Hatuwezi kukataa mikopo ya China inayolazimisha kampuni zao zitujengee?

Hatuwezi kukataa mikopo ya China inayolazimisha kampuni zao zitujengee?

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
Kwa nini Wachina wakitoa mikopo ya miondombinu kwa nchi za Afrika ni lazima kampuni zao zisuhusike katika ujenzi?

Kila kwenye miradi mikubwa walipofadhili Wachina unakuta kampuni ya China ndio contractor mkuu, Sasa hii huwa inakuwa na maana gani ukizingatia pesa zenyewe ni za mkopo lazima zirejeshwe? Kwani hatuna ubavu wa kukataa mikopo ya aina hiyo kama vile ambavyo huwa tunasema hatutaki pesa za masharti za Magharibi(japo huwa tunazichukua)??
 
Nafikiri hatuna wataalam waliobobea kujenga hivyo vitu katika ubora wa viwango vinavyotakiwa,pengne ni usimamizi wa kuhakikisha pesa inatumika kwenye mradi husika
 
Wangekua wanaweza wangekua washazikataa ufisadi ulojaa afrika kukataa pesa ama misaada ama mikataba ambayo nawao watapata chochote ni ngumu
 
Nafikiri hatuna wataalam waliobobea kujenga hivyo vitu katika ubora wa viwango vinavyotakiwa,pengne ni usimamizi wa kuhakikisha pesa inatumika kwenye mradi husika
Hatuna tutakua nao lini vyuo tulivyo navyo vina kazi gani
 
Nafikiri hatuna wataalam waliobobea kujenga hivyo vitu katika ubora wa viwango vinavyotakiwa,pengne ni usimamizi wa kuhakikisha pesa inatumika kwenye mradi husika
Tanzania ya leo tunakosa wataalamu wa kujenga barabara, madaraja na reli?
 
Kwa nini Wachina wakitoa mikopo ya miondombinu kwa nchi za Afrika ni lazima kampuni zao zisuhusike katika ujenzi?

Kila kwenye miradi mikubwa walipofadhili Wachina unakuta kampuni ya China ndio contractor mkuu, Sasa hii huwa inakuwa na maana gani ukizingatia pesa zenyewe ni za mkopo lazima zirejeshwe? Kwani hatuna ubavu wa kukataa mikopo ya aina hiyo kama vile ambavyo huwa tunasema hatutaki pesa za masharti za Magharibi(japo huwa tunazichukua)??
SAsa kwa hizi akili zenu mbovu za kumsifia sifia mama yenu kwenye kila chocho, na sasa hadi wazee walioheshimika kama yule wanayemuita askofu shoo ameingia kwenye huo ujinga, mnategemea mtakuwa hata na uadilifu wa kutumia hizi pesa mnazopewa katika ukamilifu wake au mtaishia kununua mashangingi na kulipia wasanii wanaokuja kurubuni wapiga kura.
 
SAsa kwa hizi akili zenu mbovu za kumsifia sifia mama yenu kwenye kila chocho, na sasa hadi wazee walioheshimika kama yule wanayemuita askofu shoo ameingia kwenye huo ujinga, mnategemea mtakuwa hata na uadilifu wa kutumia hizi pesa mnazopewa katika ukamilifu wake au mtaishia kununua mashangingi na kulipia wasanii wanaokuja kurubuni wapiga kura.
Kwani hizo pesa si mkopo? Si zitarudi tu hata kama zikitumika vibaya, kwani benki ikikupa mkopo wa duka huwa inakuja kukaa dukani kwako kukuagizia bidhaa na kupokea pesa za mauzo??
 
Kwani hizo pesa si mkopo? Si zitarudi tu hata kama zikitumika vibaya, kwani benki ikikupa mkopo wa duka huwa inakuja kukaa dukani kwako kukuagizia bidhaa na kupokea pesa za mauzo??
Wewe ungekuwa ni msimamizi wa taasisi inayotoa mikopo, ungekubali kumuachia mtu anayekopa kwako akasimamie matumizi ya huo mkopo wakati unamjua in and out kwamba hana uwezo wa kujisimamia ?
 
Wewe ungekuwa ni msimamizi wa taasisi inayotoa mikopo, ungekubali kumuachia mtu anayekopa kwako akasimamie matumizi ya huo mkopo wakati unamjua in and out kwamba hana uwezo wa kujisimamia ?
Kama ana dhamana za nyumba, kiwanja au gari vinavyoweza kuuzika kwa nini nisimuachie?!
Matajiri wengi wametajirika kwa njia hii.
 
Kama ana dhamana za nyumba, kiwanja au gari vinavyoweza kuuzika kwa nini nisimuachie?!
Matajiri wengi wametajirika kwa njia hii.
Lengo la mikopo ya China sio kujipatia utajiri, hence lazima msimamiwe ila matokeo yaonekane.
 
Back
Top Bottom