Pre GE2025 Hawa ‘Wakimbizi walioteuliwa kwenye nafasi za maamuzi’ ni kina nani?

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Hadi mwenye chama pia anahusishwa kuwa Ni muoman [emoji23][emoji23][emoji23]


Ila tuseme ukweli watanzania halisi kwa asili Ni wagogo tu

Ila pia wanasemaga malecela nae Ni mkongomani [emoji23][emoji23]
Labda wagogo wa Kongwa tu ndio Orijino. 🙏🙏
 
Mfano mnasema kinana sio mTz ni msomali
Haya Jwtz mlimruhusu kuingia ili iweje, ameshashika nyadhifa mbalimbali mpaka katibu mkuu CCM. Ana miaka 70's kazalisha Tanzania.
Mmechelewa!
Obama naye ni mjaluo
Sunak naye ni muhindi
Boris Johnson naye ni mturuki
Donald Trump naye ni mjerumani !

Cheap politics !
Watu wote Duniani ni wahamiaji hamiaji tu kutoka sehemu moja hadi nyingine Kutafuta maisha !
Hakuna watu walioteremshwa moja kwa moja toka mbinguni hadi hapa Dodoma !!
 
Mkimbizi kama sio jasusi, hata urais tunampa kikubwa awe na sifa.

Watanzania chuki ni kubwa bila sababu maalum, mtu km ana uwezo lazima tumpe kipaumbele sisi tusio na roho ya chuki.
Cha kuogopa ni majasusi, sio raia weny asili ya nje ya Tanzania
Mbn USA, UK au ulaya yote hawafagilii huu ujinga wetu
 
Muhimu mtu asivunje sheria hilo tu
Wakisema wafukuze wakimbizi wasanii wa Bongo fleva watabaki nusu

Serikalini robo inshort Tanzania watabaki wawili...
Aliyeanzisha thread yeye mwenyewe aje aseme katokea wapi!?
 
Mmechelewa mno tu kuujua Mkakati.
Mfano mnasema kinana sio mTz ni msomali
Haya Jwtz mlimruhusu kuingia ili iweje, ameshashika nyadhifa mbalimbali mpaka katibu mkuu CCM. Ana miaka 70's kazalisha Tanzania.
Mmechelewa!
Ni fursa.

Walichangamkia fursa na wakazitumia ipasavyo.

Mimi binafsi nina marafiki ambao kiukweli walichangamkia fursa khasa za elimu bure na mambo mengine kedekede, lakini wengi wao watokea nchi hizohizo tajwa.

Pia hawa jamaa shuleni hadi chuo kikuu walikuwa ni mahiri sana katika tasnia ya masomo.

Mimi nilikuwa sichezi mbali nao khasa kwenye vile vipindi vya prep ( kwa wale walosoma bweni) maana "brain storming" ilikuwa ya uhakika na leo hii imetujenga sana kielimu, kitaalam na kiueledi.

Katika wote hao, ni wale wa kutoka Rwanda ambao leo hii wameijenga nchi hiyo katika kila sekta, tena ndani ya miaka 30 baada ya vita.

Kiuhalisia na kwa lugha ya kistaarabu kabisa naweza kusema kwamba watanzania wengi au "majority" na ambao ndo wapiga kura, ni wale wa kuwachukulia kwa ule msemo wa "wajinga ndo waliwao".

Ukitaka kufahamu kwa undani nnachomaanisha angalieni na sikilizeni yanosemwa sasa hivi majukwaani.

Kama mtu ni mhamiaji na ana sifa kwanini asitumie fursa kwenda mbele? Mbona watu hata wahindi huko Ughaibuni wana asili ya nje lakini leo hii ni mawaziri wakuu?

Mwisho, Rwanda leo imetimiza miaka 30 tangia mauaji ya Kimbari yatokee, na raisi Paul Kagame amewataka vijana wake (wengi wana miaka 30 sasa) kuijenga Rwanda na wale wenye miaka 25 kujiandaa kuchukua kijiti cha maendeleo.

Wanyarwanda kila mwaka hufanya mkutano wa kitaifa uitwao "Umushyrikiano" ambao hujadili masuala mbalimbali yakiwemo mstakabali wa hali ya nchi, ufanisi wa mifumo ya kitaifa na umoja wa kitaifa.

NB:

Mimi si mnyarwanda lakini nina marafiki wengi sana ambao nimekuwa nao, nimesoma nao na nimeishi nao ambao ni wakongo, warundi na wanyarwanda.
 
Yaani CDF nae anataka kiki....teh teh.
 
Wenye Akili na tunaowajua vyema Wanyarwanda na Rais wao tumemuelewa vyema na kukubaliana nawe 100% kwa Ulichokiandika hapa ila sasa kaa tayari kupingwa na Mizuzu / Mijuha iliyoko hapa ambayo Kutwa tu ina Chuki na Watutsi, Rwanda na Rais Paul Kagame.
 

View: https://www.instagram.com/p/C2eJNYOiq-4/?igsh=NGdtOHRlZ29icWR2
 
Ubaguzi ni mwingi. Maandiko mengi humu yanasema Samia arudi kwao Oman. Salim Ahmed alifanyiwa fitina mpaka akaamuwa kukaa nje ya siasa. Historia yake ndani ya Umma Party, Afro Shirazi na CCM ilisahauliwa.
 
Kwa hiyo wagombea wetu wa utahisi wawe watu WA Kingwa Tu,angalau Kwa miaka 100 ijayo
Hapana !
Najaribu kuonyesha kwamba kila aliyefuata taratibu zote za sheria inavyotaka ili atambulike kuwa ni raia halali wa Tanzania ana haki zote kupata nafasi yeyote ya uongozi ndani ya Nchi. !
 
Hapa Professor Kabudi anaongea tumsikilize
 

Attachments

  • received_1063889154938221.mp4
    2.7 MB
Ajira, maisha magumu, ufisadi, utawala wa CCM, elimu mbovu,haya ndio matatizo ya bongo, hayo Mambo ya uraia, CCM wanayaleta ili kututoa kwenye reli tusijadili ya msingi, mpaka CDF naye anahusika
 
Juzi kahamia CCM kwenye mwamvuli wa uhalifu!

Sent from my V2111 using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…