Hatimaye tumekutana tena. Alinifaa kwa Jua lake leo nimemfaa kwa mvua yangu

Hatimaye tumekutana tena. Alinifaa kwa Jua lake leo nimemfaa kwa mvua yangu

Ahahahahahahahqhqh...
Umenichekesha sana mkuuu..
Wanasemaga kuwa "shida zina tabia ya kukupeleka kwa wale uliowazingua ndio wakusaidie " 🤣🤣🤣
Sasa hapo lazima tu uwe fund wa kujichekesha ili mambo yaende 😆😆
Kaka acha tu hamna muda mgumu Kama wakati unakutana na uliyemtesa alafu muda huo yamekubali ,utatabasamu Mara ujichekeshe mpaka unajionea aibu wewe
 
Je ingekuwa hajawahi kukusaidia usingemsaidia? Je unatenda wema kama malipo?
Angekua hakunisaidia maana yake tusingekua na ukaribu wa yeye kunifungukia ishu zake..
Ile siku kanisaidia ndio uhusiano wetu ulianza rasmi naweza sema maana before hapo ilikua tu kupeana hi kawaida sana.

Ila sasa kama tulivyo wanaume, licha ya kubadilishana namba ila hatukuwah wasiliana hata mara moja zaid ya mwaka mpka tumekutana hii juz kati ndio haya yakatokea
 
Huyu jamaa alishawah nisaidia nikaipata bag ya laptop niliyoibiwa nikiwa nimepaki gar ofisin na laptop nimeacha ndani ya gari.

Hanijui simjui ila alikua mpangaji mwenzagu kwenye hizo frame.

Alinisaidia baada ya kuitafuta sana kuambulia patupu nikakata tamaa. (Ni story ndefu sana).

Ila mwisho wa siku nikaipata na tukaachana na hatukuwahi onana tena miaka maana hata ofisi nikaamua kuhamisha.

Sasa juzi kati nikakutana nae TRA anafuatilia Tax clearance. Biashara yake imekua sasa na anaifanya kwa mfumo wa kampuni.

Ila ni mgeni kabisa kwenye masuala ya mahesabu na uandaaji wa taarifa kwaajil ya kodi akanielezaaa na mwisho wa siku akanambia kila anapogusa, tax consultant wa chini kabisa kamtoza 2M na hiyo pesa hana na ana haraka na hiyo certificate.

Tukabadilishana namba kisha nikapiga simu kadhaa kwa mtu wangu wa karibu tunae heshimiana nikamuomba amsaidie jamaa angu, kisha nikawaunganisha.

Baada ya siku 1 akanipigia jamaa anashukuru mnooo, maana yule mdau wangu wa hesabu alimfanyia kaz yake sawa na bure kabisa akamtoza hela ya maji tu 300k kutokana na mahusiano baina yanfu na yake.

Jamaa akafurah sana.
Nami pia nikafurahi.
Maana alishanisaidiaga kwanza before!!!.

Dunia Duara...
Malipo hapa hapa
natural law pays
 
Mimi kama roho nzuri ni maradhi basi itaniua sisubiri kuambiwa nna roho safi sana hua nautenda wema unarudi mara 10 zaidi na ukihitaji kufurahia ihsan basi fanya kwa siri inafungua sana njia hio
Waliosema wema hauozi hawakukosea aisee. Wakati mwingine unafanya wema halafu unasahau baada ya muda fulani unakutana na surprise ya kulipwa mara 10 ya ulichotoa.
 
Hapana, tukiwakamata jamaa walioiba, na ndio maana nikasema ni story ndefu maana kwenye ile laptop bag pia kulikua na wife device ambayo ilikua connected na simu yangu so ilituongoza kupata muafaka japo jamaa ali play part kwa 95% maana jamaa nafikiri ana uhusiano na polisi yale maeneo niliokuwepo
Sawa mkuu, mbarikiwe Sana...huo ndiyo ubinadamu
 
Sawa mkuu, mbarikiwe Sana...huo ndiyo ubinadamu
Amen..hakika japo ubinadam kazi maana sio wote binadam. Umakini pia ni muhim usije ukanyongwa kwa kamba yako mwenyewe au ukaponzwa na wema wako mwenyewe. Si unaelewa tena?
 
Back
Top Bottom