Hatimaye Yanga yakabidhiwa kwa Manji aiendeshe kama club Binafsi

Hakuna afadhali hao wahindi wameona kuna fursa,wanataka kufanya biashara na watapata hela nyingi sana kwa mgongo wa hizi timu

Inauma sana, tena wanagawana tu utafikiri peremende.

Mi nilikuwa najiuliza, hivi huyu Manji anawekeza vipi Mabilioni ya pesa bila kupata faida yoyote? Anaipeleka Timu Uturuki, Inapiga kambi hata wiki mbili mfululizo kwa gharama zake, hivi anapata nini???

Ebhanaeee huyu mtu mjanja sana. Leo kakabidhiwa timu puuuuuuu, wale viherehere wa kuhoji fukuzia mbali, dadekiiii....!!!!

BACK TANGANYIKA
 
mkuu mbona bado mapema sana kutoa lawama hizo ulizotoa!!? Alichokifanya manji,ndo kile kile kilichofanywa na mo dewji. Hii ni hatua ya awali,yaani kuleta wazo kwanza kwa wanachama,wanachama wa yanga wakiafiki,hatua ya pili ni kufanya marekebisho ya katiba kuweka vipengele vitakavyoruhusu huo ukodishwaji.

Kitu kibaya nilichokiona kwa manji,ni hili la kufukuza viongozi tena wa kamati ya utendaji..!! Hii pengine ni njia ya manji kuwaondoa wale ambao anajua watasimama upande wa yanga kutetea masilahi. Ki-msingi yeye ndo alipaswa kuachia ngazi leo km mwenyekiti wa yanga ili kuondoa mgongano wa masilahi...akibaki km mwenyekiti wa yanga,wakati huo huo yeye ndo mkodishaji nani atamfunga paka kengele!!??
 
Akimaliza kukodisha nasi pia tukodishwe,tanzania ya mabadiliko bado ujanja ujanja!
 
Nahic yanga wanatapeliwa mchana kweupeeeeeeeee[emoji12] [emoji12] [emoji12] [emoji12] [emoji12] [emoji12] [emoji12] [emoji12]
 
Bora wachukue tu maana sioni faida ya hizi timu
 
Wabongo bwana! Timu zinaishi kwa msaada miaka yote hata mvi zinaota na bado ni masikini. Kazaliwa Kazaliwa juzi tu, azamu na kanajimiliki, bado watu wanataka hizi timu kongwe zife zikiwa maskin? Kwa faida ipi haswa? Raha ya timu ushindi na burudani bwana. Si timu ikibahatika kucheza japo kombe la cecafa inawaza kijitoa kisa shida, wapeni timu. Ila watuuzie hisa
Kwa malengo maalum kwa wanachama na mashabiki,
 
Nashindwa kuelewa hapo kwenye kukodisha timu. Hapa Kuna kautelezi kakushtukiza.
 
Hilo ndiyo jambo la msingi, anatia mtaji kiasi gani?
 
  1. we ndio mwehu kweli eti nembo thamani yake trilioni...Yanga inaendeshwa kwa misaada kila siku mbona hiyo nembo haijawahi kuwasaidia? Mwacheni Manji apewe timu
 
  1. we ndio mwehu kweli eti nembo thamani yake trilioni...Yanga inaendeshwa kwa misaada kila siku mbona hiyo nembo haijawahi kuwasaidia? Mwacheni Manji apewe timu

Haipendezi....!!!!

Unaona ni sahihi kuniita mwehu? Sawa ungeshambulia hoja basi, kwanini kunitusi???

Nikikujibu hivi si kwamba sijui kutukana ama siwezi kukutukana.... JUST A WARNING....!!!

BACK TANGANYIKA
 
Wenzetu wametoa maamuzi ya haraka japo sidhani kama kila kitu kimezingatiwa vizuri ila ni hatua moja kubwa tofauti na upande wa Simba.Mwendo wa kinyonga.
 
We umeisaidia nini yanga kama timu labda, we kazi yako kufurahi kama shabiki, mbona TP mazembe inaendeshwa na katumbi, cha muhimu tujue iyo miaka 10 nini yanga kama club itapata
 
Katika wanachama walio makini ni Yanga! Jamaa atakodishwa timu ila ili mkataba udumu inabidi timu iwe na mafanikio miaka yote hiyo kumi otherwise kama hakuna mafanikio wanachama wa yanga wataweka kambi pale quality group na mwenyewe atarudisha timu!!
 
We umeisaidia nini yanga kama timu labda, we kazi yako kufurahi kama shabiki, mbona TP mazembe inaendeshwa na katumbi, cha muhimu tujue iyo miaka 10 nini yanga kama club itapata

Unajua maana ya ushabiki???
 
Kweli mkuu, hiyo nembo hatujaona faida yake kwa kiaka yote hiyo, ngoja tuone uwekezaje wake
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…