"RAIS SAMIA AMEVUNJA REKODI YA MIAKA 20 SEKTA YA MAJI, AMEOKOA TRILIONI 3 AMBAZO ZINGETUMIKA KUTIBU MAGONJWA YATOKANAYO NA UKOSEFU WA MAJI."
Aliyekuwa Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe David Kafulila amesema Rais Samia Suluhu Hassan amevunja rekodi ya utekelezaji wa bajeti ya maji ya miaka ishirini mfululizo iliyopita,
Mhe David Kafulila anasema, wakati nakuja Simiyu baada ya kuaminiwa na Rais Samia Suluhu Hassan nilikuta kero kubwa kuliko zote kwa Mkoa wa Simiyu ni " Maji "
Leo Mwaka mmoja huu niliokaa hapa tumeshirikiana kusimamia mabilioni ya fedha za miradi ya maji ninyi nyote mtakuwa mashahidi wangu,
Leo naondoka Mkoa Simiyu wote tunaona tatizo la maji limepungua sana hapa lazima tumshukuru Sana na kumpongeza Rais Samia Suluhu Hassan,
Simiyu upatikanaji wa maji safi na salama kwa mwaka 2020/21 nilikuta ni asilimia 56% leo tumefikia asilimia 73% na hii ni kufikia Juni 2022 lazima wana Simiyu kumshukuru Sana Rais Samia Suluhu Hassan,
Lakini Rais Samia huyu huyu tayari ametuletea mradi mkubwa wa bomba la kilometa 190 kutoka ziwa victoria wenye thamani ya Shilingi billioni 400.
Ndugu zangu Wanasimiyu mradi huu utapita zaidi ya vijiji vyenu 200 ambao kazi za awali nadhani mnaona zimeanza,Asanteni Sana kwa ushirikiano wenu huu mkubwa,
Kafulila anaendelea kusema, Niwambie ukweli, Nimesoma bajeti za miradi ya maji za miaka 20 mfululizo kuanzia ile ya mwaka 2000 mpaka ya mwaka 2020,
Nataka niwaambie kwa miaka yote hii hakuna mwaka ambao fedha za miradi ya maji zilitolewa hata kwa asilimia 80%.
Lazima mfahamu,Bajeti ya kwanza tu ya awamu ya sita( 2021/22) fedha za miradi ya maji zilizotolewa ni billioni 743 sawa na asilimia 95% ya bajeti iliyopitishwa na bunge na hii ni ndani ya miezi 9 tu Sio mwaka.
Huu ni ushahidi mwingine kuwa Rais wetu anatekeleza kauli mbiu yake ya kumtua ndoo mama kichwani kwa vitendo.
Rais Samia anaelewa kuwa maji ni uchumi, maji ni ustaarabu, maji ni afya... Maji ni Uhai,
Mtakumbuka,Ripoti ya shirika la Afya duniani mwaka 2014 ilionesha kuwa kwenye kila dola moja inayowekezwa kwenye maji, inaokoa dola 4.2 ambazo zingetumika kutibu magonjwa yanayotokana na ukosefu wa maji safi na salama( UN- News, Nov19, 2014).
Hivyo hivyo billioni 743 za miradi ya maji katika mwaka mmoja wa Rais Samia wa 2021/22 ni sawa na kusema Rais wetu kaokoa Shilingi trilioni 3.1 ambazo zingetumika kutibu magonjwa yatokanayo na ukosefu wa maji.
Kafulila anaendelea kusema, Labda niwakumbushe tu kwamba utafiti uliofanywa na taasisi ya SYNOVATE mwaka 2008 ulionesha kuwa kero namba moja kwa mtazania ni maji.
Msiojua,SYNOVATE ni taasisi 5 kwa sayansi ya uratibu wa maoni duniani wakati huo kabla haijachukulia na IPSOS ambayo kwa sasa ni moja ya taasisi 3 kubwa duniani kwa kazi hiyo(OPINION SURVEY).
Mkuu huyu wa mkoa anasema, Hiki ni kielelezo kuwa Kiongozi anaetatua tatizo la maji anagusa maisha ya watanzania walio wengi na hasa vijijini ambao inawezekana hawana kelele nyingi kwenye mitandao..wanaitwa ' silent majority'..Hivyo tunaposema Mama anaupiga mwingi sio sisi ni takwimu za kitafiti.
Hivyo tuendelee kuwasaidia wananchi kwa kuhakikisha wakandarasi wanatekeleza mikataba na tuendelee kuvunja mikataba ya wababaishaji kama tulivyofanya siku zote kuhakikisha kuwa fedha anazoleta Mhe.Rais kukabili kero ya maji zinafanya kazi kwelikweli,
Hayo yamesemwa na aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Simiyu Mhe David Kafulila leo wakati wa makabidhiano ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kati yake na Mkuu wa Mkoa Mpya Dr Yahaya Mawanda ambapo mbali ya kueleza sura ya Mkoa wa Simiyu, Kafulila ameleza pia maamuzi 9 ya kimkakati aliyotekeleza ndani ya mwaka mmoja na mwezi 1 wa Utumishi wake katika nafasi ya hiyo ya Mkuu wa Mkoa huo wa Simiyu