Haya magari ya umeme toka China yanashawishi

Sijui tunafeli wapi wanazengo ila kimsingi natamani sana kama tungeanza kuhamia huku mdogo mdogo.View attachment 2078838
Hii gari ni ya usd 8000 tu roughly kama 18.5m hivi kwa wanaonunua gari za 25-30M naona kama hii chuma inanunulika kabisa...
mkuu Extrovert unataka kununua baiskeli

πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
Mana kibongole usajili wa vyombo vya moto kipimo ni cc
 
Tatizo watu ni restance to change haya magari nimekuwa nikiyafatilia sana kwenye forum mbalimbali ,yanafanya vizuri sana , sana nikihama kwenye mazda lazima nijirupue maana wanatoa warant na garantee ya vipuli kipi nihofie?? Dola 7000$ sio shida ,Tubadilike tuache ujuaji na kukatisha watu tamaa
 
Kananunulika, tatizo vikishanunuliwa kama 10, TRA lazima wakaze uzi.....wana wivu sana wale
 
Hizi gari haziaribiki kiwepesi sababu zina less moving parts! Yani kitendo cha kuwa na motor tu kimeondoa propeller, camshaft,crankshaft, piston, valve!

Yani service kubwa ni battery ambalo pia haliaribiki leo unaweza dunda nalo mpaka kilometer laki 5 huko ndio battery ife.


Halafu hao wachina mnaowabeza ndio wanatengeneza almost bidhaa zote za brand kubwa kubwa under licence na costs ziko chini sababu ya cheap labour costs.

Wabongo wanaponda tu hata zilipokuja sanLG na Fekon walipondaga sana ila mwisho wakakubaliana tu kuwa zile ni pikipiki kama zingine tu.
 
Kilometa laki tano😁😁 mkuu hizo battery hazitoboi hata kilometa laki ....
 
Pikipiki zinaitwa baiskeli za umeme kwa hiyo ukinunua ni mtelezo tu. Na Mchina ameweza kweli maana ina pedal za baiskeli ikiisha charge ghafla unanyonga tu kama baiskeli.

Ila kwa kweli sisi wabongo/waafrika tupo nyuma sana...

Hivyo vidude umevitaja kama baiskeli za umeme, Uchinani vimekiwepo tokea early 2000's, lakini kwa bongo sasa ndio kwa mbali vimeanza kumilikiwa na watu, almost 20years later

Sijui ni lini na sisi tutakuwa na vitu vyetu, Mungu saidia...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…