Hatimaye Warioba Kuwasilisha Rasimu ya Katiba Jumanne Tarehe 18 Machi 2014

Hatimaye Warioba Kuwasilisha Rasimu ya Katiba Jumanne Tarehe 18 Machi 2014

Status
Not open for further replies.

Chabruma

JF-Expert Member
Joined
Sep 19, 2013
Posts
5,660
Reaction score
1,780
Habari za usiku wadau. Natumaini wengi wenu mmejikunyata kitandani huku mkiendelea kutafakari hali iliyojitokeza jana jioni.

Taarifa iliyo rasmi ni kwamba Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Sinde Warioba atawasilisha Rasimu ya Katiba leo Jumanne tarehe 18 Machi 2014. Mtakumbuka kuwa jana jioni bunge maalum liliahirishwa baada ya kutokea vurugu zilizosababishwa na wabunge wa vyama vya upinzani kuzomea wakati Warioba akijiandaa kutoa hotuba ya kuwasilisha Rasimu ya Katiba. Wabunge hao wa upinzani ambao wamejiunga pamoja katika umoja wao ujulikanao kama UKAWA wanadai kuwa Mwenyekiti wa Bunge Sammuel Sitta amevunja kanuni ya saba kwa kuruhusu Warioba kuwasilisha Rasimu ya Katiba kabla ya Rais hajazindua Bunge. Pia wabunge hao wa upinzani walikuwa wanalalamika kitendo cha Warioba kupewa dakika 120 tu kuzungumza muda ambao walisema kuwa hautoshi.

Kutokana na hali hiyo, ile Kamati ya mashauriano iliketi baada ya bunge kuvunjika jana jioni. Katika kikao hicho, imebainika na wabunge wa upinzani wamekiri kwamba Mwenyekiti Sitta hajavunja kanuni yoyote kwa vile kanuni hiyo ilitenguliwa kihalali jana asubuhi na bunge kwa kutumia kanuni ya 85. Kwa maana hiyo, hoja imebaki pale pale kwamba Warioba ataanza kuwasilisha na Rais atakuja kuhutubia siku ya Ijumaa kama wasaa utamruhusu

Kuhusu hoja ya Warioba kupewa muda kiduchu, Kamati ya Mashauriano imefikia muafaka wa jambo hilo kwa kumruhusu Warioba kuwasilisha hotuba yake kwa ukamilifu wake. Kwamba mara baada ya kiapo cha wabunge leo asubuhi, Warioba atawasilisha hotuba yake kuanzia saa tatu na nusu hadi saa saba mchana.

Hata hivyo, ingawa wabunge wa upinzani wamekubali kuwa kanuni ya saba haijavunjwa, hali huenda ikaendelea kama ya jana hasa ikiwa wabunge wa UKAWA watakataa muafaka uliofikiwa kupitia Kamati ya Mashauriano. Upo uwezekano kwamba baadhi ya wabunge wa UKAWA wakaendelea na msimamo wa kutaka Rais aanze kuzindua Bunge ndipo Warioba aje kuwasilisha Rasimu ya Katiba.

Hata hivyo, tuwashukuru viongozi wa kiroho ambao wameamua kuwaeleza ukweli wanasiasa. Katika kikao hicho cha Kamati ya Mashauriano, viongozi hao wa Kiroho wamewaambia bayana wanasiasa kwamba wanaonesha jeuri isiyokubalika mbele ya Mungu kwa kuweka misimamo isiyo na tija. Kwamba, wanasiasa wengi wamekuwa viburi na wamejawa na dharau kitu ambacho hakimpendezi Mungu.

Ni hayo tu wakuu.
 
..., hoja imebaki pale pale kwamba Warioba ataanza kuwasilisha na Rais atakuja kuhutubia siku ya Ijumaa kama wasaa utamruhusu
.. .. eti kama wasaa utamruhusu! Au ndiyo kusema amebanwa na uchaguzi mdogo jimbo la Chalinze?
 
Kwa hiyo hao wanaojiita UKAWA wamekubali kulayamba matapishi yao ngoja nisubiri mda ufike nione......!!!!
 
Hao "Viongozi wa kiroho" wana roho nyingine, wana mapepo, yakemewe. Wakati kanuni hizo zinatungwa, "Viongozi wa kiroho", hao, hawakuwepo????? Hao "Viongozi wa kiroho", ni mapandikizi ya CCM!!! Hakuna cha "Viongozi wa kiroho" hapa, wala cha nini, KANUNI LAZIMA ZIZINGATIWE!!!! Katiba inaanza kwa kusema,"Sisi wananchi tumeamua rasmi". Katiba ya sisi wananchi, haiwezi kupatikana kwa ubabe wa Sita, asiyekubali kushindwa !!!!!! UKAWA, hakuna kuweka silaha chini, wananchi tuko nyuma yenu!
 
Hakika mkuu. Tutaona mengi safari hii

Nyie CCM msitaki kuifanya nchi hii ya kwenu peke yenu!! Mbona mnataka kutuburuza kwa maslahi yenu na watoto wenu!!? Hakuna hata CCM mmoja ambaye yuko kwa ajili ya maslahi ya wengi... Lengo lenu mnataka kumdhalilisha Jaji Warioba ili ionekane kazi waliyoifanya haina maana.. Hebu tujiulize ni Tume ngapi zimeundwa na Serikali ya CCM na zote zimependekeza muundo wa Serikali tatu? Kipi kigeni kwenye mapendekezo yaliyotolewa na Tume ya Katiba..

Msijidanganye kwamba mtatuwala milele, jifunzeni kupitia historia. Dunia imeshuhudia tawala na falme ngapi zenye nguvu kuliko hii Serikali ya kuombaomba ya CCM zilidondoka na kusambaratika...

Mnachowafanyia watanzania Mungu hafurahii hata kidogo,, maana mko tayari kuua ili muendelee kutawala.. Hakika nawaambia dhambi hii lazima mtakuja kuilipa hata kama si ninyi hata watoto na wajukuu zenu wataibeba na kuilipa...

Endeleeni kutuburuza lakini siku yenu haiko mbali!!
 
Hao "Viongozi wa kiroho" wana roho nyingine, wana mapepo, yakemewe. Wakati kanuni hizo zinatungwa, "Viongozi wa kiroho", hao, hawakuwepo????? Hao "Viongozi wa kiroho", ni mapandikizi ya CCM!!! Hakuna cha "Viongozi wa kiroho" hapa, wala cha nini, KANUNI LAZIMA ZIZINGATIWE!!!! Katiba inaanza kwa kusema,"Sisi wananchi tumeamua rasmi". Katiba ya sisi wananchi, haiwezi kupatikana kwa ubabe wa Sita, asiyekubali kushindwa !!!!!! UKAWA, hakuna kuweka silaha chini, wananchi tuko nyuma yenu!
umeshaambiwa kanuni ilitenguliwa asubuhi na wakakubaliana,au unasemea kanuni ipi tena?
 
Nyie CCM msitaki kuifanya nchi hii ya kwenu peke yenu!! Mbona mnataka kutuburuza kwa maslahi yenu na watoto wenu!!? Hakuna hata CCM mmoja ambaye yuko kwa ajili ya maslahi ya wengi... Lengo lenu mnataka kumdhalilisha Jaji Warioba ili ionekane kazi waliyoifanya haina maana.. Hebu tujiulize ni Tume ngapi zimeundwa na Serikali ya CCM na zote zimependekeza muundo wa Serikali tatu? Kipi kigeni kwenye mapendekezo yaliyotolewa na Tume ya Katiba..

Msijidanganye kwamba mtatuwala milele, jifunzeni kupitia historia. Dunia imeshuhudia tawala na falme ngapi zenye nguvu kuliko hii Serikali ya kuombaomba ya CCM zilidondoka na kusambaratika...

Mnachowafanyia watanzania Mungu hafurahii hata kidogo,, maana mko tayari kuua ili muendelee kutawala.. Hakika nawaambia dhambi hii lazima mtakuja kuilipa hata kama si ninyi hata watoto na wajukuu zenu wataibeba na kuilipa...

Endeleeni kutuburuza lakini siku yenu haiko mbali!!
kuwepo serikali moja,mbili ama tatu hakutoi uhakika wa chama fulani kutawala,think.
 
umeshaambiwa kanuni ilitenguliwa asubuhi na wakakubaliana,au unasemea kanuni ipi tena?

Soma kwanza kanuni uzielewe, kabla ya kuchangia hapa. Kanuni hiyo, haiwezi kutenguliwa, kulingana na Kanuni ya 85(4) inayoelezea mazingira yanayoweza kusababisha kanuni itenguliwe. Hakuna habari ya maCCM kukubaliana hapa!!!!!!!!!!!!
 
Tangu lini ninyi wapagani mmeanza kujua kwamba kuna "Viongozi wa kiroho"? Mngekuwa mnajua kwamba kuna "Viongozi wa kiroho", msingetupa kapuni, majina ya Viongozi wa kiroho wa Makanisa ya Kipentekoste. Ondoeni hapa unafiki wenu!! Hakuna cha "Viongozi wa kiroho" hapa! KANUNI LAZIMA ZIZINGATIWE !!!!!!!!!!
 
kidhungudhungu.

Huyu kikwete nafasi za kuhudhuria misibani kwa dharura anapata!!!!!

Nafasi za kuwatembelea wafungwa wa makosa ya wizi wa fedha za umma anapata!!!!!?!!!

kikwete huyuhuyu anakosa nafasi kuzindua bunge la katiba kama ratiba inavyomtaka!!!!!!!!?!

asije akatokea hapo mbeleni mtu akafanya ujinga "kama alioufanya Nelson Mandela" kuwasamehe wakosaji hawa wa makosa ya makusudi huku wakikejeli.
 
Hao "Viongozi wa kiroho" wana roho nyingine, wana mapepo, yakemewe. Wakati kanuni hizo zinatungwa, "Viongozi wa kiroho", hao, hawakuwepo????? Hao "Viongozi wa kiroho", ni mapandikizi ya CCM!!! Hakuna cha "Viongozi wa kiroho" hapa, wala cha nini, KANUNI LAZIMA ZIZINGATIWE!!!! Katiba inaanza kwa kusema,"Sisi wananchi tumeamua rasmi". Katiba ya sisi wananchi, haiwezi kupatikana kwa ubabe wa Sita, asiyekubali kushindwa !!!!!! UKAWA, hakuna kuweka silaha chini, wananchi tuko nyuma yenu!
Mkuu, kanuni zinapokuwepo ama zinaweza kufuatwa, zisifuatwe au zinaweza kutenguliwa. Viongozi wa kisiasa wapo sahihi kusema ukweli
 
Baada ya jana jioni bunge la katiba kuingia katika hali ya sintofahamu iliyochangiwa pia na wabunge wa chadema,cuf na nccr- mageuzi leo asubuhi bunge litaendelea na shughuri zake kama inavyoonesha hapa chini.


1. Kuanzia saa tatu asubuhi mwenyekiti wa bunge maalumu mh samweli sitta ataweza kuwaapisha wabunge waliosalia kuapa ambao idadi yao yapata kama thelathini hivi.


2. Baada ya wabunge hao kumaliza kuapa jaji warioba ataweza kuwasilisha rasimu ya pili ya katiba ambapo imepangwa kuanza saa tatu na nusu au na dakika arobaini na tano mpaka saa saba kamili mchana.


3. Baada ya warioba kumaliza kuwasilisha rasimu mwenyekiti atalieleza bunge nini kitafuata baada ya zoezi hilo kukamilika.


Hivyo ndivyo utaratibu utakavyokuwa kwa leo karibu sana tuendelee kufuatilia katiba yetu inavyotungwa.
 
kidhungudhungu.

Huyu kikwete nafasi za kuhudhuria misibani kwa dharura anapata!!!!!

Nafasi za kuwatembelea wafungwa wa makosa ya wizi wa fedha za umma anapata!!!!!?!!!

kikwete huyuhuyu anakosa nafasi kuzindua bunge la katiba kama ratiba inavyomtaka!!!!!!!!?!

asije akatokea hapo mbeleni mtu akafanya ujinga "kama alioufanya Nelson Mandela" kuwasamehe wakosaji hawa wa makosa ya makusudi huku wakikejeli.
Mkuu, wakati mwingine Mkuu wa nchi anakuwa na majukumu mengi ya lazima nje na ndani ya nchi. Inategemea jukumu hilo lipo wapi.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom