Hawa Wainjilisti kwenye Daladala wako sahihi kweli?

Hawa Wainjilisti kwenye Daladala wako sahihi kweli?

Idofu

Senior Member
Joined
Oct 24, 2022
Posts
116
Reaction score
199
Kwanza nikiri Kabisa Mimi ni Mkristo Kabisa!

Umetokea mtindo wa baadhi ya Wainjilisti kutoa mahubiri kwenye Daladala kila Siku, sasa ninachokijua ni kuwa sisi wakristo Kuna sehemu mahususi kwa ajili ya mahubiri na Mambo mengine ambayo yanaambatana na Mambo ya kidini, Makanisani na Kwenye Jumuia ambazo ni sehemu sahihi ya kuelimishana kwa Mambo yote ya kidini.

Sasa, nakwazika na sio kwa ubaya na hawa Wainjilisti wanaohubiri Kwenye daladala, na je ikitokea dini nyingine wakaja na utaratibu huu huu wa kutoa mahuburi kwenye vyombo vya usafiri wa umma itakuwaje?

Nawaombeni, watumishi wa Mungu mtumie Nguvu nyingi kwenye makanisa yenu, Jumuia na kwenye makongamano ndio sehemu sahihi.
 
Kwanza nikiri Kabisa Mimi ni Mkristo Kabisa!

Umetokea mtindo wa baadhi ya Wainjilisti kutoa mahubiri kwenye Daladala kila Siku, sasa ninachokijua ni kuwa sisi wakristo Kuna sehemu mahususi kwa ajili ya mahubiri na Mambo mengine ambayo yanaambatana na Mambo ya kidini, Makanisani na Kwenye Jumuia ambazo ni sehemu sahihi ya kuelimishana kwa Mambo yote ya kidini.

Sasa,nakwazika na sio kwa ubaya na hawa Wainjilisti wanaohubiri Kwenye daladala, na je ikitokea dini nyingine wakaja na utaratibu huu huu wa kutoa mahuburi kwenye vyombo vya usafiri wa umma itakuwaje?

Nawaombeni, watumishi wa Mungu mtumie Nguvu nyingi kwenye makanisa yenu, Jumuia na kwenye makongamano ndio sehemu sahihi.
Wengi ni victims wa changamito za maisha haya ya sio kua na formular 90% ya walokole ni vichaa wasio jitambua, ulokole kwa matukio take kwasasa sio dini ni kama Cult inao kusanya kila aina ya waubili.
 
Wengine ni chazo cha mapato sio dini, masikini hua anambini nyingi kuishi.
Nakubaliana na wewe!!

Nijuavyo Uinjilisti ni hatua ya kupanda kwenda kwenye uchungaji!!,hawa mafunzo yao yote wanatakiwa wajifunzie Makanisani na sio kwenye daladala !!
 
Kwanza nikiri Kabisa Mimi ni Mkristo Kabisa!

Umetokea mtindo wa baadhi ya Wainjilisti kutoa mahubiri kwenye Daladala kila Siku, sasa ninachokijua ni kuwa sisi wakristo Kuna sehemu mahususi kwa ajili ya mahubiri na Mambo mengine ambayo yanaambatana na Mambo ya kidini, Makanisani na Kwenye Jumuia ambazo ni sehemu sahihi ya kuelimishana kwa Mambo yote ya kidini.

Sasa, nakwazika na sio kwa ubaya na hawa Wainjilisti wanaohubiri Kwenye daladala, na je ikitokea dini nyingine wakaja na utaratibu huu huu wa kutoa mahuburi kwenye vyombo vya usafiri wa umma itakuwaje?

Nawaombeni, watumishi wa Mungu mtumie Nguvu nyingi kwenye makanisa yenu, Jumuia na kwenye makongamano ndio sehemu sahihi.
Yesu hakusema mahubiri yafanywe ndani ya Kanisa pekee...
Hata hivyo siyo Wakristo pekee, Labda hujakutana tu na wengine.

Marko 16:15
Akawaambia, Enendeni ulimwenguni mwote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe.
 
Wanastaili flani jinsi wanavyoanza sauti huwa inaanzia chini ila kila dakika zinavyooenda ndo sauti inapanda juu inafika hatua inakua fujo kabisa, ukijidai umelala ndo anakusogelea anahubiri kwenye maskio yako
 
Utawasikia kuwa walitumwa na yesu wahubiri kila sehemu... Ila wengi wao ni chanzo cha mapato tu na si vingine... Hawafai kabisa
 
Back
Top Bottom