Hayati Lowassa alivyomponza Kikwete akatimuliwa Msasani kwa kufokewa na Mwalimu Nyerere

Hayati Lowassa alivyomponza Kikwete akatimuliwa Msasani kwa kufokewa na Mwalimu Nyerere

 
Tuliokuwa ndani ya UV CCM wakati huo tunafahamu mengi sana

kama Mama Anna Makinda angeamua kuandika kitabu au kuandika ya nyuma ya pazia angeliandika vyema sana hili

Mwalimu alimwita Anna Makinda na kuna ujumbe aliotumwa binafsi kwa Jakaya na JK kabaki na siri hiyo nadhan hajawahi kuiweka hadharan aliambiwa nini na Anna Makinda

ni kama vile Mama Getrude Mongela alipopewa ujumbe rasmi na Mwalimu ampelekee Ndugu Ally Hassan Mwinyi 1985 muda mchache kabla ya uchukuaji fomu

Siasa ina mengi sana

Hatujui kwanini Jakaya baada ya kushinda kwny CCM 1995 iliamriwa kura zipigwe tena na baada ya hapo akaomba fursa azungumze japo vijana wenzie tulitamani agome

JK alikuwa Makonda wa Mwl Nyerere kwa mliokuwa hamjui

ndie alikuwa Katibu wa vikao vyote vya vita ya Kagera

ndie alietumwa kumshawishi Salim agombee Urais

ndie alie deal na Kighoma Malima n.k

pengine alipewa maelekezo maalum kuhusu Monduli maana hata Edward Moringe alitajwa sana kuwa Mrithi wa Mwalimu na ikashindikana

Hayati Jaka Mwambi aliekuwa Balozi wetu Russia na Msiri wa JK angeweza kuandika kitabu kizuri kuhusu Siasa za Wanamtandao

Huwezi kuzungumza rafu na makando kando ya Wanamtandao bila ya kuwataja Viongozi wa Wanamtandao

JK angelegea na kuruhusu kuachia Nchi wana Mtandao angelaaniwa na kila kiumbe kinachopata sunlight
Kweli urafiki wa wanga haudumu, nani angeamini wanamtandao wangepishana pakubwa mwaka 2015?.....yote yamebaki historia Sasa.

Tungoje mitandao mipya kuelekea 2025.
 
Ongezea na mkapa akaja kuwa fisadi papa
Kwa hiyo Nyerere Hana haki ya kutambua nani malaika na Nani shetani
Interesting. Ukisoma mada kama hii unaona kuwa CCM kweli ni chanzo cha matatizo ya nchi hii. Nyerere baada ya kuacha katiba mbovu na mfumo m’bovu wa uongozi bado aliweka mkono kuchagua na kuendorse mafisadi kuwa viongozi.

Tena huyo BWM aliyemuita “Mr. Clean” alimliza mapema kabisa kwa kuuza NBC kwa “makaburu” kwa bei chee yeye akiwa hai na kushuhudia. Malalamiko yake kupinga mnada ule yalipuuzwa kabisa. Alipofariki tu biashara ya asset za serikali ikapamba moto bila hata vigezo vya haja. Viwanda vikaishia kuwa magodown. Wanunuzi wengi wakiwa madalali wa real estate badala ya wawekezaji makini.

Leo hii ukiambiwa Lowasa alikataliwa kwa sababu ya kuwa na hela nyingi au fisadi, unajiuliza huu ni mzaha au nini? Kiongozi gani wa CCM baada ya Nyerere ana rekodi safi ya kujivunia ya kutokuwa mwizi au fisadi? Angalau AH Mwinyi Nyerere alimtambua kiasi lakini bado akamgonga na “kiongozi unaweza wewe binafsi kuwa msafi. Lakini sharti uwe na uwezo wa kuwaambia ndugu na rafiki zako kwa kauli isiyo na shaka kuwa Ikulu ni mahali patakatifu”.
 
Ni kweli alimshughulikia Kighoma Malima barabara

Ufisadi fisadi wa kwanza mkubwa alikuwa waziri alikuwa Kighoma Malima mtu wa swala Tano ila fisadi hatari na sigda yake usoni na swala Tano akiwa waziri wa Fedha mikashfa kibao ya kifisadi

Raisi Mwinyi akaona atafute mtu serious kweli akampa Kikwete uwaziri wa fedha na akamtoa Kighoma Malima na akampa Kikwete , Kikwete alimshughulikia barabara bila kujali ni mtu wa Pwani mwenzie au Muislamu mwenzie account zake nje alikoficha pesa Kighoma Malima alisafiri hija kumbe anaenda kutaka kukimbia nchi akatoe pesa kule kaweka nje akaenda hija na nyumba ndogo bi mdogo kisha akaenda huko ulaya atoe pesa wale maisha ulaya huko akakuta Kikwete waziri wa fedha kazipiga pin Akaunti Zote hakuna pesa ya kutoa

Akapata presha akafa wakarudisha kuzika Tanzania Kwa hasira familia yake waliogoma hawakutaka Serikali ihusike Hadi Mwanawe mkuu wa mkoa Sasa hivi alitorokea upinzani

Kikwete ndio alikuwa waziri wa kwanza Enzi hizo kupambana na fisadi mkubwa Malima aliyekuwa waziri wa fedha Kabla yake

Kwa Hilo apewe hongera na maua yake
Mzee Mohamed Said unazo hizi taarifa ?
 
Tuliokuwa ndani ya UV CCM wakati huo tunafahamu mengi sana

kama Mama Anna Makinda angeamua kuandika kitabu au kuandika ya nyuma ya pazia angeliandika vyema sana hili

Mwalimu alimwita Anna Makinda na kuna ujumbe aliotumwa binafsi kwa Jakaya na JK kabaki na siri hiyo nadhan hajawahi kuiweka hadharan aliambiwa nini na Anna Makinda

ni kama vile Mama Getrude Mongela alipopewa ujumbe rasmi na Mwalimu ampelekee Ndugu Ally Hassan Mwinyi 1985 muda mchache kabla ya uchukuaji fomu

Siasa ina mengi sana

Hatujui kwanini Jakaya baada ya kushinda kwny CCM 1995 iliamriwa kura zipigwe tena na baada ya hapo akaomba fursa azungumze japo vijana wenzie tulitamani agome

JK alikuwa Makonda wa Mwl Nyerere kwa mliokuwa hamjui

ndie alikuwa Katibu wa vikao vyote vya vita ya Kagera

ndie alietumwa kumshawishi Salim agombee Urais

ndie alie deal na Kighoma Malima n.k

pengine alipewa maelekezo maalum kuhusu Monduli maana hata Edward Moringe alitajwa sana kuwa Mrithi wa Mwalimu na ikashindikana

Hayati Jaka Mwambi aliekuwa Balozi wetu Russia na Msiri wa JK angeweza kuandika kitabu kizuri kuhusu Siasa za Wanamtandao

Huwezi kuzungumza rafu na makando kando ya Wanamtandao bila ya kuwataja Viongozi wa Wanamtandao

JK angelegea na kuruhusu kuachia Nchi wana Mtandao angelaaniwa na kila kiumbe kinachopata sunlight
Aisee

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni vema kuweka records Sawa.
1995 majina matatu yalipelekwa mkutano mkuu.
Wagombea walikuwa
Cleopa Msuya (Waziri Mkuu na Makamu wa kwanza wa Rais)
Benjamin Mkapa (Waziri wa Elimu ya Juu, Sayansi na Teknolojia)
Jakarta Kikwete (Waziri wa Fedha)

JK aliongoza kwa kura akifuatiwa na BWM na Msuya akawa wa 3.
Katiba ya CCM ilitaka mshindi awe na zaidi ya 51%, kitu ambacho JK hakufikisha.

Ni uongo kuonesha JK alionewa.

Ndio maana aliposhinda kwa wingi wa kura 2005 kwa kuwabwaga SAS na Mark Mwandosya, alikuja na kauli..."safari hii, kura zimetosha".

Hoja za wazi ni vema zikajengewa hoja kwa uwezi maana kumbukumbu za 1995 tunazo.

Wasalaam!
Asante

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Niliona Ile hotuba kupitia TBC baada ya Mkapa kutangazwa mshindi 1995 Kikwete aliongea hotuba Moja mzuri sana. Kiasi Cha kufanya Mwalimu Nyerere asimame kupiga makofi na ukumbi mzima ukamfuta Nyerere kusimama na kupiga makofi. Marehemu Mkapa akakimbia kwenda kumkumbatia Jakaya kwa hisia kali kama mtoto anayenyonya aliyekosa kumuona mama yake siku mbili. Jakaya was matured but at that time Nyerere alikuwa sahihi juu ya kumpa Marehemu Mkapa. Jakaya alihitaji kukua zaidi.
Hahaha asante kwa hii kumbukizi mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nahisi japo sina uhakika kuwa Wewe ni kijana na pengine 2007 wakati wa kashfa ya Richmond ulikuwa mdogo

kasome report ya Richmond na uhusika wa kila mmoja ndio utajua kwanini hadi leo hakuna hata mmoja aliweza kumjibu kwa hoja kuanzia ndani ya Bunge hadi nje ya Bunge Dr Harrison Mwakyembe

Mwakyembe alitendea haki sana taaluma yake ya Uandishi wa uchunguzi na Sheria

oamoja na wingi wa wapambe hadi leo…kuhusu ile report wote walikuwa wanasema No comment na wote waliohusika waliishia kujiuzulu badala ya kujibu hoja
Hivi na hii report ya Mwakyembe ndio ilipelekea kupewa sumu sio

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nilicho gundua kuna kitu kimemkwaza jk , kwenye msiba wa El, jk anaona kuna watu wanamchafua Huku wakimsifu El , bila kujua El ni jambazi Tu 😂.

Jk kwangu ni kiongozi Bora kabisa, alijali wananchi, shida ni mtandao ndio ulikuwa ukimtia aibu
 
Tumeshazika sasa tunajibu hoja kwa hoja

Walioshadadia Kashfa ya Monduli

1) Freeman Mbowe
2) Godbless Lema
3) Chrstopher Ole sendeka
4) Anne Kilango Malecela

wote hawa wanatokea unapotokea Wewe mbaguzi

au wakati wa Kashfa ya Richmond mlikuwa bado wadogo

Waliotupiwa zigo la Monduli walifanyie kazi walikuwa Home boy ambao leo ndio hao hao wanalalamikia wakwere walivyokuwa akili nusu Mlingoti

hao hao ndio walikuwa wanamtukana Mkwere kuwalinda wana mtandao!
Mwanasiasa Mahiri na madhubuti lazima uwe mtulivu, akili nyingi sana na mvumilivu na sifa zote hizo Adui yenu mkuu anazo

Sifa kubwa sana ambayo Mkwere na Mzee wa Monduli pamoja na kutofautiana walikuwa nayo ni kutopenda kulalamika lalamika

ukim snitch anaku snitch na wakikutana kila mmoja anajibu am fine

Walimzunguka Bosi kwny Richmond nae akawapelekea moto kwa kutumia hiyo hiyo Richmond

walipotolewa nje ya Game wakaunda magenge mengi sana ya hujuma hadi migomo mikubwa mikubwa akapiga kimya akawasubiri 2015 akala kichwa

Wakahamia upande wa pili wamuoneshe show kwa kuwa wana watu na pesa nae akawaonesha ana akili na dola wakamalizana kibingwa

na wote hawakuwahi kulalamika hadharan

Kitu cha kujivunia Jk alisikiliza kilio cha Wengi cha kulipasua Kundi lake la Wanamtandao

2017 alimtumia Mzee wa Kundi Samwel Sitta kumpumzisha Ngoyai na 2010 akatumia nguvu na ushawishi wa Ngoyai kupitia NEC kuweka vipengele cha Jinsia kumpumzisha Uspika Mzee Sitta

2011 akamtumia aliekuwa Mwanamtandao wa Mzee Sumaye Ndugu Nape akampa Ukatibu wa Itikadi akaanza ku deal na mapacha watatu na Tajiri wa Igunga akavua jezi

na 2015 akakamilisha madaraka yake kwa kuhakikisha Wanamtandao hawapo tena kama kundi


Pamoja na tofauti zote na rafu zote za Siasa hakuwa na muda kuhujumu uchumi au biashara ya Mtu japo alikuwa na uwezo wa kufanya hivyo

alijua Michezo ya Siasa itaishia kwny Siasa sio kutafutana kwenye Bank Accounts na Assets za mtu
Salute
 
Ni kweli alimshughulikia Kighoma Malima barabara

Ufisadi fisadi wa kwanza mkubwa alikuwa waziri alikuwa Kighoma Malima mtu wa swala Tano ila fisadi hatari na sigda yake usoni na swala Tano akiwa waziri wa Fedha mikashfa kibao ya kifisadi

Raisi Mwinyi akaona atafute mtu serious kweli akampa Kikwete uwaziri wa fedha na akamtoa Kighoma Malima na akampa Kikwete , Kikwete alimshughulikia barabara bila kujali ni mtu wa Pwani mwenzie au Muislamu mwenzie account zake nje alikoficha pesa Kighoma Malima alisafiri hija kumbe anaenda kutaka kukimbia nchi akatoe pesa kule kaweka nje akaenda hija na nyumba ndogo bi mdogo kisha akaenda huko ulaya atoe pesa wale maisha ulaya huko akakuta Kikwete waziri wa fedha kazipiga pin Akaunti Zote hakuna pesa ya kutoa

Akapata presha akafa wakarudisha kuzika Tanzania Kwa hasira familia yake waliogoma hawakutaka Serikali ihusike Hadi Mwanawe mkuu wa mkoa Sasa hivi alitorokea upinzani

Kikwete ndio alikuwa waziri wa kwanza Enzi hizo kupambana na fisadi mkubwa Malima aliyekuwa waziri wa fedha Kabla yake

Kwa Hilo apewe hongera na maua yake
Sho...
Nimesoma hayo hapo juu kuhusu Prof. Malima na ningependa na mimi niseme machache niyajuayo kuhusu Prof. Malima.

Katika Bunge mwezi June 1994 Prof. Malima akiwa Waziri wa Fedha alileta mswada kuwa misamaha yote ya kodi iwe chini ya Waziri wa Fedha badala ya kuiachia iwe katika mamlaka nyingi tofauti.

Maadui zake ndani ya Bunge wakalalamika kuwa Prof. Malima alikuwa anataka kujijengea himaya.

(Kwa nini Prof. Malima alikuwa na maadui ni mada ya kujitegemea).

Hata hivyo fikra zilitulia na mantiki ikatawala kuwa hilo ni jambo jema na mswada ule ukapita.

Baada ya mwezi mmoja kupita wakati Prof. Malima yuko nje ya nchi Baraza la Mawaziri likaitishwa kwa shinikizo la Waziri Mkuu John Malecela akiungwa mkono na mawaziri wanne wakongwe nia ikiwa kugeuza suala la misamaha ya kodi uliopitishwa mwezi mmoja tu uliopita.

Prof. Malima aliporejea nchini na kukuta kuwa uamuzi wa Bunge kuhusu misamaha ya kodi umepinduliwa na Bunge, Prof. Malima alimtahadharisha Rais Ali Hassan Mwinyi kuhusu matokeo ya kwenda kinyume na maamuzi ya Bunge na matakwa ya wahisani.

Rais akaitisha Baraza la Mawaziri lililokaa kwa siku nne.

Prof. Malima alihimili hoja zote kutoka kwa maadui zake katika serikali akitetea uamuzi wa Bunge.

Baada ya siku nne Baraza la Mawaziri lilirejea nyuma katika uamuzi wa Bunge.

Maadui zake waliumia sana na chuki yao dhidi yake ikazidi.

Hayo yote ya kuwa Prof. Malima alikuwa fisadi si kweli.

Prof. Malima hakuwa na mali nimemuona kwa karibu sana nyumbani kwake jirani na Victoria na nimeiona nyumba yake Kisarawe siku ya mazishi yake.

Prof. Malima hakuwa na mali na kama alivyokuwa akipenda kusema katika uhai wake, ‘’Hakula cha mtu.’’

Ametajwa hapa Kikwete kuwa alipewa nafasi ya Waziri wa Fedha badala ya Prof. Malima lakini mwandishi kaishia hapo tu.

Inataka ushughulishe bongo lako ujiulize kwa nini Kikwete?

Yapo mengi.

Kwa nini hakuyasema mengine na ni muhimu katika historia ya Prof. Malima?

Hakuyasema inawezekana kwa kuwa hayajui.

1708205226666.png

 
Back
Top Bottom