Hayati Dkt. Magufuli anapohukumiwa kwa kifo chake

Hayati Dkt. Magufuli anapohukumiwa kwa kifo chake

Wapo wanadamu ambao hufa kwa sababu wameishi na kumpendeza Mungu, na baada ya kutimiza mapenzi yake, huwarudisha watakatifu wake. Na wengine, kupitia vifo vyao, Mungu hutaka kutufundisha tuliosalia kuonesha kuna watakatifu wake ambao wameishi kwa kumpenda na kumtumikia yeye tu.

Mateso na vifo vya mitume na waumini wa kale, ni moja ya vifo ambavyo vilituhakikishia kuwa kuna watakatifu wa Mungu waishio Duniani. Hawa walikufa kwa vifo vizuri maana waliilinda imani hatankatika mazingira magumu na ya mateso Makuu. Hata hivyo Mungu aliwaimarisha katika safari zao ili wayashinde mauti.

Wapo watu waliokufa kwa vito vya adhabu ili kuwalinda watu/wana wa Mungu. Askari wa Pharaoh waliuawa ili kuwalinda Waisrael. Herode alikufa ili mtoto Yesu awe salama. Kwa hiyo tutambue kuwa, ni kweli wapo wanaokufa ili kunusuru wengine. Nisiloweza kutamka, japo maisha ya Maguguli yaliondoa uhai wa baadhi ya watu, yalileta majonzi kwa wengi na kuleta mateso makubwa kwa baadhi ya watu, kama mwanadamu siwezi kusema kama kifo chake ilikuwa kuwanusuru wengi ambao wangeendelea kuangamia. Kilicho dhahiri, watanzania wengi walifunga na kuomba au marehemu apate hekima ya uongozi au uongozi wake ukome. Hawa wote walioomba, wana haki ya kumshukuru Mungu, siyo kwa sababu Magufuli amekufa bali kwa sababu ombi lao la kutaka uongozi wake ukome, sala yao imesikilizwa.
Unauhakika kwamba watanzania walifunga na kuomba ili uongozi wake ukome? Ulifanya utafiti! So mtu akifa madarakani uongozi wake mbaya? Tusihukumu na kujifanya tunajua zaidi kuliko Mungu.
Sababu za Magufuli kufa azijuae ni Mungu pekee, na anakusudi lake! Tusijifanya tunaelewa juu ya uondoaji wa roho za watu!
 
Moja kati ya nyuzi zenye mwelekeo wa kizalendo kabisa hii
Tumuenzi Raisi wa awamu ya 5 kwa yale yote mema aliyotutendea nchi hii
 
Sasa kama hukuelewa nilichosema haya maelezo yote unajibu hoja ipi?

YESU walishangilia sababu walikuwa hawampendi, wakaona heri aachiwe jambazi ila YESU aondolewe.

Kama unajua kuwa maadui ndio wanaoshangilia vifo vya watu wema unatesekea nini kutumia nguvu kueleza? Au maadui wake wanaokuzunguka ni kundi kubwa la watu?

Kama wewe huna shaka na mapenzi ya raia kwake maelezo ni ya nini na kwa nini?
Kwani kuna kanuni kuwa usipo elewa usitoe maelezo? Pia sijatumia nguvu kueleza, nimerelux na ninachekelea kuona uelewa wa watu katika mada. Mapezi ya watu kwake niyeye ila binadamu hatuna mamlaka ya kuhukumu! Narudia Kaini aliuwa lakini Mungu bado alionesha upendo kwa Kaini. Binadamu tuache kujipa ambacho Mungu ajatupatia. Hukumu ni kwake si kwetu.
 
Sielewi hata unachokiongelea, Hata Yesu alipokufa watu walifurahia! Angalia Biblia watu wengi wema walipokufa maadui zao walishangilia! Mungu wetu haukumu kwa kuangalia watu wanasema nini!
Basi kwanini watu walijazana kwenye kifo chake kama kweli alngekuwa anachukiwa kwa uzushi huo wanao usema ttungeona barabara empty!
Isome historia ya Dunia. Kifo kilichowahi kuhudhuriwa na watu wengi kuliko cha mtu yeyote ni cha Dikteta Stallin. Huyu aliua warusi kwa maelfu.

Siku ya maziko yake, maelfu ya watu walikufa kwa kukanyagana, japo taarifa ya serikali ilisema ni watu 109 tu.
 
Tatizo unajibu bila ya kufanya rejea. Mimi siye niliyeandika uharamia wa marehemu dhidi ya Ben. Kuna mchangiaji aliandika orodha ya watu waliopotezwa na utawala wa marehemu dikteta Magufuli. Wewe ukamwuliza kama ana uhakika. Ndipo nilipokujibu.

Tuliza akili ili utoe majibu yenye mantiki.

Tunaambiwa kuwa tukipandacho ndicho tukivunacho. Kama marehemu angekuwa anajua kuwa kila mwanadamu atakufa, pamoja na yeye, wala asingeona ni kitu anachoweza kuwatendea wengine.

Mungu huongea nasi kwa kupitoa wanadamu wenzetu. Hata baadhi ya maneno ya wanadamu wenzetu dhidi ya marehemu, tusiyaone tu ni maneno ya mitaani, mengine ni sauti ya Mungu ya kutukumbushaapungufu yetu kwa kupitia maisha ya kutisha na ya dhuluma dhidi ya wanadamu wenzake aliyoyaishi marehemu.
 
Isome historia ya Dunia. Kifo kilichowahi kuhudhuriwa na watu wengi kuliko cha mtu yeyote ni cha Dikteta Stallin. Huyu aliua warusi kwa maelfu.

Siku ya maziko yake, maelfu ya watu walikufa kwa kukanyagana, japo taarifa ya serikali ilisema ni watu 109 tu.
Unajua warusi wamchukuliaje Stallin? Unajua Wajerumani na baadhi ya nchi za Scandinavia zinamchukuliaje Hitler? Unajua Saddam alie hesabika na mmarekani kuwa ni dicteta alichukuliwaje na wa Iraq?

Shida tunadhani hizi nchi zinazojifanya kuwa zinaelewa kila kitu zikisema nasi tunakariri tukidhani wako sawa. Stallin haongelewi vibaya Urusi, bali maadui zake wakiongozwa na wabaya wa Urusi.

Hii misukumo ya kutoka nje kusema fulani mbaya ndo tumerithi waafrika. Tunasubiri kuambiwa kiongozi wenu mbaya. Gadaffi wa Libya pamoja na mazuri yote aliyowafanyia wa Libya wakaambiwa huyo ni dicteta akili zao zikafuata cha kuambiwa wakamuuwa.
Ndipo nampenda KIkwete kwa misemo yake yenye hekima..."Cha kuambiwa changanya na akili zako"
 
Kwani kuna kanuni kuwa usipo elewa usitoe maelezo? Pia sijatumia nguvu kueleza, nimerelux na ninachekelea kuona uelewa wa watu katika mada.
Sasa ndugu mtu anayeelezea mambo asiyoyaelewa bila kutumia nguvu, amerelax huku akichekelea huwa anaitwaje?
 
Tatizo unajibu bila ya kufanya rejea. Mimi siye niliyeandika uharamia wa marehemu dhidi ya Ben. Kuna mchangiaji aliandika orodha ya watu waliopotezwa na utawala wa marehemu dikteta Magufuli. Wewe ukamwuliza kama ana uhakika. Ndipo nilipokujibu.

Tuliza akili ili utoe majibu yenye mantiki.

Tunaambiwa kuwa tukipandacho ndicho tukivunacho. Kama marehemu angekuwa anajua kuwa kila mwanadamu atakufa, pamoja na yeye, wala asingeona ni kitu anachoweza kuwatendea wengine.

Mungu huongea nasi kwa kupitoa wanadamu wenzetu. Hata baadhi ya maneno ya wanadamu wenzetu dhidi ya marehemu, tusiyaone tu ni maneno ya mitaani, mengine ni sauti ya Mungu ya kutukumbushaapungufu yetu kwa kupitia maisha ya kutisha na ya dhuluma dhidi ya wanadamu wenzake aliyoyaishi marehemu.
Niliunganisha yule aloongelea huo uharamia nawe, na weye pia kwani mie mada imejikita kwenye hukumu. Siko hapa kusema fulani aliua au hapana. au kusema alikuwa na dhambi au lah! Mada yangu inaongelea hatuna haja ya kutoa hukumu kwani atowae hukumu ni Mungu. Ndo nikaongelea hata Kaini aliuwa, lakini Mungu alichofanya ni kumlinda kaini asije uwawa. Na akasema atake muuwa Kaini kisa tu aliuwa nduguye basi huyu mtu atahadhibiwa zaidi. Na akamweka alama Kaini ili asihadhibiwe.

Hii inaonesha Mungu hapendi sis wanadamu tuhukumu. Hata kama Magufli alitenda au hakutenda, Hukumu ni Mungu ajuae, si sisi kuanza kumuhukumu Magufuli kuwa alikufa kwa sababu ya matendo yake. Hii si kazi ya Mwanadamu. Na hatuna ushahidi kama kweli yeye aliuwa! au hakuuwa! Tumwachie Mungu. Hii ndo mada yangu inachoongelea.
 
Hakuna sehemu aliyosafishwa, na siko kusafisha, bali naongea wazi hakuna chuki ya marehemu duniani. Kujenga chuki kwa mtu alokufa nadhani ni kutokuwa na akili za kufikiri. Nimeongelea kifo chake na yasemwayo kwa hicho kifo. Sasa nimsafishe kwa nani?
Nyie ndo mtakao kufa vifo vya ajabu na vibaya! Wewe si Mungu kuhukumu!
Sasa nimtetee Magufuli kwani anagombea uRais. Soma uelewe mada chuki zako usikimbie na kuandika tofauti ya mada.
Napenda kukukumbusha utakufa pia, je umetafakari maisha yako?
Mbona Wametangulia wengi tu na hawasemwi kitu?
J Nyerere, B. Mkapa, K. Ngombale, Maalim Seif, Kijazi na weengi wengine ndani ya Serikali aliyokuwa akiongoza.
Hawasemwi ngooh! Hebu Jiulize kwanza kwa nini huyo!??

Sent from my SM-A115AZ using JamiiForums mobile app
 
Unauhakika kwamba watanzania walifunga na kuomba ili uongozi wake ukome? Ulifanya utafiti! So mtu akifa madarakani uongozi wake mbaya? Tusihukumu na kujifanya tunajua zaidi kuliko Mungu.
Sababu za Magufuli kufa azijuae ni Mungu pekee, na anakusudi lake! Tusijifanya tunaelewa juu ya uondoaji wa roho za watu!
Wapo ambao nafahamu walisali sana na kumlilia Mungu kutokana na dhuluma ya utawala wa marehemu dhidi ya wapendwa wao ambao kwa uhakika walijua hawakuwa na hatia.

Hawakuomba kifo cha Magufuli bali waliomba dhuluma na utawala wa dhuluma ukome. Ukome kwa namna gani, walimwachia Mungu. Japo siamini kama kuna aliyedhani ungekoma kwa kifo.

Nilienda Segerea mara 8, kwaajili ya kumwona ndugu yangu. Niliongea na baadhi ya watu, wazee, akina mama, watoto, n.k; ambao ndugu zao walikuwa wamerundikwa ndani kwa kusingiziwa uhujumu uchumi. Wengine walikuwa wanashindwa hata kujizuia kulia. Walisimulia huku wakitokwa machozi kwa namna ndugu zao walivyoonewa, walivyoteswa, walivyotekwa. Wengine walikuja kufahamu ndugu zao wapo Segerea baada ya miezi miwili. Ndugu yangu ambaye alikaa huko kwa zaidi ya mwaka, natambua kwa 100%, hakuwa na hatia. Baadaye aliachiwa. Niliulizia sana kutaka kujua kosa lake, nilichoambiwa baadaye ni kuwa hata ningeuliza vipi hata iwe kwa nani, hakuna atakayeniambia kosa la huyo ndugu yangu. Yalikuwa ni maagizo ya marehemu mwenyewe na ndiye atanayejua aachiwe lini.

Mmoja wa maafisa wa juu kwenye vyombo vya usalama, alieleza kuwa kosa la ndugu yangu, aliwaambia, ni kutaka kushindana naye. Katika nini, hakuna ajuaye.

Bado nasisitiza kuwa kuna watu waliomba sana, siyo kumwombea kifo bali kutaka tuwe na utawala wa haki, utawala usiodhulumu watu.

Pamoja na yote aliyofanyiwa ndugu yangu, sikufurahia kifo cha Magufuli ila ningefurahi kama angeondoka madarakani, ashuhudie watu watakavyofurahi wapatapo mtawala mwenye hekima na upendo, na hata kushtakiwa au kupata nafasi ya yeye binafsi kujutia yale mabaya aliyoyafanya dhidi ya wanadamu wenzake. Lakini ni nani mimi wa kuhoja hekima ya Mungu. Muumba wetu hakosei, hachelewi wala kuwahi kupita kiasi bali huwajalia waja wake kilicho sahihi, kwa wakati sahihi na kwa namna sahihi. Mengine tunafunulia kuyatambua tukiwa hapa Duniani, mengine hatutayajua kamwe ila tujuacho ni kuwa Mungu wetu hakosei, na utawala wake ni wenye hekima kuu.

Tuzidi kuomba kupitia kifo cha huyu mwenzetu na wengine, ili kupitia kwao tuisikie sauti ya Mungu.
 
Mada yangu haiongelei hao watu, naongelea mtu kuhukumiwa, je sisi binadamu tuna mamlaka ya kuhukumu? Hata kama mtu alifanya makosa? Soma uelewe mada usikurupuke. Ndo maana nikasema hata Kaini aliuwa kwanini Mungu bado alimlinda Kaini? Watu wengi ukurupuka wajui mada inachosema. Lakini pia hao unao wataja unaushahidi kuwa Magufuli aliwauwa? Mbona kumekuwa na tuhuma za Ben Sanane kuuwawa na Boss wake, Kumekuwa na tuhuma alie kuwa Makamu mwenyekiti wa Chadema kuuwawa na Mwenyekiti?
Lakini watu wangapi wamepoteza maisha nyakati za uongozi tofauti? Hii haiwezi kukufanya uhukumu. Anae hukumu ni Mungu pekee!
Kuwa na akili hata kidogo. Unaleta uzi huku ukiwa huna hoja.

Huelewi hata mamlaka ya rais ni yapi?

Yeye ndiye raia namba moja..na ndiye mtu pekee wa kwanza anayetakiwa kila raia wa nchi yake anakuwa salama.

Ndiyo maana majeshi na vyombo vingine vya ulinzi na usalama vipo chini yake.

Anaposhindwa, unataka tuhamishie matatizo kwa wengine.

Alipokosea acha asemwe na kuhukumiwa,maana vipimo vipo.

Aliyofanya vizuri acha apongezwe.

Binafsi, ukiacha hizo changamoto kuna mengi mazuri ambayo amefanya na yatabakia mioyoni mwa watu.

Achana na wapiga porojo ambao kwao baya moja, linaharibu mema mengi.
 
Mbona Wametangulia wengi tu na hawasemwi kitu?
J Nyerere, B. Mkapa, K. Ngombale, Maalim Seif, Kijazi na weengi wengine ndani ya Serikali aliyokuwa akiongoza.
Hawasemwi ngooh! Hebu Jiulize kwanza kwa nini huyo!??

Sent from my SM-A115AZ using JamiiForums mobile app
Kwanza sijakataa mtu kuongelewa, mada yangu inahusu kutoa hukumu kama binadamu. Watu wanasema Magufuli kafa kwa sababu ya mabaya yake. Ndo nachoeleza hapa Anae jua siri ya kifo cha Magufuli ni Mungu siyo binadamu.

Pia hata hao waliongelewa ila sijawaongelea hapa. Mfano, Nyerere tu aliongelewa hadi baadhi wakafanya sherehe, mmoja wapo alikuwa Mtikila.

Lakini leo Mch. Mtikila alie shabikia kifo cha Nyerere yuko wapi? Najua kuna watu walikuwa wanamchukia Magufuli hawakumpenda uwezi kupendwa na kila mtu. Ila hatuna mamlaka ya kuhukumu hii ndiyo mada yangu.
 
Unajua warusi wamchukuliaje Stallin? Unajua Wajerumani na baadhi ya nchi za Scandinavia zinamchukuliaje Hitler? Unajua Saddam alie hesabika na mmarekani kuwa ni dicteta alichukuliwaje na wa Iraq?
Shida tunadhani hizi nchi zinazojifanya kuwa zinaelewa kila kitu zikisema nasi tunakariri tukidhani wako sawa. Stallin haongelewi vibaya Urusi, bali maadui zake wakiongozwa na wabaya wa Urusi.
Hii misukumo ya kutoka nje kusema fulani mbaya ndo tumerithi waafrika. Tunasubiri kuambiwa kiongozi wenu mbaya. Gadaffi wa Libya pamoja na mazuri yote aliyowafanyia wa Libya wakaambiwa huyo ni dicteta akili zao zikafuata cha kuambiwa wakamuuwa.
Ndipo nampenda KIkwete kwa misemo yake yenye hekima..."Cha kuambiwa changanya na akili zako"
Inachotakiwa kufahamu pia ni kuwa hakuna mbaya asiye na rafiki wala aliye mzuri asiye na maadui. Hata jambazi kuna watu wananufaika kutokana na ujambazi wake.

Huko Libya, wapo waliopenda Gadafi lakini wapo waliomchukia sana. Na yapo maovu makubwa kabisa aliyowahi kuyatenda Gadafi dhidi ya watu wake.

Lakini pia usisahau kuwa madikteta wengi, hupenda kuwapumbaza watu kwa kudhibiti habari. Mara nyingi watu wenye akili kidogo na ambao uwezo wao wa kupata habari nje ya vyombo ambavyo hufanya kazi ya kumsifu mtawala, haupo, huwa wanaamini propaganda za huyo mtawala. Na hiyo ndiyo sababu ya kuonekana mtawala huyo anapendwa, japo mara nyingi baada ya vifo, wanaoendelea kumkumbuka kwa mazuri hupungua, lakini wapo watakaomkumbuka kwa mema maisha yao yote.

Lakini huwezi kumshawishi mtu eti ndugu wa wale maelfu waliouwawa na Stallin au Gadafi, eti walikuwa wakiwapenda hao watawala.

Usisahau kuwa watawala hao wabaya wanapofariki, ile machinery waliyoitengeneza huwa ipo vile vile. Kifo cha Stallin, wakati wengine wapo kwenye maziko, kule Sibetia walikuwa wakishangilia kwa furaha.

Mpendwa wetu alizikwa na kuliliwa na wengi, lakini hao wengi walikuwa ni asilimia ngapi ya Watanzania? Stallin alizikwa na watu wapatao milioni 2 lakini milioni 2 ni asilimia ngapi ya warusi wote? Lakini pia hata waliotendewa uovu na watawala hawa, wengi hawawezi kushangilia kifo cha aliyekuwa akiwatesa kwa hekima ile ile uliyoisema, huwezi kushangilia kwa kiti ambacho hata wewe, siku moja kitakufika.
 
Kuwa na akili hata kidogo. Unaleta uzi huku ukiwa huna hoja.

Huelewi hata mamlaka ya rais ni yapi?

Yeye ndiye raia namba moja..na ndiye mtu pekee wa kwanza anayetakiwa kila raia wa nchi yake anakuwa salama.

Ndiyo maana majeshi na vyombo vingine vya ulinzi na usalama vipo chini yake.

Anaposhindwa, unataka tuhamishie matatizo kwa wengine.

Alipokosea acha asemwe na kuhukumiwa,maana vipimo vipo.

Aliyofanya vizuri acha apongezwe.

Binafsi, ukiacha hizo changamoto kuna mengi mazuri ambayo amefanya na yatabakia mioyoni mwa watu.

Achana na wapiga porojo ambao kwao baya moja, linaharibu mema mengi.
Ati niwe na akili hata kidogo! Weye hapo unae jiona una akili ni sehemu gani ya katiba inayosema rais ni Raia namba moja, au nitajie sheria inayosema rais ni namba moja. Nachojjua na kutokuwa na akili hata kidogo, Katiba yetu inatambua binadamu wote tuna haki sawa. Natambua kuwa hakuna sheria Tanzania inayosema Raia wa kwanza ni Rais. Bali katiba inampa dhamana Rais kuongoza nchi na haisemi kuwa yeye ndo Raia namba moja.

Natambua kuwa si kazi ya Rais kulinda kila mwannchi asiuwawe, bali hiyo ni kazi ya vyombo vya ulinzi na usalama, na pia ni jukumu la mwananchi mwenyewe kujilinda. Ndo maana sheria zinaruhusu mtu kuomba ulinzi anapoona yuko hatarini au kutishiwa maisha. Rais si mungu kujua kila raia huko nyumbani kwake yukoje. Ndo maana hata sheria inamruhusu kuwa na ulinzi binafsi hata kumiliki silaha. Ingekuwa kulinda nadhani Rais wa Marekani wangejiuzuru sana kutokana na kushindwa kulinda mamia ya Raia wake wanao uana au kuuliwa.

Nashindwa kuelewa japo sina akili hata kidogo nazijua sheria za nchi na tafsiri zake. Wewe unajiona unaakili kubwa hivi ujuhi sheria za nchi yako? Ndo maana hata mtu binafsi ukitaka kujiuwa ukakutilizwa utafunguliwa makosa ua jinai kwa kujaribu kuuwa. Si Rais atakae ulizwa.
 
Inachotakiwa kufahamu pia ni kuwa hakuna mbaya asiye na rafiki wala aliye mzuri asiye na maadui. Hata jambazi kuna watu wananufaika kutokana na ujambazi wake.

Huko Libya, wapo waliopenda Gadafi lakini wapo waliomchukia sana. Na yapo maovu makubwa kabisa aliyowahi kuyatenda Gadafi dhidi ya watu wake.

Lakini pia usisahau kuwa madikteta wengi, hupenda kuwapumbaza watu kwa kudhibiti habari. Mara nyingi watu wenye akili kidogo na ambao uwezo wao wa kupata habari nje ya vyombo ambavyo hufanya kazi ya kumsifu mtawala, haupo, huwa wanaamini propaganda za huyo mtawala. Na hiyo ndiyo sababu ya kuonekana mtawala huyo anapendwa, japo mara nyingi baada ya vifo, wanaoendelea kumkumbuka kwa mazuri hupungua, lakini wapo watakaomkumbuka kwa mema maisha yao yote.

Lakini huwezi kumshawishi mtu eti ndugu wa wale maelfu waliouwawa na Stallin au Gadafi, eti walikuwa wakiwapenda hao watawala.

Usisahau kuwa watawala hao wabaya wanapofariki, ile machinery waliyoitengeneza huwa ipo vile vile. Kifo cha Stallin, wakati wengine wapo kwenye maziko, kule Sibetia walikuwa wakishangilia kwa furaha.

Mpendwa wetu alizikwa na kuliliwa na wengi, lakini hao wengi walikuwa ni asilimia ngapi ya Watanzania? Stallin alizikwa na watu wapatao milioni 2 lakini milioni 2 ni asilimia ngapi ya warusi wote? Lakini pia hata waliotendewa uovu na watawala hawa, wengi hawawezi kushangilia kifo cha aliyekuwa akiwatesa kwa hekima ile ile uliyoisema, huwezi kushangilia kwa kiti ambacho hata wewe, siku moja kitakufika.
Turudi kwenye mada, mada yangu ilikuwa kuwakumbusha jamii, tusihukumu bali hukumu ufanywa na Mungu. awe Magufuli kafanya baya au zuri hukumu ni Mungu pekee. Over!
 
Mbona Wametangulia wengi tu na hawasemwi kitu?
J Nyerere, B. Mkapa, K. Ngombale, Maalim Seif, Kijazi na weengi wengine ndani ya Serikali aliyokuwa akiongoza.
Hawasemwi ngooh! Hebu Jiulize kwanza kwa nini huyo!??

Sent from my SM-A115AZ using JamiiForums mobile app
Hivi usiposemwa ndo wewe umekuwa mwema? Kweli Mungu alisema yeye si mwanadamu ahukumuye kwa kuangalia. Bali ni Mungu atazamae ndani ya moyo wa mtu. Binadamu hatuna macho ya kuona ndani ya moyo wa mtu. Tunahukumu kwa ushabiki na kwa macho ya nyama si ya rohoni.
 
Kwanza sijakataa mtu kuongelewa, mada yangu inahusu kutoa hukumu kama binadamu. Watu wanasema Magufuli kafa kwa sababu ya mabaya yake. Ndo nachoeleza hapa Anae jua siri ya kifo cha Magufuli ni Mungu siyo binadamu.
Pia hata hao waliongelewa ila sijawaongelea hapa. Mfano, Nyerere tu aliongelewa hadi baadhi wakafanya sherehe, mmoja wapo alikuwa Mtikila.
Lakini leo Mch. Mtikila alie shabikia kifo cha Nyerere yuko wapi? Najua kuna watu walikuwa wanamchukia Magufuli hawakumpenda uwezi kupendwa na kila mtu. Ila hatuna mamlaka ya kuhukumu hii ndiyo mada yangu.
Kuhukumu siyo kazi ya mwanadamu. Maana imeandikwa, usihukumu usije ukahukumiwa.

Kufurahia kifo, hasa cha adui yako, ni hekima tu mtu lakini hakuna katazo la kiimani.

Waisrael walifurahia kifo cha Goliath akiyekuwa akiwaua.

Waisrael walifurahia kifo cha askari Pharaoh, na wakafanya adhimisho la kika mwaka, yaani Pasaka (passover), ambayo mpaka leo wakristo tunaiadhimisha.

Bikira Maria na Yusuf walifurahia kifo cha Herode.

Mimi na wewe, tunaweza tusifurahie kifo cha huyo ndugu yetu, lakini unasemaje juu ya wale ambao kila siku maisha yao yalikuwa yapo hatarini, na kila siku walikuwa wakiomba Mungu awaokoe kutoka kwenye mikono ya mtawala mwovu. Fikiria mtu kama TL na wengi walionusurika kuuawa. Wengine wakitupwa wakidhaniwa wamekufa, lakini kumbe Mungu amesihifadhi riho zao. Kisha mtawala aliyetaka kuwaua, na akiendelea kuwawinda, akatangulia, hawatakuwa na haja ya kufurahi na kumshukuru Mungu?
 
Kasome bible mkuu, Mungu hapangi kila kifo cha mtu
Mada yangu inahusu hukumu, je binadamu tumepewa mamlaka ya kuhukumu? Nadhani hujasoma vizuri ukaelewa! Hiyo Biblia naijua sana. Ndo maana nimesema Mungu ndiye anae jua yote! Uruhusu mambo fulani kwa utukufu wake, hata kama shetani kahusika au binadamu kahusika katika kifo. Ndo maana nikatoa mifano ya Ayubu alifiwa na watoto wake lakini si Mungu bali ilikuwa shetani alie sababisha vile vifo na Mungu alimkataza shetani asiguse roho ya Ayubu.
Ila mada yangu ni kukataa sisi kuhukumu. Hukumu tumwachie Mungu.
 
Back
Top Bottom