Hatimaye Nime-Confirm Kuwa Balali Amefariki!

Hatimaye Nime-Confirm Kuwa Balali Amefariki!

Status
Not open for further replies.
Quote:- Kuhani

I mean huyu mtu kasema jana kwamba kwenye State ya Massachusetts unaweza kupata info za mgonjwa kwenye internet. Watu wanaishi Marekani hapa miaka enda rudi halafu kweli mtu anatamka kitu kama hicho unaendelea kum grant credibility? Such informational and analytical travesty? I mean you would think JF is predominantly of tech-savvy, socially conscious and informed members watakao google vitu kabla kuvibugia, hata kama you have no concept of 'patient confidentiality' norms, which are almost unbreakable everywhere in America.

Quote:- Internet

Senator Kenenedy, cancer diagnosis/Brain cancer, admitted at Mass. General Hospital in Boston. Out of the the hospital, his doctors are weighing Chemotherapy and Radiation Treatments. No futher annoucemment.

source: Mass. General Hospital, Boston Massachusetts State.

Ndiyo faida ya kujifanya kujua sana, ukweli ni kwamba huwa hujui kitu sasa ni vyema ukaomba uelimishwe maana hii ni aibuuuuuu kwa mtu mzima! Ahadi yetu ni ile ile kumkoma nyani giladi mpaka kieleweke hapa!
 
field now nimejua why ur strong!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
keep it up men ukiona tunakupinga sehemu nyingine hiyo ni mawazo ya mtu kwahili tuko nyuma yako tumwagie data ,mkuu
 
Mkuu Kada,

Sio kwamba ninakuogopa, isipokuwa nimeamua kuwa sina sababu ya ku-go against you kwa sababu ninakujua mno, kwa hiyo ndio maana ninakupa nafasi ya kusema unavyotaka, lakini sitakujibu mkuu,
!

ES,
where do you get the nortion that mtu akikwambia otherwise na unavyofikiribasi anakuogopa/pingana na wewe ? hata kama mtu yupo against na wewe, isnt that why we are here ? Usiseme kwamba you cant go against na mimi kwa sababu unanijua mno (angalau ni kweli) lakini naona kama unajilimit yourself unapochukua uamuzi kama huo ! Ebu ichukulie tupo kwenye siasa, wewe waziri mkuu mimi waziri wa kawaida, nafanya ushenzi then wewe kama waziri mkuu ukae kimya kisa unanijua sana ? dont you think you might be doing the wrong thing by thinking you are doing the right thing ? AU KUSAHIHISHWA WEWE HUPENDI ??
Anyway nilichokuwa nasema ni kwamba info za kwenye net sio PRIVATE na ndio maana ziko kwenye net, ila pia vile vile kuna nyingine ambazo ni private lakini means of obtaining hizo info ni illegal !
 
Slaa: Tume ichunguze kifo cha Daudi Ballali




na Mwandishi Wetu



KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, amependekeza kuundwa kwa tume huru ya kimataifa itakayochunguza mazingira ya kifo cha Gavana wa zamani wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Daudi Ballali.

Akizungumza na Tanzania Daima kwa njia ya simu jana, Dk. Slaa ambaye ni Mbunge wa Karatu, alisema umuhimu wa kuundwa kwa tume hiyo unatokana na utata uliozingira habari zote zinazomhusu Ballali tangu alipoondoka hapa nchini Agosti mwaka jana.

Dk. Slaa, mwanasiasa aliyeibua tuhuma kadhaa dhidi ya Ballali, na mmoja wa wanasiasa waliokuwa mstari wa mbele kutaka kurejeshwa nchini, ili aje kujibu tuhuma mbalimbali zilizokuwa zikimkabili, ikiwa ni pamoja na kusaidia uchunguzi wa wizi katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) ndani ya BoT, alisema kifo chake kabla ya kukamilika kwa suala hilo, ni pigo kubwa.

‘‘Tunaiomba serikali iunde tume ya kimataifa ili ukweli ujulikane. Huyu ni mtu mkubwa, ana siri nyingi za taifa. Anahusishwa na ufisadi. Hatuwezi tukaliacha suala hili likaachwa hivi hivi tu.

‘‘Kama serikali imeficha ugonjwa, hospitali na hata hicho kifo ambacho taarifa zake zimepatikana baada ya siku nne, tunataka tume huru iundwe ihusishe majaji na watu wenye heshima katika jamii ya kimataifa,” alisema Slaa.

Mwanasiasa huyo ambaye ndiye aliyesoma orodha ya mafisadi mwaka jana na kuibua mwamko wa kipekee katika vita dhidi ya rushwa na ufisadi, alirejea kauli aliyopata kuisema siku zilizopita kuhusu Ballali na umuhimu wake wa kumrejesha hapa nchini wakati akiwa hai.

‘‘Nilipata kusema huko nyuma, na leo narejea tena kulisema hili kwamba, iwapo Ballali atakufa kabla ya hajarejeshwa nchini kujibu tuhuma za ufisadi ndani ya BoT na hata kabla hajahojiwa na Kamati ya Mwanasheria Mkuu inayochunguza kashfa ya EPA, basi damu yake itakuwa juu ya serikali,” alisema Slaa.

Alisema mwenendo mzima wa namna serikali na Rais Jakaya Kikwete walivyolishughulikia suala zima la Ballali, kuanzia kuondoka kwake kwenda nje kwa matibabu, kulazwa na baadaye kufa, ni jambo linalotia shaka na kuibua maswali mengi.

Mwanasiasa huyo alisema anaamini haiwezekani Ballali, ambaye ugavana wake ulitenguliwa na si kufukuzwa, aende nje kwa matibabu na alazwe pasipo serikali kupitia Ofisi ya Ubalozi wa Tanzania Marekani, kujua mahali aliko.

Alisema anaamini kwamba gharama zote za matibabu ya Ballali zilibebwa na serikali, kwani hata baada ya uteuzi wake wa ugavana kutenguliwa, aliendelea kubakia kuwa mtumishi wa serikali.

‘‘Hiki kiini macho cha serikali kudai eti hawajui alikokuwa amelazwa na anakoishi Ballali, ni ushahidi wa wazi kwamba serikali ilikuwa inaficha jambo.

‘‘Walikuwa wakijua aliko, na walifanya hivyo wakijua kwamba iwapo angerejea angeweza kutoa siri kwa kuwataja wahusika wengi, na hivyo kuleta mtikisiko mkubwa serikalini,” alisema Dk. Slaa.

Aliilaumu serikali kwa kutoa taarifa nyingi zinazokinzana kila mara waandishi wa habari walipokuwa wakifanya juhudi kubwa katika kufuatilia alikokuwa gavana huyo wa zamani wa BoT.

Alisema uamuzi wa serikali kukaa kimya kwa muda mrefu pasipo kutoa taarifa hata baada ya Ballali kufa, ni ushahidi mwingine wa namna ilivyokuwa ikishikwa na kigugumizi kuhusu suala hilo.

‘‘Ninachosema hapa ni kwamba, wakati serikali inapotoa majibu yenye utata na yenye kupingana, haijawahi kusimama na kusema aliyeondoka ni mtu wetu, Mtanzania mwenzetu. Ni kwa nini serikali ilikuwa haifuatilii? Kwa nini ubalozi haukufuatilia? Unaweza kuona namna serikali inavyojaribu kuficha jambo,” alisema Dk. Slaa.

Alisema ni jambo la ajabu kwamba, maofisa wa ubalozi wamekuwa wakifuatilia kwa karibu kila mara Watanzania wanapokwenda India kwa matibabu ya moyo, tena kwa watu wa kawaida kabisa na hivyo kuzua maswali ni kwa nini kwa Ballali hali ilikuwa ni tofauti.

Kama hiyo haitoshi, Dk. Slaa alieleza kushangazwa na kifo cha Ballali ambacho kimetokea siku chache tu baada ya kuwapo kwa taarifa za makachero kutumwa kumfuatilia nchini Marekani.

‘‘Ni jambo lisiloeleweka sawa sawa na linalopaswa kutolewa maelezo. Haiwezekani tunasikia makachero wamekwenda kumfuata na siku chache baadaye kupitia katika mtandao tunaambiwa amefariki na kisha siku chache baadaye inatangazwa rasmi amekufa. Nini kimemuua? Serikali itujibu,” alisema. Alisema huko nyuma na hata katika mtandao kulikuwa na taarifa za mtu huyo kuwekewa sumu, jambo ambalo serikali pamoja na kutakiwa kulitolea ufafanuzi ilikaa kimya.

Alieleza kushangazwa kwake pia na hatua ya Kamati ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali inayochunguza Kashfa ya EPA, kuwahoji watuhumiwa wengine na wamiliki wa kampuni 22, huku ikimuacha shahidi muhimu Ballali, katika muda wote wa miezi karibu mitano ya kazi yao.

‘‘Ni kwa nini wanahojiwa akina Jeetu Patel na wengine wa makampuni 22, na hawa watu hawakuteremka BoT kama Roho Mtakatifu. Ninaamini Ballali angekuwapo angeeleza siri hizo,” alisema Dk. Slaa.
 
Mimi naona Bwana Slaa atulize boli maana atapata stroke bure kutegemea Serikali kuchunguza kifo cha Balali. Serikali ijajua mengi ambayo sisi watoto wa serikali hatujui. Ukimya huu unaonyesha mengi tumuachie Mungu.Naamini atanyoosha mkono wake siku moja na ukweli utapatikana.
 
Wazola Slaa ni zuri kusema iundwe tume.
Kwa kuwa tume watatoa ripoti kwa niaba ya wananchi ambo wana dukuduku na utata.Inawezekana watu wana taarifa zingine ambazo mimi na wewe hatujui,na ikiwepo tume kila mwenye kitu ataenda atahojiwa na kutoa maelezo.
Hili la kuunda tume nalo hatuwezi hadi tumwachie Mungu?No
 
Local detectives in US hunt for Ballali

-Fresh interest in ex-BoT governor as EPA probe deadline approaches

THISDAY REPORTER
Dar es Salaam

A TEAM of local investigators is currently in the United States attempting to trace the whereabouts of former Bank of Tanzania governor Daudi Ballali, as part of ongoing investigations into the theft of over 133bn/- from the central bank's external payment arrears (EPA) account, it has been revealed.

Well-placed sources say at least seven detectives are combing Washington DC, the US capital, and Boston in a bid to locate the ex-BoT governor a central figure in the EPA investigation who has surprisingly not been officially questioned by authorities thus far.

''There is a team of Tanzanian investigators in the US right now, apparently trying to locate Ballali. It isn't clear if their orders are to arrest him or just question him,'' said a source familiar with the investigation.

''The clock is certainly ticking for the EPA probe team to wrap up its work, and there have already been suggestions that the AG (Mwanyika) will ask the president for an extension of about two months to finish the job,'' the source added.

Kwa wale wote mnaolilia credibility, ninasema hivi hapo mmegonga mwamba kabisa, ingawa sikupenda kusema wazi mambo yetu huko nyuma lakini kwa sababu credibility yetu imekuwa kwenye attack kwa sababu tu ya basketballer, sasa tuwakumbushe tu kuwa as far as dataz huwa hatuna limit tuko all over the nation,

Kwenu Kuhani na wenzako, hapo juu ni mfano mmojawapo, I mean ngoma ni nzito sana hii tena iko full, sasa nilitaka tu kuweka wazi kuwa kwa dataz tu hatuishii hapa tu JF, ila tupo national na dataz zetu zinakubalika hata national, lakini tuna commitment kubwa na nzito hapa JF, ndio maana tunaendelea kuziwkea hapa tena bure! Na wiki hii kuna kazi nyingi sana tumezifanya behind the scene na zitaanza kuonekana very soon!

Na pia we are so credible kiasi cha kwamba tuna-offer ya kujiunga na kambi moja kati ya mbili, zinajojitayarisha na urais wa 2015 tunaendelea kupiga mahesabu kabla ya kuamua moja wapo tutakayojiunga nayo! Na hii ni kutokana na credibility yetu hapa JF, na huko kwenye national level ambako tupo pia!

Anyways, nilitaka kuliweka sawa hili la sisi na credibility, nafikiri mwenye macho haambiwi ona! Kwa wale mnaotushambulia na kuhangaika huko behind the scene kujaribu kuharibu majina yetu tunasema ni kazi ya bure, kwanza hamtujui na ngoma ni nzito mno hiii!

Isipokuwa Mkuu Kuhani,

Ninaomba nikushukuru kwa one thing muhimu sana, between the last three days, umenisaidia sana kuwajua wanafiki hapa ndani, hilo ninakushukuru sana, otherwise I am looking forward na your challenge on my dataz, maana I love it!
 
Isipokuwa Mkuu Kuhani,

Ninaomba nikushukuru kwa one thing muhimu sana, between the last three days, umenisaidia sana kuwajua wanafiki hapa ndani, hilo ninakushukuru sana, otherwise I am looking forward na your challenge on my dataz, maana I love it!

Yes Indeed, huo ndio uungwana
 
1.

Nimesema kuwa Balali, nimethibitisha kuwa amefariki DC, tena nyumbani kwake Jumapili, usiku na amezikwa leo kwenye makaburi ya Heavens Of Peace kule DC, kwenye hili nyinyi mnasemaje?

Sasa Mkuu FMES,
Hapo nilipo-bold utaona kuwa hizo dataz haziko makini, sasa mtu aki-point out au kuswalisha issues kama hizo kwenye posting zako haina maana kuwa anakuonea wivu au anakutafuta ugomvi la hasha, ni katika kuwekana sawa tu.
Mfano, ninavyojua mimi, alifariki nyumbani kwake Bethesda, MD (siyo DC per se) na kuzikwa kwenye makaburi ya Gate of Heaven(as opposed to makaburi ya Heaven of Peace) kule Silver Spring, MD.

Ni hivyo tu. Tuendelee kumkoma nyani(siyo Ngabu lakini!) 🙂
 
1.
where do you get the nortion that mtu akikwambia otherwise na unavyofikiribasi anakuogopa/pingana na wewe ? hata kama mtu yupo against na wewe, isnt that why we are here ? Usiseme kwamba you cant go against na mimi kwa sababu unanijua mno (angalau ni kweli) lakini naona kama unajilimit yourself unapochukua uamuzi kama huo !

Mkuu Kada,

Heshima yako, hii ni moja ya misimamo yangu sio hapa tu, bali hata in the real life, huwa kuna watu ninaamua tu kuwa sipendi kuwagusa, hata wanitukane kiasi gani, na huwa ni kwa sababu ya kuwajua kuliko wanavyofikiri, ndio maana nimesema kuwa siwezi kwenda against you kwa sababu zangu za binafsi, kwa sababu forum ni one thing, lakini at the end of the day sisi bado ni bin-adam, ndio maana knowing you as I do nimeamua not go against you, nafikiri kwenye ishu kama hizi hata wana-forum huwa wananilelewa, kwa sababu wakiniuliza in private ninaweza kusema ni kwa nini, kwa hiyo mkuu ninarudia ninajisikia mzito sana kwenda against you, huko nyuma niliwahi ksuema the same kuwa siwezi kwenda against Freeman, kwa sababu ninamjua mno kwa hiyo mkuu hii yako sio mara ya kwanza!

2.
Ebu ichukulie tupo kwenye siasa, wewe waziri mkuu mimi waziri wa kawaida, nafanya ushenzi then wewe kama waziri mkuu ukae kimya kisa unanijua sana ? dont you think you might be doing the wrong thing by thinking you are doing the right thing ?

Mtu ninayemfahamu kwa karibu kama wewe siwezi kumpa uwaizri mimi nikiwa waziri mkuu, siwezi period no mjadala on this one, ninasema siwezi!

3.
AU KUSAHIHISHWA WEWE HUPENDI ??

Sina tatizo na kusahihishwa, Mwanakijiji amenisahihisha kuhusu Winsconsin, mimi dataz nilizopewa ni kwamba marehemu, alifia Winsconsin State, kumbe ni somewhere in DC lakini ni Winsconsin Street, wala sikubisha wala kumjibu kwa kejeli, ni kwa sababu amenisahihisha bila ugomvi, wala kejeli, au matusi tone ilikuwa ya kistaarabu na amenihakikishia kuwa ana ukweli zaidi ya nilionao kwenye hilo neno, hakuna ubishi wala matsi wala ugomvi,

Tatizo la wengine ni kwamba kwanza hawana ukweli wa wanachojaribu kunisahihisha, halafu habari niliyoitoa ni ndefu na kubwa, wao watalilia one small thing kwenye ile habari ambacho hakina umuhimu wowote na ile habari, ili tu waonekane wamenishihisha, halafu in the end wakiulizwa ukweli walionao kuhusu ile habari hawana hata moja, that I have a big problem with that, ukunisahihisha kistaarabu nitakujbu kistaarabu, ila ukija na matusi au kejeli, nafikiri you know me better on that kuwa sina tatizo kuongea lugha yoyote!

4.
Anyway nilichokuwa nasema ni kwamba info za kwenye net sio PRIVATE na ndio maana ziko kwenye net, ila pia vile vile kuna nyingine ambazo ni private lakini means of obtaining hizo info ni illegal !

Kwenye hili msimamo wangu unaeleweka na nimeuweka very clear, nilisema hivi wakati ninatafuta habari za Balali kuwepo Boston, niliwa-touch washikaji wangu wengi sana huko ambako pia niliwahi kuishi kule Cambridge, Boston miezi kama mitatu hivi na kuna mshikaji wangu mmoja huko in the 90s, kwa hiyo huko Boston sio kwamba mimi ni mgeni, sasa kama unaishi huko wewe unamjua Sir Alex, mkulu wa CUF mzee wa Real Estate ambaye niliwahi kuwa naye melini ni mshikaji wangu damu damu kwa hiyo sio kwamba nilikuwa ninajaribu kum-mislead anybody hapa, hapana huko Boston nina marafiki wengi sana wenye nafasi nzito kama kina T, na wasiokuwa na nafasi nzito kimaisha pia,

Niliweza kuthibitishiwa kuwa Balali hakuwahi kuwepo huko na moja ya sababu nilizopewa ni kwamba huko kulazwa hospital sio a private matter kisheria, unaweza kutafuta jina la hospitali na ukapata habari mgonjwa wako yupo wapi, lakini sikusema kuwa unaweza kujua habari za ugonjwa wa yule mtu kwenye internent kama ilivyokuja kugeuzwa na wenye akili hapa JF,

Na hapo juu nimethibitisha hilo kwa kuweka habari za mtu aliyelazwa hivi karibuni ambazo zipo kwenye internent, hayo yako mengine sikuyasema na wala siyajui, ila nilichosema ni kuwa habari za mgonjwa kuwepo Hospitali gani sio private matter, sasa nimeshambuliwa weee na mpaka kuuuliziwa credibility yangu kwa kitu ambacho nimekuthibitishia kuwa I was right na ukweli uko hapo juu unajisema wenyewe,

Otherwise, sina mpango wa kuwataja majina watu wa Boston, kama ni mkulu wa Springfield, nimeongea naye juzi tu kabla hajaondoka, kwa hiyo mkuu we are everywhere na hatuna noma na ukweli, lakini kuchafuliana majina kwa kutumia uongo sio vizuri, na huwa hatukurupuki na dataz au nfo, no huwa tumetulia sana,

Anyways heshima mbele mkuu, tuendelee kukata ishus!
 
1
. Hapo nilipo-bold utaona kuwa hizo dataz haziko makini, sasa mtu aki-point out au kuswalisha issues kama hizo kwenye posting zako haina maana kuwa anakuonea wivu au anakutafuta ugomvi la hasha, ni katika kuwekana sawa tu.

Mkuu kama nia yako kweli nikusahihisha, wewe ni kuweka ukweli wala hata huna haja ya kunitaja jina, ila ukija kusahihisha na matusi na kejeli then tutavina tu hakuna noma!

2.
Mfano, ninavyojua mimi, alifariki nyumbani kwake Bethesda, MD (siyo DC per se) na kuzikwa kwenye makaburi ya Gate of Heaven(as opposed to makaburi ya Heaven of Peace) kule Silver Spring, MD.

Kuhusu DC na Maryland, Baltimore hilo siwezi kukubishia, sikujui huko na siwezi kutenganisha kati ya hiyo miji, lakini kama Bethesta nilishasema siku nyingi sana wakati ndio kwanza hii habari za Balali zimeanza tu, anyways masahihisho yako ni kwamba anazikwa Gate of Haven na mimi nilisema kule nyuma kuwa ni Heaven of Peace, lakini ni huko huko Silver Spring, ambako na mimi nilisema toka majuzi sasa tatizo liko wapi mkuu?

Kwa hiyo masahihiso yako hapa ni hio jina tu, sina tatizo na hilo na pia hailiiifanyia habari yangu kuwa uongo kwa sababu nimekosea jina au nimechanaganya miji ambayo ipo karibu sana, sasa kulikuwa na shida gani kwako kusema ukweli na kuendelea, sasa mbona kuna wanaosema kuwa hajafa sasa unawajibu vipi na huu ukweli wako?

Sasa mkuu naomba uwajibu wanaosema kuwa hajafa kama kweli una ubavu kama ulivyokitokeza hapo juu!
 
hapa nilichogundua kuna watu wanajua baadhi ya vitu lakini wamekaa kimya tu . mtu kama FMES anapofanya juhudi ili kutupasha habari wao wamekaa kimya tu wanangoja kukosoa,
FMES endelea na juhudi kutupasha habari mkuu kadri ya vile utakapozipata na kuridhika kwamba kwa kiasi zilivyo zinafaa kutumegea,katika ishu kama hii ya msiba wa Balali, logic bila dataz ni sawa na maji mtoni, utayabebaje bila kibebeo?.
 
FMES Mkuu,

Hii ni kama vile kumlazimisha mgonjwa anywe dawa, ni kwanini hatuwekei hata picha ya mazishi? tunajua Balali kafa mbona unatumia nguvu sana mzee kuwalazimisha watu wakuelewe? sisi sote twajua Balali kafa,mzee wetu acha apumzike,
 
hapa nilichogundua kuna watu wanajua baadhi ya vitu lakini wamekaa kimya tu . mtu kama FMES anapofanya juhudi ili kutupasha habari wao wamekaa kimya tu wanangoja kukosoa FMES endelea na juhudi kutupasha habari mkuu kadri ya vile utakapozipata na kuridhika kwamba kwa kiasi zilivyo zinafaa kutumegea,katika ishu kama hii ya msiba wa Balali, logic bila dataz ni sawa na maji mtoni, utayabebaje bila kibebeo?.

Mkuu Wangu Gamba, Heshima mbele,

1. unajua hii tabia ya kushambulia tuu bila ukweli huwa inawatisha sana watu hapa wasiokuwa na ubavu kama wangu na kusihia kunyamaza hata kama wana ukweli,

2. Lakini tuna tatizo moja kubwa sana ambalo mkuu hujaliona , nalo ni watu kutumia majina mengi, hili linatumika kwa sababu tu ya chuki za binafsi na wivu, na kwa bahati nzuri sana huwa ninawajua karibu wote wenye hiyo tabia na mimi ndio maana huwa sina msalie nao, wewe yatizame vizuri maandishi ya Mwakilishi, hapo juu, halafu uniambie eti yeye sio one of the people ambao wamekuwa wakinishambulia kwenye hii topic, sasa sio kwamba sijamuelewa hapana nimeshamshitukia tayari, na siku zote watu wa namna hii hapa JF wenye chuki na wivu ndio tabia zao hizi!

3. I can understand, mtu ananikosoa kwa kuweka ukweli ambao ni 100% tofauti na wangu, kwa mfano ningeelewa mtu ajitokeze hapa na kusema kuwa :-

1. Balali alikuwa amelazwa Hospitali X kule Boston, kwa hiyo ES uko wrong kuwa hakulazwa kule!

2. au Balali amekufa hospitali Y kwa hiyo ES uko wrong hakufia nyumbani,

3. and then Balali amefia Carlifornia na atazikwa New Mexico,

4. Chenge hakuenda UK nimemuona jana mahali X,

I mean should this happen, ni kweli my credibility itakuwa on line, na believe me nitaishia kujiangalia upya na kufikiria tena kama ninataka tena kuendelea na this game, lakini kama ni serious challenge ya dataz zangu bado sijaiona kabisaa hapa zaidi ya chuki na wivu tu na uzandiki na unafiki wa hali ya juu sana tena kutoka hata kwa baadhi ya watu niliotaka kuwaamini, kumbe ni wale wale wamevaa ngozi ya kondooo,

Mkuu nina njia nyingi sana za kupata dataz na leo ninataka kujaribu kuweka hii ishu clear kwa sababu ni wakati muafaka kulisema hili, kwanza dataz tunazoziweka hapa JF sio hata 10% ya dataz zote tulizonano kwenye area mbali mbali za taifa letu, nyingi tunashindwa kwa sababu ziko rough, too raw au hazielezeki, kwa mfano kuna dataz moja niliwahi kupewa jinsi kiongozi mmoja wetu mashuhuri alivyo na tabia ya kuwapumulia migongoni viongozi wadogo huko mikoani na kwenye idara za serikali yetu, halafu unakuja hapa JF unakuta watu wanamfagilia kuwa anafaa sana na ni bomba sana, sasa tunaishia kubaki na dataz zetu maana utaisemaje hiyo hapa?

Kuna dataz unapewa na mfagiaji somewhere can you imagine hiyo dataz itakuwaje? Lakini one thing ni kwamba in the end ina ukweli flani, lakini hata ujaribu vipi ni too raw au rough! Halafu nyingi tunajaribu kuzigeuza ili angalau ziweze kuwahifadhi waliotupa, kwa mfano hizi za juzi za Balali, yaani ninaogopa hata kuziweka hapa kwa kuogopa kumuweka wazi aliyenipa ambaye aliniomba sana tena sana kwamba nisiziweke anywhere,

Lakini sisemi kuwa ndio iwe sababu ya watu kutokosoa dataz zangu, mimi nitashukuru sana iwapo mtu atakuja na kuzisahihisha with strong datz zaidi yake maana ndio hasa nia ya kuelimishana, lakini so far a serious challenge zaidi tu ya maneno ya chuki, uzandiki, unafiki na majungu tu, na sio mara ya kwanza ninaona haya, kuna mtu mmoja alikuja hapa huko nyuma na matusi mengi sana kwangu kuwa ninasema uongo, lakini huyo huyo tena anakuja kwenye PM na kukubali kuwa ninasema ukweli, ila anajaribu kuweka challenge tu in the end mkulu akaniomba nimfanyie mpango na yeye awe anaandika na kulipwa na CCM kama mimi maana ameambiwa kuwa mimi ninalipwa kila post na ccm, halafu huyu mtu akaanza kuwashawishi watu wengi sana hapa kuwa ana ukweli, lakini baadaye akakimbia hajarudi tena hapa!

Kwa hiyo mkuu wangu Gamba, kwanza ninashukuru kwa uelewa wako mkubwa sana on ishus hapa, na always fair na serious sijaona unandika ujinga ujinga na usiwe na hofu, mimi nitaendelea kumwaga dataz hapa zinazowezekana na wala sina wasi wasi kabisaa na wasiokuwa na dataz wanaojaribu kulilia logic ni haki yao, lakini dawa ni ukweli tu na sio anything else, wembe wangu ni ule ule, na sasa urais unakaribia kugombewa mengi yameanza kujitokeza lakini tayari tupo on the top of our game, kwa wanotaka matsu na kejeli huwa hatuna tatizo na hilo hata siku moja, na wanaotaka ustaarabu pia tuko tayari kwa ustaraabu!

na kama nilivyosema ni kwamba sasa tuko national level as far as dataz is concerning, kwa hiyo ndugu zangu tuendelee kukata ishus maana taifa liko njia panda
 
Hii ni kama vile kumlazimisha mgonjwa anywe dawa, ni kwanini hatuwekei hata picha ya mazishi? tunajua Balali kafa mbona unatumia nguvu sana mzee kuwalazimisha watu wakuelewe? sisi sote twajua Balali kafa,mzee wetu acha apumzike,

Mkuu wangu naomba niseme hivi, hawa wafiwa ni watu wangu wa karibu sana, now point yako siielewi kwamba eti ninawalazimisha kukubali kuwa amekufa, hapana sijamlazimisha mtu hapa mimi nimeweka ninayoyaamini vipi na wewe ukiweka unayoyaamini, vipi tayari umebadili jina mkuu? kwi!kwi!kwi!

Hapana mkuu sikulazimisha anything unless wewe mwenyewe unajilazimisha sijatumia nguvu ila ninajibu mapigo kwa nguvu zangu zote kwa sababu wewe na wenzako kwenye credibility mmeshindwa nafiki ndio maana una jazba mkuu walahi unanichekesha sana mkuu!

Have a nice day mkuu! anyway ninazichambua habari zaidi ili nitakapokuwa tayari nizitoa on my time, lakini picha sio utamaduni wangu hata siku moja! anyways tunawapa muda kidogo wa kuomboleza halafu tutaweka more dataz, ngoja sasa niingie kwenye DVD ambazo niliahidi kuziweka hapa JF, nafikiri by this week zitakuwa tayari kuwekwa hapa kwenye uwanja mtukufu!

Otherwise this is fun mkuu, tena a big fun! kwi!kwi!kwi!kwi!kwi! Ooooh I love JF!

Ahsante Mkuu!
 
mwanahalisi
Senior Member Join Date: Fri Apr 2008

Re: Hatimaye Nime-Confirm Kuwa Balali Amefariki!

--------------------------------------------------------------------------
field now nimejua why ur strong!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
keep it up men ukiona tunakupinga sehemu nyingine hiyo ni mawazo ya mtu kwahili tuko nyuma yako tumwagie data ,mkuu

Mkuu Wangu Mwanahalisi,

I mean I am humbled, maana it takes a lot of courage leo kusimama hapa JF na kusema maneno kama yako kabla ya kushambuliwa hapa na kwenye PM kama ninavyoambiwa na watu hapa, I mean heshima mbele mkuu mimi sina wasi wasi ni ukweli tu ndio huwa unanikomboa na sio logic wala chuki na wivu na unafiki kama sio uzandiki na majungu, wayapike vizuri lakini mimi mwendo ni mdundo tu,

Straight a head na ubarikiwe mkuu, dataz zinakuja fasten your belt mkuu!
 
FMES

Thats what we call .............. Whats up? Wasiokuwa na data wakae kimya wasome na kama hawaelewi waulize maswali badala ya kuleta vioja. Kajisemea Mzee Mwanakijiji wakishindwa hoja wanaleta viroja.

Now Balali is dead and burried, its a right time to find out who was enjoying our money with him ... Was it Che-nkapa? JK and his CCM government? Or was it Mkono and his sky rocketing firm? or was it other FISADI's?



BTW London Chenge alikuwa na FSO na EL alifuatia wamefika wapi hawa waheshimiwa? Wenye dataz ... dataz tu hadi walipakodi wafaidi angalau kidogo.
 
Yangu macho!... mkuu kumbe kuna watu humu hawafahamu nguvu ya mke au mme katika maswala ya familia nchi za nje?...duh! hii kazi kubwa sana..
Unajua kila mara mimi hujiuliza kitu kimoja hivi mbona baba na mama zetu sio ndugu wa tumbo moja lakini utawasikia wao wakiwapa ushauri watoto wao kuwa mkeo/mmeo ni mtu wa nje, mtu wa kupita kesho unaweza kuachana naye ukachukua kitu kingine..Familia ni wao.
Hata hivyo, kutokana na mgongano wa culture hizi hata sisi tumewekwa kati hatufahamu zipi bora kwetu kiasi kwamba inatujengea lawama kila siku..
Kwa mwafirka hatufahamu nani awekwe mbele Wazazi wako, Mke na wanao ama familia nzima ya uzawa yaani Wajomba, shangazi, kaka, dada na kadhalika..
Ndio maana misba yetu huzungukwa na wingu kubwa la kutafuta mchawi!, hata likikutoka chozi, watu hutazama analia kama nani?
Kazi kweli kweli!
 
Data zikiletwa na zinabase on word of mouth then still si confirmation pale inapokuja kwenye proof of the so called data.
Ina maana kwamba kama wewe si mmojawapo wa wale watu private walioalikwa...Then still una rely from a word of mouth na hiyo cannot constitute to confirmation of the death.
Tumeona kuwa kuna resouces tofauti ambazo bado zote ni conflicting
On the other hand however..Kama hao watu private walienda huko basi hata watakayoyaona ama wasiyoyaona yatakuwa ni private na nina wasiwasi wamesainishwa madocument kuwa wakisema kitu watakuwa matatani!
Wakwapi wakina M wa Kike aliyesema yumo ndani ya hao private na atatuletea pichaz?
 
Kwa wale wote wanaopenda kuendelea na mkakati wa kutaka uwajibishwaji kwa viongozi wote waliohusika na dhulma hii..Then jiungeni na kina Haki Ngowi,Bassila Mwanukuzi,Solo Thang na wengineo kutoka sehemu mbali mabali na mataifa mbali mabali!
Walioko bongo...Mapambano yanaendelea...Na sisi ni the same!
Gonga chini ukipata time jiunge na face book hata kama ni kwa jina lingine hakuna problem kwasababu hata muungawana na yeye si ana profile na hatujui kama yake ama la?
Na pia yeye amejiunga huko so tutapata na nafasi ya kumweleza ukweli straight forward!
http://www.facebook.com/group.php?gid=14717913036&ref=mf
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom