Msanii
Platinum Member
- Jul 4, 2007
- 25,252
- 36,513
Umofia kwenu wana Great Thinkers.
Nilianzisha uzi huu uitwao Rais Samia hii wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum ina ukakasi kidogo. ambapo pamoja na mambo mengine nimeona kutenganisha uzi huo na huu ninaouweka hapa hasa kuishauri serikali kwenye masuala ya kimuundo na siyo kisera.
Tunafahamu kuna thread inayotrend inayotutaka wanagenzi wa masuala ya siasa na maendeleo kuishauri serikali, lakini hapa ninaweza uzi unaohusu kuishauri serikali hasa kwenye maeneo ya kimuundo na utawala.
Tunafahamu pia kwamba, serikali hususani ofisi ya Rais wapo wataalam mbalimbali wabobezi katika masuala nyeti ya nchi mpaka eneo muhimu la utawala. Lakini haiwatoi kwenye ulingo kwamba wao si wanadamu kama sisi tunaosaka tonge kupitia umachinga na gombania goli.
Kuna vitengo vingi vya serikali vinahusika na masuala kadhaa ya kisekta lakini inawezekana idara hizo zipo kwenye eneo ambalo kimuundo linachangoa kuzorota kwake. hivyo kupitia uzi huu tuishauri serikali kuweka muundo wake kiutawala vizuri hasa kupeleka ama kuhamishia idara muhimu kwenye wizara sahihi kwa minajili ya kujenga tija.
Ninaanza na kuishauri serikali kuangalia mgawanyo wa majukumu yaliyopo ndani ya wizara ya TAMISEMI hususani usimamizi wa miundombinu ya shule. Ikumbukwe kuwa miundombinu ina wizara yake na hayo majengo ya shule na vyuo mbalimbali ni mali ya umma chini ya serikali, hivyo miundombinu ya shule zetu ikawekwa Wizara ya miundombinu chini ya wakala wa majengo ya serikali itasaidia ufanisi na kuokoa bajeti kwa sababu TAMISEMI eneo la miundombinu ni wazi lazima watoe kandarasi za wataaluma na wasanifu ili kufanikisha miradi wanayoisimamia. Kule Wizara ya Ujenzi na Miundombinu wanaweza kufanya kazi kwa ufanisi na weledi mkubwa
Serikali irejeshe jukumu la elimu na kupanga madaraja kwenye Wizara mama ya elimu, inachoweza kufanya ni kuimarisha eneo la upangaji wa madaraja na kuanzisha idara kamili ya Mitaala ambayo kazi yake kubwa itakuwa kufuatilia ufanisi, maoni na uandaaji wa mitaala na kupitia mitaala yote inayotumika nchini kwa kuifanyia verification ya ubora wake.
TAMISEMI
iongezewe jukumu la msingi la ustawishaji demokrasia kupitia idara za tawala za mikoa hususanani mgawanyo wa madaraka kuanzia mitaa, vijiji, vitongoji, Kata na tarafa. Umuhimu wa hili ni kurudisha madaraka kwa wananchi kivitendo zaidi. kusimamia ratiba za mikutano ya wananchi, kuhakiki masuala mazima ya O&OD kutoka kwenye ngazi za vihihi na mitaa.
Mambo ya Ndani
Kitengo cha Mgambo kiwekwe ndani ya wizara hii badala kuacha kusimamiwa na kamati za ulinzi na usalama pekee. Hii itawasaidia wananchi kuelewa uwajibikaji wa jeshi hili la mgambo ambalo kimsingi haijulikani lipo chini ya wizara gani
MAENDELEO YA JAMII
Hii idara ama kitengo kinahusu Wizara ya Fedha, itakuwa ni tija kubwa Wizara ya Fedha ikasimamia maendeleo ya jamii kwa sababu tunaposema maendeleo ni kugusa mianya ya uchumi kwa sehemu kubwa.
Tuendelee kuishauri serikali kimuundo
Nilianzisha uzi huu uitwao Rais Samia hii wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum ina ukakasi kidogo. ambapo pamoja na mambo mengine nimeona kutenganisha uzi huo na huu ninaouweka hapa hasa kuishauri serikali kwenye masuala ya kimuundo na siyo kisera.
Tunafahamu kuna thread inayotrend inayotutaka wanagenzi wa masuala ya siasa na maendeleo kuishauri serikali, lakini hapa ninaweza uzi unaohusu kuishauri serikali hasa kwenye maeneo ya kimuundo na utawala.
Tunafahamu pia kwamba, serikali hususani ofisi ya Rais wapo wataalam mbalimbali wabobezi katika masuala nyeti ya nchi mpaka eneo muhimu la utawala. Lakini haiwatoi kwenye ulingo kwamba wao si wanadamu kama sisi tunaosaka tonge kupitia umachinga na gombania goli.
Kuna vitengo vingi vya serikali vinahusika na masuala kadhaa ya kisekta lakini inawezekana idara hizo zipo kwenye eneo ambalo kimuundo linachangoa kuzorota kwake. hivyo kupitia uzi huu tuishauri serikali kuweka muundo wake kiutawala vizuri hasa kupeleka ama kuhamishia idara muhimu kwenye wizara sahihi kwa minajili ya kujenga tija.
Ninaanza na kuishauri serikali kuangalia mgawanyo wa majukumu yaliyopo ndani ya wizara ya TAMISEMI hususani usimamizi wa miundombinu ya shule. Ikumbukwe kuwa miundombinu ina wizara yake na hayo majengo ya shule na vyuo mbalimbali ni mali ya umma chini ya serikali, hivyo miundombinu ya shule zetu ikawekwa Wizara ya miundombinu chini ya wakala wa majengo ya serikali itasaidia ufanisi na kuokoa bajeti kwa sababu TAMISEMI eneo la miundombinu ni wazi lazima watoe kandarasi za wataaluma na wasanifu ili kufanikisha miradi wanayoisimamia. Kule Wizara ya Ujenzi na Miundombinu wanaweza kufanya kazi kwa ufanisi na weledi mkubwa
Serikali irejeshe jukumu la elimu na kupanga madaraja kwenye Wizara mama ya elimu, inachoweza kufanya ni kuimarisha eneo la upangaji wa madaraja na kuanzisha idara kamili ya Mitaala ambayo kazi yake kubwa itakuwa kufuatilia ufanisi, maoni na uandaaji wa mitaala na kupitia mitaala yote inayotumika nchini kwa kuifanyia verification ya ubora wake.
TAMISEMI
iongezewe jukumu la msingi la ustawishaji demokrasia kupitia idara za tawala za mikoa hususanani mgawanyo wa madaraka kuanzia mitaa, vijiji, vitongoji, Kata na tarafa. Umuhimu wa hili ni kurudisha madaraka kwa wananchi kivitendo zaidi. kusimamia ratiba za mikutano ya wananchi, kuhakiki masuala mazima ya O&OD kutoka kwenye ngazi za vihihi na mitaa.
Mambo ya Ndani
Kitengo cha Mgambo kiwekwe ndani ya wizara hii badala kuacha kusimamiwa na kamati za ulinzi na usalama pekee. Hii itawasaidia wananchi kuelewa uwajibikaji wa jeshi hili la mgambo ambalo kimsingi haijulikani lipo chini ya wizara gani
MAENDELEO YA JAMII
Hii idara ama kitengo kinahusu Wizara ya Fedha, itakuwa ni tija kubwa Wizara ya Fedha ikasimamia maendeleo ya jamii kwa sababu tunaposema maendeleo ni kugusa mianya ya uchumi kwa sehemu kubwa.
Tuendelee kuishauri serikali kimuundo