Hayati Magufuli alikosea kwenye mambo mengi mno. Kubwa mojawapo ni kumchagua huyu mtu

Chuki ni ugonjwa mkubwa nchi hii.

Nimekuwepo tangu Nyerere lakini sijaona Rais mwenye ubunifu kwenye maendeleo kama Samia. Nchi kubwa tu duniani kwa Sasa Zina struggle uchumi wao ila huyu mama mambo yanakwenda.

Miradi ya maji huko vijijini haijawahi kutekelezwa tangu Tanzania iumbwe.

Ward za ICU zilikuwa kwenye hospital za Muhimbili, KCMC, Bugando, Mkapa, na ile ya Moyo. Miaka miwili ya huyu usiyompenda ward za ICU ziko katika hospital zote za rufaa tena zikiwa na vifaa full.

Hakuwahi kutokea Rais yeyote kubuni mradi wa kujenga shule za kisasa zaidi ya Samia ambaye kila Wilaya anajenga shule ya standard kuanzia form 1 -6.

Ni huyuhuyu Samia ndiye Rais wa Kwanza kuja na mpango bora kabisa wa kulima kisasa.

Ni huyuhuyu unayemuona wewe kilaza, ndiye Rais aliyemaliza chaguo la pili la watoto kujiunga form one.

Ni huyuhuyu Samia ndiye Rais wa Kwanza kupeleka vitabu kwa kila mwanafunzi, kila somo tena kwa wakati kiasi kila shule sasa zimeanza kuwa na chumba maalum cha maktaba.

Tunakujuza tu huku Lindi tayari ujenzi wa vyuo vikuu viwili umeanza. Chuo Kikuu cha DSM na Chuo Kikuu cha Teknolojia Lindi.

Mwezi wa 9, anaanza kujenga Bandari ya Bagamoyo.

Scheme ya umwagiliaji Mbarali ilianzishwa na wakoloni around 1910s, hakuna Rais aliyewaza kujenga scheme mbadala wa hiyo. Kwa ubunifu wa huyu unayemuona kilaza, kwa kujua eneo lile tayari limezidiwa na pia kuna uharibufu wa mazingira anaipunguzia mzigo hiyo scheme na kujenga scheme kubwa kabisa ya umwagiliaji Rufiji ili kutopoteza maji ya Mto Rufiji kuingia baharini. Nakushauri tu, wahi Rufiji wenzenu wanachukua maeneo huko. Uzalishaji ushaanza na soon tutakuwa na "mchele wa Rufiji".

Hakuna Rais aliyeanzisha program ya kujenga kilomita zaidi ya 2000 za lami kwa wakati mmoja. Nenda vijijini tukaangalie wakandarasi wanafanya nini.

Yote haya yanafanyika bila kusimamisha miradi ya mtangulizi wake.

In short, nenda vijijini uzungumze mabaya ya Samia kama watakuelewa.
Hili la Bandari hakuna kurudi nyuma. Tutaliondoa chaka lenu la kutolipa kodi. DPW is here for port improvement. Mtake msitake.
 
Hata huyu JPM kupata huo uraisi ilikua bahati nasibu tu using kua ugomvi kati ya Lowassa na marehemu Membe JPM angekufa kama Msukuma wa kawaida.
Hii ni popular narrative vijiweni.


Ila Urais, Magufuli alipewa na Mkapa.
 
Ni hivi,Magufuli hakuwahi kuwa na nia ya kuwasaidia watz kwa ujumla.Mfano ni KIWANDA CHA SARUJI CHA DANGOTE.Kikwete aliwaangalia raia na kuwatafutia njia za kuwafanyia wepesi katika kupiga hatua kimaendeleo.Ujio wa Dangote ulilenga kuwasaidia raia katika kuleta makazi bora kwa kila raia,alikiruhusu kiwanda kizalishe Saruji ya viwango vyote ili kuwawezesha raia wa vipato vya kawaida pia kumudu gharama ya kununua Saruji kwa ujenzi wa makazi.
Kiwanda cha Dangote kilifanya Saruji huku mikoani kuuzwa kwa Tsh12000 kwa mfuko.
Magufuli alipoingia madarakani alimzuia Dangote kuzalisha Saruji ya viwango vyote na kumtaka abaki akizalisha Saruji ya viwango vya kimataifa tu ambayo mfuko mmoja ni kati ya Tsh 25000 hadi 35000.
Leo hii hakuna tena Saruji ya Dangote madukani huku mikoani,bei ya Saruji kwa sasa ni kati ya Tsh 18000 hadi 22000.

Sasa kwa mfano huu unaweza kusema Magufuli alikuwa akiwajali raia na maisha yao?.
Huo uzalendo mnaouimba toka kwake ni upi hasa?.
Kwa hiki alichokifanya kwa Saruji ya Dangote,alikifanya kwa manufaa ya nani?.
 
Achana na wajinga humu mtandao mkuu.
 
Huwa nashangaa sana kuona kila Rais anapondwa sanaa kwa madhaifu tu.

Kama hafai si ugombee uRAIS 2025 ili utuendeshee Nchi vizuri tuishi kama Mbinguni
 
Mkapa alikuwa kama nani kipindi hicho?
Mzee mwenye nguvu ndani ya chama.

Kwani wakati Nyerere anamzuia Malechela na Kikwete kuwa Marais, alikuwa Nani?

====

Hebu soma hii, thread halafu tumia akili yako ya kuzaliwa. Hii thread ni ya kabla ya uchaguzi mkuu, 2015.

 
Unatatizo mahala mpaka hapa ,kama hujui rais hana uwezo utakuwa kituko ,
Onesha huko kukosa uwezo kwa mtu ambaye ndani ya miezi sita iliyopita kavutia 5tr kwenye FDI,kaajiri wengi tangu aingie,miaka miwili kaongeza zaidi ya tr 20 kwenye uchumi,Jenga vyumba vingi vya madarasa kuliko Nyerere,mwinyi na mkapa kwa pamoja nk
 
Dola(ambayo aslimia kubwa wakatoliki) ilikua ikimuabudu Nyerere
 
Alipoteuliwa mwinyi walisema Nyerere amekosea! Akaja mkapa wakasema ccm imekosea..akaja jk mkasema anacheka sana ccm imekosea..kaja magufuli mkakimbia mpaka nchi ..Leo mnasema magu alikosea kumchagua samia mtajuta maji mtayaita mmma
 
Unachokisema nakubakiana nawe!
Ukikaa town (DSM) unaweza usione rais anafanya nini! Ila ukiwa unazunguka zunguka mikoa mingine huko njiani kuna mambo makubwa yanafanyika.
 
Kaka mshahara umepandishwa mwaka 2022 miaka saba tangu awamu ya tano ianze.

Hakuna kipindi cha KISHINDO CHA AWAMU YA SITA pale TBC, jiulize kwanini. Na miradi inamaliziwa kwa kasi ile ile.

Kuna amani kufanya biashara awamu hii kulinganisha na awamu zilizopita.

Kupanda kwa maisha ni suala la dunia nzima, huwezi kutegemea bei ziwe zile zile tu miaka mitano au kumi mfululizo wakati gharama za uzalishaji zinapanda kila kukicha, gharama za usafirishaji haswa petrol inapanda kila kukicha na inaagizwa kutoka nje ya nchi.

Angalau huyo mfanyakazi anaongezewa chochote kitu katika rekodi za mshahara wake hayo ya gharama za maisha yapo juu ya uwezo wa serikali sembuse ule uwezo wa mtu mmoja mmoja.

Na sio ajabu Mpina anakuja na mentality zile zile za kufungia biashara za watu kisa madeni ya kodi, huo unyanyasaji wa wafanya biashara ndio Mwigulu aliukataa bungeni.

Unapoua biashara moja inayoonekana madhara yanayoshuka kwa biashara nyingi zisizoonekana hadharani, unaua mzunguko wa pesa.

Kwa kifupi JPM hakuwa na DNA hata kidogo ya mambo ya biashara, alikuwa na mentality mbovu kuhusu suala zima la biashara na ikaumiza sana uchumi wakati wa miaka yake yote mitano.

Kukamilika kwa wakati kwa miradi kunatokana na maswala mengi na mengine ni ya kitaalam na mengine ni ya kirasimu tu.
 
Una mawazo ya kitoto kabisa wewe, bila shaka ni Nape mwenyewe. Lete hoja acha vitisho Samia hafai kuwa Rais, ana uwezo mdogo sana. Msijidanganye kwamba mambo yatakua "mserereko" kwenye uchaguzi wa 2025

Rashidi,

Nakubaliana na wewe kwa sehemu kubwa, lakini kumbuka mkuu uchaguzi wa Tanzania CCM inategemea dola! Unategemea nini kama Tume ya Uchaguzi ni yao! Wakuu wa Wilaya, DED"s , Polisi, nk....Mlolongo ni mrefu! Siku nyingi bila Polisi na Jeshi kutoka Bara, CCM visiwani ingekuwa ni hadithi....Ndio tumainiwalilobakiza.
 
Hata hicho kidogo kilichopatikana tushukuru Mungu. Kuna mzigo wa kuimalizia SGR unaokula matrilioni ya pesa.

Kuna ujenzi wa viwanja vya ndege unaokamilishwa muda huu na matumizi mengi tu lukuki ya pesa.
 
Ni ushauri tafuta Pesa wekeza uajiri watu kama ni ng'ombe zenu fugeni na mzibadili kuwa utajiri.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…