Yule dada kule Marekani ambaye aliwahi hadi kuhitisha maandamano kupinga serikali ya Magufuli naye juzi katika hili suala la bandari naye kamkumbuka Magufuli. Lakini pia hata Msigwa wa chadema ameshawahi kumkumbuka Magufuli kwa issue ya nidhamu kwa watumishi.Waliofai
dika na uongozi wake mbovu na upendeleo wa kikabila wanamkumbuka, akina Makonda hawatamsahau kamwe. Wabunge waliopita bila kupingwa hawatamsahau kamwe. Sabaya na wengine hawatamsahau Magufuli.
Alizalisha mtu mtoto kwenye ukok weni kisha akamkataa?Madaraja na flyover vitajengwa tena kwa hali ya juu na marais wajao. Hilo sio jambo la pekee kila serikali inajenga madaraja na barabara tangu wakoloni hadi kesho. Magufuli anabaki kuwa kiongozi hatari aliyeingiza ushenzi mkubwa Tanzania ukiwepo ukabila, ubabe, uonevu, wizi wa kimataifa, upotevu mkubwa wa fedha, nk
Mfumo nzuri wa kuhakikisha ccm inashindwa kila uchaguzi?.Na viongozi wazuri hawakumbukwi kwa miundombinu; akina Nyerere, Mandela, etc ni mifano mizuri.
Jamaa hakuchota watu akili na si kwamba watu hawakuwa wakiona mapungufu yake, hayo mambo ya maji barabara na umeme si ndio kazi za serikali hizo? Sasa iweje jamaa ajipatie wafuasi kwa kufanya mambo ambayo wenzake waliyafanya na hadi sasa yanafanyika?Naye alikuwa chenga tu. Kama alikuwa anawapenda wa TZ kwa dhati angetengeneza Katiba nzuri. Lakini ndio kwanza alikuwa anawarubuni masikini kuwa wanachohitaji ni maji, Barbara, umeme, chakula nk nk wananchi hawali Katiba. Yule mzee aliwakonga mioyo mabwege jaman. Kama kuna chuo cha siasa alichosomea yule mzee naamini kinabidi kipewe sifa sio kwa akili zile za kuchota watu akili.