Jamani, ni hulka ya wanadamu kutotangaza mema ya watu lakini wepesi sana kutangaza mabaya ya watu.
Hivi karibuni kuna madaktari kadhaa walitangazwa na wanafunzi wao kwa ubaya sana! Sijui kama tuhuma walizotangazwa kwazo zilikuwa na ukweli au la!
Huu uzi naomba tufanye kinyume, tuwaseme wakufunzi wetu wa vyuo vikuu kwa majina yao kwa namna walivyo 'committed', 'fair' na mahiri ktk kutoa mashule na hata walivyo fair ktk kutoa na ku'mark' mitihani yenu!
Kama hukujariwa kufika chuo kikuu ww muweke mwalimu aliyekufurahisha kwa umahiri wake wa kufundisha ktk kiwango cha kuu kabisa cha cha elimu ulichofikia! Niishie hapo