#COVID19 Hayati Magufuli alitia sumu masuala ya chanjo, Serikali nywesheni maziwa

Magufuli alikuwa against chanjo kuwa zimeletwa kuua watu, na hakusema chanjo za Covid pekee, alilnga chanjo zote
Mimi hiyo ya Covid pia sijachanja, sipo katika kundi la wenye risk
Ila chanjo naamini inazuia magonjwa
Magufuli alikua against na chanjo ya corona, sio chanjo zote. Uache uongo.

Zingine zilikuwepo na ziliendelea kutolewa Kama kawaida
 
Lengo la chanjo ni nini?
Kama ni kuwazuia watu wasife na corona sioni tofauti kati ya wale waliochanjwa na wasiochanjwa.
Vinginevyo ni mitego tu ya kibeberu kutengeneza fursa ya kujitengenezea utajiri kwa mgongo wa raia wa dunia hii.

Clueless.
Baeleze.

TELL HER.
 
Si huwa mnasema alikuwa hapendwi na hakuwa na wafuasi , ikawaje tena hao.wananchi wanaofuata mawazo yake ni akina nani?
 
Watanzania ninyi ni watu wa ajabu kweli
Kumbe ile kauli ya Yesu ni kweli bwana
Marko 6:4 Yesu akawaambia, Nabii hakosi heshima, isipokuwa katika nchi yake mwenyewe, na kwa jamaa zake, na nyumbani mwake

Kwa hiyo hata Ulaya na inch zingine alikuwa magufuli ndo alikuwa anakataa au
Yaani mtu akiwa na chuki binafsi zidi ya mtu mwingine wewe sema

Kuna madocter wakizungu. Wasomi wa kweli wa kizungu na watu wengine walikataa hii chanjo
Wewe jiulize mbona uko nyuma zingine hazikukatiliwa kiasi hiki
Kwa hiyo hii ya corona ilikuwa na nini mpaka kila INCH watu wafanye maandamano ya kukataa chanjo hii
Alafu una tokea magufuli alikuwa mshamba
Wewe ndiye mshamba sio magufuli na hili liweke katika akili yako Tanzania kiama kinawatafuta
 
A

Afu hapo ulipo una chanjo za tetenasi, pepopunda, tetekuwanga nk. Hikika tuliharibiwa kisaikolojia na yule mtu wenu.
Si kila samaki analiwa, kwa kuwa unakula sato, sangara, mkebuka, kibua, jodari, changu basi unafikiri na bunju nae analiwa
 
Si kila samaki analiwa, kwa kuwa unakula sato, sangara, mkebuka, kibua, jodari, changu basi unafikiri na bunju nae analiwa
Mifano ya kitoto au kijinga. Alikudanganya afu akafa kwa alichotudanganyia
 
Ni kipi ambacho kingefanya chanjo nyingine kuwa salama na za Corona zisiwe salama kwa mujibu wa Magufuli
Huu mjadala ulishazungumzwa sana. Na moja ya sababu ni namna namuda uliotumika kutengenezwa kwa chanjo.

Sio kila dawa inayotengenezwa huwa salama, hata hapa nchini kuna dawa nyingi tu zimepigwa marufuku mfano ketoconazole na cloxacillin. Lakini haimaanishi dawa nyingine nazo mbaya
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…