Hayati Dkt. Magufuli anapohukumiwa kwa kifo chake

Hayati Dkt. Magufuli anapohukumiwa kwa kifo chake

Pote
Potelea mbali sijaiba Cha mtu sijauwa mtu sijateka mtu sijafunga watu kwa kesi za uongo sijaikufuru Wala kuinajisi altare ya Mungu naamini mungu muumba wangu atanipa kifo Cha amani na cha heshima.
Hongera kwa kuwa mkamilifu.
 
Sasa kama hukumu anatoa Mungu wew hizi hukumu za Wananchi zinakuuma nini? Kwanini usiangalie hiyo hukumu ya Mungu ambayo bado sana na kufanya mambo yako kuliko kuonekana hayawani hapa.

tunaagizwa kuondoana ujinga kwa kufundishana.

ujinga sio kilema,mtu unamtoka akipewa elimu.
 
Ndio maana tunakuambia umezidiwa na mahaba mpaka sasa unakana hata maneno yako mwenyewe, mchelea mwana kulia hulia yeye, ndilo linalokukuta sasa, ulikuwa na wkati mzuri wa kumkumbusha mahaba wako huu uzi ulioweka leo hapa labda yeye angekusikia, kwa kuwa tulimuasa sana hapa kuwa aache visasi, hakusikia, mbona husemi kuwa kisasi ni Cha Mungu! Sisi hapa hatuhukumu bali tunakumbusha kuwa kama ilivyo wema kuwa ni mbegu ubaya nao ni mbegu lazima iote. Hata hukumbuki andiko juu ya kuikumbusha nyumba ya Yakobo dhambi zao!

yeye katika mada alifanya visasi kwa nani!!!

mbona uzushi haumpendezi mtu mzima kama wewe mkuu??
 
Jamaa bonge la hayawani, anasema msihukumu huku yeye anahukumu, yale yale ya msemakweli ni mpenzi wa Mungu, lakini alikuwa akiambiwa ukweli anapiga mtu shaba
Kakimbia uzi wake, me leo ningehakikisha anamtaja aliyemtuma kuja kumsafisha huyo marehemu huku.
 
yeye katika mada alifanya visasi kwa nani!!!

mbona uzushi haumpendezi mtu mzima kama wewe mkuu??
Sasa na wewe tukufundishe kusoma aeiou! Soma uelewe ndio uje hapa acha kuruka ruka kama pop corn. Nani amesema mleta uzi ana visasi!
 
Hakuna sehemu aliyosafishwa, na siko kusafisha, bali naongea wazi hakuna chuki ya marehemu duniani. Kujenga chuki kwa mtu alokufa nadhani ni kutokuwa na akili za kufikiri. Nimeongelea kifo chake na yasemwayo kwa hicho kifo. Sasa nimsafishe kwa nani?

Nyie ndo mtakao kufa vifo vya ajabu na vibaya! Wewe si Mungu kuhukumu!

Sasa nimtetee Magufuli kwani anagombea uRais. Soma uelewe mada chuki zako usikimbie na kuandika tofauti ya mada.

Napenda kukukumbusha utakufa pia, je umetafakari maisha yako?
Mwendazake alitesa sana watu. Bora alienda zake
 
tunaagizwa kuondoana ujinga kwa kufundishana.

ujinga sio kilema,mtu unamtoka akipewa elimu.
Kwakweli aliyoyafanya Jiwe ilibidi achomwe moto akiwa hai. Basi tu. Huwezi kufanya uovu duniani kwa kuua, kuteka, kutesa, kusema uongo then unataka watu waseme/wasubirie hukumu ya Mungu! Lazima uvune ulichopanda. Panda mema utavuna mema ila ukipanda uovu lazima uvune uovu.
 
Ndo haya nisemayo, kufa kwa mtu ni mpango wa Mungu, hata asingekuwa Rais angekufa. Nawe utakufa!
Wewe hasa umekazana kutetea Nini? Usikumbushe watu na kuwaudhi kuhusu utawala huo MBOVU ulioacha makovu. Tuongee mengine tu tusikumbushane inaleta hasira.
 
Well narrated Wilderness Voice

Ukweli utabaki kuwa ukweli JPM alikuwa Rais bora na kiatu chake hakuna kitakayeweza kumtosha.

Watanzania tumemkumbuka sana tunalia usiku na mchana,nchi sasa hivi HAIELEWEKI tupo tupo tu kwa kudra za Maulama.

TUSISAHAU KULIOMBEA TAIFA KILA TUSALIPO/TUOMBAPO.
Anzisheni movement ya kujitenga muwe na nchi yenu muiite Chato
 
Reformist Dr, John Mugufuli’s shoes will be quite difficult to fill.


They say hypocrisy is the homage that vice pays to virtue. Translation — even Lucifer will genuflect before Jesus. But don’t mistake the serpent’s ministrations with affection for his antagonist. He’s simply playing possum. That’s why President John Pombe Joseph Magufuli — should revel in the applause, but not believe it. Many who bid him adieu were only too happy to see him depart from this World. That’s because they want to return the Executive to the status quo ante. They didn’t choose him to be Predident. No — the forces of anti National resources for people centered gave him the hallowed office against the wishes of state apparatchiks. But Dr Mugufuli’s legacy will never die.


Today, I write to memorialise the meaning of the President John Pombe Joseph Magufuli Era for our nation. First, let’s not make the mistake of intellectual simpletons. We need to bow to the basic fact that Dr Magufuli is a rare breed.


But Dr Magufuli stands out in his humility and self-deprecation. He shuns wealth, and fame. In a country where thieves are celebrated, and murderers elevated — Dr Magufuli is the one public servant who forsook worldly possessions. Mark 8:38 asks: “For what shall it profit a man, if he shall gain the whole world and lose his own soul?” Methinks the author in the good book must have had Dr Magufuli in mind.


The simplicity of this Societal and moral giant is the one thing that remains an enigma to me and many. He always roots for the little guy. He abhors hierarchy and disdains flamboyance,he’s ruthlessly self-critical, and accepts the harshest critiques of himself. He always puts himself last. He’s a rare breed.


Second, folks should know that Dr Magufuli didn’t want to become President. He laughed off the idea when it was first suggested to him. He was dead serious. And even after he was convinced to put his name to apply for the job, he almost backed out. That’s because he’s uncomfortable with state power. I’ve never told him this — but I believe he thinks that state power atrophies the hearts of men and women, and turns them into predators. It’s possible that he was afraid he would become ogre in that office. That’s why he worked so hard to demystify the Executive, and bring the temple of Execuyive service delivery closer to common folk. This cultural transformation may be his most important legacy.


Third, Dr Magufuli lanced the boil in the Government. I know our Senior Public Servants chafe at the use of such language. But they – and we – know the Executive has traditionally been aloof and marked by impropriety and illegality.

It’s that boil that Dr Magufuli will be remembered for lancing. But as I remarked to him recently, one or two things can happen when you lance a boil – you can either cure or kill the patient. The septic shock can be fatal. The body can also be cleansed and nursed to health. He brought service delivery closer to the people in the remotest reaches of the republic.He revolutionised the way the public service work, and brought technology and empiricism to tame corruption, incompetence, and laziness.


He brought Goverment service and closer to the people in the remotest reaches of the republic.He revolutionised the way the Government work, and brought technology and empiricism to tame corruption, incompetence, and laziness.


Finally, I believe there will never be another JPM. President Samia as you have succeeded him hence bound by the energies that he unleashed. Those who believe that we can go back to the pre-John Pombe Joseph Magufuli Executive are sadly mistaken.


You can’t un-ring a bell that’s been rang. The concept doesn’t exist in science. The poor soul who succeeds Dr Magufuli shouldn’t try to fill his shoes. Those are too large. She needs to cure the patient. Rest in internal peace John Pombe Joseph Magufuli.


I never knew i could feel so much pain for his death and probably time will never heal this.
 
Sasa na wewe tukufundishe kusoma aeiou! Soma uelewe ndio uje hapa acha kuruka ruka kama pop corn. Nani amesema mleta uzi ana visasi!

nimeandika "yeye katika mada"

shida ni pombe bila kula au matumizi ya dundi kunusa kijana!!!!
 
Kwakweli aliyoyafanya Jiwe ilibidi achomwe moto akiwa hai. Basi tu. Huwezi kufanya uovu duniani kwa kuua, kuteka, kutesa, kusema uongo then unataka watu waseme/wasubirie hukumu ya Mungu! Lazima uvune ulichopanda. Panda mema utavuna mema ila ukipanda uovu lazima uvune uovu.

sasa ni Mungu alimuua au wafuasi wa mateka!!!!

jiwe keshapumzika mkuu,kama alitekwa enzi zake nyanyua pua tena,this time wanaondoka na kichwa kabisa wala hawarembi.
 
Kifo ni tukio la kiasili. Katika imani kadhaa za kidini zina elezea kifo kilitokea baada ya Adamu na Hawa (Eva) kwenda kinyume na mapenzi ya muumba wao (MUNGU). Ndipo Mungu alitamka kuwa tutakufa, au kurejea katika mavumbi.

Binadamu wa kwanza kufa alikuwa Abeli. Ambaye aliuliwa na kakaye aitwae Kaini. Kaini japo alimuuwa Abeli, bado Mungu alimlinda Kaini na hata akasema atakae muuwa kaini basi atalaaniwa. Hivyo Mungu alimpeleka Kaini nchi ya mbali. Hii yote kumuepusha na kumlinda na mabaya. Mungu alifanya haya yote japo Kaini alikuwa na dhambi ya kumuuwa nduguye.

Mungu utazama tofauti, na macho ya binadamu. Na Mungu ndiye mwenye uweza wa kuhukumu. Siku hizi Tanzania hii kumezuka, tabia ambayo inaonesha watu kufurahia kifo au vifo vya watu wengine. Na kama walikuwa hawampendi huyo mtu au watu; ndo watazusha mengi. Wabaya wake watajifanya wao ni mungu (Mungu), watahukumu, watasema huyu alifanya mabaya ndo maana kafa.

Watajiona wao waliobaki ndo wajanja, hawana makosa au dhambi mbele ya Mungu. Najiuliza hivi kuna mahala popote pale iwe katika misaafu au maandiko yoyote ya kidini na imani zinginezo, pana sema mtu anae kufa mapema au kabla ya wenzie ana dhambi na Mungu kaamua kumkomoa?

Nachojua Mungu alisema tutakufa, hakuna atakaeishi milele hapa duniani. Ndo maana watu ufa wakiwa watoto wachanga, wakiwa vijana, wakiwa wazee, na hata watoto wengine ufia tumboni mwa mama zao kabla ya kuzaliwa.

Tukidai kufa mapema ni kukomolewa na Mungu, ebu tuangalie, hawa mitume wetu, walikufa bado wakiwa vijana, na walikuwa na maadui wengi, hawakupendwa. Yesu kristo aliishi miaka isiyozidi thelathini na tatu. Na alianza kazi ya kuhubiri akiwa na miaka thelathini tu. Vile vile kwa mtume Muhamad S.W.A alikufa mapema. Si hao tu ni wengi!

Hivyo kifo ni asili. Nachoamini kila mtu anakusudi la kuwepo duniani. Na pia ana muda wake wa kuishi. Haijalishi ni miaka mingapi. Muda ukifika Mungu ndo mwamuzi wa yote, uondoke au aseme bado ubaki.

Katika kila jambo Mungu anamakusudi yake. Laweza kuwa baya au zuri, lakini Mungu anatazama tofauti na tunavyotazama sisi wanadamu.

Kikubwa tusijipe kazi ya Mungu ikawa kazi yetu. Tusijipe kuhukumu kwani hukumu ya maisha yetu utolewa na Mungu. Usihukumu usije hukumiwa.

Nimeongea haya yote ni kutokana na watu wengi, wapinzani na wana CCM kuonekana kumhukumu alie kuwa Rais wa Tanzania, J.P. Magufuli na hata kumzodoa kuwa kafa mapema, yako wapi, kuonesha tu Mungu ati kamuondoa kwa mabaya yake. Nilishangaa hata Mchungaji mmoja anajiita mzee wa upako kuongea kama vile nae anaonesha kufa kwa magufuli ni kama adhabu, eti kisa Lowasa hakuchaguliwa Urais na kuwataka watu wakamuombe Msamaha Lowasa.

Mimi niseme kwa maandiko viongozi wote wakuu wa nchi uwekwa na Mungu. Mungu angeamua Lowasa kuwa Rais angekuwa tu. Mchungaji kasahau maandiko anatumia akili za kibinadamu. Kufa kwa Magufuli si kwamba Mungu hakutaka Magufuli awe Rais, la asha. Mungu hutenda kwa wakati wake.

Jiulize katika maandiko tunaambiwa kuwa Yusufu aliuzwa utumwani na nduguze, bado huyo Yusufu akafungwa gerezani. Lakini cha ajabu akaja kuwa ndiye waziri mkuu wa nchi. Hata nduguze walipojihisi atalipiza kisasi kwa kuwafanyia mabaya, aliwaambia. Mlikusudia mabaya kwangu, lakini katika hayo mabaya Mungu alikusudia mema ili nije niwaokoe katika baa la njaa.

Mungu uona mbali zaid ya binadamu. hatujui ni kwanini Mungu aliepusha Lowasa asiwe Rais japo ilitumika njia mbaya au nzuri, lakini Mungu anakuwa na makusudi yake. Mchungaji katafakari neno la Mungu ndo utoe tamko. Hakuna lifanyikalo duniani bila Mungu kuridhia. Mungu huyo aliruhusu Ayubu apate mateso, akaruhusu watoto wake Ayubu kufa na hata mali kuharibika na kupotea lakini alikuwa na kusudi. Kifo cha Magufuli kinakusudi liwe baya au zuri ila watanzania tutajifunza kutokana na hicho kifo siku moja. Kikubwa tusijichukulie mamlaka ya kuhukumu na kusema kafa kwa sababu alikuwa katiri na kadharika. Mbona Mungu alimlinda Kaini japo alikuwa muuwaji?

Hivi kazi yetu ni kuhukumu, kwani tuliobaki hatutakufa? wangapi tumefiwa na ndugu na wazazi, je kutangulia kwao ni kwamba walitenda mabaya Mungu kawahukumu? Kwa uzoefu wa haraka tu mara nyingi watu wema hawadumu? Iwapo hadi sasa unaishi lazima ujiulize, unatakiwa kulifanyia nini Taifa lako la Tanzania, na familia yako. Si kushambulia marehemu, na kujifanya wewe ni mungu unahukumu. Leo hata viongozi wetu utasikia, oooh! Magufuli hakutenda haki, alikuwa kiongozi mbaya, alikuwa muuwaji, alitisha, hakuwa na demokrasia!

Hivi ninyi viongozi mnao sema haya si mlikuwa nae ktk uongozi wa serikali? Kwanini amkumwambia wakati huo akiwa hai kuwa ni kiongozi mbaya.

Nacho jua Magufuli alikubali kukosolewa. Naibu Waziri wa afya kipindi hicho alimkosoa kuhusu matumizi ya kujifukiza. Akamwondoa katika nafasi. Lakini baadae alimrejesha ktk wizara tofauti.

Leo wanao mkosoa magufuli haohao, wanapinga Mhe. Rais Samia kukosolewa. Wakati Rais alidai kuwepo uhuru wa kukosoa. Lakini chama chake na Bunge Wanataka asikosolewe, tumsifie hata kwa yale yasio sifiwa. Wakati wanadai wao ni wanademokrasia. Ukikosoa unahesabika msaliti, Bunge litakuita kwenye Kamati. Chama kitakaa kukuita kikuhoji kwa nini huko kinyume na Rais. Chama kinachoongozwa na mwenyekiti ambae ni Rais alie ruhusu kokosolewa.

Mungu hapendi wafitini na watu waongo, wenye roho za usaliti. Viongozi mjitafakari. Na msijione ninyi hamta kufa. Kifo kipo akijali madaraka yako. Hakuna atakae ishi milele. Kuwepo kwako pengine Mungu anataka utimize mambo fulani. Ghazabu ya Mungu ni kubwa tusihukumu tukaja hukumiwa. Magufuli kaondoka kamaliza yake. Alifanya kwa nafasi yake na kwa staili yake. Watu wote hatufanani.

Tusijione sisi ni bora kwakuwa tu watu wanatuchekea na kutusifia. Tukachekelea na kuota kiburi kuona tuko sahihi na hatukosei! Pamoja na yote Magufuli aliwapenda watanzania. Hakuwahi kusema waondoke wakaishi Burundi.

Leo kauli hiyo inaongewa na kiongozi aliepewa dhamana na watanzania. Viongozi wamejiona wako juu ya sheria, wanauwezo wa kusema chochote. Viongozi wamekuwa na dharau. Wanajiona nchi ni yao. Hata wananchi kulalamika hawaoni haja ya kuomba msamaha.

Hata kiongozi wa nchi hawakanyi anawaacha je naye kafurahishwa na hayo maneno? Je kawatuma?
Harafu hawa hawa ndo wanasema watakuwa wapole na kuwabembeleza wananchi kuliko JPM ambaye kapewa mabaya yote.
Tukumbuke kutangulia kufa si dhambi. Na ukibakia si ujanja wa kufanya kutukana waliotangulia. Bali chukua muda wa kujitafakari.

Mungu alimlinda Kaini japo alikuwa muuwaji wa nduguye. Mungu ndiye mwenye kuhukumu. Na ndiye ajuaye mwisho wa maisha yetu. Jiulize hapo ulipo matendo uyafanyao ktk vificho au wazi, je ni mema? Je wewe ni msafi zaidi ya waliotangulia kufa?

Je, wajua kifo chako kitakuwaje? Lini utakufa? Je utakufa ukiwa na umri gani? Je alie kutangulia kafa akiwa na miaka mingapi?
Si ujanja wala umaarufu kutukana marehemu, au kutafuta umaarufu ati unajilinganisha na marehemu. Huyo kesha maliza wakati wake hayupo tena. Tuache kashfa hatujui kesho yetu. Tanzania ya leo imekuwa na siasa za kujipendekeza, sifa za kijinga, badala ya kufikiria maendeleo ya kweli. Walio tangulia tuwaache, tujenge nchi.
Too long I didn't read it.
 
sasa ni Mungu alimuua au wafuasi wa mateka!!!!

jiwe keshapumzika mkuu,kama alitekwa enzi zake nyanyua pua tena,this time wanaondoka na kichwa kabisa wala hawarembi.
Mungu aliamua kuikomboa nchi, huwezi kuwa vile ukadumu. Hata kama tuliwahi kumkosea Mungu na kutuadhibu kwa kutupa jiwe lakini aliona it was too much, akatusamehe na kuliondoa jiwe.
 
Reformist Dr, John Mugufuli’s shoes will be quite difficult to fill.


They say hypocrisy is the homage that vice pays to virtue. Translation — even Lucifer will genuflect before Jesus. But don’t mistake the serpent’s ministrations with affection for his antagonist. He’s simply playing possum. That’s why President John Pombe Joseph Magufuli — should revel in the applause, but not believe it. Many who bid him adieu were only too happy to see him depart from this World. That’s because they want to return the Executive to the status quo ante. They didn’t choose him to be Predident. No — the forces of anti National resources for people centered gave him the hallowed office against the wishes of state apparatchiks. But Dr Mugufuli’s legacy will never die.


Today, I write to memorialise the meaning of the President John Pombe Joseph Magufuli Era for our nation. First, let’s not make the mistake of intellectual simpletons. We need to bow to the basic fact that Dr Magufuli is a rare breed.


But Dr Magufuli stands out in his humility and self-deprecation. He shuns wealth, and fame. In a country where thieves are celebrated, and murderers elevated — Dr Magufuli is the one public servant who forsook worldly possessions. Mark 8:38 asks: “For what shall it profit a man, if he shall gain the whole world and lose his own soul?” Methinks the author in the good book must have had Dr Magufuli in mind.


The simplicity of this Societal and moral giant is the one thing that remains an enigma to me and many. He always roots for the little guy. He abhors hierarchy and disdains flamboyance,he’s ruthlessly self-critical, and accepts the harshest critiques of himself. He always puts himself last. He’s a rare breed.


Second, folks should know that Dr Magufuli didn’t want to become President. He laughed off the idea when it was first suggested to him. He was dead serious. And even after he was convinced to put his name to apply for the job, he almost backed out. That’s because he’s uncomfortable with state power. I’ve never told him this — but I believe he thinks that state power atrophies the hearts of men and women, and turns them into predators. It’s possible that he was afraid he would become ogre in that office. That’s why he worked so hard to demystify the Executive, and bring the temple of Execuyive service delivery closer to common folk. This cultural transformation may be his most important legacy.


Third, Dr Magufuli lanced the boil in the Government. I know our Senior Public Servants chafe at the use of such language. But they – and we – know the Executive has traditionally been aloof and marked by impropriety and illegality.

It’s that boil that Dr Magufuli will be remembered for lancing. But as I remarked to him recently, one or two things can happen when you lance a boil – you can either cure or kill the patient. The septic shock can be fatal. The body can also be cleansed and nursed to health. He brought service delivery closer to the people in the remotest reaches of the republic.He revolutionised the way the public service work, and brought technology and empiricism to tame corruption, incompetence, and laziness.


He brought Goverment service and closer to the people in the remotest reaches of the republic.He revolutionised the way the Government work, and brought technology and empiricism to tame corruption, incompetence, and laziness.


Finally, I believe there will never be another JPM. President Samia as you have succeeded him hence bound by the energies that he unleashed. Those who believe that we can go back to the pre-John Pombe Joseph Magufuli Executive are sadly mistaken.


You can’t un-ring a bell that’s been rang. The concept doesn’t exist in science. The poor soul who succeeds Dr Magufuli shouldn’t try to fill his shoes. Those are too large. She needs to cure the patient. Rest in internal peace John Pombe Joseph Magufuli.


I never knew i could feel so much pain for his death and probably time will never heel this.
Hahahahaha mtaongea mpaka Lugha ya Malkia kujaribu kumsafisha jiwe ila yule hasafishiki Kwa dodoki lolote
Kwa watu Kama sisi atabaki kua
The Mwendawazimu president ever seen under the sun of Tz
Yaani vilaza na wanyonge Ndio atabaki kua best kwenu

Mimi ni jiwe kweli kweli!
 
Mungu aliamua kuikomboa nchi, huwezi kuwa vile ukadumu. Hata kama tuliwahi kumkosea Mungu na kutuadhibu kwa kutupa jiwe lakini aliona it was too much, akatusamehe na kuliondoa jiwe.

uzuri maandishi haya hayafi.

usijimalize sana ndugu.
 
Back
Top Bottom