Hayati Magufuli alikuwa na uelewa mdogo wa masuala ya dini, asilaumiwe

Hayati Magufuli alikuwa na uelewa mdogo wa masuala ya dini, asilaumiwe

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2018
Posts
28,297
Reaction score
68,017
HAYATTI MAGUFULI ALIKUWA NA UELEWA MDOGO WA MASUALA YA DINI, ASILAUMIWE.

Na, Robert Heriel.

Leo kijiweni kuna mada Moto ilikuwa ikiendelea inayohusu masuala ya UVAAJI WA BARAKOA, baadhi ya wachangiaji wa mada walimtumia zaidi Hayati Magufuli katika kutetea hoja zao kuwa hakuna ulazima wa kuvaa Barakoa, isipokuwa kumwomba Mungu pekee inatosha.

Vijana hawa niligundua wamepata elimu hiyo kutoka kwenye hotuba alizokuwa akizitoa Mzee wetu, Hayatti.

Hicho ndicho kimenifanya niandike andiko hili.

Kwanza nianze Kwa kusema kuwa, Hayati Magufuli kutokana na Hotuba zake alizokuwa akizitoa na matamshi yake, nachelea kusema Hakuwa na Uelewa, Elimu, ujuzi na maarifa ya mambo ya kiroho, Magufuli Hakuwa anaujua vizuri dini licha ya kuwa alikuwa akipenda Sana kumtaja mwenyezi MUNGU.

Na mtu yeyote ambaye anaufahamu mdogo, ujuzi hafifu, Uelewa Finyu na Elimu duni ya Kidini na Kiroho basi lazima mtu huyo awe Mpotoshaji.

Hii ni kusema Hayati alikuwa Mpotoshaji hasa wa masuala ya kiroho kwani Hakuwa na Uelewa mkubwa wa mambo hayo.

Sio ajabu ndio maana alikuwa akiwanyamba baadhi ya viongozi WA dini waliokuwa wakivaa Barakoa mpaka Kanisani. Tena alikuwa akiwadhihaki na kuwakejeli Jambo ambalo Kama angejua walau hata robo ya elimu ya Dini au mambo ya kiroho asingefanya hivyo.

Andiko hili limekusudia kuwaonya Wale wote waliokuwa wakimuamini Magufuli hasa kwenye kukataza matumizi ya Barakoa au Chanjo Kwa kutumia mgongo wa Kidini ati wamtegemee Mungu. Acheni Fikra hizo, huyo uliyemuamini Hakuwa na elimu ya Kidini wala kiroho.

Mungu hategemewi na wajinga, Mungu hategemewi na watu wasiomfahamu, wasiomjua, wasio na Uelewa naye, wasio na elimu yake, wasio na maarifa naye, Mungu hawezi kutegemewa na watu wa namna hiyo.

Neno la Mungu kasema; MJUE SANA MUNGU ILI UWE NA AMANI

Pia linaongeza kuwa Watu wangu wanaangamia Kwa kukosa Maarifa.

Kisha unaeleza pia, ya kaisari mpe kaisari; ya Mungu mpe Mungu.

Magufuli anaweza kuwa Bora kwenye Maeneo mengi tuu ambayo nilishawahi kuyaeleza lakini haimuondolei udhaifu wake wa kutokujua Elimu ya Kidini na Kiroho ambao huo ni udhaifu.

Hivyo Wale mnaofuata mafundisho yake na falsafa yake ya kutokuvaa Barakoa Kwa kutumia VIGEZO vya kiimani, VIGEZO vya Kidini mkae mkijua Mzee alikuwa anaelimu duni ya Kidini na Uelewa hafifu.

Hivyo msije mkaangamia Kwa kukosa Maarifa.

Pia nitoe onyo Kwa viongozi wengine wakisiasa, Kama huna elimu ya Jambo Fulani msipende kujifanya mnazielezea elimu msizozijua vyema, mnaathiri jamii.

Robert Herieli
Taikon wa Fasihi
0693322300
Kwa sasa Morogoro
 
Ukiangalia kwa umakini wote wanaomtetea jiwe utaona kama Wana mental disorder, wengine huita mtindio wa ubongo yani hawapo sawa

Sent from my Infinix X683 using JamiiForums mobile app

Sio kosa Lao,

Ukitumia media kuaminisha watu Jambo Fulani Kwa miaka mitano mfululizo watu huamini.

Media ni hatari Mkuu
 
Marehemu alitumia muda wake mwingi kuwapumbaza watu. Na wajinga aliwaokota hasa. Aliwadanganya watu:

1) kuhusu makinikia. Kwa mwenye uelewa wa sekta hii, alichokuwa akiongea marehemu ilikiwa ni uwongo na ujinga wa hali ya juu

2) kuhusu gas. Eti imeuzwa kwa wachina, na wajinga wakaamini

3) kuhusu uchumi, eti tupo vizuri, wakati kwenye vigezo vyote tulianguka wakati wa utawala wake

4) kuhusu matajiri, eti wote ni mafisadi na majizi

5) kuhusu uwekezaji kwenye LNG, hakueleza jinsi alivyoharibu mpaka wawekezaji kuamua kuondoka na kwenda kuwekeza Mozambique. Aliwatumia maofisa mbalimbali kutaka warudi, wakamgomea, na kumweleza kuwa watafikiria kurudi baada ya miaka mitano

6) kuhusu Barrick, hakueleza ukweli jinsi alivyorudi na kuwapigia magoti, na kuwakubalia matakwa yao ikiwemo kutumia mahakama za kimataifa badala ya mahakama za ndani alizokuwa amezinajisi

7) kuhusu masuala ya kiimani, hakuwa na uelewa hata wa ABC. Hakujua jinsi Mungu alivyomwambia Nuhu atengeneze safina. Je, Nuhu asingetengeneza safina, badala yake asubirie muujiza wa Mungu, angepona? Wala hakujiuliza ni kwa nini Bwana wetu Yesu alivyoambiwa na shetani ajirushe toka juu, naye akagoma. Hakujiuliza, kwa nini Waisrael ili kujikomboa, Mungu aliwaambia waondoke usiku, watembee na fimbo zao mikononi. Kama wangeamua kukaa pale pale kwa Wamisri, wangepona? Hakujua kuwa Mungu ametuumba tufanye kazi ili kujiokoa, ili kupata mahitaji yetu ya kila siku, naye huweka baraka na miujiza katika zile jitihada zetu.
 
Hilo ni kweli hafu hajui hata zamani wagonjwa walitengwa na Kuna magonjwa walitakiwa kunawa mikono na miguu na kujitenga siku 14 nilivo Soma bible nilishangaa nakujua dunia Haina jipya. Kuvaa barakoa doesn't Mungu hayupo yupo ila katupa utashi tutawale mazingira loh
 
Marehemu alitumia muda wake mwingi kuwapumbaza watu. Na wajinga aliwaokota hasa. Aliwadanganya watu:

1) kuhusu makinikia. Kwa mwenye uelewa wa sekta hii, alichokuwa akiongea marehemu ilikiwa ni uwongo na ujinga wa hali ya juu

2) kuhusu gas. Eti imeuzwa kwa wachina, na wajinga wakaamini

3) kuhusu uchumi, eti tupo vizuri, wakati kwenye vigezo vyote tulianguka wakati wa utawala wake

4) kuhusu matajiri, eti wote ni mafisadi na majizi

5) kuhusu uwekezaji kwenye LNG, hakueleza jinsi alivyoharibu mpaka wawekezaji kuamua kuondoka na kwenda kuwekeza Mozambique. Aliwatumia maofisa mbalimbali kutaka warudi, wakamgomea, na kumweleza kuwa watafikiria kurudi baada ya miaka mitano

6) kuhusu Barrick, hakueleza ukweli jinsi alivyorudi na kuwapigia magoti, na kuwakubalia matakwa yao ikiwemo kutumia mahakama za kimataifa badala ya mahakama za ndani alizokuwa amezinajisi

7) kuhusu masuala ya kiimani, hakuwa na uelewa hata wa ABC. Hakujua jinsi Mungu alivyomwambia Nuhu atengeneze safina. Je, Nuhu asingetengeneza safina, badala yake asubirie muujiza wa Mungu, angepona? Wala hakujiuliza ni kwa nini Bwana wetu Yesu alivyoambiwa na shetani ajirushe toka juu, naye akagoma? Hakujiuliza, kwa nini Waisrael ili kujikomboa, Mungu aliwaambia waondoke usiku, watembee na fimbo zao mikononi. Kama wangeamua kukaa pale pale kwa Wamisri, wangepona? Hakujua kuwa Mungu ametuumba tufanye kazi ili kujiokoa, ili kupata mahitaji yetu ya kila siku, naye huweka baraka ja miujiza katika zile jitihada zetu.

Huko pengine sina Uelewa Napo Sana

Ila kwenye dini Mara nyingi alikuwa akipotosha.

Viongozi wote wa dini waliozidisha unafiki waondolewe.

Kuna yule Mufti aliyesema Bwana Yesu asifiwe sijui Kwa nini Waislam hawamuondoi.
 
Hilo ni kweli hafu hajui hata zamani wagonjwa walitengwa na Kuna magonjwa walitakiwa kunawa mikono na miguu na kujitenga siku 14 nilivo Soma bible nilishangaa nakujua dunia Haina jipya. Kuvaa barakoa doesn't Mungu hayupo yupo ila katupa utashi tutawale mazingira loh
Asilaumiwe, kwani Hakuwa na Uelewa wowote wa mambo ya Kidini

Muhimu wafuasi wake waelimishwe tuu, waambiwe waliyemuamini Hakuwa na uelewe
 
Unless nyote mna Imani moja hivi kweli unaweza kumwambia mtu hujui Imani yako (yaani yeye anachokiamini ndio sawa)? Labda useme anapotosha kinachoaminiwa na watu wa imani ile, ila sio kwamba haelewi yeye anachokiamini ukizingatia zote ni Imani tu.
 
Kwa kweli lakini licha ya kuwa PhD uelewa wake ulikuwa limited hata kwa Mambo ya uongozi

Shida alikuwa much know,

Kujifanya kujua kila kitu, au kufanya kila kitu,.

Makinikia yeye
Korosha yeye
Wanafunzi wenye mimba yeye
Mungu yeye
Media yeye
Jeshi yeye
Bunge yeye

Hapo ndio tatizo lilipoanzia
 
Niko hapa nione angalau wachangiaji kumi nam nitie neno
 
Unless nyote mna Imani moja hivi kweli unaweza kumwambia mtu hujui Imani yako (yaani yeye anachokiamini ndio sawa)? Labda useme anapotosha kinachoaminiwa na watu wa imani ile, ila sio kwamba haelewi yeye anachokiamini ukizingatia zote ni Imani tu.
Umeelewa kinachozungumziwa Mkuu?

Hapo tunazungumzia Elimu ya Kidini na Kiroho, inayounda Imani.

Sijui Kama unaelewa mambo haya
 
Marehemu alitumia muda wake mwingi kuwapumbaza watu. Na wajinga aliwaokota hasa. Aliwadanganya watu:

1) kuhusu makinikia. Kwa mwenye uelewa wa sekta hii, alichokuwa akiongea marehemu ilikiwa ni uwongo na ujinga wa hali ya juu

2) kuhusu gas. Eti imeuzwa kwa wachina, na wajinga wakaamini

3) kuhusu uchumi, eti tupo vizuri, wakati kwenye vigezo vyote tulianguka wakati wa utawala wake

4) kuhusu matajiri, eti wote ni mafisadi na majizi

5) kuhusu uwekezaji kwenye LNG, hakueleza jinsi alivyoharibu mpaka wawekezaji kuamua kuondoka na kwenda kuwekeza Mozambique. Aliwatumia maofisa mbalimbali kutaka warudi, wakamgomea, na kumweleza kuwa watafikiria kurudi baada ya miaka mitano

6) kuhusu Barrick, hakueleza ukweli jinsi alivyorudi na kuwapigia magoti, na kuwakubalia matakwa yao ikiwemo kutumia mahakama za kimataifa badala ya mahakama za ndani alizokuwa amezinajisi

7) kuhusu masuala ya kiimani, hakuwa na uelewa hata wa ABC. Hakujua jinsi Mungu alivyomwambia Nuhu atengeneze safina. Je, Nuhu asingetengeneza safina, badala yake asubirie muujiza wa Mungu, angepona? Wala hakujiuliza ni kwa nini Bwana wetu Yesu alivyoambiwa na shetani ajirushe toka juu, naye akagoma. Hakujiuliza, kwa nini Waisrael ili kujikomboa, Mungu aliwaambia waondoke usiku, watembee na fimbo zao mikononi. Kama wangeamua kukaa pale pale kwa Wamisri, wangepona? Hakujua kuwa Mungu ametuumba tufanye kazi ili kujiokoa, ili kupata mahitaji yetu ya kila siku, naye huweka baraka na miujiza katika zile jitihada zetu.
Namfananisha na Maradona wakati akiwa kocha wa Argentina, hakuwa kocha bali mhamasishaji, na Magu hakuwa rais bali mhamsishaji
 
Leo hii wengi tunatazama mambo kwa mihemko ni kwa bahati mbaya Sana muda huwa hautoi nafasi ya mihemko kuendelea kushika fikra na Hadi huo muda utakapofika tutaendelea kuimba wimbo huu
Andiko Hilo nililiandika Mwaka Jana mwezi wa nane.

Pia yapo maandiko niliyoyaandika 2017

Kwa Sisi tunaojua kuchungulia tulijua pambano hili JPM angepoteza Kwa vyovyote vile
 
Shida alikuwa much know,

Kujifanya kujua kila kitu, au kufanya kila kitu,.

Makinikia yeye
Korosha yeye
Wanafunzi wenye mimba yeye
Mungu yeye
Media yeye
Jeshi yeye
Bunge yeye

Hapo ndio tatizo lilipoanzia
Raisi ni top wa yote hayo uliyoyaorodhesha pamoja na mengine yote yahusuyo nchi yake.
 
Back
Top Bottom