Hayati Dkt. Magufuli anapohukumiwa kwa kifo chake

Hayati Dkt. Magufuli anapohukumiwa kwa kifo chake

Kuhukumu siyo kazi ya mwanadamu. Maana imeandikwa, usihukumu usije ukahukumiwa.

Kufurahia kifo, hasa cha adui yako, ni hekima tu mtu lakini hakuna katazo la kiimani.

Waisrael walifurahia kifo cha Goliath akiyekuwa akiwaua.

Waisrael walifurahia kifo cha askari Pharaoh, na wakafanya adhimisho la kika mwaka, yaani Pasaka (passover), ambayo mpaka leo wakristo tunaiadhimisha.

Bikira Maria na Yusuf walifurahia kifo cha Herode.

Mimi na wewe, tunaweza tusifurahie kifo cha huyo ndugu yetu, lakini unasemaje juu ya wale ambao kila siku maisha yao yalikuwa yapo hatarini, na kila siku walikuwa wakiomba Mungu awaokoe kutoka kwenye mikono ya mtawala mwovu. Fikiria mtu kama TL na wengi walionusurika kuuawa. Wengine wakitupwa wakidhaniwa wamekufa, lakini kumbe Mungu amesihifadhi riho zao. Kisha mtawala aliyetaka kuwaua, na akiendelea kuwawinda, akatangulia, hawatakuwa na haja ya kufurahi na kumshukuru Mungu?
Hivi nani mwenye ushahidi wa kweli, tuache porojo za kusikia, kuwa Magufuli ndiye alie uwa hao unao sema, Magufuli ndiye sijui alifanya hiki. Mimi huko staki kuongelea sina ushahidi. Awe Magufuli alifanya au hakufanya. Je binadamu tuna mamlaka ya Kuhukumu? Ndo maana nilipokuwa chekechea nilishanga kwanini Mungu anamlinda mtu alie uwa. Tena alie uwa ndugu yake! Mpaka Mungu anaapiza kuwa ole wake atakae muuwa Kaini.
Hii sikuielewa wakati ule, nilimshangaa Mungu sana.
 
Mada yangu inahusu hukumu, je binadamu tumepewa mamlaka ya kuhukumu? Nadhani hujasoma vizuri ukaelewa! Hiyo Biblia naijua sana. Ndo maana nimesema Mungu ndiye anae jua yote! Uruhusu mambo fulani kwa utukufu wake, hata kama shetani kahusika au binadamu kahusika katika kifo. Ndo maana nikatoa mifano ya Ayubu alifiwa na watoto wake lakini si Mungu bali ilikuwa shetani alie sababisha vile vifo na Mungu alimkataza shetani asiguse roho ya Ayubu.
Ila mada yangu ni kukataa sisi kuhukumu. Hukumu tumwachie Mungu.
Ndugu huyo unaesema watu wanamhukumu baada ya kifo siyo kweli. Watu walianza kumsema kabla ya kufa.

Na kuhusu kuijua bible mimi naona bado sana. Wewe huyo unasema kifo Mungu ndo anapanga bila kujua kifo kilitokana na shetani. Ukihitaji mistari sema nikumiminie hapa ili utulie.
 
Hivi nani mwenye ushahidi wa kweli, tuache porojo za kusikia, kuwa Magufuli ndiye alie uwa hao unao sema, Magufuli ndiye sijui alifanya hiki. Mimi huko staki kuongelea sina ushahidi. Awe Magufuli alifanya au hakufanya. Je binadamu tuna mamlaka ya Kuhukumu? Ndo maana nilipokuwa chekechea nilishanga kwanini Mungu anamlinda mtu alie uwa. Tena alie uwa ndugu yake! Mpaka Mungu anaapiza kuwa ole wake atakae muuwa Kaini.
Hii sikuielewa wakati ule, nilimshangaa Mungu sana.
Nje kidogo ya mada:

Mungu alizuia kuawa kwa Kaini, ukoo wa Adam ungeendeleaje, kama baada ya Abel kuuawa na Kaini auawe, maana yake angesalia mtoto mmoja tu wa kiume.

Hivi unajua kuwa kifo kimtokeapo mwanadamu, huzuni na majonzi ni kwa ndugu wa karibu, siyo marehemu? Hapa ni kwa mara ya kwanza, ile adhabu ya Mungu kwa Adam na Eva, wanaionja ubaya wake.

Unakumbuka kisa cha kifo cha mtoto wa Daud kwa mke wa Uria? Mtoto alikuwa na hatia gani? Kosa la mfalme Daud, kwa nini kifo kikampate mtoto? Jibu, kifo huwaumiza walio hai na siyo marehemu. Ndiyo maana, wengine tunaona ni vema adhabu ya kifo ikafutwa.
 
Kifo ni tukio la kiasili. Katika imani kadhaa za kidini zina elezea kifo kilitokea baada ya Adamu na Hawa (Eva) kwenda kinyume na mapenzi ya muumba wao (MUNGU). Ndipo Mungu alitamka kuwa tutakufa, au kurejea katika mavumbi.
Binadamu wa kwanza kufa alikuwa Abeli. Ambaye aliuliwa na kakaye aitwae Kaini. Kaini japo alimuuwa Abeli, bado Mungu alimlinda Kaini na hata akasema atakae muuwa kaini basi atalaaniwa. Hivyo Mungu alimpeleka Kaini nchi ya mbali. Hii yote kumuepusha na kumlinda na mabaya. Mungu alifanya haya yote japo Kaini alikuwa na dhambi ya kumuuwa nduguye.

Mungu utazama tofauti, na macho ya binadamu. Na Mungu ndiye mwenye uweza wa kuhukumu. Siku hizi Tanzania hii kumezuka, tabia ambayo inaonesha watu kufurahia kifo au vifo vya watu wengine. Na kama walikuwa hawampendi huyo mtu au watu; ndo watazusha mengi. Wabaya wake watajifanya wao ni mungu (Mungu), watahukumu, watasema huyu alifanya mabaya ndo maana kafa.

Watajiona wao waliobaki ndo wajanja, hawana makosa au dhambi mbele ya Mungu. Najiuliza hivi kuna mahala popote pale iwe katika misaafu au maandiko yoyote ya kidini na imani zinginezo, pana sema mtu anae kufa mapema au kabla ya wenzie ana dhambi na Mungu kaamua kumkomoa?

Nachojua Mungu alisema tutakufa, hakuna atakaeishi milele hapa duniani. Ndo maana watu ufa wakiwa watoto wachanga, wakiwa vijana, wakiwa wazee, na hata watoto wengine ufia tumboni mwa mama zao kabla ya kuzaliwa.
Tukidai kufa mapema ni kukomolewa na Mungu, ebu tuangalie, hawa mitume wetu, walikufa bado wakiwa vijana, na walikuwa na maadui wengi, hawakupendwa. Yesu kristo aliishi miaka isiyozidi thelathini na tatu. Na alianza kazi ya kuhubiri akiwa na miaka thelathini tu. Vile vile kwa mtume Muhamad S.W.A alikufa mapema. Si hao tu ni wengi!

Hivyo kifo ni asili. Nachoamini kila mtu anakusudi la kuwepo duniani. Na pia ana muda wake wa kuishi. Haijalishi ni miaka mingapi. Muda ukifika Mungu ndo mwamuzi wa yote, uondoke au aseme bado ubaki.
Katika kila jambo Mungu anamakusudi yake. Laweza kuwa baya au zuri, lakini Mungu anatazama tofauti na tunavyotazama sisi wanadamu.

Kikubwa tusijipe kazi ya Mungu ikawa kazi yetu. Tusijipe kuhukumu kwani hukumu ya maisha yetu utolewa na Mungu. Usihukumu usije hukumiwa.

Nimeongea haya yote ni kutokana na watu wengi, wapinzani na wana CCM kuonekana kumhukumu alie kuwa Rais wa Tanzania, J.P. Magufuli na hata kumzodoa kuwa kafa mapema, yako wapi, kuonesha tu Mungu ati kamuondoa kwa mabaya yake. Nilishangaa hata Mchungaji mmoja anajiita mzee wa upako kuongea kama vile nae anaonesha kufa kwa magufuli ni kama adhabu, eti kisa Lowasa hakuchaguliwa Urais na kuwataka watu wakamuombe Msamaha Lowasa.

Mimi niseme kwa maandiko viongozi wote wakuu wa nchi uwekwa na Mungu. Mungu angeamua Lowasa kuwa Rais angekuwa tu. Mchungaji kasahau maandiko anatumia akili za kibinadamu. Kufa kwa Magufuli si kwamba Mungu hakutaka Magufuli awe Rais, la asha. Mungu hutenda kwa wakati wake.

Jiulize katika maandiko tunaambiwa kuwa Yusufu aliuzwa utumwani na nduguze, bado huyo Yusufu akafungwa gerezani. Lakini cha ajabu akaja kuwa ndiye waziri mkuu wa nchi. Hata nduguze walipojihisi atalipiza kisasi kwa kuwafanyia mabaya, aliwaambia. Mlikusudia mabaya kwangu, lakini katika hayo mabaya Mungu alikusudia mema ili nije niwaokoe katika baa la njaa.

Mungu uona mbali zaid ya binadamu. hatujui ni kwanini Mungu aliepusha Lowasa asiwe Rais japo ilitumika njia mbaya au nzuri, lakini Mungu anakuwa na makusudi yake. Mchungaji katafakari neno la Mungu ndo utoe tamko. Hakuna lifanyikalo duniani bila Mungu kuridhia. Mungu huyo aliruhusu Ayubu apate mateso, akaruhusu watoto wake Ayubu kufa na hata mali kuharibika na kupotea lakini alikuwa na kusudi. Kifo cha Magufuli kinakusudi liwe baya au zuri ila watanzania tutajifunza kutokana na hicho kifo siku moja. Kikubwa tusijichukulie mamlaka ya kuhukumu na kusema kafa kwa sababu alikuwa katiri na kadharika. Mbona Mungu alimlinda Kaini japo alikuwa muuwaji?

Hivi kazi yetu ni kuhukumu, kwani tuliobaki hatutakufa? wangapi tumefiwa na ndugu na wazazi, je kutangulia kwao ni kwamba walitenda mabaya Mungu kawahukumu?
Kwa uzoefu wa haraka tu mara nyingi watu wema hawadumu? Iwapo hadi sasa unaishi lazima ujiulize, unatakiwa kulifanyia nini Taifa lako la Tanzania, na familia yako. Si kushambulia marehemu, na kujifanya wewe ni mungu unahukumu. Leo hata viongozi wetu utasikia, oooh! Magufuli hakutenda haki, alikuwa kiongozi mbaya, alikuwa muuwaji, alitisha, hakuwa na demokrasia!

Hivi ninyi viongozi mnao sema haya si mlikuwa nae ktk uongozi wa serikali? Kwanini amkumwambia wakati huo akiwa hai kuwa ni kiongozi mbaya.
Nacho jua Magufuli alikubali kukosolewa. Naibu Waziri wa afya kipindi hicho alimkosoa kuhusu matumizi ya kujifukiza. Akamwondoa katika nafasi. Lakini baadae alimrejesha ktk wizara tofauti.
Leo wanao mkosoa magufuli haohao, wanapinga Mhe. Rais Samia kukosolewa. Wakati Rais alidai kuwepo uhuru wa kukosoa. Lakini chama chake na Bunge Wanataka asikosolewe, tumsifie hata kwa yale yasio sifiwa. Wakati wanadai wao ni wanademokrasia. Ukikosoa unahesabika msaliti, Bunge litakuita kwenye Kamati. Chama kitakaa kukuita kikuhoji kwa nini huko kinyume na Rais. Chama kinachoongozwa na mwenyekiti ambae ni Rais alie ruhusu kokosolewa.

Mungu hapendi wafitini na watu waongo, wenye roho za usaliti. Viongozi mjitafakari. Na msijione ninyi hamta kufa. Kifo kipo akijali madaraka yako. Hakuna atakae ishi milele. Kuwepo kwako pengine Mungu anataka utimize mambo fulani. Ghazabu ya Mungu ni kubwa tusihukumu tukaja hukumiwa. Magufuli kaondoka kamaliza yake. Alifanya kwa nafasi yake na kwa staili yake. Watu wote hatufanani.

Tusijione sisi ni bora kwakuwa tu watu wanatuchekea na kutusifia. Tukachekelea na kuota kiburi kuona tuko sahihi na hatukosei! Pamoja na yote Magufuli aliwapenda watanzania. Hakuwahi kusema waondoke wakaishi Burundi.
Leo kauli hiyo inaongewa na kiongozi aliepewa dhamana na watanzania. Viongozi wamejiona wako juu ya sheria, wanauwezo wa kusema chochote. Viongozi wamekuwa na dharau. Wanajiona nchi ni yao. Hata wananchi kulalamika hawaoni haja ya kuomba msamaha.
Hata kiongozi wa nchi hawakanyi anawaacha je naye kafurahishwa na hayo maneno? Je kawatuma?
Harafu hawa hawa ndo wanasema watakuwa wapole na kuwabembeleza wananchi kuliko JPM ambaye kapewa mabaya yote.
Tukumbuke kutangulia kufa si dhambi. Na ukibakia si ujanja wa kufanya kutukana waliotangulia. Bali chukua muda wa kujitafakari.

Mungu alimlinda Kaini japo alikuwa muuwaji wa nduguye. Mungu ndiye mwenye kuhukumu. Na ndiye ajuaye mwisho wa maisha yetu. Jiulize hapo ulipo matendo uyafanyao ktk vificho au wazi, je ni mema? Je wewe ni msafi zaidi ya waliotangulia kufa?
je wajua kifo chako kitakuwaje? Lini utakufa? Je utakufa ukiwa na umri gani? Je alie kutangulia kafa akiwa na miaka mingapi?
Si ujanja wala umaarufu kutukana marehemu, au kutafuta umaarufu ati unajilinganisha na marehemu. Huyo kesha maliza wakati wake hayupo tena. Tuache kashfa hatujui kesho yetu. Tanzania ya leo imekuwa na siasa za kujipendekeza, sifa za kijinga, badala ya kufikiria maendeleo ya kweli. Walio tangulia tuwaache, tujenge nchi.
Muuaji ni muuaji tu.
 
Ndugu huyo unaesema watu wanamhukumu baada ya kifo siyo kweli. Watu walianza kumsema kabla ya kufa.

Na kuhusu kuijua bible mimi naona bado sana. Wewe huyo unasema kifo Mungu ndo anapanga bila kujua kifo kilitokana na shetani. Ukihitaji mistari sema nikumiminie hapa ili utulie.
Hakuna sehemu nimesema Mungu anapanga kifo. Nadhani unasoma ukiwa na fikira zako na kupandikiza maneno. Soma tena. Nilichosema kuwa Mungu anajua sababu ya kifo, iwe mtu kauwawa na shetani, iwe mtu kauwawa na binadamu Mungu utambua. Na akiamua kutoruhusu kifo hata shetani hawezi. Mungu anakuwa hajaamuuwa mtu huyo kufa.
Ndo nikasema alimkataz ashetani asitoe roho ya Ayubu.

Mada yangu aijaongelea magufuli kusemwa kabla ya kufa. Hapa naongelea kifo cha Magufuli kinavyomhukumu! Ndugu yangu inaonesha uelewi kabisa mada hii inaongelea nini!
Mie nimejikita hukumu za watu wanazo zitoa kwa Magufuli baada ya kufa.

Ndo nikatoa rai kwa jamii tusimmuhuku Magufuli sisi si Mungu kujua kuwa kwanini magufuli kafa, na kusema kafa kwa mabaya yake. Nikasema hayo tumwachie Mungu. Awe ametenda mabaya Mungu ndiyo anajua si binadamu.

Hayo unayosema kaanza kuongelewa hajafa siyo mada yangu. Waweza kuanzisha nawe mada yako. Mada yangu ni hukumu baada ya kifo.
Kuhusu kuijua Biblia naijua sasa wewe si mwalimu wangu na sijakwambia wewe hujui. Uwa sishindani katika neno la Mungu, kwani roho wa Mungu ndiye utuwezesha na kutufunulia hata yale tusiyo yajua. Hivyo sijaja hapa kushindana.

Na pia hata shetani anaijua Biblia, alimwendea na kumjaribu Yesu kwa kutumia vifungu na mistari ya Biblia. Kikubwa ni nini kilichopo ndani ya mtu, je amejazwa na roho wa namna gani amwongozae kusema asemacho.
Hata Petro aliingiwa na shetani, Yesu akamkemea shetani na kusema rudi zako nyuma shetani. Alishajua Petro kaingiliwa na roho ya tofauti.
 
Hakuna sehemu aliyosafishwa, na siko kusafisha, bali naongea wazi hakuna chuki ya marehemu duniani. Kujenga chuki kwa mtu alokufa nadhani ni kutokuwa na akili za kufikiri. Nimeongelea kifo chake na yasemwayo kwa hicho kifo. Sasa nimsafishe kwa nani?
Nyie ndo mtakao kufa vifo vya ajabu na vibaya! Wewe si Mungu kuhukumu!
Sasa nimtetee Magufuli kwani anagombea uRais. Soma uelewe mada chuki zako usikimbie na kuandika tofauti ya mada.
Napenda kukukumbusha utakufa pia, je umetafakari maisha yako?
Tunapangiana kupenda au kuchukia tangu lini?
 
Nje kidogo ya mada:

Mungu alizuia kuawa kwa Kaini, ukoo wa Adam ungeendeleaje, kama baada ya Abel kuuawa na Kaini auawe, maana yake angesalia mtoto mmoja tu wa kiume.

Hivi unajua kuwa kifo kimtokeapo mwanadamu, huzuni na majonzi ni kwa ndugu wa karibu, siyo marehemu? Hapa ni kwa mara ya kwanza, ile adhabu ya Mungu kwa Adam na Eva, wanaionja ubaya wake.

Unakumbuka kisa cha kifo cha mtoto wa Daud kwa mke wa Uria? Mtoto alikuwa na hatia gani? Kosa la mfalme Daud, kwa nini kifo kikampate mtoto? Jibu, kifo huwaumiza walio hai na siyo marehemu. Ndiyo maana, wengine tunaona ni vema adhabu ya kifo ikafutwa.
Nafura unapojenga hoja. Kaini asingeweza kuuwawa na wazazi wake. Wakati huo alikuwepo Adam na Eva, pamoja na watoto wao wawili. Hivyo bado adamu aliendelea kuzaa si kwamba hakuendelea kuzaa, hivyo kizazi kingeendelea. Swala la kutouwawa kwa Kaini lilikuja baada ya Kaini mwenyewe kumlilia Munguhuku akiomba msamaha na kusema takuwa na maisha ya namna gani kwa hilo alilolitenda. Aliona atakoswa ushirikiano katika jamii na kuonekana mbaya na hata pengine kuuwawa nae pia. Kumbuka katika agano la kale ukiuwa nawe unauwawa.
ndipo Mungu akampunguzia adhabu na kusema mtu atakae muuwa kaini atahadhibiwa mara zaidi.
Na Mungu alimchukua na kumpeleka nchi ya mbali aliishi huko na kuwa na familia, wakati huku adamu na Eva walizaa watoto kibao.
Swala la Daudi na mke wa Uria, Mungu kweli alifanya ili Daudi ajifunze. Kuwa haikuwa haki kuchukua mke wa mtu kwa kumuuwa mmewe. Ndo maana baada ya Daudi kujua Mungu ndo katenda kifo cha mtoto kutokea uzuni ilimtoka na akavua magunia ya kuomboleza na kuvaa nguo nzuri huku akiwa mwenye furaha.
Ndo maana vifo vingi tunaambiwa tusilie sana au kusema sana tukaja kufuru. Hatujui Mungu alikuwa na sababu ipi kifo kutokea.
Nakubaliana nawe, ni heri adhabu ya kifo indolewe. Tuna baadhi ya majaji wengi wamestaafu, katika hukumu zao ukwepa sana kumhukumu mtu adhabu ya kifo.
Wakati fulani kuna jaji alisaidia dada mmoja alie muuwa mwanae wa kumzaa, japo kesi ilikuwa murder lakini jaji alisema moyo wa binadamu umejawa hofu, mpaka mtu anauwa mtoto wake mdogo wa kumzaa kuna jambo ambalo si zuri na hasa uwenda mama alikuwa na roho mchafu. Hivyo tukimpa murder yule mdada tutamuuwa kwa jambo ambalo akufanya kwa akili zake. Tanzania hakuna sheria za imani za majini na mashetani au uchawi. Yule dada alipelekwa kupimwa akili madakitari walisema ni mzima hana tatizo la akili, lakini ndugu walidai yule dada anamashetani, ndo maana alimshika mtoto wake na kumnyonga. Wakati nafagia fagia pale mahakama Kuu, jaji akawataka wanasheria kusoma sheria mbalimbali na hasa toka Afrika magharibi kule Nigeria, na kuangalia kesi za Nigeria zenye mlengo au kushabiana na kesi ya huyo dada. Nigeria wanasheria za kichawi na mashetani kulingana na mila zao. Ni moja ya kesi ambayo sinto isahau ktk maisha yangu. Ila jaji alionekana anaupendo. Nakumbuka alituita wote ofisini kwake kujadili kwanza kabla ya kesi kuanza kusikilizwa. Nami mfagiaji nikabahatika kuwepo katika mjadala huo. Usiniulize kwanini. Huyu jaji siku zote alijaribu kutotoa adhabu ya kifo.
Nilimpenda sana huyu jaji, alikuwa na moyo wa msamaha, moyo wa unyenyekevu. Aliachia watu wengi huru hasa anapokuwa kesha kaa mahabusu muda mrefu.
 
Tunapangiana kupenda au kuchukia tangu lini?
Mtu anapokuwa hana hoja. Hoja yangu binadamu hatujapewa mamlaka ya kuhukumu, ndo maana Neno la Mungu linasema usihukumu usije hukumiwa. Ni wapi nimesema mpende au upende! Niwapi nimesema uchukie? Soma na elewa mada. Narudia naongelea HUKUMU.
Na kuhukumu si kwamba unapenda au upendi au unachuki.
 
Mtu anapokuwa hana hoja. Hoja yangu binadamu hatujapewa mamlaka ya kuhukumu, ndo maana Neno la Mungu linasema usihukumu usije hukumiwa. Ni wapi nimesema mpende au upende! Niwapi nimesema uchukie? Soma na elewa mada. Narudia naongelea HUKUMU.
Na kuhukumu si kwamba unapenda au upendi au unachuki.
Weye umeona wapi huyo rafiki yako anahukumiwa?Acha kujishukushuku utayumba maishani.
 
Eti kifo Cha mwenzio isiwe kicheko kwako unakumbuka magufuli alikataza hata watu kumuombea lissu Yani alitufikisha viwango vya uadui wa juu Kama taifa kuvaa fulana za kumuombea lissu ikawa jinai kwenda hospital kumpa pole ikawa jinai khaaa baba yule hapana aisee na aendelee kuwa carbon.
Hapa sijadili matendo ya mtu najadili mwanadamu kumhukumu mwanadamu mwingine baada ya kufa. Je ni haki? Neno la Mungu linasema Usihukumu ukaja hukumiwa. naongelea kifo si penye uhai.
Swala la kuomba si lazima kujikusanya, naamini Lisu aliombewa na watu wengi binafsi. Nakumbuka hata nami nilikuwa namwombea. Na sikukatazwa kuomba binafsi ndani kwangu.
Na uzuri Mungu hapokei maombi kwa sababu ya T shirt zilizo andikwa, bali upokea maombi ya toka rohoni na yakweli. Vya kiroho uenda kiroho na si kimwili.
Makamu wa Rais mama Samia, Rais msitaafu Mwinyi, Jaji mstaafu na wengineo walienda mbona sikuona hizo jinai unazosema, ebu nitajie kesi ipi ilikuwa mahakamani kwa watu walioenda kumuona Lisu?
Watanzania tusiwe watu wa kuweka chumvi au kuzidisha maneno ili tu kutaka kuonesha uhalali.
 
Weye umeona wapi huyo rafiki yako anahukumiwa?Acha kujishukushuku utayumba maishani.
Nijishuku na nini, siishi kwa kujipendekeza, najitambua na naendesha maisha yangu bila ushabiki. Naongea kilichopo. Mwenye kuyumba ni wewe ulie na chuki za marehemu. Mtu yoyote anae ishi kwa chuki hana furaha ya maisha. Nakuona weye hapo ulivyoyumba. pole sana.
 
Huyo Magufuli wako alikuwa ndio Mungu wako? Yeye Magufuli alikuwa na mamlaka ya kuhukumu binadamu wenzake na kuwaua. ...eboo. ! Kazi ya kuwaita watu ni ya Muumba, na Magufuli hakupewa mamlaka ya kuhukumu binadamu. Watu wanaokotwa viroba baharini, Risasi mchana kweupeee na hakuna uchunguzi. Tena afe mara 2 huko Akhera...unaleta kichefu chefu
 
Vile mwendakuzimu amefurahia andiko lako refu kutokea huko kuzimu😁😁😁
162869316286936.jpg
 
Huyo Magufuli wako alikuwa ndio Mungu wako? Yeye Magufuli alikuwa na mamlaka ya kuhukumu binadamu wenzake na kuwaua. ...eboo. ! Kazi ya kuwaita watu ni ya Muumba, na Magufuli hakupewa mamlaka ya kuhukumu binadamu. Watu wanaokotwa viroba baharini, Risasi mchana kweupeee na hakuna uchunguzi. Tena afe mara 2 huko Akhera...unaleta kichefu chefu
Watu wengine wa ajabu sana mada inaongelea kitu kingine, mtu anakurupuka huko na mahesabu yake, sipo hapa kusema Magufuli alifanya hki bali... usihukumu usije ukahukumiwa.
Pia Mungu wangu nae mwamini si wakuchezea, Na mwamini Mungu mmoja tu, alie ziumba mbingu na nchi. Hivyo usiniletee za kuleta, na uwa sijibiwi ovyo, nakuonya.
Kama nakuletea kichefu chefu ingia chooni katapike. Mie natahadhalisha kuwa hatupo kuhukumu kazi ya kuhukumu ni Mungu. Magufuli awe ametenda Mabaya au mazuri anae hukumu ni Mungu tumwachie yeye.
Unapo jadili hoja jadili kwa adabu. Hivi unadhani mimi sijui matusi au dharau! Ebo!
 
Too long to go through

Labda ungeandika amefufuka ningesoma haki.
Uvivu wa mtu kusoma si dhamana kwa wengine wenye uwezo wa kusoma. Sikulaumu nami zamani nilikuwa mvivu kusoma, ila nikajikuta nimeenda kusoma sehemu fulani kwa wiki natakiwa kusoma vitabu si chini ya kumi na page kibao. Mbona nilibadilika.
Ila nikagundua ndo maana wenzetu ni waelewa wa mambo mengi. Wanasoma sana, tena sana.
 
Hitimisho langu kwenye huu mjadala baada ya hapa sitachangia chochote kwenye huu Uzi.
1.JPM alilikuwa kiongozi muuwaji.
2.JPM alikuwa kiongozi aliyedhulumu haki.
3.JPM alipenda kuabudiwa alikuwa infallible asiye na makosa na aliwaumiza waliomkosoa.
Nk
Kiufupi Marehemu magufuli alikuwa kiongozi mbaya mno katika historia ya taifa letu alipotawala taifa zima lililia juu ya ukatili wake. Watanzania walimlilia Mungu naye 17/3/2021 akasikia kilio Chao. Na kufunika ubaya wake alifanya yafuatayo.
1. Alitunga Sheria kandamizi dhidi ya media.
2.ALIUWA wakosoaji wake walioponyoka wakakimbia nchi.
3.Alitengeneza vikundi Kama MATAGA vikundi vya propaganda za kumsifu na kumuabudu hata kwa mabaya ya wazi.
4.Alitumia ujinga wa watanzania (kukosa kwao elimu) kuwahadaa aonekane mwema mfano kugawa hela mbele ya kamera kwa masifa ya kijinga wakati hata vitabu vya dini vinasema ukitoa hata mkono wako wa kushoto usijue ulichotoa.
Alijidai na kujibrand mtetezi wa wanyonge kumbe alikuwa mtetezi wa wajinga.
Alienda kwenye madhabahu ya bwana asubuhi kujionyesha yeye ni mchamungu kumbe ikifika jioni anavaa mzula usoni na kugeuka muuwaji mtekaji na mkwapuaji.

Mwisho vyombo vya ulinzi na usalama visije kamwe kuruhusu RAIS MUNGU katika ardhi ya taifa letu.
 
Hakuna sehemu aliyosafishwa, na siko kusafisha, bali naongea wazi hakuna chuki ya marehemu duniani. Kujenga chuki kwa mtu alokufa nadhani ni kutokuwa na akili za kufikiri. Nimeongelea kifo chake na yasemwayo kwa hicho kifo. Sasa nimsafishe kwa nani?
Nyie ndo mtakao kufa vifo vya ajabu na vibaya! Wewe si Mungu kuhukumu!
Sasa nimtetee Magufuli kwani anagombea uRais. Soma uelewe mada chuki zako usikimbie na kuandika tofauti ya mada.
Napenda kukukumbusha utakufa pia, je umetafakari maisha yako?
Hujambiwa unamfanyia kampeni umeambiwa unamtetea baada ya watanzania kumtia hatiani kwa makosa yake ya kujiona kuwa yeye ni bora kuliko yeyote kukandamiza watu kuzurumu na mfano wa hayo
 
Back
Top Bottom