Hatimaye dawa ya Kenya kukwamisha Maendeleo Tanzania imepatikana rasmi!

Hatimaye dawa ya Kenya kukwamisha Maendeleo Tanzania imepatikana rasmi!

Lord denning

JF-Expert Member
Joined
Jun 3, 2015
Posts
15,819
Reaction score
33,255
Tangu Awamu wa 1 Kenya alijitanabaisha kama Silent enemy wa Tanzania na hii lilisababishwa na tofauti za kiitikadi/kiuchumi baina ya Mataifa haya mawili

Ugomvi wa Kenya na Tanzania ulianza mara tu baada ya Tanzania kutangaza kufuata mrengo wa kijamaa hapo mwaka 1967 na kilichofuata baada ya hapo ni vita vya ujasusi baina ya mataifa haya 2

Katika vita hii, Kenya waziwazi aliunga mkono watu waliokuwa either wanataka Tanzania isitawalike au waliokuwa wakizipinga serikali za Chama cha Mapinduzi.

Mfano tu:

Mwaka 1967 Kenya walitumika kumtorosha mpinzani wa 1 wa Nyerere aliyejitoa kwenye serikali Ndugu Oscar Kambona. Kambona baada ya kutofautiana na Nyerere alikimbilia Uingereza kupitia Nairobi

Mwaka 1981 Kenya walimtorosha aliyeongoza kikundi cha wanajeshi waliotaka kumpindua Mwl Nyerere ndugu Khatib Ghand

Kenya pia ilitumika kama njia ya kuwatorosha marubani walioteka ndege ya Tanzania kumlazimisha Nyerere kung'atuka

Baada ya Nyerere kuondoka na Kenya kutawala uchumi wa Afrika Mashariki , Kenya ilibadili mbinu za kuidhoofisha Tanzania na kuhamia kwenye mbinu za kudhoofisha mipango yote ya maendeleo ambayo inaweza kuifanya Tanzania ikawapiku kiuchumi

Njia kuu aliyotumia Kenya kudhoofisha mipango ya Maendeleo ya Tanzania ni siasa maana aligundua mambo yote ya kimandeleo ya Tanzania yanaamuliwa kisiasa

Kupitia siasa , Kenya alifanikiwa kudhoofisha miradi ifuatayo ya Tanzania na baada ya miradi iyo kukwama Tanzania akaenda kuifanya kwake

1. Ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo
Njia kuu aliyotumia Kenya kukwamisha mradi huu ni kueneza propaganda kuwa Bagamoyo anauziwa mchina. Hoja hii ilifanya mradi huu ukakwama Tanzania na hatimaye Kenya akatengeneza Bandari kama hiyo Lamu tena kwa kupitiq mchina huyo huyo

2. Mradi wa Satellite City, Kigamboni

Kenya alijua kigamboni ikifanikiwa basi ndo itakuwa Dubai ya kwanza Afrika Mashariki na akatumia propaganda kuwa George Bush amenunua kigamboni na siasa ile ikasabisha Tanzania tushindwe kuwa nchi ya 1 ukanda huu kuwa na satellite city. Sasa Kenya ndo imekuwa ya 1 baada ya kuanzisha mradi wa Konza City

Sasa ugonjwa huu umepatiwa Dawa:
Kiukweli maraisi takribani 5 wa Tanzania kutokana na kuendekeza kuwa populist walishindwa kujinasua kutoka kwenye mbinu hizi za Kenya. Ni Samia Suluhu Hassan aliyejaribu na napenda kusema anaenda kufanikiwa kwa kuzishinda propaganda za Kenya kwenye hili suala la Loliondo/ Ngorongoro

Ni ukweli usiopingika kuwa sasa Kenya anahangaika usiku kucha ili aimalize sekta ya utalii ya Tanzania ambayo kiuhalisia ndo tishio kubwa zaidi kwa uhai wake kiuchumi ambao unategemea hasa kiutalii

Ndoto kubwa ya Kenya ni kuua uti wa Mgongo wa utalii wa Tanzania ambayo ni kaskazini mwa Tanzania. Ukiongelea kaskazini wa Tanzania unaongelea Loliondo, Ngorongoro, Serengeti na kilimanjaro bila kusahau Manyara.

Njia pekee anayotegemea Kenya kufanikisha hili ni kuhakikisha siasa inatumika ipasavyo ili shughuli za kibinadamu zisikome kwenye mbuga hizi maana kwenye shughuli za kibinadamu mnyama hakai na pasipo na mnyama basi mtalii hawezi kuja.

Katika suala la Ngorongoro/ Loliondo, Kenya kaja na propaganda ya kisiasa kuwa eneo lote lile anapewa mwekezaji hivyo Wamasai hawatakiwi kuwepo

Propaganda hii kusema kweli imefeli vibaya sana na kwa mara ya kwanza chini ya Rais Samia tumeona propaganda za Kenya zikishindwa na Serikali ikitekeleza wajibu wake kwa Maslahi mapana ya Taifa

Hongera Samia! Huo ndo mwendo wa kwenda, Kenya wametuchelewesha sana!
 
Kiongozi pekee wa Tanzania aliyewahi kuwashinda wakenya mpaka wenyewe wakasanda ni John Pombe Joseph Magufuli.. Yule bwana aliwapelekesha wakenya mpaka wakaanza kumuimba kwao Huko.. Japo naye aliwezwa kisawasawa na kagame
Magufuli alipambana nao ila alitumia sana nguvu kuliko akili
 
Japo ulichoandika kina ukweli, ila subiri wanaharakati koko na wale wamasai uchwara kutoka Kenya waje wawatetee mabwanyenye wao hapa jukwaani bila aibu.
Hoja yake ya msingi (mpambano wa kiuchumi) ni ya msingi, lakini vikorombwezo alivyotumia kuijenga hiyo hoja vingi ni porojo na mambo ya kufikirika tu.
 
Maadui wa mama wooote watapinga,
Kumbe wanajimaliza wenyewe
Hongera samua suluhu,
Najua utakuwa umeupdate mbinu za magu, safi sana,
Wakenya na wazungu si watu wazuri
 
Barabara ni moja unawezaje kusema aliyejenga kandokando mwa barabara hiyo ndiye amehusika kumtorosha mualifu?
 
Katika suala la Ngorongoro/ Loliondo, Kenya kaja na propaganda ya kisiasa kuwa eneo lote lile anapewa mwekezaji hivyo Wamasai hawatakiwi kuwepo

Propaganda hii kusema kweli imefeli vibaya sana na kwa mara ya kwanza chini ya Rais Samia tumeona propaganda za Kenya zikishindwa na Serikali ikitekeleza wajibu wake kwa Maslahi mapana ya Taifa
Pamoja na kukubaliana nawe katika mambo kadhaa, hasa jambo la msingi kwamba Kenya na Tanzania ni wapinzani katika maswala ya uchumi, lakini 'propaganda' zako ni nyepesi mno, hata pengine zaidi ya hao waKenya.

Samia hajafanya lolote la maana katika kupambana na mbinu za Kenya, na kama ataendelea hivi hivi hadi 2025, atakuwa ameachwa nyuma sana, na Tanzania itakuwa tegemezi mkubwa kwa Kenya katika mambo mengi, ukiondoa swala la chakula pekee basi!
Kama huna kumbukumbu za enzi za Kikwete, Kenya walivyokuwa wakizoa hapa, basi subiri hujaona kitu enzi za Samia.

Kuhusu swala la Loliondo na Ngorongoro uliloweka hapo juu, wewe unapiga 'propaganda' za kishamba zaidi juu ya swala hilo.
 
Mnawasingizia wakenya kila kitu sijui mna matatizo gani.

Hivi mradi wa bandari ya Bagamoyo aliyeukwamisha ni serikali ya Kenya, au viongozi wetu wasiokuwa na vipaumbele kila anayeingia ikulu anakuja na lake?

Na pesa za kukamilisha huo mradi zilikuwepo? uliwahi hata kuona mkataba wa makubaliano kati ya serikali ya Tanzania na China kuhusu huo mradi?

Chawa, hiyo ni propaganda yako ya kwanza.

Unazungumzia tena mradi wa Satellite City wa Kigamboni kwamba Kenya ndie aliyeukwamisha, hapa napo unapeleka lawama zako pasipostahili.

Ukweli ni ule ule, sababu ya kukwama kwa huo mradi ni uongozi wa nchi usiokuwa na vipaumbele, kila mmoja anakuja na lake, kama ambavyo sasa Samia ameacha Nyerere Dam ameenda kwenye LNG, taifa lisilo na vision.

Kuhusu suala la Loliondo/Ngorongoro ulilozungumzia na kusema Samia anaenda kulishinda, bado hujatuambia anaenda kulishinda vipi?

Kama kulishinda kwako ni kule kuwapiga na kuwaumiza wamasai, au kuandaa filamu ya kuwasafirisha kwa malori na mifugo yao kwenda Handeni ambayo hatuoni muendelezo wake, au kuandaa wale "masela" na kuwavika mashuka ya kimasai waende "kulia" nje ya ubalozi wa Kenya, basi huku sio kulishinda, ni kushindwa, ila chawa huwezi kuona hili.
 
Kiongozi pekee wa Tanzania aliyewahi kuwashinda wakenya mpaka wenyewe wakasanda ni John Pombe Joseph Magufuli.. Yule bwana aliwapelekesha wakenya mpaka wakaanza kumuimba kwao Huko.. Japo naye aliwezwa kisawasawa na kagame
kagame hajawahi kumweza jpm,kajiulize kwanini msibani hakufika ilikuwaje??

na vipikuhusu mzozo wa vipimo vya covid 19 kwa madereva
 
Kumbe humu kuna wakenya wengii,
Dawa yao ni kuwaukraine tu,
Tanzania kwanza,
Tumeshtukia mbinu chafu za Kenya
 
Hoja yake ya msingi (mpambano wa kiuchumi) ni ya msingi, lakini vikorombwezo alivyotumia kuijenga hiyo hoja vingi ni porojo na mambo ya kufikirika tu.
Kama wewe ni mtoto wa juzi huwezi elewa mada nzito za namna hii! Nenda jukwaa la mapenzi na mahusiano tu
 
Mnawasingizia wakenya kila kitu sijui mna matatizo gani.

Hivi mradi wa bandari ya Bagamoyo aliyeukwamisha ni serikali ya Kenya, au viongozi wetu wasiokuwa na vipaumbele kila anayeingia ikulu anakuja na lake?

Na pesa za kukamilisha huo mradi zilikuwepo? uliwahi hata kuona mkataba wa makubaliano kati ya serikali ya Tanzania na China kuhusu huo mradi?

Chawa, hiyo ni propaganda yako ya kwanza.

Unazungumzia tena mradi wa Satellite City wa Kigamboni kwamba Kenya ndie aliyeukwamisha, hapa napo unapeleka lawama zako pasipostahili.

Ukweli ni ule ule, sababu ya kukwama kwa huo mradi ni uongozi wa nchi usiokuwa na vipaumbele, kila mmoja anakuja na lake, kama ambavyo sasa Samia ameacha Nyerere Dam ameenda kwenye LNG, taifa lisilo na vision.

Kuhusu suala la Loliondo/Ngorongoro ulilozungumzia na kusema Samia anaenda kulishinda, bado hujatuambia anaenda kulishinda vipi?

Kama kulishinda kwako ni kule kuwapiga na kuwaumiza wamasai, au kuandaa filamu ya kuwasafirisha kwa malori na mifugo yao kwenda Handeni ambayo hatuoni muendelezo wake, au kuandaa wale "masela" na kuwavika mashuka ya kimasai waende "kulia" nje ya ubalozi wa Kenya, basi huku sio kulishinda, ni kushindwa, ila chawa huwezi kuona hili.
Mnaendeleaje hapo Nairobi?

Umewai kuona mkataba wa mradi gani uliofanyika hapa Tanzania? Umewahi kuhoji?

Unataka muendelezo gani kwa Wamasai kuhamia Tanga wakati unaishi Nairobi? Fuata taratibu za kisheria, toka huko Nairobi, vuka mpaka then nenda Msomera Tanga uone kama kuna muendelezo au hakuna?
 
Aliyewashinda wakenya ni magufuli alikuwa hataki ujamaa nao wa kipumbavu na hata wao waliogopa kudili na magufuli kijinga
Nadhani humjui Samia! Magufuli aliwapa show ya wazi wazi , Samia anawapa show ya kimya kimya

Juzi tu Samia kapeleka balozi kumwakilisha kwenye kikao kilichoitishwa na Mwenyekiti wa EAC Uhuru Kenyata. Ile ni meseji moja kubwa sana!
 
Back
Top Bottom