Hayati Magufuli alikuwa akielekeza vitendo vya kihalifu?

Hayati Magufuli alikuwa akielekeza vitendo vya kihalifu?

Sabaya alikua anatumwa kuwashughulikia wahalifu. Sasa msigeuze maneno kama yeye na aliekua anamtuma ndo wahalifu.

Sent from my SM-A730F using JamiiForums mobile app
Alikua anatumwa kuwakamata wahalifu yeye kama nani??alikua polisi au arusha hakukuwa na polisi wa kukamata wahalifu??....hivi hii nchi tumefika huku kweli??kwamba mkuu wa wilaya anatoka mkoa wake anaenda mkoa mwingine kupiga watu!!...Mungu alitufanyia neema kubwa kumtoa yule mtu duniani....maana kwa namna hii tungeisha...Mungu anaipenda sana tz..
 
Sabaya alikua anatumwa kuwashughulikia wahalifu. Sasa msigeuze maneno kama yeye na aliekua anamtuma ndo wahalifu.

Sent from my SM-A730F using JamiiForums mobile app
Na wengi tuna toa maoni bila kusoma alichosema ni kweli sijaona akisema alitumwa kufanya uhalifu bali kufuatilia watengeza fedha za bandia ambao kimsingi ni wahujumu uchumi na ndio maana wahusika walio tajwa ni waziri wa fedha na gavana
 
Kulingana na tunayosikia katika utetezi wa Ole Sabaya huko Arusha, ati alikuwa akiagizwa kufanya vitendo vya kihalifu na Rais Magufuli.

Kama itathibitishwa kuwa ni kweli basi hili linatoa picha ya uvunjifu mkubwa wa sheria uliokuwa ukitekelezwa na Magufuli katika Awamu yake.

Kuna minong'ono mingi ya uhalifu uliofanywa Awamu ya Tano kwa maelekezo "toka juu".
Tulikuwa tukisema sana wakati ule lakini tulionekana ni wachochezi tu!
 
Si mnawawekea kinga, kwa nini wasifanye huo uhalifu......yaani mnamwekea binadamu kinga wakati na yeye anaweza kufanya makosa au kuvunja sheria, hapa no umuhimu wa katiba mpya unapokuja. Mungu mwenyewe huwa anaapa kwa jina lake kuu ili asiende kinyume na ahadi yake, itakuwa binadamu bhanaa....
 
Kulingana na tunayosikia katika utetezi wa Ole Sabaya huko Arusha, ati alikuwa akiagizwa kufanya vitendo vya kihalifu na Rais Magufuli.

Kama itathibitishwa kuwa ni kweli basi hili linatoa picha ya uvunjifu mkubwa wa sheria uliokuwa ukitekelezwa na Magufuli katika Awamu yake.

Kuna minong'ono mingi ya uhalifu uliofanywa Awamu ya Tano kwa maelekezo "toka juu".
Je Sabaya amakana mashtaka au amekubali?

Naona anataka kumchfua shujaa wetu
 
Inaonekana ni kweli, ndio maana Sabaya licha ya kurekodiwa na camera akivamia maeneo ya watu na silaha mkononi, lakini hakuwahi kuwa na hofu yoyote na hilo.

Hili linathibitisha kweli alikuwa anatumwa akijua ana ulinzi wa kutosha upande wake, ndio maana siku ya kumuaga Magufuli jamaa alilia kama mtoto akijua fika mwisho wake umewadia.

Lakini pia hili linazidi kuthibitisha yale madai kuwa utawala wa Magufuli ulikuwa unaichukia mikoa ya Arusha na Kilimanjaro, huu unyama uliokuwa unafanywa na Sabaya, akitanguliwa na Mnyeti mikoa hiyo, haukuwahi kuonekana ukifanywa mikoa mingine Tanzania.
Mpango aitwe kujibu hoja mahakamani kama ni kweli walimtuma
 
Kulingana na tunayosikia katika utetezi wa Ole Sabaya huko Arusha, ati alikuwa akiagizwa kufanya vitendo vya kihalifu na Rais Magufuli.

Kama itathibitishwa kuwa ni kweli basi hili linatoa picha ya uvunjifu mkubwa wa sheria uliokuwa ukitekelezwa na Magufuli katika Awamu yake.

Kuna minong'ono mingi ya uhalifu uliofanywa Awamu ya Tano kwa maelekezo "toka juu".
Na ww bila kutumia akili wala kufikiria umeingia mzima mzima kwa box!!?

Watu kama ww kwa ufinyu wako wa fikra na uwezo mdogo wa kuhoji unaweza kuta mzungu akabadili fikra zako akakwambia uolewe na ww ukaolewa kweli.....!!!!
stupid
 
Kama kihongosi akiwa uvccm Iringa akatamka na ushahidi unaishi youtube hadi leo kwamba atamuua zito baada tu ya kauli hio kesho akapewa uDC,rejea kauli ya heri james watamuuwa Lisu kwa sumu,rejea mwita waitara ukikutana na mpinzani gizani mmalize, rejea za chalamila,hapi, gambo tena za kujirudia rudia kwann tusiamini ni maagizo.
 
Unyama, Ukatili na ufedhuli waliofanyiwa Wafanyabiashara wenye asili ya kiasia na Mashariki ya kati waliopo Dar haujawahi kufanyika kabisa


Watu walirudi kwenye 'Mkeka' wakashtaki kwa Hakimu asie na upendeleo na Majibu yakatoka kwa wakati

1983 ilipita dhulma mbaya sana watu wakavamiwa mjini wakaporwa mali zao fedha zao kwa kigezo cha uhujumu uchumi, watu walirudi kwenye 'Mkeka' wakalia kwa Mtenda haki Mkuu …less than 12 months later ajali ikatokea 'Goli likasawazishwa'

Tuache Dhulma…dhulma ni mbaya sana inaangamiza hadi kizazi…

kuna Mwingine kizazi chake kimejaa Vichaa kwa sababu ya dhulma aliyowafanyia watu…

kuna mwingine alikuwa Mwamba kichizi kuonea watu akitamba chezea Ndevu usichezee Serikali lakin leo hii hata choo cha chumbani kwake hawezi kukalia sink bila ya kushikwa Mkono na kukalishwa


Mafundisho ya kiislam yanatufundisha Dhambi ya Dhulma toba yake inaanza kwa kutaka msamaha kwa uliemdhulumu kabla ya kuomba kwa Mola wake, imagine umedhulumu uhai wa mtu hapo unamuombaje msamaha

Inaonekana ni kweli, ndio maana Sabaya licha ya kurekodiwa na camera akivamia maeneo ya watu na silaha mkononi, lakini hakuwahi kuwa na hofu yoyote na hilo.

Hili linathibitisha kweli alikuwa anatumwa akijua ana ulinzi wa kutosha upande wake, ndio maana siku ya kumuaga Magufuli jamaa alilia kama mtoto akijua fika mwisho wake umewadia.

Lakini pia hili linazidi kuthibitisha yale madai kuwa utawala wa Magufuli ulikuwa unaichukia mikoa ya Arusha na Kilimanjaro, huu unyama uliokuwa unafanywa na Sabaya, akitanguliwa na Mnyeti mikoa hiyo, haukuwahi kuonekana ukifanywa mikoa mingine Tanzania.
 
Back
Top Bottom