Hatua za kikanuni za Bunge zitakazochukuliwa dhidi ya Luhaga Mpina ziambatane na hatua muafaka za kikatiba za CCM kumng'atua

Hatua za kikanuni za Bunge zitakazochukuliwa dhidi ya Luhaga Mpina ziambatane na hatua muafaka za kikatiba za CCM kumng'atua


Ni wakati muafaka sasa kwa CCM kufanya wajibu wake muhimu sana, dhidi ya wenye kiburi, waongo, wabishi na wenye tamaa waliobakiza mioyo yao ccm, lakini akili zao zikiwa kwa walio watuma.

Wakati kamati ya maadili ya bunge ikiendelea na majadiliano, kufanya uchambuzi wa kina na kujiridhisha mbivu na mbichi juu ya nyaraka na vielelezo alivyo wasilisha Mh. Luhaga Mpina kwa spika, dhidi ya tuhuma anazomtuhumu waziri wa kilimo, mwenye bidii sana, mchapakazi hodari waziri Mh. Hussein Bashe.

CCM ijiandae kumchukilia Mh. Luhaga Mpina hatua stahiki za kinidhamu dhidi ya kumdharau spika, kulidharau bunge, kumzushia Mh. waziri waziri Bashe kinachofanyiwa kazi na kamati ya bunge, na kuituhumu bila hakika serikali yote sikivu ya CCM kwa ujumla.

Hii si sawa kwa taasisi imara na makini kama CCM, kuendelea kuwavumilia wanachama wake wasio zingatia misingi ya nidhamu, kanuni na katiba ya chama na kukengeuka kwa chuki isiyo na sababu.

Na baada ya kumchukilia hatua za kawaida za kinidhamu kwa mujibu wa katiba ya CCM, iwe pia ni wakati muafaka chama kiende mbali zaidi, kwa kumvua uanachama wa CCM Mh. Luhaga Mpina kwa kukiuka na kwenda kinyume na kanuni, taratibu, mila, desturi na utamaduni wa CCM, wa kufanya kazi kwa kuheshimiana na kwa umoja ili kuwaletea wananchi maendeleo.

Mh Luhaga Mpina abanduliwe CCM haraka iwezekanavyo kwa kutatiza mara kwa mara kupinga, na kijaribu kidhoofisha na kwa kupotosha kwa makusudi nia, mipango mikakati na malengo ya chama na serikali sikivu ya ccm katika kuwaletea wananchi maendeleo, na kuchochea mageuzi ya kisiasa, kijamii na kiuchumi kwenye maisha ya waTanzania wote.

Mh. Luhaga Mpina apokonywe uanachama wa CCM, ili akapate fursa na wasaa mzuri zaidi wa kuendeleza tuhuma zake na gubu binafsi alizonazo, dhidi ya baadhi ya waandamizi serikalini, ambao anahisi ndio waliosababisha na kuchochea, yeye Mh. Luhaga Mpina kutoswa kwanye baraza la mawaziri alilokua akihuduma kama waziri wa uvuvi, hapo awali.

Mh. Luhaga Mpina avuliwe uanachama ili kwa uhuru zaidi, akaungane na wenzie wa upande wa pili, wanaomtetea na waliopoteza uelekeo, walio kosa hoja, sera na wasiojua hata wana dai nini wala wanatetea nini, yaani wapo wapo tu. :pulpTRAVOLTA: :pulpTRAVOLTA:

Ni matumaini yangu, mpaka sasa kwa hali ilipofikia, pasina shaka yoyote, kupitia vyombo maalumu vya chama, CCM itakua imejiridhisha pasina shaka yoyote kwamba Mh. Luhaga Mpina kwa kiburi, jeuri na utovu wa nidhamu hana sifa wala vigezo tena vya kua mwananchama, mkereketwa wala shabiki wa CCM na anastahili kufubgashiwa virago vyake CCM.

- Spika Tulia amburuza Luhanga Mpina Kamati ya maadili
Hizo ni pigo za kizamani mnaleta zama hizi, ingekuwa Bora hoja za Mpina zijibiwe kuliko kumletea vitisho.
 
Hizo ni pigo za kizamani mnaleta zama hizi, ingekuwa Bora hoja za Mpina zijibiwe kuliko kumletea vitisho.
uongo na uzushi unajibiwaje sasa na wewe gentleman? 🐒

wew uloibua ndio unatakiwa kuthibitisha kuzushi wako kwamba ni Kweli na ndicho kamati ya bunge inamalizia kuuchambua na kubainisha mbivu na mbichi 🐒
 
bunge linaendelea na kazi hiyo kupitia kamati ya maadili na itamshauri spika hatua muafaka za kumchukulia Mh.Luhaga Mpina mbunge wa Jimbo la Kisesa...

Lakin pia CCM kupitia vyombo vyake vya kimaadili kuanzia ngazi ya tawi la Mh.Luhaga Mpina nao pia kazi inaendelea, japo tayari kwa kiasi Fulani ilishafanyika, kinachosubiriwa sasa ni taarifa ya spika...

CCM haijatuma mtu bungeni kwenda kutuhumu watu kwa uzushi na uongo, wala kwenda kumvunjia heshima spika, kulivunjia heshima bunge, mawaziri, serikali na wanainchi kwa ujumla kupitia bunge letu tukufu la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania 🐒
Wanahusika Mpina na Bashe, kwanini Bunge na CCM wajikite kumchunguza Mpina tu???
 
kwamba kuku atamkamata mwewe 🤣
We bado unaamini hayo Mausemi yenu ya kizamani
Sjui aliyeko juu mngojeee chini..
Mimi wee uko juu mimi nakupandiaaa huko huko juu alafu mimi ndiyo nakushusha

Ova
 
Hiyo ni dhana mbaya ya kufunga midomo ya wana-CCM wenye mawazo tofauti.
acha upotoshaji gentleman,

mdomo wa nani uko wazi ndio ufungwe ?🐒

kubanduliwa uanachama na kunyang'anywa ubunge sio kuziba mdomo wa mtu, that is democrats procedures and processes....

bado fursa ipo, vyama na na platforms za kisiasa zipo, you can join the stage na kufanya siasa zako vizuri tu na mambo ya mdomo hutaskia tena 🐒
 
We bado unaamini hayo Mausemi yenu ya kizamani
Sjui aliyeko juu mngojeee chini..
Mimi wee uko juu mimi nakupandiaaa huko huko juu alafu mimi ndiyo nakushusha

Ova
utapanda wap mrangi wew akati huna hata hakika hapo ulipo uko juu katikati au chini?🤣

hebu acha hadaa zako bana mchana kweupeee 🐒
 
with my dead body,
sugar companies zimempotosha pakubwa huyu muungwana ambae anakwenda kubanduliwa CCM na kupoteza ubunge wake kirahisi sana, hata sijui wamempa kiasia gani my colleague, maskini Luhaga Mpina 🐒
RUSHWA imepofusha ufahamu wako!!
 

Ni wakati muafaka sasa kwa CCM kufanya wajibu wake muhimu sana, dhidi ya wenye kiburi, waongo, wabishi na wenye tamaa waliobakiza mioyo yao ccm, lakini akili zao zikiwa kwa walio watuma.

Wakati kamati ya maadili ya bunge ikiendelea na majadiliano, kufanya uchambuzi wa kina na kujiridhisha mbivu na mbichi juu ya nyaraka na vielelezo alivyo wasilisha Mh. Luhaga Mpina kwa spika, dhidi ya tuhuma anazomtuhumu waziri wa kilimo, mwenye bidii sana, mchapakazi hodari waziri Mh. Hussein Bashe.

CCM ijiandae kumchukilia Mh. Luhaga Mpina hatua stahiki za kinidhamu dhidi ya kumdharau spika, kulidharau bunge, kumzushia Mh. waziri waziri Bashe kinachofanyiwa kazi na kamati ya bunge, na kuituhumu bila hakika serikali yote sikivu ya CCM kwa ujumla.

Hii si sawa kwa taasisi imara na makini kama CCM, kuendelea kuwavumilia wanachama wake wasio zingatia misingi ya nidhamu, kanuni na katiba ya chama na kukengeuka kwa chuki isiyo na sababu.

Na baada ya kumchukilia hatua za kawaida za kinidhamu kwa mujibu wa katiba ya CCM, iwe pia ni wakati muafaka chama kiende mbali zaidi, kwa kumvua uanachama wa CCM Mh. Luhaga Mpina kwa kukiuka na kwenda kinyume na kanuni, taratibu, mila, desturi na utamaduni wa CCM, wa kufanya kazi kwa kuheshimiana na kwa umoja ili kuwaletea wananchi maendeleo.

Mh Luhaga Mpina abanduliwe CCM haraka iwezekanavyo kwa kutatiza mara kwa mara kupinga, na kijaribu kidhoofisha na kwa kupotosha kwa makusudi nia, mipango mikakati na malengo ya chama na serikali sikivu ya ccm katika kuwaletea wananchi maendeleo, na kuchochea mageuzi ya kisiasa, kijamii na kiuchumi kwenye maisha ya waTanzania wote.

Mh. Luhaga Mpina apokonywe uanachama wa CCM, ili akapate fursa na wasaa mzuri zaidi wa kuendeleza tuhuma zake na gubu binafsi alizonazo, dhidi ya baadhi ya waandamizi serikalini, ambao anahisi ndio waliosababisha na kuchochea, yeye Mh. Luhaga Mpina kutoswa kwanye baraza la mawaziri alilokua akihuduma kama waziri wa uvuvi, hapo awali.

Mh. Luhaga Mpina avuliwe uanachama ili kwa uhuru zaidi, akaungane na wenzie wa upande wa pili, wanaomtetea na waliopoteza uelekeo, walio kosa hoja, sera na wasiojua hata wana dai nini wala wanatetea nini, yaani wapo wapo tu. :pulpTRAVOLTA: :pulpTRAVOLTA:

Ni matumaini yangu, mpaka sasa kwa hali ilipofikia, pasina shaka yoyote, kupitia vyombo maalumu vya chama, CCM itakua imejiridhisha pasina shaka yoyote kwamba Mh. Luhaga Mpina kwa kiburi, jeuri na utovu wa nidhamu hana sifa wala vigezo tena vya kua mwananchama, mkereketwa wala shabiki wa CCM na anastahili kufubgashiwa virago vyake CCM.

- Spika Tulia amburuza Luhanga Mpina Kamati ya maadili
Acha ukasuku na uchawa. Unampomtetea Bashe kuhusu vibali vya sukari uliona sukari ikishuka bei kutokana na kuingizwa sukari isiyokua na ushuru? Pumbafu nyie vibaraka wa ufisadi. Kile anadai Mpina Ni kufichua njama zinavyofanywa na wanasiasa na wafanyabiashara kufisidi taifa na kuwaumiza raia bila ya huruma.
 
Kwani ukiwa ccm lazima ukose akili?
 
Acha ukasuku na uchawa. Unampomtetea Bashe kuhusu vibali vya sukari uliona sukari ikishuka bei kutokana na kuingizwa sukari isiyokua na ushuru? Pumbafu nyie vibaraka wa ufisadi. Kile anadai Mpina Ni kufichua njama zinavyofanywa na wanasiasa na wafanyabiashara kufisidi taifa na kuwaumiza raia bila ya huruma.
Jamaa kashiba huyoo

Ova
 
hizi mada za kitaalamu sio kwaajili ya wavivu na wakurupukaji gentleman 🐒

haihitaji mihemko wala haraka kusoma taratibu zaidi ya mara4 ili kupata uelewa na ufahamu wa kutosha juu ya jambo lenyewe, na kutafakari kwa kina kabla ya kureply au kukoment...

kwa kufanya hivyo itakua umejitendea haki mwenyewe kifikra.

vinginevyo itakua ni wale wale kwa kukimbilia kwenye hitimisho kwa kejeli, ghadhabu na matusi ikiashiria dhahiri shahiri anacho weza nje ya hoja ni hicho tu 🐒

naamini wew si moja wao, jitahidi kua na bidii 🐒
Kwa kipi hasa ulichoandika chenye weledi wa kusomwa mara nne? Ulipitia chapisho la Mpina? Uliona kilichoandikwa, unaweza kuhusianisha na huu upuuzi wako unaosema tuusome mara nne?

Mkuu, msipende kuacha akili nyuma mnapokuwa ccm.
 
kwamba ukitoswa kwenye baraza la mawaziri, unakasirika na kuanza kuhisi ati fulani ndie amekuchomea ukatoswa, na sasa unajenga chuki binafsi na gubu dhidi yake kwa kubuni tuhuma za uzushi na uongo eti nae aachishwe kazi, kama yeye mchoma nyavu za wavivu wadogo wanyonge, na mpima ukubwa wa samaki tena waliorostiwa kwa rula 🤣

eti huyu ndie mtu mwema anaekimbia CMC, right?
mtu mwema aliangamiza mamilioni ya vifaranga vya kuku aise dah 🤣
Nachanganyikiwa hapa. Mpina kato tuhuma, na kaambatiza reference, (citation); sasa hata kabla hamjasoma hizo reference na kujiridhisha mmeanza kumshambulia. Mngepekua kwanza hizo reference na kuonyesha uongo wake ingeeleweka. Labda ni mimi tu ndiyo sielewi. Sasa wewe ulitaka afanyeje? Akae kimya?
 
Hebu niambie inawezekana vipi kampuni isajiliwe january 2024 na ije kupewa tenda ya kuleta sukari kuzidi viwanda vilivyo anzishwa miaka na miaka 😂😂😂😂😂😂😂
 
Akikujibu huyu Tlaatlaah
Uni tag

Ova
ndio maana nikwambia mrangi sidhani kama unaelewa uko juu, chini au katikati 🐒

anaemtuhumu mwenzie tena bungeni ndie pekee anaepaswa kuthibitisha tuhuma hizo kwa vielelezo mujarabu visivyo na chembe ya shaka🐒

sasa kama sugar companies wamekurubuni na kukuchochea kwa visenti kidogo, plus hasira za kutemwa kwenye baraza la mawaziri, akidhani ni Bashe ndie alie mchomea kwa mama akamtosa...

hilo ni jambo la kusubiri kamati ya maadili ya bunge itakavyomshauri spika hatua za kuchukua, huku CCM nayo ikijipanga kuiandikia barua Tume Huru Ya Uchaguzi juu ya uamuzi iliyouchukua, dhidi ya mbunge wake mh.Luhaga Mpina mbunge wa Jimbo la Kisesa 🐒

mrangi,
usisite kunitag na kuniuliza chochote kwa niaba ya wenzako wengine, usichokielewa kuhusu hoja hii 🐒
 
nikajuaga jamaa (mleta mada) nyege ndizo zinamdumbua kumbe alikua kwenye ukichaa stage 1 sasa naona zimepanda yupo stage 6 na anajifunza uchawa soon ataanza kuweka namba
 
Back
Top Bottom