Hatma ya Muslim University of Morogoro na Maono ya Aga Khan kuwasaidia Waislamu kujenga Chuo Kikuu

Hatma ya Muslim University of Morogoro na Maono ya Aga Khan kuwasaidia Waislamu kujenga Chuo Kikuu

Kwenye maisha jamii ikijijengea kulalamika wakati woooote kuwa wako hivyo walivyo kwa kuwa walifanyiwa hivi au vile basi jamii hii kamwe haiwezi songa mbele na ndiyo maana waafrika watabaki kuwa nyuma maana miaka nenda rudi huona hawakufanikiwa sababu ya wakoloni. Ndiyo maana black americans wako nyuma ya chinese, indians, latinos, na wengine maana wao daily hulalamikia kuwa wako nyuma maana wamefanyiwa sana madhila na wazungu hawataki kuona fursa. Waislamu dizain ya mzee huyu hawataki kuona fursa zilizopo/zijazo but wataendelea kulalamika miaka nenda rudi kuwa walifanyiwa madhila/dhuluma ndo maana wapo hivyo walivyo. Nyerere hulalamikiwa sana na waislam cha ajabu Nyerere kaondoka na ametangulia mbele ya haki wamekuja marais sasa tupo wa tano wao (waislamu 3) bado wanalalamika tu! Zanzibar ina wengi waislamu na inaongozwa na waislamu na wala haina maendeleo hayo! Yaani kwa kifupi siku zooooote jamii hii itatafuta pa kutupia lawama kamwe hawataki kuona makosa/udhaifu wao na kujirekebisha. Hawa hata wakisaidiwa vipi bado watalalamika tu! hawataki kufungua shule/vyuo vingi vilivyo bora na hakuna aliyewakataza lakini watasema mfumo kristo unawazuia wataleta historia ya naintin kweusi kuwa walizuiwa kufanya hivi/kufanya vile historia ambayo kamwe haiwasaidii chochote kwa sasa, maana hata wahenga walisema yaliyopita si ndwele aisee hii jamii ni shida sana.
Nilitarajia Zanzibar wangekua na shule kubwa,chuo kikuu cha kuweza kushindana na UDSM. Maajabu watoto wa matajiri unawakuta ST Francis,Marian girls nk. FEZA ni ya shia muslims toka Uturuki na inafanya vizuri sana kwa sababu elimu ya dini haijapewa kipaumbele.
 
Mzee Mohamed Said
Nini kinazuia sasa kwa waislamu kujenga vyuo vikuu
Kwa nini misaada ya Qatar, au UAE isiwe ya kuomba kujenga vyuo vikuu na mashule na mahospitali?
Hawa waarabu wanahela za kumwaga sana, na wanaweza kufanya hivyo,
Je serikali itazuia pia hivyo?

Hivi vyuo vya kikristo SAUT na sijui TEKU, ni vya juzi juzi tu, kwa nini pia waislamu wasijenge vyao?
Gamma...
Misri ilitoa fedha kwa EAMWS kujenga Chuo Kikuu mwaka wa 1968.
EAMWS ikapigwa marufuku na serikali wakati inataka kujenga hicho chuo.

Katika miaka ya 1970 OIC walitaka kujenga Chuo Kikuu Tanzania serikali ikawakatalia kuwapa kibali.

Mwaka wa 1997 Darul Imaan ya Saudia ilitaka kujenga Shule ya Ufundi Kibaha ghafla magazwti yote yakaja na kampeni kuwa Waarabu wamevamia Kibaha wanapora ardhi za wananchi.

Darul Imaan ikasitisha mradi ikaondoka.

Haya mswali mnaniluliza mara nyingi na ninakupeni majibu lakini nitauliza tena swali hili hili.

Inakuwaje?

Hamuelewi ukweli au hamuamini kuwa serikali inazuia ujenzi wa taasisi za elimu kwa Waislam?
 
Chuo kilichojengwa Uganda kinaitwaje Mzee wangu? Kimeweza kukuza elimu ya waislam kule Uganda,kimekua kikubwa hata kukaribia level ya Makerere university?
Ipyas,
Sina taartifa zaidi ya chuo hiki.
 
Nilitarajia Zanzibar wangekua na shule kubwa,chuo kikuu cha kuweza kushindana na UDSM. Maajabu watoto wa matajiri unawakuta ST Francis,Marian girls nk. FEZA ni ya shia muslims toka Uturuki na inafanya vizuri sana kwa sababu elimu ya dini haijapewa kipaumbele.
hawa hawakuwekeza katika elimu vyakutosha ni ukweli ambao hawataki kuukiri na lawama daily hutaka kuwatupia wakristo. Sure Zanzibar ingetakiwa iwe na maendeleo ya kutisha maana wapo wenyewe na wana nasaba na waarab lakini ndo kwanza wapo hapa walipo! utakuta wanasema ohh hospital za kikristo zinapewa ruzuku na serikali na kuna MOU utafikiri wao wamekatazwa kuanzisha hospitali, basi ingekuwa hata wanayo moja ya mfano hapo Znz maana wapo wenyewe lakini napo hola!
 
Leo tuna Afghanistan ambako mabinti wa kiislamu hawaruhusiwi kwenda shule, Tanzania jamii ya kiislam haiwekezi kwenye elimu . Saudia kama centre ya uislamu na tajiri namba 1 inawekeza kwenye ujenzi wa misikiti madrassa tu ulimwenguni.
Ipyax,
Tofauti kubwa ambayo naiona katika maswali ninayoulizwa hapa na maswali ninayoulizwa na wanafunzi wa Ph D kutoka nje ya Tanzania wanaokuja kwangu kwa utafiti ni kuwa hawa kutoka nje nikishaeleza hali hii kwanza hutaka uthibitisho wa taarifa nilizotoa.

Wakishapata uthibitisho huniambia kuwa kama wanaweza kunukuu mazungumzo yetu kwa watu wengine ambao watakwenda kwao kuwahoji.

Mwisho husema kuwa hili ni jambo kubwa sana kuwa serikali yenyewe ndiyo inahujumu juhudi za sehemu moja ya raia wake kuelimika.

Huwa hawaelewi kwa nini serikali ivunje taasisi ya dini moja na kuacha taasisi za dini nyingine.

Huwa tunamaliza mazungumzo yetu wakiwa wamelowa kabisa pale ninapowaeleza kuwa serikali ina hofu ya kujadili hili tatizo na Waislam na limeamua kuwa kimya wakitegemea kuwa litajiondoa lenyewe.

Huwaonyesha majibu na mswali nipatayo hapa JF na wao hutaka kujua uelewa wa hawa waulizaji.

(Ndiyo haya mswali mnayouliza hapa ya Saudia na Afghanistan wakati tunajadili matatizo ya Tanganyika).

Jibu langu huwa hawa ndiyo kwanza wanasoma haya kutoka kwangu hawana uelewa wowote.
 
Misri ilitoa fedha kwa EAMWS kujenga Chuo Kikuu mwaka wa 1968.
EAMWS ikapigwa marufuku na serikali wakati inataka kujenga hicho chuo.

Katika miaka ya 1970 OIC walitaka kujenga Chuo Kikuu Tanzania serikali ikawakatalia kuwapa kibali
Katika kipindi hiki, sitashangaa kwa sababu Bugando na KCMC zilitaifishwa na kuwa chini ya serikali, na pia shule nyingi kama Tosamaganga na nyinginezo zilikuwa za dini pia zilitaifishwa, kwa hiyo kipindi baada ya uhuru hakitakiwi kuwa refefence.

Mwaka wa 1997 Darul Imaan ya Saudia ilitaka kujenga Shule ya Ufundi Kibaha ghafla magazwti yote yakaja na kampeni kuwa Waarabu wamevamia Kibaha wanapora ardhi za wananchi.
Kwa kweli hatutaki chuo cha ufundi, kwanini isiwe University, mbona tuna Al Maktoum college of Engineering and Technology? mbona hiki hakijaziuwa?

Naamini aidha hatujui kujipanga na kuongea na nchi wafadhili kutujengea vyuo vikuu na mashule, kwa sababu ya uongozi wa BAKWATA umejaa watu walioweka mbele elimu ya dini ndio maana wanaomba ufadhili wa kujengewa misikitu tu...
 
Stux...
Wa kutoa majibu wamekuwa kimya hata pale tatizo hili lilipoletwa Bungeni.

Wewe unajibu kama nani?
Sisi tunasubiri majibu kutoka serikalini.
mbona misikiti mnachangishana,kwanini msichangishane kujenga vyuo vikuu?utalia lia hivi mpaka lini wakati Nyerere alishafiki?
Samia mvaa kobazi mwenzio peleka proposal wacha kulia kwenye vijiwe vya kahawa mwinyimkuu,suna,butiama nk.
 
Tuanze hapa tulipo hivi sasa kisha nitaweka tulipotokea baada ya uhuru:

TUJIKUMBUSHE

Waislam wa Tanzania na Tatizo la Udini Katika Wizara ya Elimu.

Ndugu Waziri,
Kwa muda mrefu sasa, kumekuwa na maswali mengi wakijiuliza Waislamu, moja likiwa inakuwaje katika maeneo yenye Waislamu wengi ambapo idadi ya wanafunzi Waislamu inakuwa zaidi ya asilimia 70, lakini wanapochaguliwa kwenda sekondari, idadi ya watoto wa Kiislamu huporomoka na kuwa chini ya asilimia 20.

Swali na kitendawili hiki kimekuwepo kwa muda mrefu bila kupatiwa majibu.

Hata lilipofikishwa Bungeni mwaka 1999 na aliyekuwa Mbunge wa Kigamboni, Mzee Kitwana Selemani Kondo, bado halikupatiwa jibu.

Akihoji juu hali hiyo, Mzee Kitwana Kondo alitoa mfano jinsi hali ilivyokuwa katika shule ya Pembamnazi iliyokuwa na Waislamu watupu na kwa miaka mingi mfululizo kulikuwa hakuna hata mtoto mmoja aliyekuwa akichaguliwa kwenda sekondari kutoka katika shule hiyo.

Aidha alisema kuwa, katika mkoa wa Dar es Salaam na Pwani, takwimu zinaonyesha kuwa idadi ya watoto wa Kiislamu katika shule za msingi ilikuwa zaidi ya asilimia 70 lakini inapokuja kuchaguliwa kwenda sekondari, idadi ya Waislamu iliporomoka na kuwa chini ya asilimia 20.

Akizungumza Bungeni tarehe 2 Februari, 1999 alisema kuwa katika watoto waliofanya mtihani wa darasa la saba mwaka 1998, idadi ya Waislamu ilikuwa asilimia 71 na Wakristo 29%. Hata hivyo akasema, ilipotoka orodha ya waliochaguliwa kwenda sekondari, idadi ya Wakristo ikawa asilimia 79 (79%) na Waislamu 21%.

Je, hiyo ilikuwa na maana kuwa watoto wa Kiislamu kwa asili yao hawana akili?

Alitaka kujua Mzee Kitwana Kondo. Lakini hakuweza kupata jibu.

Mheshimiwa Waziri,
Ni wazi kuwa Waziri wa Elimu au Waziri Mkuu ambaye ndiye msimamizi wa mambo ya serikali Bungeni asingeweza kutoa majibu ya uhakika kwa sababu swali lilihitaji kufanyika uchunguzi huru wa kina na makini kwanza.

Mheshimiwa Waziri,
Mwaka 1987 aliyekuwa Waziri wa Elimu, Profesa Kighoma Ali Malima, aliweka utaratibu mpya wa ufanyaji wa mtihani wa darasa la saba ambapo namba zilitumika toka kufanya mtihani, kusahihisha na kuchagua wanafunzi wa kwenda kidato cha kwanza.

Namba zilivishwa majina baada ya taratibu zote hizo kukamilika. Mwaka huo idadi ya watoto wa Kiislamu waliokwenda kidato cha kwanza iliongezeka kwa asilimia 40 ikilinganishwa na miaka ya nyuma.

Hata hivyo, mara aliondolewa Waziri Malima katika wizara hiyo na utaratibu wa zamani ukarejeshwa ambapo yalikuwa yakichaguliwa majina na idadi ya Waislamu ikaporomoka na kurudi chini ya asilimia 20.

Mheshimiwa Waziri,
Hali kama hii hapana shaka inazua maswali mengi ambayo yanahitaji majibu na majibu hayo hayawezi kupatikana bila ya kufanyika uchunguzi.

Labda tuongeze mifano ili kuliweka wazi zaidi jambo hili.

Mwaka 1983 mwanafunzi aliyekuwa akiitwa Kopa Abdallah akisoma katika shule ya msingi Kichangani, Kilosa, alikosa kuchaguliwa kwenda sekondari.

Yeye binafsi, wazazi wake na hata walimu wake hawakuamini matokeo yale kutokana na alivyokuwa akifanya vizuri kuliko wanafunzi wote.

Baadae ilikuja kugundulika kuwa nafasi yake alipewa mwanafunzi aliyekuwa akiitwa Antoni Samirani ambaye alikuwa na uwezo mdogo sana ikilinganiswa na Abdallah.

Kilichofanyika ni kuwa jina la Abdallah lilifichwa na baadae Antoni akapewa jina hilo kimya kimya na kwenda kusoma sekondari akitumia jina Abdallah wakati yeye ni Antoni.

Taarifa zinasema kuwa Kopa Abdallah alipogundua hakuweza kufanya kitu akaishia kuwa dereva.

Hali kama hiyo ilimkuta pia Adam Ramadhani aliyekuwa akisoma shule ya msingi Rutihinda jijini Dar es Salaam na kumaliza darasa la saba mwaka 1999. Yalipotoka matokeo ya mtihani wa darasa la saba na kuonekana kuwa Adam hakuchaguliwa, baba yake hakuamini kuwa mtoto wake anaweza kufeli kutokana na uwezo aliokuwa nao na zaidi akitizama walivyochaguliwa watoto ambao Adam alikuwa mwalimu wao shuleni na mitaani.

Katika kufuatilia suala hilo wizarani, ilikuwa aibu kwa wizara baada ya kuonekana kuwa walichaguliwa watoto wa Kikristo wenye alama za chini kabisa huku akiachwa Adam Ramadhani aliyekuwa na alama za juu kuliko wote.

Mheshimiwa Waziri,
Mifano kama hii ni mingi mno na ipo katika ngazi zote kwa maana kutoka elimu ya msingi kwenda sekondari, kutoka kidato cha nne kwenda kidato cha tano na kutoka kidato cha sita kwenda Chuo Kikuu.

Kwamba hata kutoka kidato cha nne kwenda kidato cha tano, wapo watu waliopata kushuhudia majina ya wanafunzi wa Kiislamu yakiwekwa pembeni japo walikuwa na sifa za kuchaguliwa.

Mheshimiwa Waziri,
Ukiacha hujuma katika kuwaacha wanafunzi Waislamu wenye sifa kuendelea na masomo, matatizo huanzia kwenye kuamua nani amefaulu na nani kafeli.

Tuhuma zilizopo ni kuwa wapo wanafunzi wanapewa madaraja ya juu wakati alama zao ni za chini na wapo wanaopewa madaraja ya chini wakati alama zao ni za juu.

Na hii ni kwa masomo yote.

Mheshimiwa Waziri,
Kumekuwa na utamaduni katika nchi hii wa kukataa ukweli.

Kufuatia uchunguzi uliofanywa na Kamati za Bunge, tumeshuhudia wizi na ufisadi wa kutisha ukifichuliwa Bungeni hivi karibuni hali iliyopelekea mpaka Mheshimiwa Rais kubadili Baraza lake la Mawaziri.

Sasa baada ya kuyasema yote hayo, tunasema kuwa Baraza la Mitihani la Tanzania, limekuwa likilalamikiwa kwa zaidi ya miaka 30, lakini malalamiko hayo yamekuwa yakipokewa kwa sikio la uziwi.

Imefikia mahali tunasema kuwa hatuna tena imani na Baraza hilo.

Mheshimiwa Waziri,
Ili kupata ukweli wa malalamiko na shutuma hizi, na ili kujibu lile swali juu ya watoto wa Kiislamu ambalo halikupata jibu Bungeni, tunaitaka serikali kufanya yafuatayo:

1. Tume huru iundwe kuchunguza Baraza la Mitihani la Tanzania na utendaji wake kazi kwa kipindi cha miaka kumi iliyopita.

2. Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani (NECTA) ajiuzulu mara moja ili kulinda heshima ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzaani na Baraza la Mitihani.

Watendaji wakuu wa kitengo cha mitihani na wanaohusika na mfumo wa Kumputa ya Baraza la Mitihani nao wawajibishwe mara moja.

3. Hatua za kisheria na kibinadamu zichukuliwe dhidi ya watumishi wa Baraza la Mitihani watakaothibitika kuhusika na kashfa hii.

4. Muundo wa Baraza la Mitihani uzingatie uwiano wa kidini, kitendo cha chombo nyeti kama hiki kujazana watu wa dini moja kunaliondolea Baraza la Mitihani sura ya kitaifa, kwani takwimu zinaonyesha Makatibu Wakuu Watendaji na Manaibu Katibu Wakuu wamekuwa Wakristo na Wenyeviti wa Baraza hilo ni Wakristo tangu lilipoanzishwa mwaka 1973, mpaka hii leo na takwimu tunazo.

Mheshimiwa Waziri,
Tunaomba ieleweke kuwa tunachotaka ni kupatikana haki na kufanyika uadilifu kwa watu wote.

Hatudai wala hatutaki upendeleo kwa Waislamu na wala hatutaki kuona mtu yeyote anaonewa au kuporwa haki yake, awe Mwislamu au mtu wa dini nyingine.

Tunachoamini ni kuwa kama Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi haina cha kuficha, basi itaunda Tume hiyo kwa haraka na kuhakikisha kuwa ni Tume ya kuaminika itakayofanya kazi yake kwa umakini, kwa kina na kwa uadilifu wa hali ya juu kabisa.

Lakini kama Wizara yako itaona kuwa haiwezi kuunda Tume ya uchunguzi, tunacho kuhakikishia ni kuwa sisi tutafanya kila liwezekanalo na kwa namna yoyote kuhakikisha kuwa Tume hiyo inaundwa.

Na ikigundulika kuwa kuna hujuma zinafanyika katika utendaji wa Baraza, basi itabidi uwajibikaji uanze kwenye Wizara kabla ya kuwawajibisha watendaji wa Baraza la Mitihani.

Ni imani yetu kuwa utayapokea madai ya Waislamu na kuyafanyia kazi kwa umakini na kwa haraka ili kujenga mustakbali mwema wa nchi hii na watu wake.

Tunaomba kuwasilisha,

Mwenyekiti,
Baraza Kuu la Jumuiya na Taasisi za Kiislamu

Sasa turudi nyuma wakati tumepata uhuru:


Ipyax,
Yametokea.
Serikali haiko tayari kutoa majibu.

Nina mengi naweza kukueleza muhimu ni wewe uwe tayari kusikiliza.

Marais Waislam hawakuchaguliwa kuchunguza watendaji Wakristo ndani ya serikali wana mchango gani katika matatizo haya yanayoelezwa na Waislam.

Endapo Rais Muislam ataingia madarakani na kuanza kuchunguza tatizo hili atakuwa anatengeneza tatizo kubwa zaidi linaloweza kuigawa nchi zaidi.

Hili la Waislam kuwekeza katika elimu hapa si mahali pake ila ningependa kukufahamisha kuwa baada ya kupatikana uhuru mwaka wa 1961 Mufti Sheikh Hassan bin Ameir alijiuzulu siasa na kuanzisha taasisi yake, "Daawat Islamiyya," yeye akiwa Mwenyekiti na Katibu wake Schneider Abdillah Plantan.

Sheikh Hassan bin Ameir akasema sababu ya yeye kujiuzulu siasa ni kuwaongoza Waislam katika kutafuta elimu kama alivyowaongoza katika kupigania uhuru wa Tanganyika.

(Naamini inawezekana historia hii ninayokueleza ikakupa tabu kwani hujapata kuisoma popote kuwa Mufti wa Tanganyika Sheikh Hassan bin Ameir alikuwa mwanachama wa TANU na kapigania uhuru.

Schneider Plantan yeye ndiye aliyesimama mwaka wa 1950 kuutoa uongozi wa wazee katika TAA Rais ambae ni kaka yake, Thomas Plantan na Katibu Clement Mohamed Mtamila na kuingiza uongozi wa vijana Dr. Vedasto Kyaruzi kama President na Abdul Sykes Katibu).

Mwaka wa 1962 Sheikh Hassan bin Ameir akishirikiana na EAMWS wakaitisha Muslim Congress agenda kuu ikiwa elimu.

Hii Muislam Congress ndiyo iliyoweka mpango wa kujenga shule Tanganyika nzima na Chuo Kikuu na kazi ilianza mara moja.

Mwaka wa 1968 Rais Julius Nyerere akaweka jiwe la msingi kujenga Chuo Kikuu.

Miezi miezi michache baadae Rais Nyerere akaivunja EAMWS na kuunda BAKWATA.

Uwekezaji wa Waislam katika elimu na ujenzi wa Chuo Kikuu na shule ukakoma hapo.

Historia hii ni ndefu lakini naamini nimekujibu swali lako na umeelewa matatizo yanayowakabili Waislam.
wewe mzee unazeeka vibaya
hawa wote waislam rais,waziri mkuu,jaji mkuu,katibu mkuu necta,usalama nk lakini babu jojo kila uchwao unalia lia ...unataka hii nchi yote mpewe nyinyi mjenge misikiti na iongozwe kigaidi kama taliban?
 
Ipyax,
Tofauti kubwa ambayo naiona katika maswali ninayoulizwa hapa na maswali ninayoulizwa na wanafunzi wa Ph D kutoka nje ya Tanzania wanaokuja kwangu kwa utafiti ni kuwa hawa kutoka nje nikishaeleza hali hii kwanza hutaka uthibitisho wa taarifa nilizotoa.

Wakishapata uthibitisho huniambia kuwa kama wanaweza kunukuu mazungumzo yetu kwa watu wengine ambao watakwenda kwao kuwahoji.

Mwisho husema kuwa hili ni jambo kubwa sana kuwa serikali yenyewe ndiyo inahujumu juhudi za sehemu moja ya raia wake kuelimika.

Huwa hawaelewi kwa nini serikali ivunje taasisi ya dini moja na kuacha taasisi za dini nyingine.

Huwa tunamaliza mazungumzo yetu wakiwa wamelowa kabisa pale ninapowaeleza kuwa serikali ina hofu ya kujadili hili tatizo na Waislam na limeamua kuwa kimya wakitegemea kuwa litajiondoa lenyewe.

Huwaonyesha majibu na mswali nipatayo hapa JF na wao hutaka kujua uelewa wa hawa waulizaji.

(Ndiyo haya mswali mnayouliza hapa ya Saudia na Afghanistan wakati tunajadili matatizo ya Tanganyika).

Jibu langu huwa hawa ndiyo kwanza wanasoma haya kutoka kwangu hawana uelewa wowote.
Mohamed Said
Umesema kuna wanafunzi wa PHD kutoka nje ya nchi huja kwako kwa utafiti, hebu tuwekee hapa ushahidi wa kuwa wamekuwa wakikubaliana na kuthibitisha kiutafiti maneno yako kwenye tafiti zao ya kuwa;
serikali inavunja taasisi ya dini moja na kuacha taasisi za dini nyingine.
 
Huyo mzee anajivika uanaharakati wa dini wakati yeye kasoma na Rafiki zake wengi wasomi.
Kwa exposure aliyonayo na network aliyonayo angeweza kabisa hata kuanzisha shule ya mfano au hata hospital ya mfano. Ila kila siku yuko hapa kutumbia kitabu chake cha sykes kipo toleo la ngapi sijui na story za Mtendeni
 
Mpaji Mungu,
Takataka ni yapi?

Ni hii makala niliyoeleza Muslim Congress ya 1962 iliyoamua kujenga shule na Chuo Kikuu chini ya EAMWS au barua kwa Waziri wa Elimu inayoeleza tatizo la udini ndani ya wizara hiyo?

Ningependa kujua.
1962,mwaka 1970,1980?,1990?,2000? na sasa 2023 mmefanya nini kujenga shule na vyuo zaidi kuomba kanzu kwa mashia na tende na mikeka ya kuswalia.Unakuja hapa kulia lia tu.Utakufa kihoro we mzee.
 
Kipindi cha Ali Hassan Mwinyi, Aga Khan alikuja nchini kwa mara ya kwanza baada ya kutokanyaga ardhi ya Tanzania kwa miaka 20. Kwa maneno ya Mohamed Said Aga Khan aliitisha mkutano wa Waislamu ambao una mchanganyiko wa BAKWATA na wawakilishi wa iliyokuwa EAMWS. Na kwenye mkutano huo HAKUKUWA na MKRISTU hata mmoja. Yasemekana Songambele alisema Waislamu hawahitaji Chuo Kikuu.

Mwaka 2000 wakati wa B W Mkapa, akaamua kuwapa jamii ya Waislamu kilichokuwa Chuo cha TANESCO pale Morogoro.

Je ni Waislamu wangapi wenye passmark za juu za A- Level wanadahiliwa pale Morogoro dhidi ya Waislamu wanaochagua kwenda vyuo visivyo na itikadi ya dini kama UDSM, Mzumbe, SUA, SAUT na MUHAS?


Mumeshindwa kujua mnchotaka, bado Mohamed Said unawalaumu JK Nyerere na WAKRISTU kuhusu elimu.

Mzee yule ni loser na anawadanganya watu wasiotaka kuukabili ukweli. Nyerere ametoka madarakani 1985 nikiwa darasa la pili. Leo hii unamlaumu kwa lipi wakati wamekuja watu wengi na majanga wameyaleta mengi kuliko hata Nyerere? Kumkabili Nyerere ni project binafsi ya yule Mzee. Uzuri ni kuwa njia ya muongo ni fupi.
Muda unaenda na mambo mengi yanajieleza bila kusubiri mutu muongo kuyasimulia.
 
hawa hawakuwekeza katika elimu vyakutosha ni ukweli ambao hawataki kuukiri na lawama daily hutaka kuwatupia wakristo. Sure Zanzibar ingetakiwa iwe na maendeleo ya kutisha maana wapo wenyewe na wana nasaba na waarab lakini ndo kwanza wapo hapa walipo! utakuta wanasema ohh hospital za kikristo zinapewa ruzuku na serikali na kuna MOU utafikiri wao wamekatazwa kuanzisha hospitali, basi ingekuwa hata wanayo moja ya mfano hapo Znz maana wapo wenyewe lakini napo hola!

1962,mwaka 1970,1980?,1990?,2000? na sasa 2023 mmefanya nini kujenga shule na vyuo zaidi kuomba kanzu kwa mashia na tende na mikeka ya kuswalia.Unakuja hapa kulia lia tu.Utakufa kihoro we mzee.
Luku...
Ahsante nimekusoma.
 
Kwa exposure aliyonayo na network aliyonayo angeweza kabisa hata kuanzisha shule ya mfano au hata hospital ya mfano. Ila kila siku yuko hapa kutumbia kitabu chake cha sykes kipo toleo la ngapi sijui na story za Mtendeni
Kinyungu,
Nakueleza kuwa kitabu kinakwenda toleo la tano kukufahamisha kuwa kitabu kimependwa kwa ukweli ulioko ndani yake.

Ikiwa hili linakuudhi ni bahato mbaya sikukusudia hilo.

1704912363838.jpeg

1704912467627.png
 
1962,mwaka 1970,1980?,1990?,2000? na sasa 2023 mmefanya nini kujenga shule na vyuo zaidi kuomba kanzu kwa mashia na tende na mikeka ya kuswalia.Unakuja hapa kulia lia tu.Utakufa kihoro we mzee.
Luku...
Nimekuuliza kuhusu takataka.
Umekaa muda mrefu hukunijibu.
 
Mohamed Said
Umesema kuna wanafunzi wa PHD kutoka nje ya nchi huja kwako kwa utafiti, hebu tuwekee hapa ushahidi wa kuwa wamekuwa wakikubaliana na kuthibitisha kiutafiti maneno yako kwenye tafiti zao ya kuwa;
Salari,
Umenipa kazi kubwa nitajaribu kutafuta nikipata nitakuwekea hapa.
Unazungumza kazi nilizofanya karibu miaka 20 iliyopita.

Andika Ph D.

Hivi ndivyo sawa.
 
wewe mzee unazeeka vibaya
hawa wote waislam rais,waziri mkuu,jaji mkuu,katibu mkuu necta,usalama nk lakini babu jojo kila uchwao unalia lia ...unataka hii nchi yote mpewe nyinyi mjenge misikiti na iongozwe kigaidi kama taliban?
Luku...
Nimekusoma.
Ahsante
 
Katika kipindi hiki, sitashangaa kwa sababu Bugando na KCMC zilitaifishwa na kuwa chini ya serikali, na pia shule nyingi kama Tosamaganga na nyinginezo zilikuwa za dini pia zilitaifishwa, kwa hiyo kipindi baada ya uhuru hakitakiwi kuwa refefence.


Kwa kweli hatutaki chuo cha ufundi, kwanini isiwe University, mbona tuna Al Maktoum college of Engineering and Technology? mbona hiki hakijaziuwa?

Naamini aidha hatujui kujipanga na kuongea na nchi wafadhili kutujengea vyuo vikuu na mashule, kwa sababu ya uongozi wa BAKWATA umejaa watu walioweka mbele elimu ya dini ndio maana wanaomba ufadhili wa kujengewa misikitu tu...
Gamma...
Huna lolote la kusema kuhusu vyuo vya EAMWS na OIC?
 
mbona misikiti mnachangishana,kwanini msichangishane kujenga vyuo vikuu?utalia lia hivi mpaka lini wakati Nyerere alishafiki?
Samia mvaa kobazi mwenzio peleka proposal wacha kulia kwenye vijiwe vya kahawa mwinyimkuu,suna,butiama nk.
Luku...
Nimekusoma.
Ahsante.
 
Back
Top Bottom