Hayati Dkt. Magufuli anapohukumiwa kwa kifo chake

Eti kifo Cha mwenzio isiwe kicheko kwako unakumbuka magufuli alikataza hata watu kumuombea lissu Yani alitufikisha viwango vya uadui wa juu Kama taifa kuvaa fulana za kumuombea lissu ikawa jinai kwenda hospital kumpa pole ikawa jinai khaaa baba yule hapana aisee na aendelee kuwa carbon.
 
Pote
Potelea mbali sijaiba Cha mtu sijauwa mtu sijateka mtu sijafunga watu kwa kesi za uongo sijaikufuru Wala kuinajisi altare ya Mungu naamini mungu muumba wangu atanipa kifo Cha amani na cha heshima.
Ukisoma maandiko kuna watakatifu walikufa vifo vibaya, kuna waliokata vichwa, kuna waliokaangwa kenye mafuta. Acha kiburi cha uzima wewe uwezi jua kifo chako. Usijisifie kwa ujionavyo wewe! Jiulize Mungu anakuonaje? Hakuna dhambi kubwa wala ndogo! Pia hata kumsema mwenzio si haki mbele za Mungu!
 
Hapo umekosea sana.

Hivyo vifo vyote ulivyovitaja, pamoja na shambulio dhidi ya Lisu, kama kusingekuwa na maelekezo au baraka zake, hakika uchunguzi ungefanyika. Lakini alizuia, na hata wengine walioenda kumwona Lisu hospitali, kama walikuwa Serikalini, ilikuwa mwisho wa ajira zao.
 
We piga kelele Ila mwamba wenu ushaondoka yeye hakuyapa maisha ya wenzie thamani aliona kumpoteza Ben Rabiu Saanane ni sawa na kupoteza kitimoto bandani Sasa nayeye katoeshwa milele na hatorudi aban we are happy at last.
 
Haya ayanihusu, naongelea binadamu kuhukumu. Sijaja hapa kuongelea Lisu au sijui Ben Sanane, kama unahitaji kuwaongelea toa mada zinazowahusu. Nachofahamu Mungu uona kwa jicho la tofauti! Mungu wetu ndiye anae hukumu na kusamehe, mimi ni nani nichukue mamlaka ya Mungu? Kaini aliuwa bado mungu akampa ulinzi. Soma mada vizuri.
 
Mada yako inashangaza.

Imagine unakutana na watu wanapiga yowe kwamba kuna mtoto kazaliwa......
Lazma utajiuliza huyo mtoto ana nini kwanini wanalia badala ya kufurahi?

Kwa kawaida watu huuzunika sana mtu mwema akifa na si kumuhukumu au kufurahia.

Sasa huyu aliyetangulia ana tatizo gani na watu waliokuzunguka mpaka wamuhukumu na kufurahi?
 
We piga kelele Ila mwamba wenu ushaondoka yeye hakuyapa maisha ya wenzie thamani aliona kumpoteza Ben Rabiu Saanane ni sawa na kupoteza kitimoto bandani Sasa nayeye katoeshwa milele na hatorudi aban we are happy at last.
Heri yako unae dhani utakufa na kuwa anae kufa ni alie kosea. Sijamtaja Ben nadhani soma uelewe kinachoongelewa.
 
Unatuletea propaganda za kipumbavu a haya ndio mambo yaliyochangiwa magufuli kuchukiwa Sana kuunda vikundi vya kimungiki kuchafua watu.

Mfano kifo Cha Ben Rabiu Saanane hivi mbowe amuuwe Ben halafu magufuli alivyomchukia mbowe asiamrishe hata chembe ya uchunguzi akili zako Basi zitakuwa za kipumbavu. Nakuapia Kama kweli chadema ingehusika au mbowe angehusika na kifo Cha Ben chacha wangwe au shambulio la lissu wazandiki wa ccm wangeitumia hiyo Kama hoja kuu ya kuiadhibu chadema na kuifuta kabisa.jpm aliasisi uhuni wa hovyo Sana katika ikulu ya nchi yetu.
 
Unatangatanga, bila ya kuwa na kumbukumbu. Ni nani aliyeuliza kama kuna ushahidi kuwa ni marehemu ndiye aliyewaua/kuwapoteza Ben na akina Gwanda. Siyo wewe? Kwa nini unapojibiwa unakana kuwa siyo mada iliyopo? Basi nawe usingewaongelea kabisa.
 
Mada yako inashangaza.

Imagine unakutana na watu wanapiga yowe kwamba kuna mtoto kazaliwa......
Lazma utajiuliza huyo mtoto ana nini kwanini wanalia badala ya kufurahi?

Kwa kawaida watu huuzunika sana mtu mwema akifa na si kumuhukumu au kufurahia.
Sielewi hata unachokiongelea, Hata Yesu alipokufa watu walifurahia! Angalia Biblia watu wengi wema walipokufa maadui zao walishangilia! Mungu wetu haukumu kwa kuangalia watu wanasema nini!

Basi kwanini watu walijazana kwenye kifo chake kama kweli alngekuwa anachukiwa kwa uzushi huo wanao usema ttungeona barabara empty!
 
Uzi wako hapo juu #1 ni unafiki mtupu. Unasema Lowassa hata kama njia zilizomfanya asiwe Rais hazikuwa za haki. Eti bado aliyeingia aliwekwa na Mungu ?!. How !! Unafiki .

Kwanini chaguzi si za haki ?!. Then wanaopitishwa waabudiwe ?! Unafiki
 
Porojo hizi. Maneno meengi kumbe pumba tupu.
 
Mpumbavu ni yule anae dhani wenzake ni wapumbavu. Na mpumbavu ni yule hajui mada inaongelea nini anakurupuka na kuleta mada zingine. Na mpumbavu ni yule asie jadili mada bali anadhani matusi ndiyo njia pekee ya kuonesha anajua wakati hajui. Mpumbavu ni mtu ambae ueleza vitu kwa ushabiki pasipo kuwa na uhakika au kweli ya kile kisemacho.
Mpumbavu utanguliza upumbavu kabla hajaanza kujadili mada.
 
CCM wenzao inaonekana walishampani kitambo sana. Tumeona baada ya yeye kufa.
 
Unatangatanga, bila ya kuwa na kumbukumbu. Ni nani aliyeuliza kama kuna ushahidi kuwa ni marehemu ndiye aliyewaua/kuwapoteza Ben na akina Gwanda. Siyo wewe? Kwa nini unapojibiwa unakana kuwa siyo mada iliyopo? Basi nawe usingewaongelea kabisa.
Umesoma mada kuu, hilo jibu lilitolewa kwa swali ulilo uliza. swali ujibiwa lilivyo ulizwa. Weye ndo unatangatanga kwani nilieleza ukarukia Ben.
 
Hivi angekuwa hai hai leo !
WATANZANIA wangapi wangekuwa wameuliwa?
Unaambiwa kumfunga mbowe ilikuwa ni plan b Ila jiwe lilishampitishia hukumu ya kifo lissu aliponea chupuchupu kwenye geti la ubalozi wa German evarist chahali juzi tumemsikia akisema wazi kwamba alishatumiwa watu kumuuwa. Sasa jiulize hao ni manusura je hit list ilikuwa na wangapi na wangapi walipotezwa?
 
Uzi wako hapo juu #1 ni unafiki mtupu. Unasema Lowassa hata kama njia zilizomfanya asiwe Rais hazikuwa za haki. Eti bado aliyeingia aliwekwa na Mungu ?!. How !! Unafiki .

Kwanini chaguzi si za haki ?!. Then wanaopitishwa waabudiwe ?! Unafiki
Kuna mambo yamekaa kirho na wenye kuyatambua inabidi wawe katika roho!
 
Wapo wanadamu ambao hufa kwa sababu wameishi na kumpendeza Mungu, na baada ya kutimiza mapenzi yake, huwarudisha watakatifu wake. Na wengine, kupitia vifo vyao, Mungu hutaka kutufundisha tuliosalia kuonesha kuna watakatifu wake ambao wameishi kwa kumpenda na kumtumikia yeye tu.

Mateso na vifo vya mitume na waumini wa kale, ni moja ya vifo ambavyo vilituhakikishia kuwa kuna watakatifu wa Mungu waishio Duniani. Hawa walikufa kwa vifo vizuri maana waliilinda imani hatankatika mazingira magumu na ya mateso Makuu. Hata hivyo Mungu aliwaimarisha katika safari zao ili wayashinde mauti.

Wapo watu waliokufa kwa vito vya adhabu ili kuwalinda watu/wana wa Mungu. Askari wa Pharaoh waliuawa ili kuwalinda Waisrael. Herode alikufa ili mtoto Yesu awe salama. Kwa hiyo tutambue kuwa, ni kweli wapo wanaokufa ili kunusuru wengine. Nisiloweza kutamka, japo maisha ya Maguguli yaliondoa uhai wa baadhi ya watu, yalileta majonzi kwa wengi na kuleta mateso makubwa kwa baadhi ya watu, kama mwanadamu siwezi kusema kama kifo chake ilikuwa kuwanusuru wengi ambao wangeendelea kuangamia.

Kilicho dhahiri, watanzania wengi walifunga na kuomba au marehemu apate hekima ya uongozi au uongozi wake ukome. Hawa wote walioomba, wana haki ya kumshukuru Mungu, siyo kwa sababu Magufuli amekufa bali kwa sababu ombi lao la kutaka uongozi wake ukome, sala yao imesikilizwa.
 
Sasa kama hukuelewa nilichosema haya maelezo yote unajibu hoja ipi?

YESU walishangilia sababu walikuwa hawampendi, wakaona heri aachiwe jambazi ila YESU aondolewe.

Kama unajua kuwa maadui ndio wanaoshangilia vifo vya watu wema unatesekea nini kutumia nguvu kueleza? Au maadui wake wanaokuzunguka ni kundi kubwa la watu?

Kama wewe huna shaka na mapenzi ya raia wake kwake, na umeshuhudia watu wakimlilia na kujaa barabarani maelezo ya hukumu na kufurahia ni ya nini na kwa nini?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…