Havana: Shirika la Umeme la CUBA Limesema Halina uwezo wa Kusambaza Umeme Kulingana na Mahitaji ya Nchi.

Havana: Shirika la Umeme la CUBA Limesema Halina uwezo wa Kusambaza Umeme Kulingana na Mahitaji ya Nchi.

Yawezekana aslimia zaidi ya 90 waliokomenti kwenye huu uzi ni watoto wa elfu mbili, lah! basi kama nchi bado sana swala la ELIMU! ni changamoto. Hii elimu ya nchi yetu bado inashindwa kuandaa raia wenye kuwa na uwezo wa kuwa na CRITICAL na ANALYTICAL minds!!!imebidi nitumie lugha ya kimombo yamkini nisiandike sana.

HIvi ni nchi gani hasa ilioendelea kwa hao mnawaita WAWEKEZAJI/MADALALI NA MATAPELI wakaendesha uchumi wa nchi na inchi ikapaa kiuchumi.

Mnashindwa kuelewa na kutambua kuwa nchi kama CUBA imewekewa VIKWAZO na ndo chanzo cha mdororo wa kiuchumi ila mmekaririshwa kuwa ujamaa ndo umewafanya hivyo, hivi huko shule mlienda kusomea UJINGA?!!!Hizi cheap PROPAGANDA muwe na uwezo wa kuzitambua na kuzipuuza.

Mnataka CUBA akubali kuolewa na U.S.A kama SOUTH KOREA au JAPAN?? hawa wenyewe wameshachoka kuburuzwa wanaanza kutoka usingizini na kutaka kujitawala wenyewe.

Kwanini vijana mnakuwa matahira kiasi hiki. Nchi ya Cuba imejipambanua kimlengo wake ila wivu wa wanajiita wanademokrasi( U.S.A) inatumia mbinu tangu enzi kuididimiza CUBA na bado wamefeli.
China,USA,India and many others
 
Hali ya upatikanaji wa umeme Nchini CUBA imezorota baada ya shirika la Umeme la Taifa yaani Tanesco ya Cuba kusema halina umeme wa kuweza kuwafikishia Wananchi ambapo umeme unaohitajika ni megawatt 3000 na uliopp ni megawatt 500 tuu.

---
SHIRIKA la umeme nchini CUBA limesema linauwezo mdogo wa kusambaza umeme megawati 533 tu kati ya megawati zaidi ya 3,000 zinazohitajika.

Mapema serikali ya nchini humo imesema kipaumbele kwa sasa ni kupeleka umeme mahospitalini na vituo vya kusambaza maji na mashuleni na huduma zisizo za lazima za serikali zimefungwa hadi hapo baadaye.

Mji mkuu wa Havana unaendelea kusalia kwenye giza ingawa Shirika hilo la umeme kudai imetoa huduma hiyo kwa zaidi ya wateja 260,000 waliohitaji huduma ya umeme.

Utoaji wa huduma ya umeme nchini Cuba unadaiwa kushindwa kutokana na uhaba wa mafuta, majanga na mizozo ya kiuchumi.


Chanzo: Dw

My Take
Vinchi vya Kijinga kama hivi Huwa Vinaaekeza kwenye propaganda na Jeshi badala ya kuwekeza kwenye mambo ya msingi ya Nchi.

Tanzania tusije fikia level hizo za Nchi Maskini kama Cuba na ni aibu eti wanatupa na misaada.
Kafulila ataitumia hii kumtetea yule tapeli wake
 
Bila magufuli kutawala. Tanzania tulikuwa tunaelekea huku.

Madalali wa gesi walishavamia
Watu wanampinga Magufuli ni mashetani tu. Mwamba alikua anaitazama Tanzania ya kesho, yeye na Mkapa ndio unaona walikua na mipango ya kesho ya Tanzania, the rest wapo busy na mambo ya chap chap, upendwe leo lakini ukiisha toka madarakani hakuna kitu tangible ulicho kiacha, Watanzania tulio wengi ndio tunapenda hivo. RIP JPM
 
Watu wanampinga Magufuli ni mashetani tu. Mwamba alikua anaitazama Tanzania ya kesho, yeye na Mkapa ndio unaona walikua na mipango ya kesho ya Tanzania, the rest wapo busy na mambo ya chap chap, upendwe leo lakini ukiisha toka madarakani hakuna kitu tangible ulicho kiacha, Watanzania tulio wengi ndio tunapenda hivo. RIP JPM
Mambo ya mbele ni kama yapi ambayo wengine hawakufanya na hawafanyi?

Ujinga na kushikiwa akili ni mzigo
 
Putin mwenyewe kwenye issue ya kuanzisha sarafu ya BRICS ili kuiondoa dollar amesema alikuwa anatania tu
Urusi hategemei Marekani kwa chichote kile wewe pimbi, Urusi kama ni umeme anai hadi wa kuuzia Ulaya huko, Urusi ni moja ya nchi zenye umeme hadi wa ziada, anauza umeme hadi China. endelea kujifariji
 
Bila magufuli kutawala. Tanzania tulikuwa tunaelekea huku.

Madalali wa gesi walishavamia
Naungana na wewe. Kwenye nishati na usafirishaji hasa SGR HAKUNA KAMA MAGUFULI. fikiria hivi sasa eti wanashindwa kudhibiti hujuma ndogondogo.
Magufuli nilikuwa nampinga kwenye mambo mengine ila sio swala la nishati kwa unumla
 
Naungana na wewe. Kwenye nishati na usafirishaji hasa SGR HAKUNA KAMA MAGUFULI. fikiria hivi sasa egi wanashindwa kudhibiti hujuma ndogondogo.
Magufuli nilikuwa nampinga kwenye mambo mengine ila sio swala la nishati kwa unumla
Unawezaje kushangilia uwekezaji wa Sgr wa Trilioni 13 kuanzia Dar-Dom kwenye Nchi ambayo 80% ya Barabara ni mavumbi na Mikoa haijaunganishwa?

Ni kichaa tuu na mpumbavu ndio anaweza shangilia jambo la kufanya watu Waendelee kuwa mafukara milele.

Hata bila Magufuli umeme ungepatikana kama ambavyo ulipatikana kabla ya bwawa la Nyerere na hata Sasa miradi mingine inaendelea
 
Unawezaje kushangilia uwekezaji wa Sgr wa Trilioni 13 kuanzia Dar-Dom kwenye Nchi ambayo 80% ya Barabara ni mavumbi na Mikoa haijaunganishwa?

Ni kichaa tuu na mpumbavu ndio anaweza shangilia jambo la kufanya watu Waendelee kuwa mafukara milele.

Hata bila Magufuli umeme ungepatikana kama ambavyo ulipatikana kabla ya bwawa la Nyerere na hata Sasa miradi mingine inaendelea
Nashangilia nishati.
 
Mambo ya mbele ni kama yapi ambayo wengine hawakufanya na hawafanyi?

Ujinga na kushikiwa akili ni mzigo
Nikukumbushe tu; Tanzania imeanza kuonja mgao wa umeme mwaka 1992, wakati huo rais akiwa ni Ali Hassan Mwinyi, think tank ya wakati huo ikaona iingie mkataba na IPTL, nadhani unajua IPTL ndio iliokuja kuzaa escrow account scandal. Ni miaka hiyo hiyo ndio tulipowauzia Waarabu mbuga ya Loliondo, hadi leo mie binafsi sijawahi kuelewa why tuliuza mbuga ile na baadae watu wakaigeuza kua nchi ndani ya nchi, tabia hiyo hiyo imerudia tena awamu hi. Sina hakika kama walau unaweza kunambia taifa linapata faida gani kwa hatua hizo.
Mashirika mengi ya umma yalianza kuporomoka kibiashara, wizi, ufisadi kwenye mashirika hayo ulikua mkubwa mno, nyakati zile wafanyakazi wa umma na wafanyabiashara walikua na pesa kuliko serikali, nikukumbushe tu, ilifika hatua IMF, world bank, Paris club wakakataa kutoa misaada na mikopo kwa Tanzania wakidai, sie tunasamehe wafanyabiashara KODI, waziri wa fedha wa wakati huo alikua ni professional wa uchumi bwana Kighoma Ali Malima, alifukuzwa barazani kwa shinikizo kutoka nje na hapa sasa ndio umaarufu wa J. Kikwete ulipopanda. Yapo mengi, now mzee wa Lupaso akaaingia madarakani (RIP ) huyu sasa ndio aliyeanza kuleta heshima makazini, watu wapande vyeo kwa elimu; walimu wa UPE walitakiwa kujiendeleza ili walau wapate vyeti vya form 4, elimu ikaanza kua na maana (that's future) akaanza kujenga misingi ua utawala bora, taasisi nyingi unazo zijua leo zimetengenezwa na BWM, tukaanza kuona hata ujenzi wa barabara, viwanja vya ndege nk. Enzi zake mwamba yule, mgao wa umeme yes ulikiwepo but sio kila mwaka kama ilivokua kwa mtangulizi wake na aliyemfuata. Mgao mkali (kama nitakua nakumbuka vizuri ) ulikua mwaka 1998, aliyemfuata sasa ndio khaa, mgao hadi masaa 16 kwa siku halafu kila mwaka, tukaingia kwenye mikataba ambayo sio ya utatuzi wa umeme kwa maana ya future, ni temporary tu, ndio ikaja Richmond/Dowans, baadae sijui Symbio nk, mwishoni mwa utawala wake ndio ikapigwa pesa ya maana hasa, Escrow account. Magufuli alipokuja akaanza kurekebisha mambo, umeme huo hapo, katanua gati za bandari ya Dar, mikataba ya madini hasa dhahabu I think umeona, nchi ikaanza kua na heshima, baadhi ya mataifa ya Africa yakaanza ku copy from us. Hatimae mwamba yule akafariki.
Vipi, niendelee?
 
Ya uhakika imepatikana baada ya huu mradi. Ya uhakika ilikuwa inapatikana tu kwenye taasisi nyeti za kiserikali. Huku majumbani ilikuwa ovyoovyo
Nchi ilikosa Nishati ya uhakika baada ya Mkapa Kushindwa kuwekeza kwenye Tanesco Kwa miaka 5 Kwa sababu Tanesco iliwekwa pending Ili ibinafsishwe.

Hadi maamuzi ya kuacha kubinafsisha ndio akawa Anatokea madarakani,athari zake zinaonekana Kwa JK .

JK akawekeza kwenye gesi na umeme ukapatikana.Anatoka Madarakani amejenga Bomba la gesi anaingia Mwendazake ambae akaachana na gesi akaanza mradi wa bwawa.

Anatoka akaacha shida Kwa Samia ,umeme wa gesi hautoshi na bwawa halina dalili ya kukamilika.

Samia amepambana na bwawa limekamilika shida ya umeme imekata.

Lakini umeme huu hauna hata miaka 5 ijayo utakuwa umekwisha ndio maana Serikali inaendelea na uwekezaji mwingine kwenye vyanzo vipya.

By the way hakuna tena shida ya umeme itakuja kutokea Kwa miaka hata 20 ijayo Kwa sababu Grid za umeme Kwa Sasa ziko interconnected ,tutatumia umeme wa Ethiopia au DRC in case kuna upungufu.
 
Nikukumbushe tu; Tanzania imeanza kuonja mgao wa umeme mwaka 1992, wakati huo rais akiwa ni Ali Hassan Mwinyi, think tank ya wakati huo ikaona iingie mkataba na IPTL, nadhani unajua IPTL ndio iliokuja kuzaa escrow account scandal. Ni miaka hiyo hiyo ndio tulipowauzia Waarabu mbuga ya Loliondo, hadi leo mie binafsi sijawahi kuelewa why tuliuza mbuga ile na baadae watu wakaigeuza kua nchi ndani ya nchi, tabia hiyo hiyo imerudia tena awamu hi. Sina hakika kama walau unaweza kunambia taifa linapata faida gani kwa hatua hizo.
Mashirika mengi ya umma yalianza kuporomoka kibiashara, wizi, ufisadi kwenye mashirika hayo ulikua mkubwa mno, nyakati zile wafanyakazi wa umma na wafanyabiashara walikua na pesa kuliko serikali, nikukumbushe tu, ilifika hatua IMF, world bank, Paris club wakakataa kutoa misaada na mikopo kwa Tanzania wakidai, sie tunasamehe wafanyabiashara KODI, waziri wa fedha wa wakati huo alikua ni professional wa uchumi bwana Kighoma Ali Malima, alifukuzwa barazani kwa shinikizo kutoka nje na hapa sasa ndio umaarufu wa J. Kikwete ulipopanda. Yapo mengi, now mzee wa Lupaso akaaingia madarakani (RIP ) huyu sasa ndio aliyeanza kuleta heshima makazini, watu wapande vyeo kwa elimu; walimu wa UPE walitakiwa kujiendeleza ili walau wapate vyeti vya form 4, elimu ikaanza kua na maana (that's future) akaanza kujenga misingi ua utawala bora, taasisi nyingi unazo zijua leo zimetengenezwa na BWM, tukaanza kuona hata ujenzi wa barabara, viwanja vya ndege nk. Enzi zake mwamba yule, mgao wa umeme yes ulikiwepo but sio kila mwaka kama ilivokua kwa mtangulizi wake na aliyemfuata. Mgao mkali (kama nitakua nakumbuka vizuri ) ulikua mwaka 1998, aliyemfuata sasa ndio khaa, mgao hadi masaa 16 kwa siku halafu kila mwaka, tukaingia kwenye mikataba ambayo sio ya utatuzi wa umeme kwa maana ya future, ni temporary tu, ndio ikaja Richmond/Dowans, baadae sijui Symbio nk, mwishoni mwa utawala wake ndio ikapigwa pesa ya maana hasa, Escrow account. Magufuli alipokuja akaanza kurekebisha mambo, umeme huo hapo, katanua gati za bandari ya Dar, mikataba ya madini hasa dhahabu I think umeona, nchi ikaanza kua na heshima, baadhi ya mataifa ya Africa yakaanza ku copy from us. Hatimae mwamba yule akafariki.
Vipi, niendelee?
Mgao wa umeme chanzo ni Kushindwa Kwa Nyerere kuwekeza kwenye vyanzo vipya akamuuzia mbuzi Mwinyi.

Kosa la pili alifanya Mkapa.kwa kutowekeza kwenye umeme Kwa sababu walitaka kubinafsisha Tanesco,miaka 5 bila uwekezaji Mpya akauzia mbuzi JK.

Kosa la 3 alifanya Mwendazake akijua kabisa ujenzi wa bwawa utachukua mda mrefu hakuandaa umeme wa matumizi kipindi Cha mpito,akamuangushia Zigi Samia.

Mwisho usitegemee tena mgao ,ukiacha mipango na miradi ya ndani lakini grid interconnectivity kuanzia Ethiopia Hadi South Africa tayari so shida ya kukosa umeme haitakuja kutokea tena.
 
Urusi hategemei Marekani kwa chichote kile wewe pimbi, Urusi kama ni umeme anai hadi wa kuuzia Ulaya huko, Urusi ni moja ya nchi zenye umeme hadi wa ziada, anauza umeme hadi China. endelea kujifariji
Sasa hii comment yako inahusiana vipi na kauli ya Putin? Uuna akili kweli, aongee Putin halafu wewe uje kunibong'olea mimi
 
Back
Top Bottom