Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 28,297
- 68,017
Embu ona!
CHADEMA unapozungumzia watu wenye ushawishi, utamtaja Lisu, Heche, Lema, Mbowe na Sugu. Msigwa kama Msigwa angekuwa hajahama CHADEMA angekuwa kwenye top 6 ya viongozi wenye ushawishi CHADEMA.
Wajumbe wengi wa kanda ya Kati hawawezi kuacha kumsikiliza Lisu ndugu Yao ati wamsikilize Mbowe. Hiyo naturally inamkataa
Wajumbe ya kanda ya Ziwa hawawezi kumuacha Heche ati wamchague Mbowe yaani hiyo ni kitu ngumu. Wapo Wachache watafanya hivyo lakini wengi watamchagua Lisu kwa sababu tayari Heche kiongozi wao mwenye ushawishi kashatoa uelekeo.
Kusini, ingawaje Msigwa kahama kwenda CCM lakini bado anaushawishi kwa ukanda huo kwani yeye alidai ameonewa na Rushwa ilitumika kumuangusha. Jambo ambalo miezi iliyofuata tuhuma za Rushwa kutoka kwa Abdul kwenda kwa viongozi wa CHADEMA zilichachamaa. Hii itamaanisha wafuasi na wajumbe kutoka Kusini waliokuwa wafuasi wa Msigwa watamlipia Kisasi Msigwa kwa kumkataa Mbowe na Wenje.
Ukizingatia tayari wanaharakati kama Mdude CHADEMA ashatoa Msimamo wake kumuunga Mkono Lisu na bila Shaka Heche.
Sugu, ukimtazama Sugu ushawishi wake umepungua na kosa alilolifanya zaidi ni kujiunga na Mbowe ambaye siasa za Mbowe zipo mbali Sana na watu kutoka Nyanda za juu kusini hasa Mkoa wa Mbeya na Songwe.
Watu kutoka Mbeya ni watu wa Itikadi Kali hivyo unaona Kabisa hawatakubali Kumchagua Mbowe ambaye siasa na Msimamo wake ni ule uliopoa.
Hii inamaanisha Mikoa ya Iringa, Mbeya na Songwe lazima Lisu ashinde.
Kuna wanachadema wanamsikiliza Mwakabusi ingawaje Mwakabusi huenda sio CHADEMA.
Ukimtazama Mwakabusi siasa zake ni zile Kali zisizohitaji kubembelezana ambazo ndizo Nyanda za juu kusini wanazozihitajj.
Hapo atabaki, Lema.
Lema yeye yupo dilemma, Kwanza yeye ni mchagga. Hii inamuwia vigumu kufanya maamuzi aende na upande gani. Kumsaliti Mbowe Mchaga mwenzake au kwenda na Lisu mtu mwenye siasa Kali kama yeye alivyo. Siasa za kutokubembelezana.
Huyo Mbowe anashinda kutokea wapi?
Haya!
CHADEMA unapozungumzia watu wenye ushawishi, utamtaja Lisu, Heche, Lema, Mbowe na Sugu. Msigwa kama Msigwa angekuwa hajahama CHADEMA angekuwa kwenye top 6 ya viongozi wenye ushawishi CHADEMA.
Wajumbe wengi wa kanda ya Kati hawawezi kuacha kumsikiliza Lisu ndugu Yao ati wamsikilize Mbowe. Hiyo naturally inamkataa
Wajumbe ya kanda ya Ziwa hawawezi kumuacha Heche ati wamchague Mbowe yaani hiyo ni kitu ngumu. Wapo Wachache watafanya hivyo lakini wengi watamchagua Lisu kwa sababu tayari Heche kiongozi wao mwenye ushawishi kashatoa uelekeo.
Kusini, ingawaje Msigwa kahama kwenda CCM lakini bado anaushawishi kwa ukanda huo kwani yeye alidai ameonewa na Rushwa ilitumika kumuangusha. Jambo ambalo miezi iliyofuata tuhuma za Rushwa kutoka kwa Abdul kwenda kwa viongozi wa CHADEMA zilichachamaa. Hii itamaanisha wafuasi na wajumbe kutoka Kusini waliokuwa wafuasi wa Msigwa watamlipia Kisasi Msigwa kwa kumkataa Mbowe na Wenje.
Ukizingatia tayari wanaharakati kama Mdude CHADEMA ashatoa Msimamo wake kumuunga Mkono Lisu na bila Shaka Heche.
Sugu, ukimtazama Sugu ushawishi wake umepungua na kosa alilolifanya zaidi ni kujiunga na Mbowe ambaye siasa za Mbowe zipo mbali Sana na watu kutoka Nyanda za juu kusini hasa Mkoa wa Mbeya na Songwe.
Watu kutoka Mbeya ni watu wa Itikadi Kali hivyo unaona Kabisa hawatakubali Kumchagua Mbowe ambaye siasa na Msimamo wake ni ule uliopoa.
Hii inamaanisha Mikoa ya Iringa, Mbeya na Songwe lazima Lisu ashinde.
Kuna wanachadema wanamsikiliza Mwakabusi ingawaje Mwakabusi huenda sio CHADEMA.
Ukimtazama Mwakabusi siasa zake ni zile Kali zisizohitaji kubembelezana ambazo ndizo Nyanda za juu kusini wanazozihitajj.
Hapo atabaki, Lema.
Lema yeye yupo dilemma, Kwanza yeye ni mchagga. Hii inamuwia vigumu kufanya maamuzi aende na upande gani. Kumsaliti Mbowe Mchaga mwenzake au kwenda na Lisu mtu mwenye siasa Kali kama yeye alivyo. Siasa za kutokubembelezana.
Huyo Mbowe anashinda kutokea wapi?
Haya!