Hatma ya ndoa yangu leo usiku imekuwa hatari kwa maisha yangu

Hatma ya ndoa yangu leo usiku imekuwa hatari kwa maisha yangu

UWOGA=UMASKINI

JF-Expert Member
Joined
Dec 30, 2013
Posts
2,399
Reaction score
1,014
Labda kwa kuanza tu niwasalim wote na nawaomba muwe miongoni mwa mtakaookoa nafsi yangu iliyojaa maumivu yasiyo na kifani

Nilianza kuishi na mke wangu huyu 2008 kabla ya ndoa na tukabahatika kupata watoto wawili na mwaka 2018 january tukaamua kubariki ndoa

Na kilichokuwa kinachelewesha ndoa ilikuwa dini tofauti mimi ni mkristo yeye ni mwislam ila mwisho aliamua kubadili dini mwanzoni mwa mwaka 2009 na tukawa tunahudhuria ibada pamoja na wanetu mpaka january hii na tupo mkoa mmoja lakini wilaya tofauti

Point ya ushauri hii hapa naohitaji kwenu waungwana

Leo usiku huu kaniambia anarudia imani yake kwa kina na anahudhuria ibada na maadili yote ya imani yake (islamic) na hakuna wa kumrudisha nyuma tena

Ila pia anakiri kurudi kwenye imani yake hana maana kwamba hanipendi ananipenda na ataendelea kuniheshimu kama mume wake na pia hataachana na mimi labda mimi nitakapoamua kumuacha

Na pia naendelea kuniambia ameshaomba toba kwa mwenyezi mungu amsamehe madhambi yake yote aliyotenda kwa kipindi chote alichimchangana nabii issa na mungu

Hakuchoka wala kuishia hapo aliendelea kuniambia nimsamehe kwa maamuzi hayo na maisha yaendelea kama kawaida na pia alifanya ndoa kuweza kuturidhisha mimi na ndugu zangu

Japo anasema jambo hilo anaamini haliwezi vunja uhusiano wetu na hata akibaki katika imani hii ataendelea kupretend ambavyo yeye hataki kupritend na niliogopa kukuambia mda ila leo nimeamua kukuambia tu

Na haya yote yanatokea baada ya kumpeleka kwenye shule kurisit mtihani wake wa kidato 4 katika shule za kislam

Sasa naomba mnishauri nifanye nini kwa kuwa naona kama moyo unatoboka sijapata usingizi toka nilivyojaribu kulala saa 2 ya leo

Pili kiimani ikoje tena hii ndoa baada ya mwenzangu kuamua hivyo

Je kuna umuhimu wa kuendelea na mipango ya maisha ya pamoja mfano tulikuwa tumenunua viwanja vitatu na kimoja nimeandika jina langu viwili majina ya watoto na pia kiwanja kimojawapo tumeshaanza ujenzi na nilipanga kumalizia nyumba yetu mwezi wa nne je kuna umuhimu wa kufanya hivyo ?

Nb sikuweza kuamini yaliyotokea kwa kuwa yeye alibadili na kuwa mkisto bila kushawishiwa na mtu yeyote na kwa kweli tulipendana na nawapenda sana yeye na wanangu

Na kabla hajafanya maamuzi ya kuhamia ukristo 2009 alikuwa anateswa sana sana na mapepo na alipohamia tu ukristo toka kipindi hicho hajawahi kuangushwa na mapepo.
 
Labda kwa kuanza tu niwasalim wote na nawaomba muwe miongoni mwa mtakaookoa nafsi yangu iliyojaa MAUMIVU YASIYO NA KIFANI

NILIANZA KUISHI NA MKE WANGU HUYU 2008 KABLA YA NDOA NA TUKABAHATIKA KUPATA WATOTO WAWILI NA MWAKA 2018 JANUARY TUKAAMUA KUBARIKI NDOA

NA KILICHOKUWA KINACHELEWESHA NDOA ILIKUWA DINI TOFAUTI MIMI NI MKRISTO YEYE NI MWISLAM ILA MWISHO ALIAMUA KUBADILI DINI
WHY WASTE YOUR TIME WITH A MERE HYPOCRATE WHO HAS NO LOCUS STADI,SHE IS A HABITUAL LIAR, run for your life sir
 
Angelikua ni muumini wa kiislamkweli angekushauli na wewe uingie dini maana wanaamini ndio dini ya kweli.Maadam anakwambia mutaendelea kuishi kila mtu na dini yake huyo bado hana msimamo

Sent using Jamii Forums mobile app
Nakuambia amehudhuria kanisani miaka kumi na kubatizwa kabatizwa sasa nashindwa elewa na nimemwuliza uko serious akaniambia hawazi kurudi nyuma coz amepretendi mda mrefu dini ya kweli in uislam pekee hakuna nyinginee
 
Uko tayari kuona watoto wako wanalelewa na mama wa kambo? Je, unampenda mkeo? Katika hii miaka 11 ya kuwa pamoja purukushani za hapa na pale hazikosi, katika muda huo wa kuwa pamoja bado unaweza kutamka ni mke mwema ni mama mwema kwa watoto wenu?

Ukiweza kuyajibu maswali hayo kwa ufasaha bila kigugumizi basi unajua maamuzi yako yataegemea upande upi.

Kila la heri kwenye kufanya maamuzi magumu na mrejesho ukiweza muhimu.
 
Asante sana vip kuhusu wapenzi wanangu ndugu
Wenzio tunasubiriaga penati kama hizi tuvunje ndoa wewe bado unataka ushauri JF. Wakati ni huu usizubae! Watoto wana shida gani, wewe si ndio baba yao? Tatizo lipo wapi? Unakwama wapi Mr. Woga=Umaskini?
** piga chini fasta, kakamate mwanakwaya uendelee kufurahia maisha.
 
Kama wewe kweli ni Mkristo tafakari maneno haya kutoka 1 Kor 7 : 1-16

Maagizo kuhusu Ndoa
1Basi kwa habari ya mambo yale mliyoandika, ni heri mwanamume asimguse mwanamke.

2Lakini kwa sababu ya zinaa kila mwanamume na awe na mke wake mwenyewe, na kila mwanamke na awe na mume wake mwenyewe.

3Mume na ampe mkewe haki yake, na vivyo hivyo mke na ampe mumewe haki yake.

4Mke hana amri juu ya mwili wake, bali mumewe; vivyo hivyo mume hana amri juu ya mwili wake, bali mkewe.

5Msinyimane isipokuwa mmepatana kwa muda, ili mpate faragha kwa kusali; mkajiane tena, Shetani asije akawajaribu kwa kutokuwa na kiasi kwenu.

6Lakini nasema hayo, kwa kutoa idhini yangu, si kwa amri.

7Ila nipendalo ni kwamba watu wote wawe kama mimi nilivyo; walakini kila mtu ana karama yake mwenyewe itokayo kwa Mungu, huyu hivi, na huyu hivi.

8Lakini nawaambia wale wasiooa bado, na wajane, Ni heri wakae kama mimi nilivyo.

9Lakini ikiwa hawawezi kujizuia, na waoe; maana ni afadhali kuoa kuliko kuwaka tamaa.

10 Lakini wale waliokwisha kuoana nawaagiza; wala hapo si mimi, ila Bwana; mke asiachane na mumewe;

11lakini, ikiwa ameachana naye, na akae asiolewe, au apatane na mumewe; tena mume asimwache mkewe.

12Lakini watu wengine nawaambia mimi, wala si Bwana, ya kwamba iwapo ndugu mmoja ana mke asiyeamini, na mke huyo anakubali kukaa naye asimwache.

13Na mwanamke, ambaye ana mume asiyeamini, na mume huyo anakubali kukaa naye, asimwache mumewe.

14Kwa maana yule mume asiyeamini hutakaswa katika mkewe; na yule mke asiyeamini hutakaswa katika mumewe; kama isingekuwa hivyo, watoto wenu wangekuwa si safi; bali sasa ni watakatifu.

15Lakini yule asiyeamini akiondoka, na aondoke. Hapo huyo ndugu mume au ndugu mke hafungiki. Lakini Mungu ametuita katika amani.

16Kwa maana wajuaje, wewe mwanamke, kama utamwokoa mumeo? Au wajuaje, wewe mwanamume, kama utamwokoa mkeo?
 
Pole sana mkuu, ila asilimia kubwa ya wanaobadili huwa wanarudia Dini zao za awali chamsingi ni kukaa na kuelewana new lifestyle tu,maana hapo hajaamua leo ni maamuzi ya muda mrefu sema ilikuwa bado tu kukwambia
 
Back
Top Bottom