Hatoi matumizi ya mtoto, kaomba nimkopeshe pesa

Hatoi matumizi ya mtoto, kaomba nimkopeshe pesa

Habari za weekend wapendwa,

I hope you are all doing great.Mimi ni single mum ambaye nalea mwanangu mwenyewe toka mjamzito.Babake alikataa mimba na kuomba niitoe but niligoma kuuwa kiumbe kisicho na hatia.

Nikaamua kulea mwenyewe na baada ya kujifungua, bado akakataa mtoto hivyo tukafanya DNA( kwa gharama zangu pia) na mtoto akawa ni wake.

Ilibidi aanze kutoa matumizi ya mtoto ambayo alitoa kwa miezi mitatu tu.So nikawa namkumbusha but anakwepa nikaona isiwe shida nikampotezea nikaamua kuongeza nguvu zaidi katika upambanaji.

Ndugu zake huwa wananipigia na kumjulia hali mtoto,wakiomba picha nawatumia ndo nahisi huwa wanamtumia jamaa pia.

So leo , nimekaa nawaza zangu maisha na kucheza na mrembo wangu,ghafla babake anapiga simu na kutujulia hali na kuomba nimkopeshe laki tano..Nilimjibu tu kistaarabu kuwa sina.

Na huyu jamaa anafanya kazi kwenye taasisi kubwa tu na analipwa vizuri ila amesusia matumizi ya mtoto wake na leo ana uthubutu wa kunikopa pesa. Mtoto ana miaka miwili saiv na alimhudumia kwa miezi mitatu tu baada ya DNA.

Wanaume, nimewainulia mikono.

Jumapili njema wapenzi.
Huyo hana mapenzi na wewe,na anayafahamu madhaifu yako anatumia kama silaha kukufanya anavyotaka! Fanya maamuzi songa mbele,la sivyo utajikuta hauna kitu at the end.
 
Best hapana bwanaa,kuna wanaume wanajua kutesa wanawake,.hata kama haibadilishi ukweli yeye alishindwaje kumuhudumia mtoto ingali kipato anacho??leo kakwama anamfuata huyohuyo ambaye usiku na mchana ana pambana kwa ajili yake binafsi na damu yao...akakope tuu bank asee...
Yaani dada ni dharau kubwa sana,uo ujasiri huyo mwanaume anaupataje kama siyo dharau ni nini
 
Hata kama huna roho mbaya shoga usimpe..acha apambane tuu na hali yake halafu hawezi barikiwa hata angekuwa anafanya kazi juu ya anga hizo ni laana na ukimpa utageuzwa bank,hiyo laki tano bora umuwekee mwanao kwenye account itawafaa siku mkikwama,.kuna wanaume hawana haya jamanii khaa!!!
ahaha,,we kauzu bibie
 
Habari za weekend wapendwa,

I hope you are all doing great.Mimi ni single mum ambaye nalea mwanangu mwenyewe toka mjamzito.Babake alikataa mimba na kuomba niitoe but niligoma kuuwa kiumbe kisicho na hatia.

Nikaamua kulea mwenyewe na baada ya kujifungua, bado akakataa mtoto hivyo tukafanya DNA( kwa gharama zangu pia) na mtoto akawa ni wake.

Ilibidi aanze kutoa matumizi ya mtoto ambayo alitoa kwa miezi mitatu tu.So nikawa namkumbusha but anakwepa nikaona isiwe shida nikampotezea nikaamua kuongeza nguvu zaidi katika upambanaji.

Ndugu zake huwa wananipigia na kumjulia hali mtoto,wakiomba picha nawatumia ndo nahisi huwa wanamtumia jamaa pia.

So leo , nimekaa nawaza zangu maisha na kucheza na mrembo wangu,ghafla babake anapiga simu na kutujulia hali na kuomba nimkopeshe laki tano..Nilimjibu tu kistaarabu kuwa sina.

Na huyu jamaa anafanya kazi kwenye taasisi kubwa tu na analipwa vizuri ila amesusia matumizi ya mtoto wake na leo ana uthubutu wa kunikopa pesa. Mtoto ana miaka miwili saiv na alimhudumia kwa miezi mitatu tu baada ya DNA.

Wanaume, nimewainulia mikono.

Jumapili njema wapenzi.
there's is thin line between love and hate

huyu huyu jamaa akitaka kupasha kiporo anapata
 
Pia nilimblock na katumia namba ngeni .Na kama kosa ni kukopesha,ningemkopesha kwa maandishi na angerudisha kwa riba.
Uondo mwanzo wa kurudisha penz upya mtakopeshana we mwisho atakwambia muish pamoja mlee mtoto ata kudanganya hana mtu na haja pata mtu sahii kama wewe, atakuita uende kichukua pesaza mtoto na muongee Zaid.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huendaa jamaa hakuwa tayari kulea mtoto ....

Muwe mnashirikishana kwenye hatua za kubeba ujauzito, sio mnaanza kulialia badae bila sababu ....
Hakuwa tayari alipoiweka pekupeku alikuwa anatarajia nn?halafu Inaonyesha hana shida ni child support kutoa nayo ni shida...Dada usimpe hata 100 ila usiache kudai matumizi ya MTT ni wake
 
Best hapana bwanaa,kuna wanaume wanajua kutesa wanawake,.hata kama haibadilishi ukweli yeye alishindwaje kumuhudumia mtoto ingali kipato anacho??leo kakwama anamfuata huyohuyo ambaye usiku na mchana ana pambana kwa ajili yake binafsi na damu yao...akakope tuu bank asee...
Ni kweli, lakini nikukumbushe tu kuwa ukiona mpaka mtu ana kila kitu kisha anakataa mimba hadi anakuja kudai DNA ya mtoto ili apate uhakika ujue hapo kuna tatizo sio bure, hapo Kuna kila dalili ya kutokuwepo kwa uaminifu kati yao ( ujue kila mtu anamfahamu vema mwenza wake) Kama mtu anaona Kuna kila dalili ya kusalitiwa au mabye umeona kwa macho yako then mtu anakuja kukwambia anamimba yako unadhani ni rahisi namna hiyo kukubali?

Sio kila anaye kataa mimba basi ni kwa ujinga, kukimbia majukumu au roho mbaya no wakati mwingine Kuna vitu vinatokea kwenye mahusiano vinashawishi mtu kukataa mimba ila havisemwi wazi badala yake point inayo onekana ni ile tu ya kukataa basi ila vyanzo haviangaliwi kabisa.

Mfano Kama huyu ana kila kitu kwa mujibu wa maelezo hufikirii kwanini kakataa hadi anadai vipimo vya DNA unayajua maumivu ya kabambikiwa mimba unalea mtoto si wako miaka kibao bila kujua then unakuja kustuka badae ushagharamika vya kutosha?

Okay, baada ya vipimo akakubali mwanae na akaanza kutoa matunzo ila ghafla akaacha hadi kafikia hatua ya kuja kukukopa pesa unadhani Kuna nini hapo kilimpata huyu jamaa?
Unadhani alikuwa anamkopa pesa kwa kumdhihahi au kumtapeli?

Best narudia kusema maisha yetu haya yana mambo mengi mno, katika mada kama hizi Kuna vitu haviwekwi wazi kisha anashambuliwa mtu mmoja.
Sawa lakini yote ni maisha na hakuna asiye kosea.
 
Ushauri wangu

Fanya vyoyote utakavyofanya uhakikishe huyo baba anatoa matunzo yote ya mtoto hata ikibidi kumpeleka ustawi wa jamii au mahakamani mpeleke! Mathalan imethibitika mtoto ni wake, hana budi kumlea tena na hiyo miezi ambayo hajalipa andika kama deni na lazima alipe!

Kwanini nasema hivi?

Wewe na jamaa inawezekana mmegombana, lakini mtoto na baba yake hawajagombana. Utapambana mwenyewe apo kujidai kumlea mtoto, baadae mtoto akiwa mkubwa atakusumbua sana umpeleke kwa baba yake! Usipompeleka utajenga uhasama mkubwa na mtoto ambae umemtesekea wewe mwenyewe na atakuona mbaya! Ukija kumpeleka kwa baba yake baadae, na akagundua baba ana hela, atakulaumu sana kwa kumkosesha fursa katika maisha!! And trust me, huwezi kumtenganisha mtoto wa kike na baba yake, bora ata angekua wa kiume.

Ishu kama hii ilimtokea dada yangu, kapambana na mtoto saizi yuko chuo. Mtoto kamtafuta baba yake mpaka kampata na sasa hivi mtoto na baba lao moja, mama ndio anaonekana kituko!


Sina "uduazi" huo
 
Kushirikishana kupi kwingine unakokutaka?
Mtu anavua boxer, anagonga kavu kavu, anapiga bao anakojoa humo humo.
Anarudia hizo process mara kadhaa. Halafu unataka kuaminisha kuwa hakukua na ushirikishwaji wa baba?
Unataka ushirikishwaji upi mwingine mkuu?
Mwanaume shabash aliekamilika, akishiriki hizo process zote hapo juu, na mimba ikanasa hawezi kuanza kulalama eti mdada kashika mimba bila kumshirikisha. Kitu pekee ninachoweza mlaumu huyu binti ni kumvulia chupi mwanaume mpumbavu.
Dr. umeua [emoji23][emoji23][emoji23][emoji1544]
 
Ushauri wangu

Fanya vyoyote utakavyofanya uhakikishe huyo baba anatoa matunzo yote ya mtoto hata ikibidi kumpeleka ustawi wa jamii au mahakamani mpeleke! Mathalan imethibitika mtoto ni wake, hana budi kumlea tena na hiyo miezi ambayo hajalipa andika kama deni na lazima alipe!

Kwanini nasema hivi?

Wewe na jamaa inawezekana mmegombana, lakini mtoto na baba yake hawajagombana. Utapambana mwenyewe apo kujidai kumlea mtoto, baadae mtoto akiwa mkubwa atakusumbua sana umpeleke kwa baba yake! Usipompeleka utajenga uhasama mkubwa na mtoto ambae umemtesekea wewe mwenyewe na atakuona mbaya! Ukija kumpeleka kwa baba yake baadae, na akagundua baba ana hela, atakulaumu sana kwa kumkosesha fursa katika maisha!! And trust me, huwezi kumtenganisha mtoto wa kike na baba yake, bora ata angekua wa kiume.

Ishu kama hii ilimtokea dada yangu, kapambana na mtoto saizi yuko chuo. Mtoto kamtafuta baba yake mpaka kampata na sasa hivi mtoto na baba lao moja, mama ndio anaonekana kituko!
Asante mkuu.Nilishafanya yote hayo hadi mahakamani but niliambulia patupu. Nikaona napoteza pesa kwa mwanasheria na muda.Thats why nikaachana nayo.

For now, ngoja niwekee mambo yangu kwenye mstari kuliko kumfikiria mtu mzima mwenye meno 32 asiyejua majukumu yake.

All in all, najua sehemu ya kumkomesha
 
Maisha ni kusameheana,kusaidiana na kurekebishana.Binafsi nakushauri kama unao uwezo mkopeshe tu huyo ni mzazi mwenzio hata kama utamchukia vipi ila mwisho wa siku ni mzazi mwenzio tu..cha msingi mueleze ukweli kuwa anakosea sana anaposhindwa kumlea mwanae,anamnyima haki yake mtoto..
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Kuna vitu vingine vinachekesha na kusikitisha walah!!
 
lady Jay sasa nimejua ni binti. Maskini huyo mwanaume bado hajielewi! Mtoto wa Kike ndiye mkombozi wa mwanaume uzeeni. Ni kosa kubwa kwa mwanaume kumtupa mtoto wa Kike. Unapoinvest kwa mtoto wa kike unajiwekea security, hata akiwa na shilling mbili lazima atakupa moja abakie na moja. Mtoto wa kiume akikua atahangaika na mama yake na girlfriend wake. Wewe hata kukupigia simu inakuwa ni mtihani.

Jitahidi mama kuhakikisha baba yake anawajibika maana sie tumeyaona, baba hakumtunza mtoto ila akikua lazima ahangaike na baba yake. Mtoto wa Kike kwa baba ni Chanda na pete. Watoto wa kiume tunawazalia mama zao tu.

kwa upande wangu kila wakati najitahidi mtoto wa Kike afike mbali kielimu. Wakiume including me tunaboa kwa kusahau baba zetu
 
Back
Top Bottom