Hayati Dkt. Magufuli anapohukumiwa kwa kifo chake

Dah umenitoa machozi mkuu. Hakika ghazabu ya Mungu kwa wanaokebehi kifo cha Dkt Magufuli yaja. Dkt Magufuli kila alilolifanya lilikuwa kwa ajili ya Tanzania na Watanzania. Alipokataa kusafiri nje kwa ajili ya kubana matumizi alimfikiria mwananchi wa kijijini ambaye ni masikini anahitaji dawa, yeye akaone bora niwakilishwe ili hela nitakayoiokoa imsaidie mtanzania maskini. Nadhani nchi kama nchi bado tupo darasani kuhusu kifo cha Dkt Magufuli. Ni Muhimu Mama Samia akaligundua mapema na kulirekebisha. Maana ni ajabu sana aliachia Dkt Magufuli achafuliwe, atukanwe, kudhalilishwa, kudhihakiwa na kupewa adhabu ya kifo na wahusika kama vile wao ndiyo walipanga kifo cha Dkt Magufuli. Mbona Dkt Magufuli alizuia Dkt JK asitukanwe, na mbona Dkt JK alizuia Mkapa asitukanwe. Mama Samia aelewe familia yake itapata tabu sana siku akiondoka madarakani kama hatajenga msimamo wa watangulizi kutokudhalilishwa. Anapoachia kauli zinatolewa kuonesha eti Dkt Magufuli alikuwa katili na yeye siyo katili hiyo haisaidii maana mamlaka ni ile ile na akiondoka na yeye atazodolewa sana.
 
Ubaya au Wema wa mtu ni kama mchana hauhitaji tochi kuumulika
 
Mama Samia aelewe familia yake itapata tabu sana siku akiondoka madarakani kama hatajenga msimamo wa watangulizi kutokudhalilishwa.
Acha kumtisha Mh. Rais,hakuna wa kufanya huu ujinga.
 
Acha kumtisha Mh. Rais,hakuna wa kufanya huu ujinga.
Simtishi, ni uhalisia wa mambo yanavyoweza kutokea. Unadhani urais ni mtu, ni mfumo wa mimi na wewe. Watu watamtukana na kumdhalilisha kama alivyokubali mwenzake aitwe majina yote mabaya na yeye Mama kushangilia as if anafanya kitu kizuri. Kwanza hapakuwa na haja na kujitenga na serikali ya awamu ya Dkt Magufuli. Yeye alipaswa aoneshe msimamo toka mwanzo lakini sasa karuhusu watu eti wamuone yeye ni bora na afadhali Dkt Magufuli alikufa kwa sababu eti alikuwa mkali na kwa sababu eti alikuwa anatuma wawakilishi tu kwenda nje.
 
Watu watamtukana na kumdhalilisha kama alivyokubali mwenzake aitwe majina yote mabaya na yeye Mama kushangilia as if anafanya kitu kizuri.
Mama hakuwahi kushangilia mtangulizi wake akidhalilishwa acha kumzushia uongo.

Kwanza hapakuwa na haja na kujitenga na serikali ya awamu ya Dkt Magufuli.
Hakuwahi kujitenga na serikali ya mtangulizi wake wala hawezi kujitenga nayo maana alikuwa sehemu ya utawala huo, tena kwenye madaraka makubwa ndio maana aliweza kumrithi.


Yeye alipaswa aoneshe msimamo toka mwanzo lakini sasa karuhusu watu eti wamuone yeye ni bora na afadhali Dkt Magufuli alikufa kwa sababu eti alikuwa mkali na kwa sababu eti alikuwa anatuma wawakilishi tu kwenda nje
Huwezi kuzuia watu kukuona bora au hufai, ndio maana wapo wanaompongeza na kumpinga vile vile (kama wewe).

Acha kumtwisha lawama zisizo na ukweli.
 
Mungu ukupa kondoo uwaongoze na sio uwahukumu
 

kila mtu apambane na umasikini wa kwake,hata hao chadema wanaokudanyanya wana nia njema,wanakudharau ndio maana.
 
Bahati mbaya,mabaya ndio hukaa kwenye kumbukumbu kwa muda mrefu zaidi kuliko "mema"
"Heri wafu wafao katika Bwana naam asema roho wapate kupumzika kwa maana matendo yao hufuatana nao" jamaa hataki matendo ya mahaba wake yafuatane nae! Bila kusahau aya "Kuluhakah wanaikarah mulah" sema kweli japo moyo unauma.
 
Kusema mtu alivyo sio kumhukumu, ni kutoa maoni. Hukumu duniani hutolewa na majaji na ya kwenda Jehanamu hutolea na Mungu.
 
Mama alitaka kujiuzuru huo umakamu wa Rais kwa sababu ya huyu mshamba wenu kama ulikuwa hujui.
 
Mnahangaika sana pro Jiwe. Huyo hawezi kurudi wala kudumu kwenye mipango ya nchi hii. Aliupata kwa bahati mbaya na bahati mbaya pia amekomea njiani bila kuacha sumu zaidi .

Mtu yeyote aliye serious ktk kutafuta maisha ya family yake. Hawezi kushobokea mwendazake labda wanyonge waliopumgazwa na propaganda.
 
kama wewe ni zao la ccm,basi ni team mapoda au msoga inc & company.

hakuna mwana ccm au mwanacdm makini na taifa hili anayembeza jpm,ni viazi mbatata wazee wa slope ndio alijua kuwafirigisa.
hahahaaha wazelendo uchwara wa sukuma gang mnateseka Sana Si mlijifanya wajanja nyie yaani mlitoka kwenu kolomije na chattle Kwa kudandia malori kuja town,halafu mnajitia kuujua mji na nchi kiujumla haya Leo ujuaji wenu upo wapi?

Spidi na mbwembwe nyiiingi za kujimwambafai na kutukana wakubwa zenu Leo mmemute Kama Kobe sisi tuliwaambia mapema Kwa ushamba wenu na propaganda uchwara za kianology na mungumtu wenu Jiwe aliejaliwa roho mbaya,katili na ujuaji hamtafika Mbali
Leo Kiko wapi?
Karma!
😁😁😁😁
 
Ndo haya nisemayo, kufa kwa mtu ni mpango wa Mungu, hata asingekuwa Rais ange

Umeongea vyema sana ndugu! Ila mtoa mada huyu siyo bure, utadhani ni kama mzimu wa Magufuli unamtetea Magufuli. Huyu Mtoa mada ni kama aliyevaa miwani ya mbao, hawezi kuona hoja nyingine nzuri ya mtu mwingine kwa vile tu inapingana na hoja yake. Pili, kuna watu wanajua 100% kuwa wameonewa, na Magu mwenyewe alikuwa anajua wameonewa kwa sababu zake tu za kisiasa na masifa yake tu. Lakini yeye Magu alifika mbali kusema uwongo madhabahuni (kwa kitu ambacho sisi tunajua ukweli wake 100%). Yule bwana kulikuwa na kipande cha kichwa chake kilikuwa na kichaa kabisa na alikuwa hajui kama ni kichaa, kama ambavyo kichaa wa kawaida huwa hajui kama yuko uchi, yeye anadhani nyie wenye nguo ndo mko uchi.

Mtoa mada, mshukuru sana Mungu kama hukuwahi kuguswa na negative part ya Magufuli. CCM wenyewe asilimia kubwa walionja shubiri, viongozi hata waliotaka kujiuzulu kupinga dhuluma walishindwa kwa vile wangeonekana wazi wanampinga, na hivyo wangekiona cha mtema kuni wao na ''shangazi'' zao na ndugu zao na network zao zote. Ikabaki kuwa nchi ya unafiki na kusifia kwa kwenda mbele. Critical minds za Vyuo Vikuu zikanyamaza kimyaaa.

Kwa ujumla, tujue tu kuwa hatuwezi kuwazuia watu kuongea ukweli wanaoujua wenyewe, na hata hisia zao. Mungu atajua anayesema ukweli na ayesema uwongo. Tuwaachie waseme mema na mabaya, ili watawala wengine wajifunze. Huhitaji kutumia nguvu nyingi kutetea wema wa Kiongozi- unakuwa uko wazi ; na pia ubaya wa Kiongozi huwezi kuuficha unakuwa uko wazi tu.

Namna unavyoishi, unavyofanya, unavyoongoza, unavyoongea etc- yaani mwenendo na tabia zako wewe, ndizo zinazofundisha watu wengine namna ambavyo wataku-treat. The way you behave, teaches others how they should treat you.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…