Haya ndio maswali yangu machache yaliyokosa majibu. Je, wewe unaweza kunijibu?

Haya ndio maswali yangu machache yaliyokosa majibu. Je, wewe unaweza kunijibu?

6 Pack

JF-Expert Member
Joined
Apr 17, 2022
Posts
2,819
Reaction score
5,996
Vipi hali zenu ndugu zangu?

Nimekuwa na maswali kadhaa akilini kwangu, lakini kila nikijaribu kuwauliza wana historia wanashindwa kunipa majibu yanayoeleweka. Anyway ngoja niyalete hapa huenda watapatikana wenye majibu yanayoeleweka.

Kwanza kabla ya kuendelea naomba niseme kwamba mada yangu hii haihusiani na kashfa kwa dini yoyote. Kwahiyo naomba wachangiaji mchangie kulingana na mada inavyotaka mchangie, sio kushambuliani kwa vigezo vya dini nk.

Sasa ndugu zangu tukifuatilia vitabu vya dini zetu kubwa mbili yani uislam na ukristo, vinatuambia kwamba mzee wetu au baba yetu wa imani Ibrahim alikuwa na asili ya Iraq, yani alitokea Iraq na lugha yake kilikuwa ni ki Ibrania hii pia ni lugha iliyokuwa inaongelewa Iraq miaka hiyo.

Historia inasema kwamba baadae Ibrahim alipata watoto wawili ambao ni Isihaka ambae ndio chimbuko la waisrael na Ismael ambae ndio chimbuko la waarabu. Kama nimekosea naomba nisahihishwe.

Sasa swali langu la kwanza kwa upande wa uzao wa Ismael.

Ikiwa Ibrahim ambae ni baba wa Ismael alikuwa mu Iraq na lugha yake kuu ni kiibrania.

a) Je, hii lugha ya kiarabu ilitokea wapi na ilianzishwa na nani?

Ikiwa waarabu wametokana na Ismael mtoto wa Ibrahim

b) Je, kabla ya hapo hiyo ardhi ya arabians ilikuwa inaishi watu wa jamii gani?

Swali la pili ni kwa uzao wa Isihaka

Ikiwa Ibrahim ambae ni baba wa Isihaka alikuwa mu Iraq.

a) Je, hawa waisrael tunaowaona leo kina Netanyahu na wengine ni uzao ule ule wa Isihaka au kuna tofauti? Kama ni wale wale waliotokana na uzao wa Ibrahim.

b) Mbona kirangi na kimuonekano ni kama vile wazungu yani hawafanani kabisa na ndugu zao wa Iraq alipotokea babu yao Ibrahim?

Swali la mwisho ikiwa waarabu na waisrael walitokana na uzao wa Ibrahim.

Je, Wahindi na Wachina huko Asia walitokana na uzao wa nani?
 
Forbidden Knowledge.

No one will tell you the truth. Sanasana watakwambia tu Netanyau ni zao la Waroma (kwasababu eti kafanana na Pontius Pilate)
 
Mkuu maswali yako mazuri lakini hayakusaidii kuurithi ufalme wa mbinguni.

Unaonaje kama ungejikita kwenye kuurithi ufalme wa mbinguni kwanza, halafu haya mengine ukaenda kumwuliza huyo mwamba huko huko?
 
Mkuu maswali yako mazuri lakini hayakusaidii kuurithi ufalme wa mbinguni.

Unaonaje kama ungejikita kwenye kuurithi ufalme wa mbinguni kwanza, halafu haya mengine ukaenda kumwuliza huyo mwamba huko huko?
Urithi nina uhakika nitaurithu mkuu kwa sababu
1) Nina amini uwepo wa Mungu
2) Nitajiepusha kutenda dhambi
3) Ninatoa sadaka kwa wale wasiojiweza
4) Ninafanya anayoyapenda Mungu
Na mengine mengi ambayo sio lazima kuyaandika hapa.
 
mkuu mbona sijaona watu weusi hapo au basi subiri niende kwenye uzi wa mizimu kule
Sio weusi tu hata wazungu sikuwataja kwa sababu mada inazungumzia watu wa bara la Asia.
 
Kwani hii historia wewe umeipata kutoka wapi? Aliyekuelimisha kidogo mfuate tena akuelimishe zaidi
Hata na wewe kama unajua baadhi yake naomba utuongezee ujuzi kidogo.
 
Umiza kichwa kutafuta namna bora ya kuingiza hela kila siku. Kuumiza kichwa kwa mambo ya kufikirika, ni matumizi mabaya ya akili.
Mkuu mpaka kuona mimi nimekaa chini kuandika mambo haya, basi jua nimeshashiba. Niko vizuri kimaisha na kimipango.
 
Kwa uelewa wangu mimi historia nyingi zimefutwa na chache zilizobaki zinafichwa ili ukweli usijulikane..........ndio maana hata stori ya muafrika inaanzia baada ya ukoloni pia kufuta na kuficha mambo kunafanya washindwe kujua ni nani aliyejenga piramid za giza pale misri na alitumia teknolojia gan kupandisha jiwe la tani 3 kwenye urefu wa futi zaidi ya 100 kwenda juu

Hoja yangu ni kwamba kama ukweli wa hapa afrika ni ngumu kuujua.....usiamini kama utakuja kujua ukweli wa hoa weupe......yaani hata hivi vitabu vya dini vimejaa utata sana.....niulizw utata gan ntakwambia
 
Kwa uelewa wangu mimi historia nyingi zimefutwa na chache zilizobaki zinafichwa ili ukweli usijulikane..........ndio maana hata stori ya muafrika inaanzia baada ya ukoloni pia kufuta na kuficha mambo kunafanya washindwe kujua ni nani aliyejenga piramid za giza pale misri na alitumia teknolojia gan kupandisha jiwe la tani 3 kwenye urefu wa futi zaidi ya 100 kwenda juu

Hoja yangu ni kwamba kama ukweli wa hapa afrika ni ngumu kuujua.....usiamini kama utakuja kujua ukweli wa hoa weupe......yaani hata hivi vitabu vimejaa utata sana.....niulizw utata gan ntakwambia
Ulichoandika nakubaliana nacho mkuu. Ila hapo kwenye utata naomba utuambie ni utata gani?
 
Vipi hali zenu ndugu zangu?

Nimekuwa na maswali kadhaa akilini kwangu, lakini kila nikijaribu kuwauliza wana historia wanashindwa kunipa majibu yanayoeleweka.
Anyway ngoja niyalete hapa huenda watapatikana wenye majibu yanayoeleweka.

Kwanza kabla ya kuendelea naomba niseme kwamba mada yangu hii haihusiani na kashfa kwa dini yoyote. Kwahiyo naomba wachangiaji mchangie kulingana na mada inavyotaka mchangie, sio kushambuliani kwa vigezo vya dini nk.

Sasa ndugu zangu tukifuatilia vitabu vya dini zetu kubwa mbili yani uislam na ukristo, vinatuambia kwamba mzee wetu au baba yetu wa imani Ibrahim alikuwa na asili ya Iraq, yani alitokea Iraq na lugha yake kilikuwa ni ki Ibrania hii pia ni lugha iliyokuwa inaongelewa Iraq miaka hiyo.

Historia inasema kwamba baadae Ibrahim alipata watoto wawili ambao ni Isihaka ambae ndio chimbuko la waisrael na Ismael ambae ndio chimbuko la waarabu. Kama nimekosea naomba nisahihishwe.

Sasa swali langu la kwanza kwa upande wa uzao wa Ismael.

Ikiwa Ibrahim ambae ni baba wa Ismael alikuwa mu Iraq na lugha yake kuu ni ki ibrania

a) Je hii lugha ya kiarabu ilitokea wapi na ilianzishwa na nani?

Ikiwa waarabu wametokana na Ismael mtoto wa Ibrahim
b) Je kabya ya hapo hiyo ardhi ya arabians ilikuwa inaishi watu wa jamii gani?

Swali la pili ni kwa uzao wa Isihaka

Ikiwa Ibrahim ambae ni baba wa Isihaka alikuwa mu Iraq

a) Je hawa waisrael tunaowaona leo kina Netanyahu na wengine ni uzao ule ule wa Isihaka au kuna tofauti?
Kama ni wale wale waliotokana na uzao wa Ibrahim

b) mbona kirangi na kimuonekano ni kama vile wazungu yani hawafanani kabisa na ndugu zao wa Iraq alipotokea babu yao Ibrahim?

Swali la mwisho ikiwa waarabu na waisrael walitokana na uzao wa Ibrahim
Je wahindi na wachina huko Asia walitokana na uzao wa nani?
Mbona historia hiyohiyo inasema binadamu tumetokana na nyani lakini hatufanani na nyani tipically?

Haya mambo ukihoji sana unaweza kuhisi kila kitu tunachojifunza kutokana na historia ni uongo kutokana na kuwa maswali mengi hayana uthibitisho bayana.

Kwahyo nakushauri tuendelee kuishi tu humohumo kila mmoja akiamini kwa dhati dhamira za dini zetu kuwa ni kutuweka katika mstari wa kuwa na ubinadamu.



Hivi ulishawahi kujiuliza kama kusingekuwa na dini binadamu tungekuwa na roho mbaya kiasi gani?
 
Mbona historia hiyohiyo inasema binadamu tumetokana na nyani lakini hatufanani na nyani tipically?

Haya mambo ukihoji sana unaweza kuhisi kila kitu tunachojifunza kutokana na historia ni uongo kutokana na kuwa maswali mengi hayana uthibitisho bayana.

Kwahyo nakushauri tuendelee kuishi tu humohumo kila mmoja akiamini kwa dhati dhamira za dini zetu kuwa ni kutuweka katika mstari wa kuwa na ubinadamu.



Hivi ulishawahi kujiuliza kama kusingekuwa na dini binadamu tungekuwa na roho mbaya kiasi gani?
Hakika katika hili nakubaliana tena na wewe.
Dini zimesaidia kutujenga na kutuweka mbali na mabaya ambayo bila dini labda yangekuwa ni sehemu ya maisha yetu ya kawaida. Yani mtu kuuwa, kujeruhi au kudhulumu lingekuwa ni jambo la kawaida.
 
Ulichoandika nakubaliana nacho mkuu. Ila hapo kwenye utata naomba utuambie ni utata gani?
Kaini baada yakumuua abel MUNGU akaweka alama kwenye paji la uso wa kain lakin kain akamwambia MUNGU hii alama unayoniweka watu wakioniona na hii alama watanikataa sasa je hao watu ni kina nani

Lakin pia uyouyo kain baada ya kumuua abel akaondoka na kuelekea huko mji wa NODI biblia inasema huko akaoa na kuanzisha familia kumbuka adam na eva wana watoto wawili tu kain na abel na abel kashakufa sasa je huko NODI alikokimbila kain alioa mtoto wa nani na wakina nani aliogopa watamuua wakimuona na hio alama
 
Mkuu maswali yako mazuri lakini hayakusaidii kuurithi ufalme wa mbinguni.

Unaonaje kama ungejikita kwenye kuurithi ufalme wa mbinguni kwanza, halafu haya mengine ukaenda kumwuliza huyo mwamba huko huko?
Cha msingi hpo nikumtafuta mungu bila kuitegemea dini
 
Vipi hali zenu ndugu zangu?

Nimekuwa na maswali kadhaa akilini kwangu, lakini kila nikijaribu kuwauliza wana historia wanashindwa kunipa majibu yanayoeleweka.
Anyway ngoja niyalete hapa huenda watapatikana wenye majibu yanayoeleweka.

Kwanza kabla ya kuendelea naomba niseme kwamba mada yangu hii haihusiani na kashfa kwa dini yoyote. Kwahiyo naomba wachangiaji mchangie kulingana na mada inavyotaka mchangie, sio kushambuliani kwa vigezo vya dini nk.

Sasa ndugu zangu tukifuatilia vitabu vya dini zetu kubwa mbili yani uislam na ukristo, vinatuambia kwamba mzee wetu au baba yetu wa imani Ibrahim alikuwa na asili ya Iraq, yani alitokea Iraq na lugha yake kilikuwa ni ki Ibrania hii pia ni lugha iliyokuwa inaongelewa Iraq miaka hiyo.

Historia inasema kwamba baadae Ibrahim alipata watoto wawili ambao ni Isihaka ambae ndio chimbuko la waisrael na Ismael ambae ndio chimbuko la waarabu. Kama nimekosea naomba nisahihishwe.

Sasa swali langu la kwanza kwa upande wa uzao wa Ismael.

Ikiwa Ibrahim ambae ni baba wa Ismael alikuwa mu Iraq na lugha yake kuu ni ki ibrania

a) Je hii lugha ya kiarabu ilitokea wapi na ilianzishwa na nani?

Ikiwa waarabu wametokana na Ismael mtoto wa Ibrahim
b) Je kabya ya hapo hiyo ardhi ya arabians ilikuwa inaishi watu wa jamii gani?

Swali la pili ni kwa uzao wa Isihaka

Ikiwa Ibrahim ambae ni baba wa Isihaka alikuwa mu Iraq

a) Je hawa waisrael tunaowaona leo kina Netanyahu na wengine ni uzao ule ule wa Isihaka au kuna tofauti?
Kama ni wale wale waliotokana na uzao wa Ibrahim

b) mbona kirangi na kimuonekano ni kama vile wazungu yani hawafanani kabisa na ndugu zao wa Iraq alipotokea babu yao Ibrahim?

Swali la mwisho ikiwa waarabu na waisrael walitokana na uzao wa Ibrahim
Je wahindi na wachina huko Asia walitokana na uzao wa nani?
AI response:
==
A| GPT-3.5

Kwanza, ni muhimu kuelewa kwamba masuala ya asili na uzao wa watu ni ya kihistoria na yanahusisha ukweli wa kihistoria pamoja na uchambuzi wa kisayansi. Kwa hivyo, majibu yangu yanategemea ukweli wa kihistoria na uchambuzi wa kisayansi.

a) Kuhusu asili ya lugha ya Kiarabu, inaaminika kuwa ilianzia katika eneo la Peninsula ya Arabia karne ya 4 au 5 BK. Lugha hii ilikuwa lugha ya makabila ya Kiarabu yaliyokaa katika eneo hilo na ilikuwa inatumika kwa mawasiliano ya kila siku na biashara. Haijulikani haswa ni nani alianzisha lugha ya Kiarabu, lakini kuna ushahidi wa kuwepo kwa lugha ya Kiarabu katika maandishi ya kale ya Kiarabu na ushahidi wa athari za lugha ya Kiarabu katika lugha nyingine za kihistoria.

b) Kabla ya kuwepo kwa Waarabu, eneo la Peninsula ya Arabia lilikuwa na makabila mbalimbali ya watu ambao walikuwa wakizungumza lugha tofauti-tofauti. Kuna ushahidi wa kuwepo kwa makabila ya Kiarabu kabla ya kuzaliwa kwa Ismael, lakini hawakuwa na umoja wa kikabila na hawakuzungumza lugha moja. Ismael anatajwa katika Biblia na Qur'an kama baba wa Waarabu, na inaaminika kuwa yeye na wafuasi wake walikuwa wakiishi katika eneo la Hijaz (sasa Saudi Arabia). Baada ya Ismael, Waarabu walikuwa na umoja wa kikabila na lugha ya Kiarabu ikaanza kuenea katika eneo hilo.

a) Waisraeli wa leo wana asili ya kikabila kutoka kwa wana wa Isihaka na ndugu yake Esau, ambaye alikuwa mkubwa kuliko Isihaka. Kwa hivyo, Netanyahu na wengine ni wana wa Isihaka. Hata hivyo, waisraeli wa leo wamepata athari kutoka kwa tamaduni na makabila mengine, na kwa hivyo wanaweza kuwa na rangi na muonekano tofauti.

b) Kiwango cha rangi na tabia za kibinafsi haziwezi kutumiwa kama njia ya kuhusisha watu na asili yao. Waisraeli wa leo wanatoka katika makabila mbalimbali na wamepata athari kutoka kwa tamaduni na makabila mengine, na kwa hivyo wanaweza kuwa na rangi na muonekano tofauti.

Haijulikani haswa kuhusu asili ya watu wa India na China, lakini kwa ujumla, kabla ya kuwepo kwa tamaduni na mataifa yaliyopo sasa, eneo la Asia lilikuwa na makabila mbalimbali ya watu ambao walikuwa wakizungumza lugha tofauti-tofauti. Kwa hivyo, haiwezekani kusema kwamba watu wa India na China walitokana na uzao wa mtu fulani au kabila fulani.

===
B | Claude-instant
  1. Kuhusu asili ya lugha ya kiarabu. Lugha ya kiarabu ilianzishwa na Waarabu wakati wa Ukiislamu, hasa baada ya kutangazwa kwa Qurani ya Mtukufu Mtume Muhammad. Asili halisi ilitokea Arabia, maeneo ya magharibi na kusini mwa bahari ya Kiarabu. Waarabu ndio waliianzisha lugha hii na kuifanya lugha rasmi ya Kiislamu. Hivyo, Waarabu ndio waawanzilishi halisi wa kiarabu.
  2. Kabya na jamii zilizoishi halali ya Arabian hapo zamani ni Waarabu Qahtan, Adnan na Yam. Waarabu Qahtan walikuwa wenyeji wa mwanzo wa Arabian, lakini waligawanyika katika kabila nyingi. Walikuwa washindi na wafuafu. Adnan walikuwa ndugu zake Qahtan lakini walikusanya kabila zao katika tunuwa moja - ndilo chimbuko la Waarabu ambao leo tunawajua. Yam walikuja baadae na kujumiri kwa Waarabu.
  3. Waisraeli wa leo na wa Biblia ni ndugu zetu wa karibu. Wote walitoka kwa Ibrahim na asili moja. Ilipita muda mrefu tangu hapo lakini genetiki inaonyesha ushawishi mkubwa. Tofauti yao yaonekana ni kutokana na historia tofauti, mazingira tofauti na ibada tofauti. Hawakuwa waarabu lakini walitoka kwa Ibrahimu kama waarabu.
  4. Waarabu, Waisraeli na wengine wavulana wa mama moja - Ibrahimu. Waarabu na Waisraeli ndio mlio wastani tu. Wahindi na Wachina walitoka kwa uzao mwingine wa mwanadamu. Hawakuwa kizazi cha Ibrahimu.

==
My take| Nilichofanya ni copy na ku_paste posti ya kwanza yote, katika AI mbili
  • GPT-3.5
  • Claude-instant
 
Kaini baada yakumuua abel MUNGU akaweka alama kwenye paji la uso wa kain lakin kain akamwambia MUNGU hii alama unayoniweka watu wakioniona na hii alama watanikataa sasa je hao watu ni kina nani

Lakin pia uyouyo kain baada ya kumuua abel akaondoka na kuelekea huko mji wa NODI biblia inasema huko akaoa na kuanzisha familia kumbuka adam na eva wana watoto wawili tu kain na abel na abel kashakufa sasa je huko NODI alikokimbila kain alioa mtoto wa nani na wakina nani aliogopa watamuua wakimuona na hio alama
Duh inafikirisha sana ki ukweli.
 
Back
Top Bottom