Hatimaye Klabu ya Yanga imefutiwa marufuku ya kusajili

Hatimaye Klabu ya Yanga imefutiwa marufuku ya kusajili

Tate Mkuu

JF-Expert Member
Joined
Jan 24, 2019
Posts
33,092
Reaction score
96,127
Kwa mashabiki, wanachama, na wadau wote wa michezo kwa ujumla! Habari ndiyo hiyo.
TFF na FIFA kwa pamoja wameifuta ile marufuku yao ya kuizuia klabu ya Yanga kufanya usajili.

Na hii ni baada ya mchezaji Lazarus Kambole kumalizana kwa amani na Wanajangwani.

Rai yangu kwa Yanga;
1. Timu ya wanasheria wa klabu iweke mazingira mazuri ya mikataba na wachezaji/makocha wanao ajiriwa na klabu, ili kuzuia migogoro na matukio kama haya kuendelea kujirudia mara kwa mara. Maana inaiharibia klabu ile taswira yake nzuri iliyojijengea ndani ya hii miaka michache iliyopita.

2. Uongozi/kamati ya usajili/ benchi la ufundi, nk. Wajiridhishe ipasavyo kabla ya kuwasajili wachezaji kama Lazarus Kambole, Gael Bigirimana, nk. Ili kuondokana na hasara zinazoweza kuzuilika.
 
Sisi hatuna haja ya kusajili
Guede peke yake anaweza kuwanyoosha Makolo msimu ujao muhimu apewe beki mzuri
Yule Guede wako bado ananiweka katika wakati mgumu sana. Simuoni kama ni mchezaji mwenye unyumbulifu eti. Namuona kama ni mchezaji wa kupenda kuletewa tu, na kufunga.
 
Yule Guede wako bado ananiweka katika wakati mgumu sana. Simuoni kama ni mchezaji mwenye unyumbulifu eti. Namuona kama ni mchezaji wa kupenda kuletewa tu, na kufunga.
Ataendelea kuwepo Yanga, atakiwasha sawasawa subiri msimu ujao uone..!🤸
 
Ataendelea kuwepo Yanga, atakiwasha sawasawa subiri msimu ujao uone..!🤸
Binafsi namuombea heri. Maana akikiwasha, atasababisha uwe na furaha. Na hiki ndicho kitu nikipendacho kutoka kwako. Uwe tu na furaha.
 
Back
Top Bottom