Waziri wa TAMISEMI, Angellah Kairuki amesema wanafunzi 129,830 wakiwemo wasichana 66,343 na wavulana 63,487 sawa na 69% ya wanafunzi wenye sifa, wamechaguliwa kujiunga na shule za sekondari za kidato cha tano.
Angellah Kairuki ameyasema hayo leo Juni 11, 2023, wakati akizungumza na waandishi, Jijini Dodoma.