Hawa wezi wauawe tu aisee, nimeibiwa milioni 10 kwenye gari langu(nissan juke)

Wewe utakuwa tajiri sana.Mtu wa kipato cha kawaida hawezi kuacha hata milioni mbili kwenye gari na asilock mlango labda uwe boss wa polisi.Alafu mwanaume unaendeshaje gari iliyobinuka matako kama Juke.
 
Unatembeaje na large cash kirahis hivyo halafu unaacha kwenye gari? Man think about strategy zako again, uko so exposed
 
Unatudhalilisha sisi mabilionea asee. Unaliliaje milioni 10?!!
 
Nissan Juke itakuwa ya mkeo pia
 
Acha uibiwe unapenda sana sifa aisee. Nissan juke namba E aiseee
 
Nahisi ni chai hii. Mbona Nissan Juke inatajwa sana? Halafu mimi hako kagari nakaonaga kama kamdoli fulani hivi kachurachura.
 
Pole aisee, maana kwenye ili bandiko lako kuna "aisee" kama zote aisee.

Kwahiyo umechukua hatua gani aisee?
aisee huyu mbona kama anatembelea nyota ya tajiri mkubwa kuliko wote jf aisee πŸ˜‚πŸ˜‚ aisee
 
Umenunua Mgodi Geita.

Halafu unaendesha Nissan Juke?

Haya sawa.
 
Hapo Mbezi Magufuli sio kabisa, mwenyewe juzi wameniliza bilioni 246 niliacha kwenye siti ya private jet yangu mbele ya hilo jengo
 
Na bilionea haupo.... uzuri wamekuachia akili za kuandika JF
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…