Hatma ya maisha yangu ipo mikononi mwa kijana wa Buguruni

Hatma ya maisha yangu ipo mikononi mwa kijana wa Buguruni

Me Najua basi, hilo neno mm si nimelirukia kwa Michelle ambaye ni Dada yake na Caryn
Hahaha uko smart sana mkuu, ila story bado sio ya kweli. Uko tayari nikupe mtego mwingine au niache?
 
ILIPOISHIA [emoji1484]

Caryn: "Sorry Dad, first of all I want to know where these kids came from?

Tukaanza kuangaliana na yule jamaa aliyekuwa anaendesha Gari, Wakati najipanga kujibu.....

Caryn: BM, You should answer this question

Nikamuambia wametoka Buguruni Rozana

Caryn: "Dad, I think you should change your strategy on how to help these kids

The food we're gonna give them was it gonna change their life?
So as a rich man if you think you want to help someone give them the kind of help that would transform their life not leaving them with food in my opinion"


MUENDELEZO [emoji1484]

Mzee akamuangalia Caryn halafu akaniangalia na Mimi, Akasema "Kwahiyo unashauri tufanye nini Binti yangu"

Caryn: Let me speak swahili so that they can understand me, Hawa watoto kwa umri waliokuwa nao wanatakiwa wawepo shuleni, labda mtasema mnawapatia chakula kwasababu hawajafika umri wa kujishughulisha na shughuli zozote za kujiingizia kipato, huyo Kaka yao je maana anaoneka ni mtu mzima

Caryn: "How old...ooh sorry, Una miaka mingapi kaka?"

Kijana: "Kumi na Saba"

Mzee: Kumi na Saba Bado mdogo sheria haruhusu

Caryn: Come on Dady, Kwahiyo kama sheria hairuhusu ndio abaki kuomba omba, Kuna situation ikikufika hutakiwi kuangalia Sheria inasemaje inakubidi kufanya kile unachotakiwa kufanya ili u survive, Kijana you have to do whatever it takes to survive out here in this jungle called life

Michelle: Sometimes you sound more like an adult than a teenager

Caryn: You sound like you're better than me, and you're not

Mama: Na nyie mshaanza sasa na malumbano yenu, ebu Kuweni na adabu hata kidogo mbele za watu msiowajua

Caryn: Ambae hana adabu ni huyo mwanao mama, Watu tunaongea vitu serious yeye analeta utani, mm teenager sawa, yeye huo utu uzima umemsaidia Nini hadi sasa, Anawaza Mapenzi tu......

Mzee: "Caryn basi Inatosha, unajua huyo atabaki kuwa Dada yako inabidi umuheshimu, halafu kwanini siku hizi nyie watu hampendani?"

Caryn: "Kwasababu nimekuambia Habari za huyo bwana ake wa huko Kibaha, I told you Dady na nakuambia tena the guy is more interested in money hakuna Mapenzi hapo"

Mzee: Caryn hiyo ni topic ya siku nyingine all in all nimeipenda maoni yako kuhusu Hawa vijana wadogo

Ila Caryn hapana asee [emoji1544] yule Demu kachukua akili za Baba yake, ni PISI KALI halafu sauti yake ni kama ya Bahati Bukuku na mara nyingi anakuaga serious, nyumba nzima hapa kwa Mzee ni yeye tu ndio sijawahi kumuona akicheka

Tukamaliza kula, Mzee akawahoji wale watoto mambo kadhaa, akawapatia na Pesa halafu akanambia "BM Nadhani Ushauri wa Caryn ni mzuri, Sasa ule mtihani nililokuambia nitakupa umekaribia get yourself ready. chukueni Gari warudisheni Hawa watoto halafu na Kijana atakudrop kwako,

Basi tukaondoka, tukawadrop madogo na mm nikadropiwa, kufika kwa nyumba nikamkuta Annie nikakuta ameandaa my favorite food Wali Nazi Njegere Nazi, Asee halafu nimetoka kubonya Pilau la Kuku kwa Mzee, nikaona hapa busara ni kula hata kama ni nusu sahani, Unajua Annie anajua natoka Kazi hakujua ratiba yangu imeendaje na Wala hajui Mahali nimetoka

Akaniwekea food kwa meza nimeipiga kama vijiko vitatu ivi nikamuuliza "Are you sure it's not Christmas yet?"

Annie: "of course it's not"

Maana sio utamu huu wa msosi, saa hiyo mm nikiendelea kula Annie alionyesha kuwa na mawazo, nikamuuliza nini mbaya?

Annie: You know what BM, now i believe that circumstances change people

Me: Unamaanisha nini?

Annie: Hadi hapa tulipofikia life has taught me not to plant my seed in other people's garden

Nikawa nishajua alichokuwa anamaanisha, TURUDI NYUMA Kidogo ili na wewe umuelewe Annie

Ukisema "Table turns" Mtu wa kwanza kuelewa ni Annie, niulize kwanini? Okay ilikuwa hivi, Miaka mitano nyuma Annie alikuwa mtoto wa kishua nikisema wakishua wakishua haswa haya maisha acheni nyie,

Natamani niandike mengi kuhusu Annie lakini haitawezekana kwasababu code yake nimeifungua, ndio muhusika pekee Jina lake ni halisi kwenye hii story wengine wote nimetunga majina na baadhi yao niliishia kuwaita Mzee, Mama, Jamaa nk

Ila kwa kifupi ni kwamba Annie alipiga taff sana enzi hizo wakiwa bado wako vizuri, Alinilipia hadi ada ya mwaka wa mwisho chuoni. Baba yake alikuja kupata matatizo flani kipindi Cha awamu ya 5, na Annie Mama yake Alishaaga kitambo so alibaki na Baba, Baba nae ndio hivyo akapotezwa, acheni asee kila nikikumbuka roho inaniuma ndio maana nakuwa mzito kumuachia huyu mwanamke

LEO

Nikamwambia Najua unachoniwazia ila nikwambie tu unaniwazia vibaya, acha nikuambie ukweli pengine utakuumiza ila ni Bora kuliko kudanganyana, inawezekana nimekucheat lakini sio kwa mazingira niliyoyaandaa, Najua nilishakuambia mengi kuhusu yule mwanamke (Accountant) lakini hili la kucheat nilikuficha kwasababu sikudhamilia mimi na kuhusu swala la kuacha kazi ili kumkwepa yule mwanamke sidhani kama ni sahihi kwasababu unajua hali halisi ya maisha ilivyo Mimi nakuomba tu uridhie Mimi kundelea kufanya kazi Mimi nitajua tu jinsi ya kudeal na yule mwanamke na nakuahidi sitarudia kosa, Nakuomba usikatae, ni swala la muda tu nikakamilisha malengo yangu flani naachana rasmi na Ile Kampuni

Annie: Okay! i trust you BM, you can go ahead, but remember not everyone in this life gets a second chance to write their wrongs

Me: Nakuahidi haitojirudia, na nakupenda sana japokuwa ww mara nyingi husemi kwa Mdomo kama unanipenda

Annie: Ushaanza, listen BM 'I trust you' is better compliment than 'I love you' because you may not always trust the person you love but you can always love the person you trust

Me: Wow! thanks, i didn't even know that

Basi Mama lao akatoa vyombo pale, Leo hajaachwa mtu Sebuleni, Najua mshaelewa. siku zilikatika mambo yalikuwa mswano na Annie

Asubuhi ya Jumamosi moja nimeamka nimechelewa sana kwenda job, nikajiandaa fasta nikasepa nikafika eneo langu la kazi Sasa wakati naingia Ofisini nikamkuta Accountant kakaa kwenye kiti changu ni kama alikuwa ananisubiri kwa hamu, nikamsalimia akaitikia halafu akanambia

Accountant: Naona maisha yako yanaenda kuwa mazuri ila endapo tu utafanya Maamuzi sahihi

BM: Nikamuuliza Maamuzi gani?

Accountant: Usiwe na haraka BM, Mama alikuwa anakuulizia amesema ukifika tu nikwambie uende Ofisini kwake so we nenda kaonane na Mama

Nikawa najiuliza Kuna jipya gani maana Accountant anafuraha kupita maelezo na si kawaida yake, basi Mimi nikaelekea ofisini kwa Mama, nikasalimia nae halafu nikakaa kwenye kiti

Mama: Mwanangu si kawaida yako kuchelewa kazini, Leo imekuaje?

BM: Jana nilichoki sana Mama, hali iliyosababisha kupitiwa na usingizi Leo na kuchelewa kuamka

Mama: Ooh, halafu hata hivyo hukuwahi kuchukua likizo ya kueleweka tangu uanze kufanya kazi kwenye hii Kampuni

BM: Yeah ni kweli Mama lakini sikuona ilazima huo

Mama: Sasa Mimi nakupa likizo ya mwezi mmoja ya lazima hata kama hutaki, japokuwa hapa nilikuitia jambo lingine lakini Nadhani tutapata nafasi Nzuri zaidi ya kulijadili hilo jambo akili yako Ikiwa refreshed

BM: Ni jambo gani hilo Mama?

Mama: Nilijadili na mwenzako lile swala la wewe kurithi hii nafasi yangu, amefurahi sana lakini ametaka mvishane kwanza Pete ya kabla ya kukalia hiki kiti, na Mimi Nadhani ni jambo zuri so nilikuitia hapa ili tupange siku ya kufanya zoezi hili, lakini wewe nenda kwanza likizo ukirudi tutapanga vizuri.

Nikamuitikia tu "Sawa Mama" huku nikimuwaza Accountant, ndio kashaanza kuchezesha Karata zake kama alivyoniahidi, Basi mm Nikatoka Ofisini kwa Mama, nilimkuta Accountant Bado yupo pale kwenye kiti changu, Nilifika tu nakumwambia kwa userious wa hali ya juu "nipishe Mimi niendelee na Kazi"

Accountant: I hope umefanya Maamuzi ya kiume, halafu kumbe huwa mnaongeaga mambo mengi na Mama bila kunishirikisha, ivi unajua maamuzi mengi anayoyafanya mama juu yako ni kwasababu anajua Mimi na wewe ni wapenzi, Sasa isije ikawa umeshaharibu mambo huko

BM: Sikiliza **** (Accountant) naomba kwasasa uende kwenye ofisi yako, Nina mambo mengi ya kufanya, sitakiwi kuacha kiporo Cha aina yoyote kwasababu kuanzia Jumatatu siji kazini

Accountant: Unasemaje wewe?

Alivyosikia "Kuanzia Jumatatu siji kazini" alipagawa sijui alidhani nimeshaacha kazi, Alitoka mbio sijui kaelekea wapi ila itakua tu kwa Mama yake bila shaka

Nimekaa kidogo akarudi akanambia "Inawezekana wewe ndio umeomba hii likizo ili ukajipange maana inaonesha Kazi unaitaka lakini mwenye kazi humtaki, Sasa Mimi nakuambia hivi, we nenda hiyo likizo lakini siku utakayorudi hapa uwe umeshaamua jambo moja kati ya haya mawili, UNIOE au uandike barua ya kuacha kazi, Sitakubari uwe Director wa hii Kampuni a halafu raha unakula unakula watu wengine" alivyomaliza hakutaka nimjibu akaondoka

Aliniacha na mawazo, kusema ukweli hii nafasi naitaka ili niweze kufikia malengo yangu lakini ndio hivyo tena ili ni qualify kwenye hiyo nafasi basi nilazima nimuoe Accountant, nikifanya hivyo Annie wangu nitamuweka katika nafasi gani na Jana tu tumetoka kula kiapo, na huyu Accountant mwenyewe hana sifa hata moja ya wife ila kitandani kwakweli yupo vizuri japokuwa ilikuwa ni mara moja na kwa bahati mbaya na hiyo dhambi nishaimbea msamaha kwa Annie na kanisamehe kwa kumuahidi kutorudia tena

Siku ikaisha na ndio ikawa nimeianza likizo yangu ya mwezi mmoja rasmi, lakini ya mawazo kwasababu natakiwa kufanya uamuzi sahihi, hapa kichwa kiliniuma zaidi kwasababu ya mtihani wa Mzee niliopewa,

Wakati naandika huu Uzi nilikuwa Bado sijapewa likizo, Uzi nimeuanza kuaandika jumatano ya tarehe 6/7/2022 na likizo nimepewa juzi Jumamosi tarehe 9/7/2022 hii siku kama mnakumbuka nilicomment hapa hiyo comment ipo namba 272 kama sikosei nilitoa maelezo kwanini hii story imekua ndefu Sasa siku hii ndio nilipewa likizo ya lazima so hili tukio ndio nimeliunganisha kwenye Uzi.

Na Uzi ulikuwa una muhusi Mzee ila niliongea story zingine kwasababu ili kufaulu mtihani wa Mzee inategemea pia mm kuendelea kubaki kazini

Inatakiwa Utulivu wa hali ya juu kuelewa, TURUDI NYUMA KWENYE MTIHANI NILIOPEWA NA MZEE

Ilikuwa Alhamisi, saa nne na Dakika thelathini na Saba sekunde ya sita simu ya Mzee iliingia nikiwa Ofisini najiandaa kwenda Zanzibar na Boti ya mchana

Mzee: [emoji338]"Kijana wangu hujambo?"

BM: "Sijambo Mzee, Shikamoo"

Mzee: "Marhaba, Sasa nataka kukujuza kwamba siku ya Jumapili jioni nasafiri hivyo nakuomba tuonane siku hiyo kabla sijaondoka

BM: "Sawa Mzee Haina shida"[emoji3513]

Basi nilienda Zanzibar nakurudi kesho yake, Jumapili Ikafika nikajua kabisa LEO NDIO ILE SIKU, Ile siku ya kupatiwa mtihani, Nakumbuka nilienda kwa Mzee mida ya saa sita mchana, nimeingia kwenye Ile nyumba harafu za misosi tu ndio zimetamalaki,

Kama kawaida chimbo langu na Mzee ni Backyard tukaongea sana mambo mengi, Sasa bhana safari yenyewe kumbe ni ya nje ya nchi, Mimi nilijua ni zile safari zake za mkoani kumbe Mzee anaenda United Kingdom (Uingereza) na atakaa huko kwa muda wa miezi miwili na nusu

Acha nifungue code kwenye Biashara moja ya Mzee, Ni hivi, Mzee ana mabiashara mengi ila moja ya hizo Biashara ni maduka ya Ex UK, Sasa huko UK alikua anaenda kibiashara zaidi, Sasa Mzee alinambia kwa muda wote. huo ambao atakuwa nje ya nchi niwe natembelea familia yake mara kwa mara, muda wa msosi ukafika tukakutana wote mezani yani Mimi, Michelle, Caryn, Mama na Mzee, Wakati tunaendelea kula mazungumzo nayo yaliendelea

Mama: "BM usipotee sana kwasababu Baba hayupo, uwe inakuja nyumbani tena mara kwa mara zaidi

Mzee: "Nimeshamsisitizia hilo, halafu BM kuhusu ule mtihani niliosema nitakupatia maelezo yote anayo Caryn, So ni wewe Tu kutafuta muda ukae chini na Caryn akuelezee

Nikajibu "Sawa Mzee" huku nikimuangalia Caryn na yeye akinipiga jicho la kimtindo

Michelle: "Baba kwani ni mtihani gani huo?"

Mzee: "Hili halikuhusu Michelle, wewe si ulishafeli wa kwako, Majukumu anayofanya Caryn ulipaswa kufanya wewe. Na Caryn zidisha umakini katika kumsaidia Mama yako majukumu ya Ofisini, Kuna baadhi ya mambo Mama yako anasahau

Caryn: Okay Dady, we will miss you

Eeh!!! nilishangaa, kumbe Caryn ndio anapewa majukumu makubwa kiasi hiki, basi tulimaliza kula tukakaa kama 1 hour tukaanza safari ya kuelekea Airport, hii ndio ilikuwa mara yangu ya kwanza kupanda 'Jeep Wrangler' halafu Mzee akaniambia nikae mbele, Guess Sasa nani anaendesha? ni Caryn jamani dah!

Tukafika Airport Wakati tunamuaga Mzee akanambia "BM nikirudi nikukute ushapata Driving Licence" Nikamwambia "nitajitahidi Mzee" Basi ndio hvyo tena Mzee akaingia kwenye kale ka mlango kalikoandikwa DEPARTURE sisi tukaenda kwenye Gari na kurudi nyumbani,

Wakati tumefika Tazara tunacross kuelekea Buguruni Nikamwambia Caryn "Mimi mtanidrop hapo Tabata"

Caryn: "Okay, I will text you, Dady gave me your number"

Tukafika Tabata wakanishusha nikatafuta Daladala la kuelekea Tabata Kimanga

Blue Monday mapema kabisa nimeamka kwaajili ya kwenda kazi, nashika simu kuangalia muda naona meseji ya namba ngeni kuifungua "Hey! Mornie, It's me Caryn" Nika reply "I got you" then nikasave namba yake

Wakati nipo Ofisini Caryn akanipigia akanambia kuwa yupo ofisini kwa Baba yake atatoka jioni na kuelekea **** ni Ile Hotel ambayo nilikutana na Baba yake, hivyo akaniambia nimkute hapo

Sasa yeye aliwahi sana kutoka siunajua wao ndio mabosi so wanajiamulia muda wa kutoka, mm ilibidi nisubiri Hadi ifike angalau saa kumi na nusu, Mida ikafika ya kutoka kazi moja kwa moja nikaelekea Hotelini lakini hiyo foleni niliyokutana nayo Njiani siyo ya kitoto, nikajua yule mtoto (Caryn) alivyo serious katika Kila Kitu sidhani kama nitamkuta, Mungu alisaidia nikamkuta Ile nimefika tu nikakaribishwa na

Caryn: "why are you late, you kept me waiting almost 2 hours?"

BM: "It wasn't deliberate the traffic was crazy it was terrible"

Caryn: "That is the senseless excuse"

BM: "Ok, let's discuss what brought us here"

Caryn: "let me start by asking you a question, Have you ever...."

BM: "Wait pls, Sijawahi kusikia ukitumia kiswahili japo kwa sentensi 3 mfululizo, naomba Leo tutumie kiswahili kwenye haya mazungumzo"

Caryn: "Ni sawa tu, as you wish

Nikasema 'Yes' maana Nisingemuwahi huyu angenitemea Yai[emoji1639] hapa mwanzo mwisho na hata misamiati mingine nisingeielewa

Caryn: "Umeshawahi kufanya Biashara?"

BM: "Kama Biashara gani labda?"

Caryn: "Typical Tanzanian man you're answering questions for questions"

BM: "Madam anayejibu swali kwa swali mwisho wa siku jibu lake linakuwa la uhakika, yani hiyo ni njia ya kulielewa swali vizuri zaidi, ila na wewe Kingereza unakipenda sana bhana

Caryn: "Okay, Just any Business hata kama ya kuuza chupi"

BM: "Hapata, sijawahi Fanya Biashara"

Caryn: "Interesting, kama ni hivyo hukuwa katika nafasi ya kujibu Swali kwa swali kama ulivyofanya"

BM: "Nimekosa mimi, twende kwenye Point"(Nikajisemea moyoni Leo kazi ninayo)

Caryn: "Ebu kwanza nieleze kuhusu yule kijana aliyekuja na wadogo zake pamoja na watoto wengine"

BM: "Nikueleze nini?"

Caryn: "Ooh shit! same mistake, Are sure you will handle this?"

BM: "You wasn't specific enough, ukiuliza swali jaribu kuwa specific zaidi"

Caryn: "You're not smart enough as I expected, I see that you're even worse than i imagined"

BM: "Madam mimi naomba niende tu, maana naona Sasa umekuja kunichora tu

Nikanyanyuka kwenye kiti, kabla sijapiga hatua akanambia "Ebu acha utoto Kaa chini na unisikilize kwa Makini, naku challenge kidogo na wewe umejaa kweli"

Nikakaa chini moyoni namsema huyu mtu inabidi nimsome akili yake ndio nitaenda nae sawa lasivyo atanitoa knock out

BM: "Caryn jaribu kuwa serious kidogo, unajua kama ningekuwa na Mzee hapa tungekuwa tushamaliza maongezi"

Caryn: "Thus why I am not Mzee, you know what BM, kwa muda huu mchache tuliokaa hapa Kuna Kitu nishakisoma kutoka kwako

BM; "Kitu gani?"

Caryn: "Unakosa some confidence pengine hasa ukiwa na mtu ambae hujamzoea, kwa Mfano kwenye swala la Kingereza sidhani kama ww hujui Kingereza, unakijua vizuri tu lakini ukataka niongee kiswahili, chaajabu nikawa naongea Kingereza makusudi na wewe unanijibu Kingereza, hiyo maana yake Nini?"

BM: "Sawa nimekusikia, nitayafanyia kazi si ni hayo tu?" (Katika siku ambayo nimejihisi mdhaifu ni leo)

Caryn: "Hapana! sio hayo tu, Pia una shida katika kuongea japokuwa tuko pale pale kwenye confidence, nimekusoma wewe ni mjanja ambae huna confidence, Sasa ukiongea mbele ya mtu ambae hayupo Makini atajua una confidence kumbe ni ujanja tu, So you should talk like gentleman with confidence"

BM: "Dah! Leo kazi ninayo, kama mambo yenyewe ndio haya nyumbani kule si wanapata shida sana?"

Caryn: "Nadhani utakuwa umenielewa, acha niende straight tu the point, Japokuwa nilikuuliza swali mara ya kwanza ila ukaleta ujuaji, Yule kijana uliyemleta siku ile nyumbani na wadogo zake, Mzee kasema kamtafutie nyumba umpangie halafu utaniambiaa Kodi ni kiasi gani nikupatie pesa ya Kodi ya miezi sita, hiyo ni moja mbili Sasa, Amesema umpatie pesa ya mtaji afanye Biashara na uhakikishe katika hiyo Biashara atakayofanya huyo kijana ndani ya miezi sita iwe imeshasimama na waweze kujilipia Kodi,"

BM: "Biashara gani sasa na mtaji kiasi gani?

Caryn: "Hapo kwenye Biashara amesema wewe ndio utakayemchagulia na mtaji pia hajakuwekea limitation kwasababu wewe ndio utakayetoa hiyo pesa ila ameweka vigezo katika nyumba utakayo watafutia, Amesema Nyumba isiwe chini ya shilingi laki 1"

BM: "Dah! Baba yako sijamuelewa hapo kwenye swala la nyumba tu, kwasababu kama mm mtu ambae najiweza nakaa nyumba ya laki na nusu iweje yule kijana tumtafutie nyumba ya pesa yote hio Ikiwa ndio anaanza maisha?"

(Kabla ya kujibu Caryn akacheka kwanza)

Caryn: "I'm so proud to have him as my Dady, Sasa acha nikuambie ni Kwanini amekuwekea vigezo hapo kwenye nyumba, Cha kwanza hapo Dady ameshaku limit katika upande wa kuchagua Biashara, kwasababu asingefanya hivyo ungemtafutia tu yule kijana chumba Cha elfu 10 halafu ungempa na mtaji wa Biashara ya karanga"

BM: "Mbona kama mtihani wenyewe nishafeli, kwasababu ili mtu aweze kula na kufanya mambo mengine na aweze kulipa Kodi ya laki moja kwa mwezi basi hiyo Biashara mtaji wake usiwe chini ya milioni 1

Caryn: "What do you mean? huna hiyo pesa?

BM; "Tatizo sio Pesa, nawaza ni Biashara gani hiyo yule kijana ataimudu kuendesha ya kiwango hicho Cha pesa"

Caryn: "Ndio maana mwanzo nilikuambia nieleze kuhusu kijana ili nikishakupa haya maelezo niweze kukushauri lakini ukajifanya mjuaji"

BM: "Yule kijana kwanza kaishia form 3, katika kumuhoji kanambia hajawahi kufanya hata Biashara ya mtualikua anaishiaga kupata vibarua vya kawaida tu

Caryn: "Too late, hili swali ulitakiwa ulijibu pale pale nilivyokuuliza, kwasababu unaweza kuulizwa swali Dar ukiwa unaelekea Mwanza na usione mantiki kwenye swali uliloulizwa ila ukifika Mwanza sasa ndio akili inakukaa sawa na hapo inakuwa too late, So next time uwe Makini ukiwa unazungumza na Mimi"

BM: "Kwahiyo unanisaidiaje katika hili?"

Caryn: "Cha kukusaidia labda nikupe maelezo ya mwisho ambayo ndio ya umuhimu zaidi, Baba Amesema ukifaulu kwenye huu mtihani basi na wewe utakuwa katika nafasi ya kutaja kiasi chochote cha pesa as mtaji wa kufanyia Biashara

BM: "Caryn! some jokes are too experience, you don't meat it.... right?"

Caryn: "I am serious but don't cheat on this, I know my Dady....have a wonderful night"

Caryn ndio ameenda hivyo, na mazungumzo yakaishia hapo


Nakumbusha huu mtihani nilipewa kabla sijapewa likizo ya lazima, so Wakati nikitafakari vile nitafanya ili kufaulu mtihani wa Mzee ndio stress nyingine ya Ofisini ikaja

Wadau natoboa kweli hapa kwenye Situation zote mbili? TRUE STORY



MWISHO
Carleen unamuona mnyamwezi mwenzio 😅😅😅🔥🔥🔥
 
Kuna episode ulisema ulipokea SMS ya Mzee na Annie asubuhi. Je, unaweza kuscreenshot hizo sms tuzione.

Ukiscreenshot nakuruhusu kucrop ili tusione namba zao ila ukicrop pale kwenye tarehe paache ili tuhakikishe tu kwamba sio za leo..
Mkuu Ile simu ilipotea bhana, tena nilipoteza kizembe sana, nakumbuka hiyo siku nimetoka Zanzibar nikapeleka mizigo store Sasa nahakiki mizigo niyoifikisha niliwasha tochi ya simu nikampa mmoja wa wale waliokuwa wanashusha mizigo animulikie maana umeme ulikatika, Sasa nilivyomaliza nikaondoka zangu nikasahau kuchukua simu, kesho yake namuuliza yule jamaa akakataa kabisa kuwa sijampa simu, akadai eti nitakuwa nimechanga labda niliyempatia nimemsahau

Ila wale vijana paka Leo wapo wote wanapiga kazi hakuna aliyeondoka, ange'miss' mmoja ningemshuku huyo huyo
 
Mkuu Ile simu ilipotea bhana, tena nilipoteza kizembe sana, nakumbuka hiyo siku nimetoka Zanzibar nikapeleka mizigo store Sasa nahakiki mizigo niyoifikisha niliwasha tochi ya simu nikampa mmoja wa wale waliokuwa wanashusha mizigo animulikie maana umeme ulikatika, Sasa nilivyomaliza nikaondoka zangu nikasahau kuchukua simu, kesho yake namuuliza yule jamaa akakataa kabisa kuwa sijampa simu, akadai eti nitakuwa nimechanga labda niliyempatia nimemsahau

Ila wale vijana paka Leo wapo wote wanapiga kazi hakuna aliyeondoka, ange'miss' mmoja ningemshuku huyo huyo
Hahahahahaha sawa mkuu..

Tuendelee na episodes..
 
Hahahahahaha sawa mkuu..

Tuendelee na episodes..
Likizo yangu inaisha August 9, na Mzee sijajua tarehe rasmi ila kuanzia September 20 maana ndio itakua imepita miezi miwili na nusu, Kuanzia hapo kama kutakuwa na jipya tutajuzana mkuu

Ila kwasasa matukio ni ya kawaida hayana changamoto, labda Kijana wa Buguruni alete miyeyusho
 
Kwahiyo Kazini kule nisiwaze sio....haya je ikitokea kama ulivyosema kati ya Annie na Caryn unadhani wapi ni chaguo sahihi?
Hapo ni annie tu, kama huyo caryn ana akili timamu ukimueleza kilichojiri ataelewa.
 
Hakuna upande wa kubaki...

Kwanza umekosea sana kuingiza mapenzi sehemu za kazini, Acha kabisa...
Accountant atakuharibia kazi...

Hivyo huna kazi...

Pili umekuwa umekuwa unapenda vya bure, wewe mtoto wa kiume pambana kwa jasho...

Mzee anakupelekesha tu ka mtumwa...kama anataka kukusaidia mbona masharti...

Pia msaada angetoa yeye mwenyewe kwa hao watoto wa mtaaani...

Anataka kitu kutoka kwako mwishoe utaambiwa uoe mtoto wake...

Mi nafikiri Acha vyote ufanye biashara yako mwenyewe achana na Mzee na Achana na kazi ya mama Accountant
Ushaur gan ni ushauri gan.wewe tulia mpe huyo kijana mtaji wa kufanya biashara ya vitumbua na juis wewe mtafutie baiskel design jiko lake awe anachoma vitumbua pia hapo jipange
 
Hakuna upande wa kubaki...

Kwanza umekosea sana kuingiza mapenzi sehemu za kazini, Acha kabisa...
Accountant atakuharibia kazi...

Hivyo huna kazi...

Pili umekuwa umekuwa unapenda vya bure, wewe mtoto wa kiume pambana kwa jasho...

Mzee anakupelekesha tu ka mtumwa...kama anataka kukusaidia mbona masharti...

Pia msaada angetoa yeye mwenyewe kwa hao watoto wa mtaaani...

Anataka kitu kutoka kwako mwishoe utaambiwa uoe mtoto wake...

Mi nafikiri Acha vyote ufanye biashara yako mwenyewe achana na Mzee na Achana na kazi ya mama Accountant
Duh! Huu ushauri wako kiboko, ila wala sio kupenda vya bure Dada angu, sema unajua nini? Opportunities kama hizo are very rare to find, so if you find them, grab them keep them and handle with care
 
Annie: Okay! i trust you BM, you can go ahead, but remember not everyone in this life gets a second chance to RIGHT their wrongs
[emoji848]Mimi sijaandika hivi mkuu
 
Hapo ni annie tu, kama huyo caryn ana akili timamu ukimueleza kilichojiri ataelewa.
Hata hivyo Caryn mm namuogopa, nishamzoea mnyonge wangu Annie, nikimuambia nyamaza ananyamaza, huyu Caryn tutawezana kweli?
 
Mhh bro hapo kipengele,mzee anakupima hapo sidhan kama kweli mtu unaanza life kwakupanga room ya gharama namna hyo na biashara ya mtaji kama huo....hapo kaka inabidi ufanye mambo katika uhalisia isionekane unaamrishwa cha kufanya fanya kama ambavyo anataka but be realistic.

Kuhusu likizo nadhan hapo inabidi ujiandae kisaikolojia kwamba kazi hamna na mzee itakuwa vyema asipojua...focus na shamba darasa la dogo ila be really[emoji16][emoji16][emoji16]
 
Ni wapi ulisema ana hiyo miaka? Umemwita teenager au maana ya teenager hujui?
Hakumuita teenager, ila alisema dada yake yaan Michelle ndo alimuita hivyo wakat Caren anatoa ushauri wa kuwasaidia hao watoto
 
Maono yangu.

BM X6 una kipaji kizuri cha kutunga hadithi na kuipangilia vizuri. Hakika imeburudisha wengi, japo kwangu haina uhalisia.

1. Hali ya kujiamini kupita kiasi cha bint Caren imenipa wasiwas yeye ni teenager japo wanauwezo alipaswa kuku respect kama kaka yake.

2. Wew una zali gani mpaka upendwe na watoto wa familia bora tu na tena waliozaliwa peke yao kwa wazazi wao?. Mtoto wa bosi wako (Accountant) umesema ni mtoto wa pekee na ni familia bora. Pili mpenzi wako Annie pia umesema ni mtoto wa pekee kwao na walikuwa familia bora sana kiasi cha kuweza kukusaidia baadh ya stuffs ulipokuwa unasoma.

3. Nyumbani kwa mzee ambako ni nyumba ya kisasa, ina maana hakuna mtu yeyote zaidi ya wanafamilia?. Yaan Mzee, mama na na mabint zake wawil?. Ambao kuna muda pia wanakuwa hawapo, kwa maelezo yako wanakuwa Kibaha. Sasa walakini wangu upo katika

a. Suala la ulinzi katika hayo mazingira, japo kuna CCTV lkn pia kuwa kwa mtu wa ziada ni muhimu kwan kuna muda umesema nyumba huwa inabaki bila mtu.

b. Mfanyakazi wa kusaidia usafi wa ndan na nje. Ni ngumu sana kwa familia bora ukute wao ndio wanapiga deki, kufagia uwanja na hata kufyeka majani.

Ni hayo tu mkuu, nakutakia likizo njema[emoji1][emoji1]
Dah mkuu sawa kama huamini lakini mazali yanatokeaga tu mkuu japokuwa Mimi siyachukulii kama ma'zali'

Kuhusu Dada wa kazi yupo yule wa kuja na kuondoka na haendi Kila siku

Mlinzi pia Sasa hivi ameshawekwa ila mwanzo alikuwa hayupo, unajua na nyumba yenyewe ni mpya mpya sio ya kitambo, kama unakumbuka katika story nilielezea kwamba Mzee anajenga nyumba ya mlinzi pembeni ya Geti, so alifanikisha Hilo kabla ya kusafiri
 
BM X6 wewe ni kijana mdogo sana bila shaka na pia ni rika la vijana wa kileo , najua una ndoto ndugu na unahitaji kuzifikia kabla haujaswaliwa au haujazikwa, sasa ndugu BM X6 ipo hivi÷

Kama ujuavyo kwa kimalikia wahenga wanasema GOLDEN CHANCE NEVER COME TWICE , ila pia binadamu hubadilika si Annie wala accountant sasa jitizame wewe ni wapi umetoka kimaisha na kimaadili alafu waza ni kipi unahitaji mbele

Annie ni mwanamke wa moyo wako na maisha yako ila accountant n passer girl kama wale wengine uliolala nao hivyo

Annie hata umsaliti leo ila ataendelea kuwepo kama ni mipango ya yule Mungu unayemuabudu ila kama si mipango yake hatakuelewa na mtaishia hapo

Sasa ni hivi nenda kamvishe pete Accountant ili ule shavu ila kumbuka kujiwekeza mpaka pale utapoona sasa unaweza kujisimamia bila kampuni huku binti kimwali Annie mueleze uhalisia akupe muda kama ni miaka miwili hata saba sawa ili ukamilishe mission yako

Akikubali akikataa ni non of your bussiness ili ufikie kwenye ndoto zako kwanza , usiseme ni dhambi kwani umefanya mangapi mpaka sasa ambayo mengine hata kuyasema huwezi na usisaha hautakuwa wa kwanza kupambania ndoto zako kwa ubaya ilimradi ufike pale unapoota .

Sasa huyo kijana wa buguruni , ndipo penye sehemu ya kukusaidia wewe na Annie mdumu au muachane kwanini ?
Sababu ikiwa huko utafanikisha basi hata kazi waweza kuacha ili ufanye mambo yako na binti kimwali Annie .

Nenda sehemu za stand either makumbusho au mbagala zakiem au keko karibu na kituo cha polisi omba nafasi fungua duka lenye atleast wa mtaji wa milioni tano na huduma za m_pesa na huduma za kibenki hasa za miamala na pia uza vinywaji hapo vya kila namna , hii itakufanya hata kwa siku asikose hata elfu sabini kwa siku .

Ila kaa kitako na huyo kijana muombe awe msiri kwa mzee hiyo biashara ifanye yako ila yeye ndiye msimamizi ila baada ya miezi sita utamkabidhi , ndugu BM X6 hakikisha hiyo biashara unaisimamia vizuri mauzo na kila kiingiacho na kitokacho ila usisahau kijana ana wadogo zake hivyo wanahitaji huduma pia

Ndugu yangu poteza kidogo upate kikubwa hivyo jitahidi sana uwe unatoa kidogo katika kale kamshahara kako ili uwatunze wale watoto pasipo kujali kwenye biashara uliyofungua ukizingatia nahisi kapochi kako katanona baada ya kupanda cheo hapo kwa mama mkwe [emoji1787][emoji1787].

Mwisho ni kuwa hakikisha faida ya kipindi chote cha miezi sita aliyotoa mzee , hakikisha unaitunza kwa account ili baada ya miezi sita iwe ni starting point ya KIJANA WA BUGURUNI ili aishi vyema

Kaka kama ukifeli katika biashara hiyo basi nenda chuo chochote ila nakushauri vyuo vifuatavyo DUCE , NIT NA UHASIBU mara nyingi tenda za wauza vyakula(wazabuni) maeneo hayo uwa hazidumu sababu ya usimamizi mbovu hivyo kushindwa kulipa kodi kwa vyuo husika .

Sasa nenda mtafute muhusika mpoze kidogo akupe tender kwenye hiko chuo utachopata na hapo tayari utatakiwa kuwatafuta wapishi ambao ni akina mama ila hakikisha kijana wa buguruni awe ni msimamizi wa mwisho katika hiyo biashara na kipindi ambacho wewe haupo ila faida na expenses za hiyo biashara zote zipite kwako .

Nakuona unaniuliza mbona vyuo vinaenda kufunga sasa , hapana BM X6 nimekutajia vyuo ambavyo the whol3 year wanafunzi wapo sababu hawatoi degree tu ila hata certificate na diploma hivyo kujikuta mwaka mzima wapo wanafunzi around hayo maeneo

Ndugu kwa haya nakuona ukipewa hiyo hela ya biashara na kuanza mambo yako na kumrudia binti kimwali Annie kwa kumpa talaka takatifu ndugu ACCOUNTANT .

Japo katika biashara hiyo ya vyakula hakikisha mzee akupe angalau milioni kumi ya kufanya biashara ila usisahau kuwa systematic katika kila jambo ili hata mzee asikuwaze vibaya kuwa muwazi na ukiamua kumpiga mpige kisomi au sio ndugu yangu Mtanzania ? (In magufuli's voice)
USIOGOPE KUFANYA LOLOTE SABABU MPAKA SASA NI MENGI YA DHAMBI UMEFANYA HIVYO TENDA KADRI YA MOYO NA HULKA ILI UIONE KESHO ANGAVU

Ushauri tu ndugu yangu BM X6

TEKERI.
 
BM X6 wewe ni kijana mdogo sana bila shaka na pia ni rika la vijana wa kileo , najua una ndoto ndugu na unahitaji kuzifikia kabla haujaswaliwa au haujazikwa, sasa ndugu BM X6 ipo hivi÷

Kama ujuavyo kwa kimalikia wahenga wanasema GOLDEN CHANCE NEVER COME TWICE , ila pia binadamu hubadilika si Annie wala accountant sasa jitizame wewe ni wapi umetoka kimaisha na kimaadili alafu waza ni kipi unahitaji mbele

Annie ni mwanamke wa moyo wako na maisha yako ila accountant n passer girl kama wale wengine uliolala nao hivyo

Annie hata umsaliti leo ila ataendelea kuwepo kama ni mipango ya yule Mungu unayemuabudu ila kama si mipango yake hatakuelewa na mtaishia hapo

Sasa ni hivi nenda kamvishe pete Accountant ili ule shavu ila kumbuka kujiwekeza mpaka pale utapoona sasa unaweza kujisimamia bila kampuni huku binti kimwali Annie mueleze uhalisia akupe muda kama ni miaka miwili hata saba sawa ili ukamilishe mission yako

Akikubali akikataa ni non of your bussiness ili ufikie kwenye ndoto zako kwanza , usiseme ni dhambi kwani umefanya mangapi mpaka sasa ambayo mengine hata kuyasema huwezi na usisaha hautakuwa wa kwanza kupambania ndoto zako kwa ubaya ilimradi ufike pale unapoota .

Sasa huyo kijana wa buguruni , ndipo penye sehemu ya kukusaidia wewe na Annie mdumu au muachane kwanini ?
Sababu ikiwa huko utafanikisha basi hata kazi waweza kuacha ili ufanye mambo yako na binti kimwali Annie .

Nenda sehemu za stand either makumbusho au mbagala zakiem au keko karibu na kituo cha polisi omba nafasi fungua duka lenye atleast wa mtaji wa milioni tano na huduma za m_pesa na huduma za kibenki hasa za miamala na pia uza vinywaji hapo vya kila namna , hii itakufanya hata kwa siku asikose hata elfu sabini kwa siku .

Ila kaa kitako na huyo kijana muombe awe msiri kwa mzee hiyo biashara ifanye yako ila yeye ndiye msimamizi ila baada ya miezi sita utamkabidhi , ndugu BM X6 hakikisha hiyo biashara unaisimamia vizuri mauzo na kila kiingiacho na kitokacho ila usisahau kijana ana wadogo zake hivyo wanahitaji huduma pia

Ndugu yangu poteza kidogo upate kikubwa hivyo jitahidi sana uwe unatoa kidogo katika kale kamshahara kako ili uwatunze wale watoto pasipo kujali kwenye biashara uliyofungua ukizingatia nahisi kapochi kako katanona baada ya kupanda cheo hapo kwa mama mkwe [emoji1787][emoji1787].

Mwisho ni kuwa hakikisha faida ya kipindi chote cha miezi sita aliyotoa mzee , hakikisha unaitunza kwa account ili baada ya miezi sita iwe ni starting point ya KIJANA WA BUGURUNI ili aishi vyema

Kaka kama ukifeli katika biashara hiyo basi nenda chuo chochote ila nakushauri vyuo vifuatavyo DUCE , NIT NA UHASIBU mara nyingi tenda za wauza vyakula(wazabuni) maeneo hayo uwa hazidumu sababu ya usimamizi mbovu hivyo kushindwa kulipa kodi kwa vyuo husika .

Sasa nenda mtafute muhusika mpoze kidogo akupe tender kwenye hiko chuo utachopata na hapo tayari utatakiwa kuwatafuta wapishi ambao ni akina mama ila hakikisha kijana wa buguruni awe ni msimamizi wa mwisho katika hiyo biashara na kipindi ambacho wewe haupo ila faida na expenses za hiyo biashara zote zipite kwako .

Nakuona unaniuliza mbona vyuo vinaenda kufunga sasa , hapana BM X6 nimekutajia vyuo ambavyo the whol3 year wanafunzi wapo sababu hawatoi degree tu ila hata certificate na diploma hivyo kujikuta mwaka mzima wapo wanafunzi around hayo maeneo

Ndugu kwa haya nakuona ukipewa hiyo hela ya biashara na kuanza mambo yako na kumrudia binti kimwali Annie kwa kumpa talaka takatifu ndugu ACCOUNTANT .

Japo katika biashara hiyo ya vyakula hakikisha mzee akupe angalau milioni kumi ya kufanya biashara ila usisahau kuwa systematic katika kila jambo ili hata mzee asikuwaze vibaya kuwa muwazi na ukiamua kumpiga mpige kisomi au sio ndugu yangu Mtanzania ? (In magufuli's voice)
USIOGOPE KUFANYA LOLOTE SABABU MPAKA SASA NI MENGI YA DHAMBI UMEFANYA HIVYO TENDA KADRI YA MOYO NA HULKA ILI UIONE KESHO ANGAVU

Ushauri tu ndugu yangu BM X6

TEKERI.
Blaza huu ushauri wako ni konki sana[emoji1544], nimeusoma wote ila kwa heshima zaidi naomba niusome tena badae kwa utulivu kabisa ili kama Kuna Cha kukuuliza nikuulize mapema[emoji1545]
 
Back
Top Bottom