudumia hii mbuga.

Wenzetu wa-kenya wanajenga viwanja vya ndege vikubwa vilivyi katika umbali usiokuwa mkubwa ilimradi kuna sababu. Mfano angalia umbali wa viwanja vya Nairobi Kia na Taveta. Pia Nairobi Nakuuru Masai Mara na Kisumu. Au hapa Tanzania kuna Kia Arusha na Moshi.

Basi ni halali kujenga na kuboresha viwanja vya Mwanza Kigoma Simiyu Tabora Singida Shinyanga Chato Bukoba na MUSOMA kwa ukubwa tofauti kulingana na vigezo vya kiuchumi kijamii na kijiografia.

Msisitizo ni kwamba mbuga ya serengeti italeta faida kwa taifa hili kama serikali watanzania wote na wakazi wa mikoa ya Mara na Simiyu wataona umuhimu wa kuwekeza kwenye miundombinu ya kuihudumia mbuga hiyo. Kama maji barabara hoteli uwanja wa ndege nk. ndani ya mikoa husika.
Kwa taarifa tu mkuu, kuboreshwa kwa Uwanja wa Mwanza lilikuwa wazo miaka ya 80 wakati waziri wa maliasili na utalii akiwa Jetrude Mongela- Wakaskazini wote ndani ya utumishi wa serkali na Umma wakaupinga na kuhakikisha kuwa Mongela anaongolewa wizarani hapo na KIA ikajengwa badala yake. Sasa leo hao hao wa KASKAZINI wanakuja na oho CHATO huu ni muendelezo wa siasa za kuchafuana, uchanguzi wa 2015, na maandalizi ya uchaguzi wa 2020. Kutesa kwa zamu- wacha kanda ya ziwa nao watese- na wanahasira na KASKAZINI
 
Hivyo badala ya kupugia debe uwanja wa Mwanza kuhudumia serengeti ungesema ukweli kwamba uwanja wa kuihudumia mbuga hii ujengwe ndani au karibu na mbuga hii. Nani ya mkoa wa mara au wa sumiyu.

Lengo hapa ni kuonyesha uhalisia. Sote tunakubali uwanja wa ndege wa mwanza unahitajika na ulitakiwa uwepo kabla ya ule wa KIA.

Kipigi,

Naungana na wewe.

Pist yake kwangu imekosa mantiki pale aliposema uwanja wa chato usijengwe ili kuboresha wa mwanza wakati anatambua kwamba

1. Maboresho ya uwanja wa mwanza yanaendelea hadi sasa na ujenzi wa uwanja wa chato hauja athiri maboresho ya uwanja wa mwanza.
Ndugu yangu Eudorite,
Hivi barafu anaupigia chapuo Uwanja wa Mwanza au alichosema ni kwamba, ikiwa hapakuwa na namna ya kujenga Serengeti basi option ingekuwa ni kujenga Mwanza badala ya Chato! Sehemu ya thread yake ni hii:
Kwa mahesabu hayo,kama ujenzi wa Uwanja wa ndege Serengeti ulishindikana,basi Uwanja wa ndege wa Mwanza ndio suluhisho la haraka ktk kuwafikisha watalii kwa urahisi ktk mbuga hiyo.Tukiusahau uwanja huo na kutazama zaidi ule wa Chato, tunaweza kuhoji dhamira hii ya maendeleo ktk kufika uchumi wa kati. Na kuhoji kwetu kusiababishe "hasira" kwa wenye mamlaka, bali ichukuliwe ni kama changamoto za raia kwa serikali yao.
Ingawaje umeleta habari za ukanda; nitangulie kusema kwamba, binafsi sina maslahi yoyote ama iwe na Kanda ya Kaskazini ambayo hamuishi kuisemanga na wala kanda ya Ziwa!

But on top of that, sina hata maslahi kwenye siasa za upinzani haidhuru hata kama wengine wanaweza kuona hivyo kwavile huwa napinga mambo mengi. Hata hizo Bombadier ambazo ndugu yangu barafu anaziunga mkono; mimi nimeanza kuzipinga since Day 1 na nitaendelea kuzipinga japo kwa sasa! Na si hivyo tu, nilianza kupinga ununuzi wa ndege tangia enzi za JK!!!!

Lakini pamoja na yote hayo, barafu yupo sahihi kwa 100%.

Kama umemsoma vizuri best option kwake ni Serengeti and not Mwanza!

Lakini ikiwa hapana namna ya kujenga Uwanja wa Serengeti, basi best option kwa sasa ni Mwanza kwa sababu ndio shortest economical distance to Serengeti lakini sio Chato unless kama unataka kutuambia ni rahisi zaidi kufika Serengenti kutokea Chato kuliko kutokea Mwanza!

That's one but second, hata kama ingekuwa ni rahisi zaidi kufika Serengeti kutokea Chato kuliko Mwanza; bado hiyo peke yake haiwezi kuwa decisive criteria ya kufikia maamuzi ya kuchagua Chato badala ya Mwanza!

Moja ya mambo ambayo wachumi watahoji; is Chato economically viable compared to Mwanza? Kwamba, fine... ni rahisi Watalii kutokea Chato kuliko Mwanza... ni hilo tu?! Watalii wana msimu wake... je, wakati wa offseason uwanja utaendelea kutumika?!

Hapo nimejaribu kuupendelea Uwanja wa Chato kwamba utakuwa unahudumia watalii (you know it's impractical) lakini pamoja na yote hayo, bado tunaona hatari ya kuwa underutilized wakati wa offseason.

Ukweli huo hapo juu ndio unajibu hoja yako kwamba huoni ni kwanini Uwanja usijengwe Chato! Sababu ni moja tu, Chato hawana uchumi wa ku-utilize international airport throughout the year! As of now, Chato Airport haiwezi kuendeshwa economically... NO WAY!

I hate to say this but ukweli ni kwamba, ingawaje Chato Airport is too big even to kule kwetu Mafia; lakini ni bora Mafia ungeweza kutumika throughout the year hata kama ungetumiwa na ndege ndogo compared to Chato!!
 
Tutakifanya kiwe ni kiwanja pekee kwa kusafirisha organic food zote, mboga za majani, maua holtculture kwa ujumla na minofu ya samaki yote iendayo abroad. Na mambo mengine yote ya kuingizia taifa pesa
 
Ni kweli Mlau balafu anakosea sana! Tena sana! Ata Nyerere alijenga Butiama International Airport(BIA), Mh. Alhaj Mwinyi alijenga Pemba International Airport, mh. Mkapa naye alijenga Newala International Airport(NIA), Mh. Jakaya naye alijenga Msoga International Airport.
Sawa bwana lakini Musoma tuna uwanja mzuri tu.nimekusoma tu.
 
Najiuliza kwanini tumekataa majina yetu tukakubali ya wazungu na waarabu
 
Back
Top Bottom