Hayati Magufuli aliwezaje kukopa kwa Wazungu ikiwa aliharibu uhusiano na nchi za Ulaya?

Hayati Magufuli aliwezaje kukopa kwa Wazungu ikiwa aliharibu uhusiano na nchi za Ulaya?

Magufuli alikuwa anakopa zaidi pesa kutoka benki za kibiashara ambapo riba huwa kubwa na huko hawana tatizo na mkopaji, maana ni suala la kibiashara na sio kisiasa.
Lakini hata hivyo tuliingia uchumi wa kati na sasa tumeshuka ghafla.
Je, nani kichwa, anayekopa kwa riba kubwa halafu Nchi inaingia uchumi wa kati au yule anayekopa kwa riba ndogo lakini uchumi na mambo mengine yote Nchini yanaporomoka?
 
Kwani hujui mkopo ni biashara

Screenshot_20220518-214154.png
 
Economic leakage ni
1. Taxation
2. Savings
3. imports
While Economic Injections ni
1. Government Expenditure
2. investments
3. Exports
 
Wanasema Jpm alikopa halafu hela ikabaki nayo Serikali ,wapigaji hivi leo wanasifia wanasema Mama anakopa halafu pesa inafika kwako;-

Wanasema Jpm alitumia Contractionary economic Policies ndio zimeongeza umaskini kwa Watanzania..,
Sababu serikali ilikuwa inaondoa pesa kwenye mzunguko na kuzifungia benki kuu kuziachia katika mtiririko usio na usawa, hivyo pesa kuishia mikononi mwa Serikali haikufika kwa wapigaji,madowntown,misheni town na
Walamba asali
 
Kwani hakuna Miradi iliyojengwa kwa fedha za ndani? Unafahamu kama kuna Miradi ilifanyika kwa kuahirishwa shughuli fulani za Serikali na pesa kupelekwa kwenye hiyo Miradi?
Acha kukoleza uongo, mtu ambaye alidhulumu mpaka pesa za maafa kule Kagera ndiyo afanye miradi kwa pesa za ndani?
 
Mkuu sang'udi, Kama uwezo upo ni sahihi kabisa, na sina tatizo kupata kiongozi mwenye uthubutu wa kiwango hicho na kwa hilo [emoji122][emoji122][emoji106][emoji106] kwa JPM(RIP)

Nitaandika kwa urefu ila tafadhali kama hutojali soma ili uelewe hoja yangu.

Pamoja na hayo aliyofanya, biashara hazikupaswa zifungwe, account za wafanyabiashara hazikupaswa zifungwe, mishahara kwa kiasi fulani ilipaswa iongezwe, huduma za uuzaji mazao hazikupaswa kuondolewa kwa wafanya biashara na kufanya ni state business na mengine mengi.

Nasema hivi kwasababu hivi ndivyo vitu vinavyomwezesha raia wa kawaida kufanya maendeleo binafsi na kurithisha vizazi vya mbele wakati yeye akiendelea kupokea pension ya uraisi na kushuhudia vizazi vyake vikifurahia urithi alioacha na akiendelea kupokea sifa za treni na ndege alizoacha.

NITAKUPA MFANO HAI WA MAMBO YALIYOTOKEA CHINI YA SERIKALI YA JPM:

Wote tunajua sheria zetu wakati mwingine huwa zinakuwa na mapungufu ya kuzitekeleza, mfano sheria za kuwataka wenye kampuni za consultancy wajisajili na VAT na waandae mahesabu bila kujali uwezo wa mtaji.

Kama mtu ana kakampuni kake ka sheria, kameajiri watu 5, sheria inamtaka aandae mahesabu kila mwaka na ajiunge VAT. Gharama ya kuandaa mahesabu si chini ya Tsh 500,000 mpaka 1,000,000 nje ya gharama za uhasibu, gharama ya kufile VAT si chini ya 50,000 mpaka 100,000 kila mwezi.

Sasa huyu mwenye kakampuni hakuwa akifile hesabu za mwisho kwa kutokujua au kwa kupuuza kwa sababu ya gharama za ukaguzi na uhasibu, na akawa anaenda kufanya makadirio kila mwaka kisha analipa kodi anaendelea na biashara kama presumptive tax payers wanavyofanya ilihali yeye ni corporate.

Sasa serikali kwa sababu ina marejesho ya mkopo wa reli ikatumia sheria ya kutokupeleka hesabu TRA ya adhabu ya Tsh 225,000 kila mwezi, na ikatumia sheria ya kutoa assessment kukadiria kodi ambayo huenda ingepatikana kwa kufanya examination of books of accounts.

Ikachukua % ya turnover ya miaka 5 ikaiita profit ikacharge penalty na interest kila mwezi ikapata makisio ya kodi ikajumlisha na zile 225,000 kila mwezi za miaka 5 na kumtaka mfanya biashara alipe plus interest each month for 5 years na kuzuia akaunti yake ya biashara huenda yenye pesa za wateja ikimlazimisha kodi ilipwe, mfanyabiashara akashindwa, biashara ikafungwa. Ukumbuke kwa huo mfumo uliotumika inaweza kuja hata kodi ya M40-M50, pesa ambayo mfanya biashara huyo hajawahi kuota kuishika kwa pamoja.

Kisheria raisi alikuwa sahihi na atakuwa alipata rejesho, ila katika uhalisia aliwanyima raia wake haki ya kufanya maendeleo binafsi kwa kuchukua mishahara yao huenda ya miaka 10 mbele ambayo wangelipwa kama angetumia busara na hako kakampuni kakaendelea kuwepo.

Sawa atapeleka rejesho ila, wale watu 5 ambao mshahara wao ameuchukua? Watoto wao mbeleni itakuwa vipi watakapokuta baba zao walilipia treni ila hawana pa kulala?

Sasa ukute baba anahako kakampuni na mama ni mwajiriwa kwenye kahoteli kalikokuwa kanategemea vikao vya wafanyakazi wa serikali vilivyopigwa marafuku kufanyika kwenye mahoteli hako kahoteli kakafungwa huku mzee wao akiwa anacheti cha darasa la saba akaondolewa kazini akiwa na miaka 57.
[emoji122][emoji122][emoji122][emoji122][emoji122][emoji122][emoji122][emoji122]
 
  • Thanks
Reactions: Tsh
Wakati wa JPM sera ilikuwa ni kupunguza kukopa na kutumia fedha zetu za ndani,na kwa mifani tuliona China ikichukua dhamana ya nchi ilizozikopesha ikaonekana China si mwema sana maana hana nia nzuri na Afrika,basi tupunguze kukopa China ili kuepukana na dhamana tutakayoweka kuja kuchukuliwa kama ilivyotokea kwa Sri Lanka, Zambia na Bandari ya Mombasa,Kenya baada ya kushindwa kulipa mkopo wa SGR.
 
Mwaka 1970 China walitusaidia kujenga reli ya Tazara,huku China kwa kipindi iko ikipitia kipindi kigumu cha uchumi mbaya katika nchi yao,Rais wa China, Mwenyekiti Mao alimwambia Mwalimu Nyerere "Ninyi mna matatizo kama sisi tu,lakini matatizo yenu ni tofauti na ya kwetu,lakini tutawasaidia kujenga reli ya Tazara hata kama sisi tutachelewa kuanza kujenga reli yetu,hivi leo Watanzania na Wazambia tumeshindwa kuiendesha reli hiyo ya Tazara,tunapaswa kujifunza kuitunza miradi mikubwa tunayojenga kwa mikopo na hili ndio lilifanya JPM achague kujenga SGR kwa kodi za zetu Watanzania bila kukopa kwa kipande cha Dar hadi Morogoro.
 
Tatizo la sasa awamu hii ni kwamba si nani anatukopesha bali anatukopeshaje,kwa masharti gani,tunaitumia mikopo hiyo kufanya nini,na pia tunapoona China ikiichukua Zambia au Kenya kwa kushindwa kulipa mkopo kazima tujifunze,maana madini yetu Watanzania yatachukuliwa yote kwa kushindwa kulipa mikopo,maliasili zetu zitakuwa mashakani kutwaliwa na Wachina kwa kushindwa kulipa mikopo yao,pengine pa kuangalia ni kusaini mikataba ya kimangungo wa Msovelo kwenda kusaini Ulaya na Dubai ndani ya jakuzi huku umelewa mvinyo matokeo yake unasaini kuiuza nchi yetu kwa kipande cha mkate,
 
Back
Top Bottom