Hatma ya Muungano Tanganyika na Zanzibar

Hatma ya Muungano Tanganyika na Zanzibar

hivi inaruhusiwa mwananchi wa kawaida kwenda kusikiliza kesi kama zifanyazo Mahakama nyingine?
 
Muungano hauwez kuvunjika kamwe Mungu anaulinda umoja Ni nguvu
 
Muungano hauwez kuvunjika kamwe Mungu anaulinda umoja Ni nguvu


WEWE UNAJIFANYA MUNGU ???

Muungano wa Kisoviet wenye mabomu ya nyuklia ulivunjika baada miaka zaidi ya 70 utakuwa huu wenye matatizo siku zote
 
Ukweli mchungu ambao Mzee Nyerere aliona lakini alikataa kuukiri ni kwamba siku ambayo Zanzibar inatoka kwenye huu Muungano kutakuwa na machafuko makubwa sana huko Zanzibar. Lakini baada ya muda Zanzibar itatulia na kuwa taifa moja tajiri sana Afrika ya Mashariki, siyo tajiri kwa kubahatisha bali tajiri haswaaa na kitakuwa ndicho kitovu kikubwa cha dini ya Uislamu kusini mwa jangwa la sahara. Itafika kipindi hata kama tunaweza kuwawekea vikwazo vya kiuchumi wao wanaweza kuishi vizuri kabisa bila bughudha ya Tanganyika.

Kardinali Pengo na baadhi ya viongozi wa dini wanaujua sana huu ukweli,
Mzee Nyerere alilijua hili ndiyo maana "akasema ukiwaacha Wazanzibari watapewa mapesa mengi kutoa kwa waarabu"
Ukikaa na Wazanzibari utakuja kugundua mbali na tofuati zao, wana kitu cha ziada ambacho sisi Watanganyika hatuna kabisa: Kwenya maslahi mapana ya Zanzibar CUF na CCM visiwani wote huwa na sauti moja.

NB: Kimkakati Zanzibar kutoka kwenye Muungano kunaweza kuwanufaisha sana kwasababu eno lao limekaa vizuri sana kijographia. Hasa hasa ukiangalia Maritime Silk Road inapita hapo baada ya Kutoka The Strait of Malacca kwa upande wa Bahari ya Pasifiki na Suez Canal ukiwa umetoka Ulaya. Kama wataamua kutanua bandari yao basi wanaweza kujihakikishia kuwa na soko kubwa sana la biashara za kimataifa kama ilivyo Dubai. Pia inaweza kuwapunguzia sana kutegemea Tanganyika kwasababu bidhaa zao wanaweza kuzipata kutoka Asia, Ulaya, Uarabuni na Mombasa (Haya yatafanyika kama watapata viongozi wenye akili na upeo mkubwa wa kufikiri bila kutumiwa kama vibaraka wa Tanganyika ili kuwagawanya Wazanzibar kama ilivyo sasa hivi)

Tanganyika wakiacha siasa za kidini na kibaguzi basi wanaweza kuitumia Zanzibar kama moja ya kitega uchumi kikubwa,
Pia Zanzibar inaweza ikaongezewa uhuru (Commercial Autonomy) kwenya masuala ya kibiashara kama Bandari na Kodi ili kuutenga mfumo wa kodi wa Muungano ili kuweza kutengeneza soko la kimtaifa ambapo wafanya biashara wa Tanganyika na Zanzibar wanaweza kupata bidhaa nyingi kwa bei ndogo kutoka Ulaya, Asia ya Mbali na Ghuba ya Uajemi. Haya yanawezekana kama tu, tutaamua kukaa kama Taifa na kuweka siasa na udini pembeni......ZANZIBAR INAWEZA KUUINGIZIA MUUNGANO PESA NYINGI SANA....

LONG LIVE THE UNION.............
THE FUTURE IS VERY BRIGHT FOR TANGANYIKA AND ZANZIBAR!


Matatizo ya Zanzibar hupikwa kutoka Tanganyika

soma hapa wavuti: Jisomee online: Kwaheri Ukoloni, Kwaheri Uhuru! Zanzibar na Mapinduzi ya Afrabia
 
Mtafuteni mwandishi wa makala ndugu Joseph Mihangwa anaijua Zanzibar kuliko hata kina shen na Maalim Seif.




Huu muungano wetu kwa mujibu wa viongozi wa ccm ni "Muungano wa kipekee"



Ni wa kipekee kwa CCM kwa sababu unawanufaisha kwa kujaza matumbo yao na familia zao. Ndio wakaunda hao watu wasiojulikana kuwasaidia kubakia madarakani. Huku wakitumia mtutu wa bunduki kutumia vyombo vya dola na kuuwa watu .Wanajua bila muungano watapotea milele
 
Nijuavyo mimi, hakuna kesi yoyote hapo, kwa sababu hatuna mahakama yenye jurisdiction kusikiliza kesi ya kikatiba. Muungano ni suala la kikatiba, mahakama yenye uwezo huo ni mahakama ya katiba, ambayo haijawahi kuwa constituted Tanzania, labda sasa ndio tui constitute.

P
 
kwani kabla ya muungano, wazanzibar walikuwa wanaishije? au kisiwa hakikuwa na watu
 
Nijuavyo mimi, hakuna kesi yoyote hapo, kwa sababu hatuna mahakama yenye jurisdiction kusikiliza kesi ya kikatiba. Muungano ni suala la kikatiba, mahakama yenye uwezo huo ni mahakama ya katiba, ambayo haijawahi kuwa constituted Tanzania, labda sasa ndio tui constitute.

P


Itakavyokuwa vyovyote watu wanataka hayo majibu waende mbele
 
Sultani hakuwa na mamlaka yoyote. Mwenye mamlaka alikuwa ni mkoloni muingereza . Na ndio ukatafutwa uhuru wa Disemba 1963 . Ukisoma kitabu hichi utajua mengi wavuti: Jisomee online: Kwaheri Ukoloni, Kwaheri Uhuru! Zanzibar na Mapinduzi ya Afrabia

Tusitegemee nakala moja tu ya kihistoria,
Uingereza alikuja kuitawala Zanzibar baadae sana.
Eneo kubwa la Pwani ya Afrika Mashariki ilikuwa inatawaliwa na Sultani ambaye nyaraka za wazungu zinasema alikuwa tajiri sana. Haya basi tukubali kwamba mwenye mamlaka Zanzibar alikuwa ni Muingereza, lakini tusisahau mbinu-mkakati wa Utawala wa Uingereza ulikuwa siyo wa moja kwa moja (Indirect Rule);

Hivyo basi hata kama Sultani alikuwa ni mtu wa pili alikuwa bado ana sehemu kubwa sana kiushawishi huko visiwani, kwasababu tofauti na sehemu nyingine alizotawala Muingereza, Zanzibar ilikuwa na idadi kubwa sana ya wafuasi wa dini ya Kiislamu. Kutawala nchi ya namna hii huwezi kufanikiwa bila kufanya makubaliano (Concessions) fulani na muhusika mkuu (Sultani).
 
Nijuavyo mimi, hakuna kesi yoyote hapo, kwa sababu hatuna mahakama yenye jurisdiction kusikiliza kesi ya kikatiba. Muungano ni suala la kikatiba, mahakama yenye uwezo huo ni mahakama ya katiba, ambayo haijawahi kuwa constituted Tanzania, labda sasa ndio tui constitute.

P

Kwahiyo bwana Pascal unataka kutuambia kwamba zile kesi zote za kikatiba ambazo zimejenga Jurisprudence ya nchi hii zilisikilizwa kimakosa ??? Au kwa minajili hiyo unataka kuwaaminisha watanzania kwamba Tanzania hakuwajawahi kuwepo na migogoro ya kikatiba tokea tumefanyia hii katiba yetu Marekebisho ???

CC: Prof
 
Tusitegemee nakala moja tu ya kihistoria,
Uingereza alikuja kuitawala Zanzibar baadae sana.
Eneo kubwa la Pwani ya Afrika Mashariki ilikuwa inatawaliwa na Sultani ambaye nyaraka za wazungu zinasema alikuwa tajiri sana. Haya basi tukubali kwamba mwenye mamlaka Zanzibar alikuwa ni Muingereza, lakini tusisahau mbinu-mkakati wa Utawala wa Uingereza ulikuwa siyo wa moja kwa moja (Indirect Rule); Hivyo basi hata kama Sultani alikuwa ni mtu wa pili alikuwa bado ana sehemu kubwa sana kiushawishi huko visiwani, kwasababu tofauti na sehemu nyingine alizotawala Muingereza, Zanzibar ilikuwa na idadi kubwa sana ya wafuasi wa dini ya Kiislamu. Kutawala nchi ya namna hii huwezi kufanikiwa bila kufanya makubaliano (Concessions) fulani na muhusika mkuu (Sultani).


Unasema Sultani alikuwa tajiri sana

Hebu niambie alikuwa na mali zipi ???

Kwa taarifa mali alizokuwa nazo sultani hazishindi hata mali walizo nazo viongozi wa CCM hivi sasa , wachilia mbali Maraisi wote kuanzia Karume Sr. hadi huyu Shein . Nakuambia tena Mali za mfalme hazishindi mali za viongozi wa CCM na wapambe wao

Usiwe mvivu wa kusoma vitabu ,soma hicho kitabu nilichokuwekea , kidogo kidogo
 
HIZI NI BAADHI YA NCHI ZINAZOENDELEWA KUTAWALIWA KIMABAVU NA MABWANA ZAO

USA wanazitawala nchi za (alaska, guam ,hawaii etc)

MOROCCO wanatawala nchi ya SAHARA MAGHARIBI

ENGLAND inazitawala nchi za IRERAND YA KASKAZINI, WALES NA SCOTTLAND

TANGANYIKA inaitawala nchi ya ZANZIBAR kimabavu.

Nazenginezo...
 
Kutenga kwa Zanzibar sio shida shida ni ngawanyiko siku Zanzibar akijitawala yatakua kama ya UK kujitoa Euro nchi nyingine zinataka kubaki nyingine nyingine kutoka sitashangaa wamakonde wa mafia kusema wao ni Tanganyika huku ukabila ukitawala Pemba na unguja
 
Wazanzibar wanaohoji na wanaotaka muungano uvunjike ni wale ambao mbwa kachoka Kama Mimi,wasiokuwa na Maisha na ambao hawajui kesho kutakuchaje,lakini ukimwambia mtu Kama makamu wa Rais Kuwa unataka muungano uvunjike atatamani kukutandika.
 
Back
Top Bottom