Hawa ni watu maarufu duniani ambao viatu vyao vimekosa mvaaji

Hawa ni watu maarufu duniani ambao viatu vyao vimekosa mvaaji

Wakati Pele anacheza soka hakukua hata na sheria ya Offside,alikua anatupia tu kambani,

MESSI ndio mfalme wa soka hata makocha wakubwa wanatambua hilo,

Ila ruksa kwako kuamini kua Pele ndio King.
Mzee unatudanganya makusudi..sheria ya offside ipo toka 1863 huko tena ilikuwa ngumu zaidi kipindi cha kina pele, imeenda inapunguzwa makali 1990 hadi leo kina messi wameikuta ni mdebwedo. Siku hizi ili uwe onside inabidi uwe level na defense line wakati zamani ilikuwa lazima mbele yako wawepo wapinzani watatu kisha ikapunguzwa kuwa wawili.
 
Ebuuu Mleta uzi chokoza mada watu watuletee List ya Wanasayansi bora dunian, Maana nishashindwa kumlinganisha Newton na Washkaj zake wa enzi hizo.
Uzi huo upo hapa JF..Mabishano Ni makali Kati ya Einstein.. Newton na Tesla Nani mkali
 
Mzee unatudanganya makusudi..sheria ya offside ipo toka 1863 huko tena ilikuwa ngumu zaidi kipindi cha kina pele, imeenda inapunguzwa makali 1990 hadi leo kina messi wameikuta ni mdebwedo. Siku hizi ili uwe onside inabidi uwe level na defense line wakati zamani ilikuwa lazima mbele yako wawepo wapinzani watatu kisha ikapunguzwa kuwa wawili.
I see..!
Waache ubishi..PELE ni zaidi
 
Kila anguko Lina sababu zake. Anguko la Ali kupigwa na Smokin Frazier nk. So sababu ya Ali kuonekana hakua Bora kwa yaliyompata. Historia itamwandika hivyohivyo i'la itataja na sababu..
Mike Iron Tyson alipigwa na Holy field katika 2005 binafsi sikushangaa .. zipo sababu za anguko lile.. lakini halizuii historia kusema Kwamba Tyson alikua Bora lakini aliyepigwa Mara kadhaa...
We'we boss Ni Kama unahisi Ni hatia kusema Kwamba Ali alipigwa Mara kadhaa
Mkuu mbona niliandika katika thread kuwa pamoj na ubora wake lkn kuna baadhi ya mapambano ambayo alipigwa, au haukusome thread yote vizuri?
Na pia nnachokumbuka Tyson alipigwa na Holyfield mwaka 1996. Tyson alikuwa bora na ataendelea kuwa na heshima hiyo hata baada ya kifo chake, lkn hii haiondoi ukweli kwamba Mohammad Ali ndio king haswa wa mchezo huo.
 
Sijawahi ona bondia wa uzito wa juu mwenye mapigo ya Mike Iron Tyson. Tofauti na Ali ambaye alikua Mwanaharakati dhidi ya ubaguzi na Vita Kwa Mike yeye alikua mtu asiyejali mwenye vurugu Mara kadhaa akituhumiwa kubaka, kupigana mashabiki na hata Polisi.
Ali hakuwa mwenye makasiriko Bali mpole, nidhamu, licha ya changamoto kadhaa zilizomletea migogoro kadha wa kadha.
Tyson alikuwa vizuri kwenye kutupa ngumi, yani akikupiga ngumi lazima uhisi kitu kizito mithili ya gunia la kilo 100 kimekuangukia kichwani. Pia sifa za ukorofi na hasira za hapa na pale alikuwa nazo sana. Hii ni kutokana na maisha aliyokulia, Mike amekulia mitaani kwahiyo zile tabia bado alikuwa nazo mpaka ukubwani.

Kwa upande wa Ali yeye alikuwa mwamba wa kukwepa masumbwi. Ali alikuwa na uwezo wa kumchezesha adui yake ulingoni round nzima bila kupigwa ngumi hata 1 (kama unavyoona hapo pichan), yani anamsogezea sura adui lkn adui akirusha kombora hola. Ali akishaona adui amechoka sasa ndo anaanza kumuadhibu kwa namna anavyotaka yeye. Wengine alikuwa anawaonea hata huruma anawanyanyua baada ya kuwaangusha kwa KO.
Kuhusu tabia Ali alikuwa ni mtu mwenye kiburi, mwenye kujiamini na asiependa dharau wala kushikiwa akili na mtu yoyote. Ndo maana serikali ilichemsha kumpeleka Vietnam kupigana.
Licha ya hivyo Ali alikuwa mwenye upendo kwa watu wote bila kujali rangi zao, lkn pia alikuwa anapenda kufanya u comedy kwa watu mbali mbali.
 

Attachments

  • images (35).jpeg
    images (35).jpeg
    19.2 KB · Views: 11
  • images (36).jpeg
    images (36).jpeg
    19.8 KB · Views: 10
  • images (34).jpeg
    images (34).jpeg
    26.8 KB · Views: 10
Mzee unatudanganya makusudi..sheria ya offside ipo toka 1863 huko tena ilikuwa ngumu zaidi kipindi cha kina pele, imeenda inapunguzwa makali 1990 hadi leo kina messi wameikuta ni mdebwedo. Siku hizi ili uwe onside inabidi uwe level na defense line wakati zamani ilikuwa lazima mbele yako wawepo wapinzani watatu kisha ikapunguzwa kuwa wawili.
Asante mkuu kwa kuweka comment bora yenye mafunzo kwa wale wasioelewa tasnia ya soka na sheria zake kwa ujumla. Huyu anamzungumzia Mesi ambae asingeweza kufanya lolote mbele ya wakongwe kina Zidane, Ronaldo de Lima, Ronaldinho nk.
Mesi angekutana na ukuta kama ule wa Robert Carlos asingeweza kupenya kwa namna yoyote ile. Enzi hizo ulitakiwa uwe na nguvu, akili, maarifa na mpira na mbio. Sasa Mesi anakimbia na mpira na kuanguka mwenyewe unafikiri angewezaje game lile.
 
Vya kale dhahabu,hata Marcelo kafanya yote aliyofanya Carlos lakini tuzo ufalme WA namba 3 ni WA Roberto carlos
Shukran mkuu, jamaa nimemfafanulia vizuri kwahiyo post ya hapo juu kabla ya hii kwamba Mesi mbele ya Carlos asingeweza kuthubutu kutia mguu. Ule ukuta wa Carlos ulikuwa ni wa chuma mkuu, Mesi asingeweza kupiga chenga hata 1.
 
Asante mkuu kwa kuweka comment bora yenye mafunzo kwa wale wasioelewa tasnia ya soka na sheria zake kwa ujumla. Huyu anamzungumzia Mesi ambae asingeweza kufanya lolote mbele ya wakongwe kina Zidane, Ronaldo de Lima, Ronaldinho nk.
Mesi angekutana na ukuta kama ule wa Robert Carlos asingeweza kupenya kwa namna yoyote ile. Enzi hizo ulitakiwa uwe na nguvu, akili, maarifa na mpira na mbio. Sasa Mesi anakimbia na mpira na kuanguka mwenyewe unafikiri angewezaje game lile.
Acheni unazi bila facts. Messi kaanza kucheza Barca wakati hao wote uliowataja bado wanacheza. Sijui hizo info zenu huwa mnazitoa wapi?
 
Mkuu mbona niliandika katika thread kuwa pamoj na ubora wake lkn kuna baadhi ya mapambano ambayo alipigwa, au haukusome thread yote vizuri?
Na pia nnachokumbuka Tyson alipigwa na Holyfield mwaka 1996. Tyson alikuwa bora na ataendelea kuwa na heshima hiyo hata baada ya kifo chake, lkn hii haiondoi ukweli kwamba Mohammad Ali ndio king haswa wa mchezo huo.
Pambano la pili 2005 . Alipomn'gata skio Holyfield
 
Tyson alikuwa vizuri kwenye kutupa ngumi, yani akikupiga ngumi lazima uhisi kitu kizito mithili ya gunia la kilo 100 kimekuangukia kichwani. Pia sifa za ukorofi na hasira za hapa na pale alikuwa nazo sana. Hii ni kutokana na maisha aliyokulia, Mike amekulia mitaani kwahiyo zile tabia bado alikuwa nazo mpaka ukubwani.

Kwa upande wa Ali yeye alikuwa mwamba wa kukwepa masumbwi. Ali alikuwa na uwezo wa kumchezesha adui yake ulingoni round nzima bila kupigwa ngumi hata 1 (kama unavyoona hapo pichan), yani anamsogezea sura adui lkn adui akirusha kombora hola. Ali akishaona adui amechoka sasa ndo anaanza kumuadhibu kwa namna anavyotaka yeye. Wengine alikuwa anawaonea hata huruma anawanyanyua baada ya kuwaangusha kwa KO.
Kuhusu tabia Ali alikuwa ni mtu mwenye kiburi, mwenye kujiamini na asiependa dharau wala kushikiwa akili na mtu yoyote. Ndo maana serikali ilichemsha kumpeleka Vietnam kupigana.
Licha ya hivyo Ali alikuwa mwenye upendo kwa watu wote bila kujali rangi zao, lkn pia alikuwa anapenda kufanya u comedy kwa watu mbali mbali.
Well said br
 
Za asubuhi wakuu, leo nakuja na makala ya watu maarufu duniani, ambao wameacha alama kubwa katika tasnia zao na mpaka leo hakuna alietokea kuziba mapengo yao.

1) Mohammedi Ali
Huyu ni bingwa, mbabe na mtemi wa masumbwi ulimwenguni kote. Mohammed Ali ambae alizaliwa 17 January 1942, huko Louisville, Kentucky Marekani na kufariki 3 June 2016, huko Scottsdale, Arizona Marekani. Alikuwa ni bondia wa pekee kuufanya mchezo huo uwe na wapenzi na waangaliaji wengi ulimwenguni.

Licha ya kwamba mchezo huo ulikuwepo maelfu ya miaka kabla ya ujio wake Ali, lkn ni yeye ndio aliefanya watu waanze kuupenda zaidi mchezo huo na kuchukua nafasi ya pili kwa kupendwa duniani baada ya mchezo wa mpira wa miguu. Ali ambae alikuwa na uwezo mkubwa wa kumiliki ulingo, kukwepa ngumi, na mwepesi wa kupiga ngumi za haraka haraka. Lakini pia alikuwa na mbinu nyingi za kuweza kumchosha na kummaliza kbs mpinzani wake wakati wowote alioutaka yeye ulingoni.

Ali alikuwa na uwezo wa kumsogezea mpinzani sura, lkn utashangaa hadi round nzima inaisha bila mpinzan wake kufanikiwa kumpiga ngumi hata 1 tu usoni (kama tuonavyo pichani) sometimes unakuta mpinzani wake anarusha ngumi (kota) na kuanguka mwenyewe, huku Ali akimtizama kwa dharau 😂😂🤣🤣

Pamoja na yote lkn kama ilivyo michezo mingine na yey kuna muda alikuwa anapoteza baadhi ya mapambano pia, aidha kwa kutokana na mchoko wa mazoezi makali anayokuwa amefanya kabla ya pambano nk. Toka Ali alipostaafu ngumi mpaka kifo chake, hakuna bondia ambae ashawahi kufikia rekodi ya upiganaji wake na vituko vyake awapo ulingoni na nje ya ulingo.

Mabondia wengi kama kina Mike Tyson, Evander, Lenox Lewis na wengineo walikuwa wanakwenda kumuona na kupata mbinu mbali mbali za kupigana ulingoni kupitia mfalme huyo wa ngumi ulimwenguni. Huyu ndio Mohammed Ali alieacha alama kubwa ktk mchezo huo maarufu wa ngumi duniani. Hakuna na hatotokea Mohammed Ali mungine, Never.
Mungu ailaze roho ya huyu Legend mahali pema peponi.

View attachment 2335340

2) Bob Marley
Bob Marley alizaliwa 6 Feb 1945, huko Nine Mile, Jamaica, na kufariki 11 May 1981, huko Florida Marekani.

Alipozaliwa aliukuta mzikiwa reggae ukiwa ulimwenguni miaka na miaka. Lkn kwa kipaji chake na uwezo wake akaanza kuleta mabadiliko makubwa katika mziki huo, hadi kufikia hatua ya kusikilizwa na viongozi wakubwa wa nchi mbali mbali. Japo kulikuwa na waimbaji wengine wakubwa kama kina Peter Tosh, Burn Spear nk, lkn ni yeye Bob Marley ndio aliefanya reggae ipendwe na walio wengi. Hadi anakufa Bob Marley aliacha muziki huo ukiwa na mamilioni ya wasikilizaji ulimwenguni.

Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi.

View attachment 2335341

3) Bruce Lee
Bruce Lee alizaliwa 27 Nov 1940, huko San Francisco, California Marekani na kufariki 20 July 1973 huko Kow loon Tong, Hong Kong.

Bruce alizaliwa na kuukuta mchezo wa kung fu au karate ulimwenguni. Lakini kwa kipaji alichozaliwa nacho, alianza kuleta mabadiliko makubwa kwenye mchezo huo hadi kushawishi mamilioni ya watu ulimwenguni kuupenda na kuanza kuufuatilia mchezo huu. Bruce alikuwa na uwezo mkubwa wa kucheza na hisia za adui na kujua ni wapi atapopiga lazima adui atakaa tu hata awe na mwili kama jumba.

Ikafika kipindi watu wakamshauri ajiunge kwenye tasnia ya uigizaji ili kuwavutia watu zaidi kuupenda mchezo huo, lkn pia kujifunza baadhi ya mbinu za upambanaji kupitia movie zake. Mpaka toka Bruce afariki mpaka leo bado anapewa heshima kubwa na magwiji wa mchezo huo wakiwemo wacheza sinema kama vile Jackie Chan, Jet Lee nk. Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi.

View attachment 2335338

Wanaofuatia ni 👇
4) Michael Jackson king wa Pop na mitelezo.

5) 2pac Shakur king wa Hip hop aliekuwa haiogopi serikali ktk kuwatetea wamarekani weusi wenzake na jamii nyingine zilizobaguliwa nchini Marekani, pia alipambana sana na polisi kuhusu unyanyasaji wowote uliofanywa na jeshi hilo kwa vijana mbali mbali hadi alipouwawa. Aliwahi kuwa na kesi ya kuwashambulia polisi wawili na bunduki, baada ya 2pac kupita sehem na gari aliwakuta polisi wakiwa wamemfunga pingu mtu mweusi huku wanampiga, kitendo kile kilimuuzi 2pac ndipo alipoamua kutoa bastola yake na kuwashambulia polisi, japo baadae polisi wale waliwahishwa hospital na kupona.
Katika kesi ile 2pac hakuhukumiwa baada ya kuonekana kuwa wale polisi walikuwa na makosa ya kiutendaji kwa mtuhumiwa waliekuwa wamemkamata.
Mungu awalaze roho zao mahali pema peponi.

6) Michael Jordan
Mzee wa kudumbukiza kikapuni. Huyu alikuwa na uwezo wa kuruka juu zaidi na kuonekana kama ameganda kwa sekunde kadhaa hewani kabla ya kutia mpira kapuni na kushuka chini. Toka astaafu bado hajapatikana Jordan mungine, japo bwana mdogo hayati Kobe Bryant alijitahidi kwa namna fulan, lkn bado hakufikia kule alipofikia mzee wa kazi.

View attachment 2335342

Hawa ni baadhi ya watu ambae mpaka leo viatu vyao viko wazi, havijapata wa kuvivaa vikawatosha.
Hapo wacko jacko, bob marley na bruce lee nimewajua nikiwa mtoto tu wengine nilikuja kuwajulia ukubwani
 
Back
Top Bottom