Hayati Magufuli aliharibu sana hii nchi, Rais Samia atapata tabu kuongoza asipokuwa mkali

Hayati Magufuli aliharibu sana hii nchi, Rais Samia atapata tabu kuongoza asipokuwa mkali

Johnny Sack

JF-Expert Member
Joined
Jan 21, 2017
Posts
8,984
Reaction score
19,288
Wakuu Habari

Baada ya ziara ya Samia ya kwenda Kenya na kuondoa mtanziko wa kibiashara na kidiplomasia kati ya nchi hizi mbili na malori ya Tanzania kuruhusiwa kupeleka bidhaa zetu huko nilisoma maoni ya baadhi ya Watanzania ndipo nikajua Magufuli aliharibu hii nchi kiasi gani.

Kwanza kitendo hiki cha Samia badala ya kupongezwa na kila Mtanzania kuna watu wngi nawajua ni wasomi wenye akili kabisa walikuwa wakiponda eti hii ni ziara ya kujipendekeza na ameingia mtegoni, ukiwauliza sababu hawana, yaani wao wanaona kufanya biashara na nchi jirani ni hasara kwa sababu Magufuli alina haifai.

Pili kaui ya Samia ya kuwaasa TRA kukusanya kodi kwa njia ambayo ni sustainable, ambayo itawezesha Serikali kupata mapato na hapo hapo sekta binafsi kuendelea kukua na kutoa ajira na kukuzauchumi, hili likaonekana tena ni udhaifu

Tatu Serikali ilipoagiza vibanda vya machinga viondolewe katikati ya barabara, jambo ambalo ni la mantiki kabisa kwa kuwa huwezi kufanya biashara barabarani, watu amba0o hata sio machinga nao walipinga vikali wakisema watamkumbuka Magufuli.

Nne Samia alipomsimamisha Sabaya baada ya tuhuma nyingi ambapo pia na yeye alikiri kutumia mabavu badala ya sheria kwenye mahaojiano yake na Clouds Tv, Samia amemsimamisha watu wengi wanalalamika eti kamuondoa kiongozi imara alitakiwa ampandishe cheo.

Tano Samia alipotangaza ataunda tume huru ya wataalamu wetu wa ndani (kwa kigezo cha Magufuli kuwa wazungu wanataka kutuua na chanjo) ili kujua ukweli wa hili , watu hawa pia walipinga vikali wakidai tamko la Magufuli kuwa chanjo hifai ndio linatakiwa kufuatwa japo halikuwa na msingi wowote wa Kisayansi.

Na leo wataalamu hao walipotoa majibu hayo na ku prove nadharia za Magufuli kuwa ni za uongo, nao wanashambuliwa vikali na Rais Samia pia anashambuliwa, kwa sababu tu wanaenda kinyume na tamko la Magufuli kuwa chanjo hazifai.

Kwa kweli Samia anatakiwa awe aggressive kudeal na haya magenge ya apotoshaji la sivyo atapata tabu mno.
 
Rais hayati Magufuli alikuwa yuko sahihi kwa UONI WAKE.

Rais Samia Suluhu Hassan yuko sahihi mno kwa MTAZAMO WAKE.

Nchi ipo na itakuwepo ila APPROACHES zinatofautiana Kati ya kiongozi mmoja na mwingine na NJIA ZA KIDIPLOMASIA haziko "fixed" bali MASLAHI ya nchi huwa yako "fixed"!

Alale pema peponi mwendazake aamin!

TUMUUNGE MKONO RAIS WETU SAMIA SULUHU HASSAN!

#StaunchSupporterOfTanzania
#DieHardFanOfCCM!!!
 
Uzuri wa mama yuko very strategic, unadhani atapata taabu yoyote? Kwanini apate taabu kwa maneno ya mtandaoni. Sema haya majitu ndio yatapata taabu. Hayalali kuwaza namna ya kumnanga mama wa watu.

Hivi hamjiulizi kwanini mama aliunda hii tume? Ni very likely mama majibu alishakuwa nayo anataka kufanya nini na pengine kutokana na vifo vya kina kijazi na kina Jiwe (likely?). Mama hataki kufa kihivyo na anataka kuwaokoa mataga nyie acheni kushupaa. Mama yuko jikoni, anaelewa nini kimemuua nani so mwacheni afanye anachoona kinafaa.

Muulizeni Dr Mpango kilichomkuta hadi akatolewa wodini kuja kuongea na waandishi wa habari

Hii ya kuambiwa kama ni kufa tutakufa tu, kusema kweli haina nafasi kwa sasa
 
Bora wamechelewa kuleta hii report yao wangeleta mwaka 2020 hali ingekuwa mbaya sana kwa watanzania.

Wakitangaza lockdown watajilock wenyewe.

# hongera biswalo mganga kwa kuapishwa
 
Huko kwa wenzetu ambako tunakopi na kupaste, wameambiwa kuvua barakoa kwa wale waliochanjwa chanjo zote mbili....na kuwaomba ambao walikataa kuchanjwa waendelee kuvaa barakoa!
Habari ya kuhuzunisha ni kuwa hata waliochanjwa chanjo zote wamebainika kupatwa na maambukizi ya covid 19....ngoma bado mbichi ati!

Bill Maher has tested positive for COVID-19, forcing the cancellation of the Friday taping of his HBO show "Real Time with Bill Maher," the show announced Thursday. The comedian is fully vaccinated, asymptomatic and "feels fine," the show said.

No other staff or crew members have tested positive, the show said. Neil deGrasse Tyson, Max Brooks and Dan Carlin were the guests scheduled for the canceled show on Friday.
 
Rais hayati Magufuli alikuwa yuko sahihi kwa UONI WAKE...

Rais Samia Suluhu Hassan yuko sahihi mno kwa MTAZAMO WAKE...
Mkuu majibu mawili yanayotofautiana hayawezi kuwa sahihi. Yaani mmoja aseme yes mwingine no kisha wote wawe sahihi?
 
Umesoma mapendekezo ya kamati? Kuna sehemu wamesema nchi iwekwe lockdown?

Wengi humu mnaandika pumba kwasababu hamjaisoma ripoti na .hamtaki kuisoma mmebaki kama kasuku.
Akili za watu zimeharibiwa sana mkuu. Nadhani unajionea mwenyewe
 
Jambo la muhimu ni utawala wa sheria za haki na muhimu zaidi Katiba mpya.Mambo ya ukali, chuma na upole yamepitwa na wakati.
 
Mpaka sasa tunapambana na corona kwa njia za kisayansi. Mh Samia suluhu amesikiliza maoni ya wapinzani kupamba kwa njia za kitaalam.
 
Ni hatari sana
Bora wamechelewa kuleta hii report yao wangeleta mwaka 2020 hali ingekuwa mbaya sana kwa watanzania.

Wakitangaza lockdown watajilock wenyewe.

# hongera biswalo mganga kwa kuapishwa kuwa jaji ili sasa Lema akome kabisa.
 
Back
Top Bottom