Hawa ni watu maarufu duniani ambao viatu vyao vimekosa mvaaji

Hawa ni watu maarufu duniani ambao viatu vyao vimekosa mvaaji

Yani Bob alikufa na mika 36 tuu jamani lakini aliacha watoto kadhaa si haba
Bob Marley alikufa akaacha watoto 12 wanaotambulika kisheria. Aliacha watoto wa kiume 7, na wa kike 5.
Watoto wa kiume alioacha ni 👇

1) Ziggy Marley
2) Damian Marley
3) Rohan Marley
4) Stephen Marley
5) Ky- Mani Marley
6) Julian Marley
7) Robert Marley

Na wa kike alioacha ni 👇

1) Cedalla Marley
2) Sharon Marley
3) Stephanie Marley
4) Karen Marley
5) Makeda Jahnesta Marley

Hao ni wale wanaofahamika kweny public, sasa haijulikani kama pembeni aliacha wangapi.
 
Bob Marley alikufa akaacha watoto 12 wanaotambulika kisheria. Aliacha watoto wa kiume 7, na wa kike 5.
Watoto wa kiume alioacha ni 👇

1) Ziggy Marley
2) Damian Marley
3) Rohan Marley
4) Stephen Marley
5) Ky- Mani Marley
6) Julian Marley
7) Robert Marley

Na wa kike alioacha ni 👇

1) Cedalla Marley
2) Sharon Marley
3) Stephanie Marley
4) Karen Marley
5) Makeda Jahnesta Marley

Hao ni wale wanaofahamika kweny public, sasa haijulikani kama pembeni aliacha wangapi.
Alikua shababi
 
Bruce nae alikufa mdogo sana nini kilimuua huyu mwamba?
Huyu mwamba Bruce Lee inasemekana aliwekewa sumu, japo mpaka leo haijathibitishwa aliwekewajwe wekewajwe sumu? Na nani? Na kwa malengo gani?
Kila mtu anaongea lake, ila mwamba na yey aliacha watoto wawili. Wa kiume mmoja alieitwa Brandon Lee (marehemu) na wa kike mmoja anaeitwa Shannon Lee.
 
Alikua shababi
Huyu kila kiungo chake kilikuwa na kazi yake.
I) kichwa kilitunga nyimbo
2) mikono iliandika
3) mdomo uliimba
4) kiuno kilileta watoto 😂😂😂
5) miguu ilitembea na kucheza reggae kwa style yake mwenyewe.
 
Mnamuachaje ndala kasheba aisee
Ya mwamba alikuwa vizuri ila bado alikumbana na vichwa vikubwa kama kina Marijani Rajabu, Mbaraka Mwinshehe nk. Hao niliowataja walikuwa ni moto wa kuotea mbali sana.
Ukifuatilia kwa makini utagundua kuna mambo mengi yalioimbwa na Marijani ndio yanatokea sasa.
Jamaa ni kama vile alikuwa akitabiri mambo mengi na yakatokea na zingine ni visa vya kweli vilivyomgusa yeye binafsi, rafiki au ndugu zake, so ni vigumu ndala kuweka mguu kwa huyu mwamba wa Jojina, usia wa baba, mwanameka, sadiki, masudi, ndoa ya mateso, dunia uwanja wa fujo nk.
 
Ingawa uzi wako umechanganya musicians na wasio musicians, binafsi charity start at home,Said Mabera Ile solo yake inayakabana koo na piano, sitegemei nchi hii itampata mbadala wake ohoooo Shabaan Dede.....Fatumaaaaaaaa nasafiri mamaaaa, naona niishei hapa maana nimeshaanza kuwa emotional hapa
[emoji15] Hapa namuweka Shaaban Yohana "WANTED huyu mwamba kwa TZ ni habari nyingine.
 
[emoji15] Hapa namuweka Shaaban Yohana "WANTED huyu mwamba kwa TZ ni habari nyingine.
Ya ni kweli, huyu mwamba nae aliacha legacy kubwa kwenye tasnia ya mzikj wetu. RIP Shaban Wanted.
 
Hapo kwa Bob Male
nadhani umemsahau Lucky Dube alivivaa na vikamtosha kabisa sema wenye roho mbaya wanapitia kipindi cha pili dakika ya 89.5
Lucky alifanya mambo makubwa kweny mziki wa reggae mpaka waJamaika walianza kumchukia bila sababu. Waliona jamaa anawapoteza katika ulimwengu wa reggae.
 
G.O.A.TS
 

Attachments

  • FB_IMG_16622804695642221.jpg
    FB_IMG_16622804695642221.jpg
    37 KB · Views: 15
Za asubuhi wakuu, leo nakuja na makala ya watu maarufu duniani, ambao wameacha alama kubwa katika tasnia zao na mpaka leo hakuna alietokea kuziba mapengo yao.

1) Mohammedi Ali
Huyu ni bingwa, mbabe na mtemi wa masumbwi ulimwenguni kote. Mohammed Ali ambae alizaliwa 17 January 1942, huko Louisville, Kentucky Marekani na kufariki 3 June 2016, huko Scottsdale, Arizona Marekani. Alikuwa ni bondia wa pekee kuufanya mchezo huo uwe na wapenzi na waangaliaji wengi ulimwenguni.

Licha ya kwamba mchezo huo ulikuwepo maelfu ya miaka kabla ya ujio wake Ali, lkn ni yeye ndio aliefanya watu waanze kuupenda zaidi mchezo huo na kuchukua nafasi ya pili kwa kupendwa duniani baada ya mchezo wa mpira wa miguu. Ali ambae alikuwa na uwezo mkubwa wa kumiliki ulingo, kukwepa ngumi, na mwepesi wa kupiga ngumi za haraka haraka. Lakini pia alikuwa na mbinu nyingi za kuweza kumchosha na kummaliza kbs mpinzani wake wakati wowote alioutaka yeye ulingoni.

Ali alikuwa na uwezo wa kumsogezea mpinzani sura, lkn utashangaa hadi round nzima inaisha bila mpinzan wake kufanikiwa kumpiga ngumi hata 1 tu usoni (kama tuonavyo pichani) sometimes unakuta mpinzani wake anarusha ngumi (kota) na kuanguka mwenyewe, huku Ali akimtizama kwa dharau 😂😂🤣🤣

Pamoja na yote lkn kama ilivyo michezo mingine na yey kuna muda alikuwa anapoteza baadhi ya mapambano pia, aidha kwa kutokana na mchoko wa mazoezi makali anayokuwa amefanya kabla ya pambano nk. Toka Ali alipostaafu ngumi mpaka kifo chake, hakuna bondia ambae ashawahi kufikia rekodi ya upiganaji wake na vituko vyake awapo ulingoni na nje ya ulingo.

Mabondia wengi kama kina Mike Tyson, Evander, Lenox Lewis na wengineo walikuwa wanakwenda kumuona na kupata mbinu mbali mbali za kupigana ulingoni kupitia mfalme huyo wa ngumi ulimwenguni. Huyu ndio Mohammed Ali alieacha alama kubwa ktk mchezo huo maarufu wa ngumi duniani. Hakuna na hatotokea Mohammed Ali mungine, Never.
Mungu ailaze roho ya huyu Legend mahali pema peponi.

View attachment 2335340

2) Bob Marley
Bob Marley alizaliwa 6 Feb 1945, huko Nine Mile, Jamaica, na kufariki 11 May 1981, huko Florida Marekani.

Alipozaliwa aliukuta mzikiwa reggae ukiwa ulimwenguni miaka na miaka. Lkn kwa kipaji chake na uwezo wake akaanza kuleta mabadiliko makubwa katika mziki huo, hadi kufikia hatua ya kusikilizwa na viongozi wakubwa wa nchi mbali mbali. Japo kulikuwa na waimbaji wengine wakubwa kama kina Peter Tosh, Burn Spear nk, lkn ni yeye Bob Marley ndio aliefanya reggae ipendwe na walio wengi. Hadi anakufa Bob Marley aliacha muziki huo ukiwa na mamilioni ya wasikilizaji ulimwenguni.

Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi.

View attachment 2335341

3) Bruce Lee
Bruce Lee alizaliwa 27 Nov 1940, huko San Francisco, California Marekani na kufariki 20 July 1973 huko Kow loon Tong, Hong Kong.

Bruce alizaliwa na kuukuta mchezo wa kung fu au karate ulimwenguni. Lakini kwa kipaji alichozaliwa nacho, alianza kuleta mabadiliko makubwa kwenye mchezo huo hadi kushawishi mamilioni ya watu ulimwenguni kuupenda na kuanza kuufuatilia mchezo huu. Bruce alikuwa na uwezo mkubwa wa kucheza na hisia za adui na kujua ni wapi atapopiga lazima adui atakaa tu hata awe na mwili kama jumba.

Ikafika kipindi watu wakamshauri ajiunge kwenye tasnia ya uigizaji ili kuwavutia watu zaidi kuupenda mchezo huo, lkn pia kujifunza baadhi ya mbinu za upambanaji kupitia movie zake. Mpaka toka Bruce afariki mpaka leo bado anapewa heshima kubwa na magwiji wa mchezo huo wakiwemo wacheza sinema kama vile Jackie Chan, Jet Lee nk. Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi.

View attachment 2335338

Wanaofuatia ni 👇
4) Michael Jackson king wa Pop na mitelezo.

5) 2pac Shakur king wa Hip hop aliekuwa haiogopi serikali ktk kuwatetea wamarekani weusi wenzake na jamii nyingine zilizobaguliwa nchini Marekani, pia alipambana sana na polisi kuhusu unyanyasaji wowote uliofanywa na jeshi hilo kwa vijana mbali mbali hadi alipouwawa. Aliwahi kuwa na kesi ya kuwashambulia polisi wawili na bunduki, baada ya 2pac kupita sehem na gari aliwakuta polisi wakiwa wamemfunga pingu mtu mweusi huku wanampiga, kitendo kile kilimuuzi 2pac ndipo alipoamua kutoa bastola yake na kuwashambulia polisi, japo baadae polisi wale waliwahishwa hospital na kupona.
Katika kesi ile 2pac hakuhukumiwa baada ya kuonekana kuwa wale polisi walikuwa na makosa ya kiutendaji kwa mtuhumiwa waliekuwa wamemkamata.
Mungu awalaze roho zao mahali pema peponi.

6) Michael Jordan
Mzee wa kudumbukiza kikapuni. Huyu alikuwa na uwezo wa kuruka juu zaidi na kuonekana kama ameganda kwa sekunde kadhaa hewani kabla ya kutia mpira kapuni na kushuka chini. Toka astaafu bado hajapatikana Jordan mungine, japo bwana mdogo hayati Kobe Bryant alijitahidi kwa namna fulan, lkn bado hakufikia kule alipofikia mzee wa kazi.

View attachment 2335342

Hawa ni baadhi ya watu ambae mpaka leo viatu vyao viko wazi, havijapata wa kuvivaa vikawatosha.
Wengine wote sawa, ila kwa 2Pac umechemka.
 
😂😂😂 hakuna king wawili kwenye tasnia. Hapo kwenye mpira tayari kaishabana mzee Pele wa brazil toka miaka hiyo. Hata waliotaka na Maradonna aongezwe walichemsha, sembuse ije kuwa bwana mdogo Mesi??
RIP gwiji na mfalme wa mpira wa miguu Edson Arantes do Nascimento aka "Pele". Dunia itakukumbuka kwa umahiri wako wa kulisakata kabumbu na kushinda mabao mengi zaidi katika historia ya mchezo huu wa mpira.
 
Back
Top Bottom