Dakika tano zilizopita nimefanikiwa kupata dataz za ukweli 100% kuwa kweli Balali, amefariki napenda kutoa pole kwa ndugu,
According to the dataz amefia Winsconsin State, katika Hospitali moja kwenye kitongoji cha mji wa Madison,
Na the more dataz ni kwamba kabla hajafa, alikuwa na masaa kama 24 ya siri kwa mazungumzo na Mbunge Mkono.......,
Mazishi ni kesho DC, nitarudi baadaye kwa dataz zaidi!
Ahsante Wakuu, na Mods Mnaeza kuiunganisha hii ikiisha expire!
pengine maiti imeharibika sura jee! alaa mnataka mpaka mjue kalishwa sumu gani!
Habari za Balali ni utata tupu. Inawezekana kweli kafa na inawezekana wakawa wamefake kifo hiki. Yote yanawezekana. Leo hii bado utata juu ya kifo cha Hitler uko palepale. Sababu kubwa ya utata huu ni serikali hii hii kutokuwa straight kwenye issue hii. Nashangaa kwamba kwanza imechukua siku nyingi kutangaza kifo cha mtu mashuhuri kama huyu nchini mwetu. Lakini ni mara ya pili nasikia maziko ya mtu mashuhuri ambaye nimeamini siku zote ni mtizedi yanafanyika nje ya nchi bila sababu ya msingi. Mara ya kwanza alikuwa ni yule mtanzania wa asia aliwahi kuwa waziri katika awamu ya kwanza aliitwa Jamal nadhani kama sijapoteza kumbukumbu. Yeye alipostaafu tunaambiwa alikwend kuishi na bintiye Canada na akafia huko. Hadi leo siamini kwamba alikwenda kuishi na bintiye bali alifanya kama wafanyavyo hao ndugu zetu wanaoitwa watanzania wa asia ambao leo yuko Tz lakini akili na mipango yake iko kuishi milele Canada au Us au UK. Sasa naona na huyu habari zake zinachanganya. Mara alikuwa raia wa Us ohhhh mara ni Mtz basi hali ndivyo inavyotuchanganya. Lakini swali ambalo halijanitoka kichwani mwangu ni je, nchini hapa tunaajili watu wasio raia katika posts nyeti kama hizo kweli? Si siku moja tutamuajili hata rais au waziri mkuu au waziri wa utawala bora au waziri wa mambo ya ndani asiye raia? hapa ndio tuanelekea uelekeo upi? Ebu wote tujiulize hili!!!
Jamani BALALI HAJAFA
Check this out....
Baada ya kupata habari kuwa makachero wameingia US kumsaka Balali, wakajua kuwa hawana ujanja, jamaa angekamatwa tuu, njia pekee na ya mwisho iliobaki plus kusolve hii issue once and for all ni kufake death (jamaa hela anayo kufanikisha hilo ni kazi ndogo sana)
Tarehe za kifo kila mtu anatoa yake plus eti ndugu walichelewa kutoa taarifa ya kifo sbb ilikuwa inasubiri serikali iseme... iseme nini???
huku home hakuna dalili yeyote ya msiba nyumbani kwake...si jambo la kawaida kwetu waafrika
Maiti ya balali haita ruhusiwa kutazamwa/kuagwa
hii Info ya kifo mpaka kila mtu kaipata, imeoriginate form ANNA MUGANDA, of all the ppl...... ANNA MUGANDA simuamini hata kidogo yeye ni mweizi mwingine huyu, mtuhumiwa mwingine aliekula hela zetu
Ushauri, baada ya hayo "maziko" hao makachero waliotumwa mumfata BAlali, sasa wambebe huyo ANNA MUGANDA, kuja kujibu ili kujua aje kujibu nini rejea tanzania mafioso PDF
Wabongo bana...yana hata kifo cha mtu kinakuwa na utata....jamani mtu akifa si kafa tu? Utata unatokea wapi sasa? Ingekuwa utata upo kwa jinsi alivyokufa hapo ningeelewa.....aaaahhh...Ndivyo Tulivyo bana....
Re: Hatimaye Nime-Confirm Kuwa Balali Amefariki!(HAPANA UKWELI HAPA)
--------------------------------------------------------------------------------
Sisi ngozi nyeusi tuna matatizo sana.
Hivi hamjiulizi hata maswali kwa nini akimbilie kuzikwa nchi za watu wengine tena eti na sikia kwa kuchomwa moto!
Turudi nyuma kidogo kwenye mali ya uma (EPA) walisema wakidhibitishwa wezi (mafisadi ) walioiba watachukuliwa hatua ikiwa pamoja na kufikishwa mahakamani sasa tangu Fedha zirudishwe sijasikia mtu aliyepandishwa mahakamani mpaka dakika hii alafu tena walivyokosa haya wanatangaza kuwa Fedha za EPA zimerudishwa BOT.
Na hisi huyu Mh. Kisura naye anajifunga kwa kuruhusu watu kutangazia uma mambo kama hayo wakati hayana ukweli wowote.
Namkumbuka sana Baba wa taifa alisema Mtoto mdogo ukimpa uhuru utakula asara sasa Chama tawara wamejiachia sana kiasi kwamba wanaumbuana wenyewe kwa wenyewe sometimes nasema bora kafa ili uma utambue ufisadi mkubwa unaofanywa na Chama (Kioo cha jamii)
Sikatai wote sisi ni mafisadi wadogo lkn hata Mzazi anapomwona mtoto anadokoa anamkomesha na anaacha, wabishi ndio wanaoendelea na sisi tunahaki ya kuwafundisha tukiwa kama Wazazi au Kioo kwao sisi ni binadamu sio malaika na ili ufanikishe lazima ukubari kuambiwa ukweli ndio utarekebishika.
Kweli siamini kuwa Bilali amefariki kwa sababu Fedha ni kisima Jeuri, so anaweza akatumia Fedha kubadilisha SURA, JINA , (Akajibadilisha ) alafu sisi huku tukatangaziwa kuwa Amefariki dunia ilimladi tu kupoteza ushahidi.
Kweli nitaamini tu pale nitakapoiona maiti yake kwa macho yangu na nitakwenda kwa gharama yoyote mkoani kwake Iringa kumwaga ndio nitaamini kuwa Balali amefariki Kweli kweli.
Samahani wapenzi kwa kuwa rudisha nyuma lakini ni lazima muwe na Msimamo.
Mkuu,
Kama huna data za Jamal basi uliza. Huyo mtu alikuwa mzalendo wa TZ, akalitumikia taifa, baadaye akatelekezwa kama akina Apiyo.
Ndugu zake wakaamua kumchukua na kwenda kuishi naye Canada. Alipofariki wakaona azikwe huko huko ili angalau waendelee kulihudumia kaburi lake.
Pia kuna mama yule secretary wa mwalimu, baada ya elimu yake ya maana Oxford, akaacha uongozi kwenye Labour party kuja kumsaidia mwalimu. Alipozeeka ikabidi arudi UK kuja kufaidi matunda ya NHS maana vinginevyo TZ angeshindwa hata kulipia huduma bora ya afya.
Je utawalinganisha watu kama hao na Balali?[/QU
ASANTE KWA KUNIPA MWANGA HUU. KWA KWELI HUWEZI KUWALINGANISHA. HAWA WALIKUWA WATUMISHI WALIOTUKUKA. LAKINI BADO SIKUBALIANI NA KUAJIRI WATU WASIO RAIA KATIKA POST NYETI KAMA YA UGAVANA KATIKA KARNE HII TULIYONAYO. SIKUBALI NA SINTAKUBALI
Mkuu ES,
Tumekusikia ila naona wengine macho yetu sasa mpaka yameziba kabisa maana michanga tunayorushiwa imezidi kiasi.
Sasa kama jamaa alikuwa na afya njema, je imekuwaje akafa ghafla? Je kajinyonga? Mtu wa Iringa huyo, huwa hawakawii kujitundika.
Sasa Fisadi kweli atamwachia data fisadi?
Nafikiri Ballali alikuwa ni hatari kwa muungwana kuliko Mkapa, maana waliofanya aumbuke ni akina JK na wala sio Mkapa.