Pre GE2025 Hawa ‘Wakimbizi walioteuliwa kwenye nafasi za maamuzi’ ni kina nani?

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Mkuu naheshimu sana ID yako. Unaweza kutusaidia makampuni au majina ya watusi waliyopewa migodi waliyonyang'anywa wazawa?
 
Bila ya shaka watakuwa wamepata somo la kupunguza kuropoka. Yaani watanzania walivyo na chuki na mafanikio ya wenzao huku ni kutoa sababu tu za kutaka kuona watu wa aina wafulani waonekane ni raia daraja la pili hawastahili kushika nafasi za uongozi.

Very irresponsible statement nchi zilizoendelea kwa kauli yenye kugawa jamii kama ivyo kwa nafasi yake kesho magazeti yanaanzisha harakati za kumtaka astaafu.

Jamani failures zetu za maisha katika uwanja ambao changamoto zetu zinafanana, mwingine akitoboa ni maarifa yake au baraka zake kutoka kwa muumba; sio tena kuwatafutia sababu hawastahili.

Huko Mtwara ni wamakonde wa Tanzania ndio waliokuwa wakiwaficha wenzao wa msumbiji; sasa tuitimishe wamakonde hawastahili kushika nafasi Tanzania, wakati tushakuwa na raisi wa kabila hilo.

Kwenye ili kamanda kapotoka, ile sio kauli ya kujenga nchi; isipokuwa ni ya kubomoa mshikamano wa nchi.
 
Baada ya hotba lazma amiri jeshi mkuu apewe makartasi yote kama wapo hao walioteuliwa watajulikana tu
 
Walichokitafuta wamekipata watu sasa wanatafuta mbuzi wa kafara.

Dotto Biteko unajua pacha wake Kulwa ni civil servant wizara ya mambo nje, mara ya mwisho alikuwa na Kipilimba Namibia (wengi hawa wa kwenye admin za mabalozi uwa ni maafisa usalama). Tena jamaa alishinda kura ya maoni ubunge jimbo linalopakana na Dotto akakatwa tu na Magufuli.

Pelekeni watoto shule acheni kulalamikia mafanikio ya wenzenu. Kuna wahangaza kibao wanaongea kinywarwanda ushawahi kukaa nao, ebu tafuta walio nje ya nchi si wangekuwa wanatafuta wanyarwanda kwenye pingu za mbona wengi wanaishia kutafuta watanzania wenzao wa kabila lolote, wapo kwenye jumuiya za Tanzania ni kwa sababu wao wanajitambua ni watanzania.

Acheni huo ubaguzi
 
Hili la wakimbizi kujipenyeza kwenye maamuzi ni la siku nyingi kuanzia miaka ya 1970. lifike mwisho kiusalama siyo la kucheka nalo. likiota mizizi litaigharimu nchi.wengi wanapitia kwenye siasa.
 
Huyu hapa mwingine
 
Mwingine huyu hapa
 
We mjinga umesoma nilichoandika? Kwa hivyo nikiandika Bashe msomali kusahihisha aliyesema Bashe mnyamwezi nami naingia kwenye hao mahasidi? Jitambue
 
Unawazungumza wahutu? Unasahau wamakonde, wangoni na wamasai? Hivi wamanyema na wahangaza asili zao wapi? Huyo Aliemuita mwenzie Mkimbizi nae ukimchunguza ni walewale, mesut Ozil na ukimbizi wake alikuwa shujaa wao wajerumani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…