Hatukuwahi kuwa na maji ya Bomba, Rais Samia ametuletea

Hatukuwahi kuwa na maji ya Bomba, Rais Samia ametuletea

kalacha mateo

Senior Member
Joined
Sep 27, 2021
Posts
119
Reaction score
240
Wakazi wa Kijiji cha Ilela, Wilaya ya Ludewa mkoani Njombe waliokuwa wanakabiliwa na kero ya maji safi na salama wameondokana na adha hiyo baada ya serikali ya awamu ya sita chini ya Dkt. Samia Suluhu kuwapelekea mradi wa maji ikiwa ni muendelezo wa utekelezaji wa kampeni ya kumtua mwanamke ndoo kichwani.

Mradi huo umekamilika kwa 100% utawanufaisha wakazi 980 wa kijiji hicho ambao hawajawahi kupata maji ya bomba tangu uhuru walikua wanatumia maji ya ziwa Nyasa ambayo wanayafata kilometa moja. Diwani wa kata ya Ruhuhu, Athanas Haule alisema mradi huo wa maji ni ukombozi mkubwa kwa wananchi wa kijiji hicho hasa wakati wa kiangazi kwa kuwa wakati wa masika wananchi wanatumia maji yanayotiririka kutoka milimani.

AAAAAA.jpg
 
wanasiasa ndio wanachelewesha maendeleo.hivi vitu ni lazima wala sio vya kuuliza na kusifu. nyie ccm
 
Nilikuwa najiuliza kwann waasi wanapopindua nchi huwa wanaua watu wasio na hatia wala silaha na kuchoma vijiji vyao.

Ila the way nimestudy jamii ya mtanzania nimegundua kuwa hawa wenzetu wa maeneo ya vijijini ndio wanaongoza kwa kuwasapoti serikali inayokuwa kandamizi na wanakubali kutumika kuiweka madarakani. So waasi huwa wanakuwa na hasira nao na kuwatokomeza kama masalia ya serikali dhalimu.

Now ndio naelewa kwann inakuwa vile.
 
Watanzania asilimia zaid ya 80 wanaishi vijijini pia wale wakijengewaga vimiladi midogo midogo basi wanaitukuza ccm vibaya mno, watu wa vijijin hawanaga mahitaji makubwa sana ya kimiundombinu na hawa ndio wanaologwa sana na wanasiasa, wakijengewa matundu ya vyoo mawili basi serikali ya ccm inatukuzwa vibaya
 
Socialists will make you think "maendeleo" ni favor na sio wajibu wao.
 
Rais Samia Suluhu aliahidi kumtua mama ndoo kichwani na sasa anaendelea kutimiza katika maeneo mbalimbali yaliyokuwa yamesahaulika
 
Watanzania asilimia zaid ya 80 wanaishi vijijini pia wale wakijengewaga vimiladi midogo midogo basi wanaitukuza ccm vibaya mno, watu wa vijijin hawanaga mahitaji makubwa sana ya kimiundombinu na hawa ndio wanaologwa sana na wanasiasa, wakijengewa matundu ya vyoo mawili basi serikali ya ccm inatukuzwa vibaya
Maji ni kitu muhimu sana mzee na ndio maana Rais Samia Suluhu ameipa kipaumbele na sasa asilimia kubwa ya vijiji maji safi na salama yanapatikana na miundombinu imeboreshwa pia fatilia miradi mbalimbali inayotekelezwa na Rais Samia Suluhu utagundua Mama haachi gepu mpaka vijijini
 
Umeongea kweli tupu yani hawa wajinga wa vijijini maji ni haki yao wao lakini wanaona hisani.
Nilikuwa najiuliza kwann waasi wanapopindua nchi huwa wanaua watu wasio na hatia wala silaha na kuchoma vijiji vyao.

Ila the way nimestudy jamii ya mtanzania nimegundua kuwa hawa wenzetu wa maeneo ya vijijini ndio wanaongoza kwa kuwasapoti serikali inayokuwa kandamizi na wanakubali kutumika kuiweka madarakani. So waasi huwa wanakuwa na hasira nao na kuwatokomeza kama masalia ya serikali dhalimu.

Now ndio naelewa kwann inakuwa vile.
 
Maji ni kitu muhimu sana mzee na ndio maana Rais Samia Suluhu ameipa kipaumbele na sasa asilimia kubwa ya vijiji maji safi na salama yanapatikana na miundombinu imeboreshwa pia fatilia miradi mbalimbali inayotekelezwa na Rais Samia Suluhu utagundua Mama haachi gepu mpaka vijijini
uko mnapasikia ni kule kunapooneshwa kwenye media, kuna vijiji vinapitia hali ngumu sana
 
Hayo magari mawilia tu hapo si ajabu yana thamani kuliko mradi na pengine karibia nyumba zote hapo kijijini kisha unapost ujinga huo hapa
 
Back
Top Bottom