Hayati Magufuli alivyoalika wazee wa kimila Ikulu kupiga dua(kutambika) ili mvua zinyeshe

Hayati Magufuli alivyoalika wazee wa kimila Ikulu kupiga dua(kutambika) ili mvua zinyeshe

Wazee wa kimila ni neno la kupunguza ukakasi ru ila walitakiwa kuitwa wachawi tu
Nimecheka kama nawaona mlivyonyeshewa mvua
Ilikuwa kijijini so viatu tulivibeba mikononi afu maeneo yale kuna tope baada ya mvua kukatika MC aliomba wageni waalikwa wanawe hata miguu.
 
Ushirikina ni imani. Na imani kama hizo zinatumika sana kuwapumbaza watu.

Nimezaluwa kijijini, na mpaka leo, naenda kijijini si chini ya mara 2 kwa mwaka. Sijawahi kushuhudia habari ya eti kuroga ili mvua ije, lakini Nyanda za Juu Kusini, ndiyo eneo linalipata mvua nyingi kuliko maeneo mengi ya Tanzania. Mikoa ya Nyanda za Juu Kusini ukijumuisha na mkoa wa Tuvuma (Kanda ya Kusini), ndiyo eneo linalozalisha zaidi ya 70% ya chakula chote Tanzania. Zamani mikoa hii iliitwa, the BIG FOUR (Iringa, Mbeya, Rukwa na Ruvuma).

Mikoa hiyo, hata sasa, pamoja na shida ya upungufu wa mvua nchi nzima, inaendelea kupata mvua, na bila shaka, itapata mavuno ya kuridhisha. Kwenye hiyo mikoa yote, hakuna habari ya kuroga eti ili mvua inyeshe.

Kuroga ni ushirikina. Kiimani, huenda mikoa hiyo inayotegemea sana ushirikina, inaweza kuwa inakosa mvua kutokana na ushirikina uliokithiri. Ukweli ni kwamba maeneo mengi ambayo wakazi wake wengi ni washirikina, huwa hakuna maendeleo.

Kisayansi, yawezekana maeneo yenye matatizo makubwa ya mvua yapo katika maeneo ambayo kutokana na mgandamizo wa hewa, pepo zenye unyevu hazivumi kuelekea huko. Lakini pia yawezekana ni kutokana na ukataji mkubwa wa miti.

Uchawi ni fikra. Uchawi hauwezi kukupa mafanikio ya kudumu. Mobutu, timu ya Taifa ya DRC ilipopata nafasi ya kucheza Kombe la Dunia, alikusanya wachawi 200 maarufu kwenye nchi yake ili wakaroge, wapate ushindi. Na wakamhakikishia kuwa hiyo ni kazi ndogo. Timu yao ikafungwa magoli 11. Kama wachawi wangekuwa na uwezo ambao baadhi ya wenye imani za kishirikina wanaamini, basi Afrika tungeishinda Dunia katika kila jambo. Kama uchawi unafabya kazi, basi kazi hiyo ni kumwangamiza mwandamu, ndiyo matatizo ya kila aina hujirundika Afrika.
Kama umeanza tu kwa kuandika ushirikina ni imani, basi usipinge imani za wenzio, mambo ya mvua kunyesha au kutonyesha na sababu zake ndio imani zenyewe ambazo kila mmoja na zake.
 
Kwanini wasichezee account za mabenki ili wapate hela? Sasa hivi kuna mabadiliko ya tabia nchi, hivyo hao wazee wanajua wanaishi kwenye jamii ya wajinga, hivyo wanawaambia wanaweza kuzuia mvua, na nyie Kwa vile ni jamii ya wajinga, mnaamini wana uwezo huo.
Ipo siku utaelewa kuna jamaa alinunua gari kijijini akaandika bora mchawi kuliko mnafiki,siku alipojikuta amelala juu ya mbuyu alifuta yale maneno
 
Kwenye ile sherehe mzee mmoja akaomba kilo tatu za nyama. Mwenye sherehe akasem huyo babu mpeni kilo nne za nyama. Wahinjaji wakamyima eti ni mchoyo. Sherehe ikaanza saa 6mchana nyie tulinyeshewa nvua non stop.

Mwenye sherehe akauliza kwani yule mzee hakupewa nyama? Wakajibu mchoyo yule aje ale na wengine, aiseee mwenye sherehe alichukuwa kilo tano fasta akakimbia kwa yule babu saa 10 jion mvua ikakata na miziki ikaanza.
Aiiiiiiii walokuja na nguo zao mpya ungeziona nyie msicheze na hawa wazee.
Naona unajifariji na the so called legacy ya jpm😅
 
Hivi nyie mnao jiongelesha hapa mnajua siku ya send off au ndoa ni mangapi yanafanyika nvua isinyeshe?

Tatizo lenu mkishakulaga mkavimvea hamjui imekuwaje sherehe ikaisha vizuri.nyie ni kula tu na kulewa hamjui kazi kubwa inayofanyika usiku wa kuamkia sherehe.

Iko hivi sherehe ni kesho leo atatafutwa mtaalamu wa nvua akiamka asubuhi atafanya yake ila haruhusiwi kugusa maji siku hiyo hakuna kupiga hata mswaki.

Anavaki ndani siku nzima mpaka bibi harusi na wageni watakapo ondoka chakula anakula kwa kijiko hanywi hata maji.

Kama nadanganya wewe siku ya sherehe kwenu kawaulize shangazi zako na bibi zako kuna vibibi vinakaaga huko chumbani siku nzima havitoki hivyo vitaalamu.
 
Nakumbuka kuna siku Magufuli "alitingishwa" kule Mtwara na hakuwahi kukanyaga kule tena mpaka mauti yalipomkuta..

Kwa hiyo unamaanisha ule ukame uliotokea mwaka jana, mpaka pakawepo na mgao wa maji Dsm, na mgao wa umeme karibia nchi nzima, shida ilikuwa ni kwasababu "wazee hawakutafutwa"?
Ni Lindi. "Alifukishwa"
 
Nikiri tu kuwa mimi nimezaliwa kwenye jamii zenye zinazodumisha mila zetu za asili(matambiko nisehemu ya maisha yetu).
Bibi yangu na babu yangu wapo vizuri.
Waliwahi kuniambia kuwa hakuna kazi nyepesi kama wa kuzuia au kuleta mvua.

Wazee wetu hawa wakiwa field huwa wanajaribiwa kwa hicho kitu,ukifeli unarudia somo.kuleta mvua au kuzuia mvua ni somo rahisi katika mitaala ya wazee wa kimila

Tangu uzaliwe ni lini ukaona mkutano wa vyama vya siasa ukavunjika kisa mvua?kwa taharifa yako mikutano hii huwa kuna kamati ya ufundi kuzuia mvua.

Hayati Magufuli baada ya kuingia madarakani aliwaita hawa wazee wa kimila (tamka wachawi)
toka kila mkoa Ikulu na kuwaambia kuwa anawapenda watanzania na asingependa kuona wanakufa njaa.hivyo aliwaomba wamsaidie kupiga dua(tamka kuroga) ili nchi iwe na mvua za kutosha.

Baada ya dua kila mzee alikutana na baasha nene ya kaki ikiwa na nauli na posho ya maana,

Wazee hawa hawakumuangusha ,mvua tuliziona,sasa mama Samia unafeli wapi?Babu yangu ni mmoja kati ya hawa wazee,mwaka wa pili sasa sijasikia simu yake kuwa anakwenda Dar au Dodoma Ikulu kupiga dua

Tangu mama aingie mjengoni mvua hazieleweki,sio mbaya kuiga mazuri ya JPM ,njaa zitatuua,mchele kilo 3500!!!
Tofautisha kati ya Dini na ushirikina, Mama ni Muisilamu mzuri, hawezi kujiingiza kwenye ushirikina
 
Back
Top Bottom