Hatimaye Gerald Hando aaga rasmi kambi ya Ukapela

Zamani mtu ukivuta jiko au kuoa.....unaheshimika sana mbele ya jamiii.......na kuwa mfano wa kuigwa kwa vijana wenzako......

Kutokana na ndoa kugeuka kuwa magereza ya mateso.....na vifungo vya dhiki.....kijana kuoa imekuwa habari ya kushangaza sana na pengine kukuonea huruma.....

Wakati wao wanakushangaa.....na wewe unawashangaaa.....
 
Hongera kwake mana kuna umri ukifika bado hujaoa lazima ujiulize mara 2 na kama mama/baba yako yupo hai ugomvi wa kukuhimiza uoe hautakuwa ukiisha
 
Ukiingia hapa JamiiForums unaweza ukahisi hakuna mahusiano mazuri ya kimapenzi. Wachache waliopatwa na majanga kwenye mahusiano wanataka kutuaminisha wote kuwa mahusiano ni kitu kibaya.

Wanaofurahia mahusiano yao wangesema waje huku kusifia pasingetosha humu ni vile wapo busy ku-Socialize na wapenzi wao.

Don't get twisted, love is a beautiful thing.
 
Hongera kwake mana kuna umri ukifika bado hujaoa lazima ujiulize mara 2 na kama mama/baba yako yupo hai ugomvi wa kukuhimiza uoe hautakuwa ukiisha
Si mama angu wala baba angu amewahi kuniuliza achilia mbali kunihimiza kuoa! Sana sana walimshangaa mdogo wangu kutaka kuoa wakati bado kalikuwa kavulana ka miaka 24 tu!!

Long Live Bachelors Community... hatutaki shida na mtu!
 
Ulichoandika hapa ni sawa na kumkaribisha Mgeni chai isiyo na sukari alafu unamwambia 'sukari ipo tele kule jikoni lakini sijakuwekea' sasa sijui kama wewe ndio Mgeni hapo utamuuliza nini huyo Mwenyeji wako.

Kama wapo wengi wanaofurahia basi ngoja tuendelee kuwasubiri waje kutoa ushuhuda.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…