Hatimaye Mungu amebatilisha Ushindi wa kulazimisha baada ya mechi kuchezwa dakika 108

Hatimaye Mungu amebatilisha Ushindi wa kulazimisha baada ya mechi kuchezwa dakika 108

1 - 1
FG wameonewa sana leo. Yaani hadi utoaji wa kadi ya njano na nyekundu kwa mkupua wa refa, alionyesha ana hasira,kana kwamba nimeshakula nusu ya hela za watu halafu wasishinde? asimamishwe na kuchunguzwa. Kama alikula kitu na box afungiwe. Marefa wa Tz ni vituko vitupu.
Yani refa ana hasira mpaka katoa kadi3 🤣🤣
HApo hapo mpaka dakika ya 100 hawa wasiwasi yuko kwenye box la Fountain anaendeleza mpira
 
🤣🤣🤣🤣 Zile kadi alizinyofoa kwa gadhabu kali mno
Refa mjinga sana akapimwe akili. Huwexi kuonyesga kadi mbili kwa wakati mmoja kwa mikono yote miwili.

Yote ni hasira ya kuhakikisha aweze kufanikisha apate 9 mil. iliyobakia.

-421684119.jpg
 
Jamani mpira ni burudani tu.

Na wala kushinda sio lazima.

Hata akina PSG au Liverpool huko ng'ambo hawashindi kila siku.

Kwa hiyo Simba na Yanga Pokeeni meseji hiyo.

Nimejionea leo uhusika wa MUNGU dhidi ya dhulma.

Lile kosa la kibinadamu la chasambi lililopelekea Fountain kupata goli halikuja bure...

Ile Ilikuwa ni reaction ya Mungu dhidi ya uonevu wa muda mrefu kwa timu ndogo ambao umekithiri mno kwny ligi ya Tanzania.

Kumlaumu Chasambi ni kumuonea.

Kwa alichofanya Mwamuzi, bila uhusika wa MUNGU, Fountain Gate angefungwa kivyovyote vile.

Baada ya kuona mbinu zinataka kushindikana akampa red card golikipa huku akijua wazi kwamba Fountain tayari wamemaliza kutumia sub zote...Hivyo watalazimika kutumia mchezaji wa ndani ili iwe rahisi Simba kupata goli.

Soma Pia: Full Time: Fountain Gates FC 1-1 Simba SC | NBC Premier League | Kwaraa Stadium, Babati | 06-02-2025

Bado ikawa ngumu, akaona aongeze dakika 4 zaidi baada ya kuisha zile 9.
Jumla mchezo umechezwa dakika 108.....ukijumlisha 45+5 kwa kipindi cha kwanza na 45+13 kipindi cha pili.

Kwa ufupi tu Mchezo wa leo umetawaliwa na uonevu sana

Hata lile goli la kuongoza, lilikuwa la kihuni. Fikiria scenario hiyo ingefanywa na Fountain Gate, goli lingekubalika?

Ushauri wangu kwa vilabu wahanga ni kwamba;
Kwa kuwa TFF imeshindwa kutatua hili tatizo..Ni dhahiri hizi rushwa kwa Waamuzi zina baraka ya TFF.

Wakutane wajaribu kutikisa kiberiti,

Watoe tamko kali la kususia kuendelea na michezo ya Ligi...mpaka TFF itakapo-wahakikishia kuwa mambo haya hayajirudii.

Hapo wakakuwa wamekomesha.

Bila kuja na shocking decision, TFF haiwezi kuogopa.
Shida ya watu wanaojifanya wanamjua Mungu sana,, ukishakua hvo lazima uwe shida kwa jamii
 
Back
Top Bottom